CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO: Sehemu ya 6 | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 29 March 2017

CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO: Sehemu ya 6

Image result for booty ebonyCHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA SITA
Siku mbili zilizofuatia tuliishi katika mtindo huu.
Wakati nimeanza kuchoshwa na maisha haya katika siku ya tatu na nikiwa tayari kumwambia Akimu turudi Dar es salaam; ndipo lilipotokea lile ambalo ni miongoni mwa mambo matatu muhimu yalinifanya nishike peni na karatasi na kuandika mkasa wangu huu ambao Uncle Wamaywa ameamua kuuita chombezo.
‘’Jiandae Ibra,’’ Akimu Aliniambia kwa bashasha. ‘’Leo kuna ngoma! Watoto aina kwa aina wanakusanyika toka kata nzima. Hii hakuna kulala ni kutimbwirika hadi majogoo!”
Nikamtazama nisimuelewe! Ngoma ni miongoni mwa vitu ambavyo sikuwa na hobi navyo, Nikamuuliza taratibu hali nikiwa nimemkazia macho. ‘’Najua unajua kwamba mimi sipendi ngoma!”
‘’Najua sana, lakini hii tunaita ngoma kimazoea! Jina lake hasa ni mnanda!”
“Mnanda?!”
‘’Ndiyo!”
‘’Mnanda ni nini na Ngoma ni nini?!”
‘’Yanini tuandikie mate il-hali wino upo? mnanda unaanza saa kumi na mbili jioni na sasa ni saa kumi jioni subiria masaa mawili tu utapata majibu timilifu, majibu ya vitendo! Jiandae tu!”
Maswali yalikuwa mengi kichwani, lakini kila nilipomuuliza Akimu jibu lake lilikuwa moja tu. ‘’Jiandae, jiandae!’’
Nikajiandaa.
Kweli, jioni tukakusanyika mnandani watu aina na aina wakijisogeza na kumsherehekea binti huyu anayeolewa. Wasichana na niseme wanawake walikuwa wamejikwatua vilivyo na walikuwa wakijituma hasa pale dimbani.
Image result for booty ebony
Nikashangaa kwa kuwa sikuwa nimewaona kabla. Akimu akinijulisha kuwa nisingeweza kuwaona kwa kuwa ule ni mkusanyiko wa watu kutoka kata nzima na pengine tarafa.
‘’Mambo zaidi utayaona usiku!’’ akahitimisha wakati nikianza kusisimkwa! Ule uchezaji wao ulivutia kwa hakika, ulikuwa uchezaji ambao ungekulazimisha kuangalia huku mwili ukipatwa na joto ghafla.
Wachezaji walio wengi walikuwa akina mama ambao walikuwa na kanga mbili tu, moja kifuani na nyingine kiunoni. Ile ya kiunoni ilikunjwa kiustadi ikaweza kufunika matiti na tumbo kwa kiasi kidogo.
Ile ya kiunoni ilifungwa kinamna kiasi cha kuweza kuonyesha shanga za kutosha zilizosheheni pale kiunoni. Wachezaji walijenga duara kwa mirindimo yao na katikati ya duara hilo kulikuwa na meza iliyojengwa mfano wa jukwaa na kuwekwa nguzo katikati yake.
Kadiri ngoma ilivyokuwa ikinoga, ndivyo mwanamke mmoja alivyochepuka kutoka katika mduara na kuiparamia ile stage ya meza, akainama na kuishikilia ile nguzo kama nyenzo ya kumfanya asianguke!
Hapa tena atayabinua makalio yake ambayo hayakuwa na kitu ndani zaidi ya ile khanga iliyofungwa chini kidogo ya shanga. Halafu angeanza kuzungusha kiuno katika namna ambayo usingetamani aache.
Mwingine midadi ilipomzidia kabla mwenzie hajashuka basi angeinama tu na kumwaga vitu, atamwaga vitu kweli kweli. Mara mbili ngoma ilizimwa, mpiga ngoma akasikilizwa.
