Kiuno changu ndicho kinachoniweka Mjini – Gigy Money | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 29 November 2016

Kiuno changu ndicho kinachoniweka Mjini – Gigy Money

Video queen ambaye haishiwi vituko, Gigy Money amefunguka kwa kusema kuwa mauno yake ya mwendokasi ndio kitu ambacho kinawafanya wasanii wengi wamtafute kwa ajili ya kufanya naye kazi.

Mrembo huyo ambaye pia ni mtangazaji wa Choice FM, amesema kuwa video queen ni kazi ambayo inalipa tofauti na watu wanavyofikia.

“Unajua kazi yoyote ukiiheshimu ni rahisi nayo ikakuheshimu,” alisema Gigy Money. “Mimi hii kazi naiheshimu ndio maana imeniweka mpaka hapa nilipo. Sasa hivi mimi ni mtangazaji wa kituo kikubwa cha redio, kwa hiyo mimi naweza kuwaambia watu wanatakiwa kuiheshimu hii kazi kama kazi nyingine,”

Aliongeza,”Kusema kweli sasa hivi mimi ni moja kati ya video queen ambao tunafanya kazi nyingi lakini haya yote yanatokana na nikipata kazi naifanya isavyo, napiga mauno ya mwendokasi mpaka mtu labda alipanga kunipa scene moja anajikuta nanipa mbili au tatu,”

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us