Ni katika wakati huu nilipogundua kuwa Akimu hayupo! Unadhani nilimtafuta? Thubutu, ule uchezaji ulishanikamata na kunifanya mateka kabisaa! Akimu nitamtafuta baadae! Nilijiambia nikiendelea kuufuatilia muziki ule wa asili.
Naam huu ulikuwa mduara orijino wa Segere au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa.
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda.
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa!
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipo watazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta ambalo nalo lilikuwa tayari likinishinikiza tufanye mapenzi! Vile nilivyokuwa na ukata wa mwanamke, vile ambavyo jimama yule alikuwa amenihamasisha vya kutosha sikujivunga mwanaume! Nikampa kitu na box!
Tukaneng’eneka kisawa sawa.
‘’Ngoma ilipoanza kupigwa tena ishara ya kuwaita watu warejee ngomani, mimi na yule jimama hatukurudi. Tulikuwa tumeianza ngwe ya pili. Ngwe ambayo ilikuwa na urefu usiochusha wala kuudhi, urefu mtamu.
Ufundi wote aliouonyesha katika ngoma sasa aliuonyesha mbele yangu juu ya nyonga yangu. Nilifaidi hasa, nilifaidi mno! Nilifaidi ukweli wa kufaidi. Mpaka tunafika tamati na kumwaga mizigo yetu ya kuni pale, kila mmoja wetu alikuwa ameridhika.
‘’Ahsante anti!’’ Nikamshukuru
‘’Asante nawe! U’ngangari na unayaweza kwa hakika!’’ akajibu yule jimama.
‘’Sikushindi wewe!’’
‘’Ahsante’’
Ukimya mfupi ukapita
‘’Unaitwa nani?”
‘’Havijawa! Havijawa Mawimbe! Na wewe?’’
‘’Ibra! Ibrahim Semkee Kinara! Ni mgeni hapa nimetokea Dar es salaam!”
‘’Najua kama umetokea Dar!’’
‘’Eeh?”
‘’Ndiyo!’’
“Umejuaje?’’
‘’Pale ulipofikia yupo anti Hidaya, Hidaya ametujuza kila kitu kuwahusu, kuwa mmekuja huku kuburudisha mioyo akili na mawazo! Na manta hofu Ibrahim, hapa hamtaburudisha mioyo tu, bali na miili pia!‘’ Akanambia, nikabaki hoi.
Nikamuuliza maswali kadhaa kuhusu mnanda, akanieleza mengi ambayo sikuyajua, mengi mno!. Nilipoagana nae tukawa tumeachiana namba za simu.
Kesho yake tulipoonana na Akimu nyumbani kila mtu alikuwa na kitu cha kumuhadithia mwenzake. Nae yalimkuta kama yangu! Tulikaa Gobbah kwa siku kadhaa halafu tukarejea Dar.
Ambacho Akimu hakukijua ni kuwa mie niliendelea kuwasiliana na Havijawa na nikawa mgeni wa Gobah kila baada ya siku kadhaa. Minanda nikaizoea, nikawa mzaramo hasa.
Vile Havijawa alikuwa akijuana na wale wapiga ngoma ambao walikuwa wakimpa ratiba ya kazi. Wiki hii tutapiga kijiji X, mwezi ujao tutamtoa na kumfunda mwali kijiji Y!
Ngoma zote nikawa nahudhuria! Mara nyingi nikiwa na Havijawa.
* * *Image result for booty ebony
‘’Leo jioni kuna ngoma!” Sauti nyembamba niliyoifahamu fika ikapenya masikioni mwangu. Nikasisimkwa furaha ikinitawala nusu nusu.
‘’Unasema?’’ Nikauliza tena.
‘’Nasema hivi…,” akarudia kwa msisitizo tunaoweza kuuita wa herufi kubwa “Leo kuna ngoma, nyumbani kwetu!’’
‘’Eti?!’’
‘’We bwana ni kiziwi au kitu gani? Leo kuna ngoma bwana! ‘mnanda!’ nyumbani kwetu!’’
‘’Kwa hiyo nije?’’
‘’Unauliza majibu? Njoo!’’
Nikaenda. Niliyoyakuta yalinitoa jasho! Havijawa alikuwa amenipokea vizuri japokuwa hakutaka kuwa karibu na mimi, kila niliposema nimsogelee aliongea na mimi kwa mkato mkato tu kabla ya kunitaka radhi na kutoweka!
Una nini leo? Nilikuwa nimekumbuka kumuuliza hivi kwenye sms kupitia simu ya mkononi mara kadhaa, pasipo kupata majibu. Ngoma ilipozimwa kwa mara ya kwanza na watu kwenda kupoza makoo mie nilibakia mpweke nikitandikwa na baridi.
Ilipozimwa mara ya pili hali kadhalika.
Mara ya tatu nikiwa nimeanza kupandwa na ghadhabu ndipo yule mpiga ngoma mmoja ambae nilikuwa nimekaa karibu naye na ambae alianza kuwa rafiki yangu aliponiambia kitu kilichoniogopesha kama sio kunitisha. Hii ilikuwa baada ya yeye kuniuliza, nami kumtajia Havijawa.
“Kaka bora utafute mwanamke haraka sana!’’
‘’Mmh hilo nalijua, ndio maana namsubiria Havijawa’’
‘’Huyo hakufai kwa sasa hivi huyo ni moto!’’
Nikashtuka na kumuuliza kwa pupa ‘’Una maana gani?!”
‘’Havijawa ni mke wa mtu!’’
‘’Eti?” Nikasikia nanga zinapaa.
‘’Enhe na mwenyewe keshajua kuwa kuna doezi linalomuibia mali zake ambalo ni lilevi la ngoma ingawa sio lizaramo! Kwa taarifa yako Ngoma hii ni mtego! Mnasubiriwa wewe na Havijawa tu mwende mkaneng’eneke mkamatwe wewe ugeuzwe asusa, baadae mshikaki ili liwe fundisho kwa wengine, ndio maana nakwambia tafuta mwanamke mwingine!’’
Yakaniingia! Nikaweza kuunganisha moja na moja na kupata mbili, baadae kama mpelelezi niliyefundwa vyema, nikafanya mbili na mbili na kupata nne. Havijawa alijua huu ni mtego na hakutaka kunitosa ndio maana akawa mbali.
Akashindwa hata kujibu meseji zangu. Sikujua yuko wapi kwa sasa na sikujua yuko katika hali gani. May be yuko katika kibano kilichopatiliza, na kama hivyo ndivyo basi hata simu yangu kuendelea kuwa hewani ni kosa, nikaizima.
Nikamdodosa rafiki yangu mila na taratibu za pale nae akanifahamisha kuwa adhabu ya ugoni ni kifo. Nikazidi kuogopa ngoma ikiendelea yule bwana akazidi kuwa rafiki yangu.
Ilipozimwa kwa mara ya nne na ya mwisho, Havijawa akatokea! Hakuwa na furaha na bashasha kama ilivyo ada yake. Sura yake ilisawijika na kupoteza nuru, yaelekea alikuwa akilia kwa muda mefu.
Nikijua mtego ndio unakaribia kufyatuka, sikumgusa!
Badala yake nilikwapua mwanamke mwingine nikatokomea nae migombani na kwenda kuneng’eneka nae, Nikamuacha Havijawa pale pale uwanjani. Mwanamke niliyemchukua hakuwa haba, alikuwa bora kwa kila hali.
Nikamuuliza kama ameolewa akasema bado, nikamuomba niwe mgeni wake kwa siku hiyo akakubali. Sikurudi uwanjani nikaenda kulala kwa mwanamke huyu mpya.
**Ni mambo juu ya mambo katika NILAMBE HUMOHUMO……..nini kitajiri…….HAVIJAWA!!!!!!

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us