KINGAZI BLOG: 08/29/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 29 August 2016

Maajabu!! Aliyefariki miaka 200 iliyopita apatikana tena akiwa hai

Dk Barry Kerzin ndiye alieufanyia uchunguzi mwili huo na kuthibitisha kuwa binadamu huyo aliishi mnamo karne ya nne au ya sita kabla ya kuzaliwa kristo na tangu alipofariki ni zaidi ya miaka 200 imepita.

Wananchi wa eneo hilo wanaamini jambo hilo lina imani za kishirikina ndani yake na wengine wakidai mizimu hiyo huonekana mara kwa mara nchini India.

ASAMOH GYAN arudi kwa kishindo Uingereza.

Nahodha wa kikosi cha soka nchini Ghana Asamoah Gyan anatarajiwa kujiunga na klabu ya Reading kwa mkopo kutoka timu ya China Shanghai SIPG.

Mchezaji huyo wa zamani wa klabu ya Sunderland anafanyiwa ukaguzi wa matibabu na klabu hiyo ya daraja la kwanza.

Gyan aliifungia mabao 30 Sunderland alipoichezea timu hiyo kwa misimu miwili,kutoka mwaka 2010 kabla ya kuelekea Al-Ain ya Umoja wa Milki za kiarabu UAE.

Alijiunga na Shanghai 2015 wakati huo na alikuwa miongoni mwa mchezaji wanaolipwa zaidi duniani.


Mkutano wa Kamati kuu ya CHADEMA wavurugika baada ya polisi kuingilia kati. Lowasa, Mbowe, Mnyika washikiliwa.


Kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichokuwa kinafanyika katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi jijini Dar, kimezingirwa na jeshi la polisi huku viongozi wake wakikamatwa na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.


Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema waliokamatwa na polisi kwa ajili ya mahojiano ni Edward Lowassa, Freeman Mbowe, John Mnyika, Dk Vincent Mashinji na  Said Issah

“Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kiako walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo la lilitokataza mikutano.”

Laana!! MTOTO WA MIAKA 14 AFUMWA GEST NA JIBABA LA MIAKA 60


August 29 2016 Kupitia Hekaheka ya Clouds FM Geah Habib ametuletea Hekaheka iliyotokea Tanga ambapo mzee mmoja kafumaniwa na mkewe akiwa na mtoto wa shule wa miaka 14.

Mjomba wa mtoto ameeleza kuwa mtoto amekuwa akijiandaa asubuhi na mapema sana na anaaga anaenda shule lakini anapitia kwa huyo mzee na baadaye muda wa saa moja anaena shule……

Mahusiano yameanza tangia January, mpaka sasa hivi ni mwezi wa nane na sisi mpaka tumekuja kugundua ni baada ya kutokea ugomvi, mke wake yule mzee amempiga na kumng’ata mtoto ameumia na sisi ndio tukajua hilo suala.

Mtoto wangu ana miaka kumi nne na mzee huyo ana kama 60 mpaka 70 maana ni babu kabisa, sisi halikuwa hatujui tulikuwa tunajua anaenda shule na alikuwa anamuaga bibi yake maana anakaa na bibi yake kwamba wanatakiwa kuwahi namba kumbe asubuhi anaanza kwanza kwa huyo baba.

Jumatano asubuhi walipokutana na huyo baba kupewa hela mara mke wa huyo baba akatoa akaanza kumshambulia na kumng’ata

Hebu jionee photos za, warembo wenye shepu bomba zaidi duniani

Chuchu Hans: Nikiwa na Ray Nahisi Kama Dunia Yote ni Yangu

Miss Tanga mwaka 2005, Chuchu Hans amesema kuwa ndani ya mahusiano ya kimapenzi na staa wa filamu, Ray Kigosi anajiona kama dunia yote ni yake.
Muigizaji huyo amesema anajisikia furaha sana jinsi anavyoishi kwa kusikilizana na mpenzi wake huyo.
“Nikiwa na Ray wangu, huwa nahisi kama dunia yote ni yangu, Ray ananidekeza sana,”Chuchu aliliambia gazeti la Mtanzania.“Ana mapenzi ya kweli, ananipenda mimi na watoto wangu wawili, amekuwa baba bora sana na hilo ndiyo linanifanya nijivunie na kuachana na maneno ya watu,”
Aliongeza, “Kufunga ndoa ni riziki na ninaamini haijafika siku yake, siku ikifika basi kila kitu kitakuwa wazi na hakuna atakayeweza kukwepa jambo hili, ila mapenzi na thamani tunayopeana ni ya mke na mume.”
Kwa sasa Chuchu na Ray Kigosi wamefunguka kampuni ya filamu iitwayo ‘Chura’.

Mastaa Hawa Wamekopi na Kupesti Hadi Nywele

 Harmonize
Andrew Carlos
MASTAA wa Bongo bwana! Baada ya kukopi na kupesti staili ya kuimba na biti zao nyingi kufanana na za Sauz na Nigeria ni kama wamehamia kwenye staili mpya ya usukwaji nywele inayotumika hasa kwa mastaa nchini Marekani.
Ukiwaangalia muonekano wa vichwa vyao, baadhi ya mastaa hawa wakiongozwa na Jux, Romy Jones, Harmonize na wengine kibao utagundua kuna kitu wamekopi na kupesti kutoka kwa mastaa wa mbele ambao ni Chris Brown, Post Malone, The Game, Omario na wengineo
Inaitwaje?
Staili hii iliyotokea kujizolea umaarufu mkubwa kwa mastaa mbalimbali hususan wa muziki inajulikana kama Dutch Braid japokuwa chimbuko hasa la staili hii lilikuwa likijulikana kama French Braid.
 Omarion
Staili hii ipoje?
Usukwaji wake huwa wa nywele kuanzia njia mbili kubwa kisha kwa nyuma inafungwa ama kuachiwa mikia.
Mastaa wengi wa kike kama Kim Kardashian, Karrueche na wengineo wanapenda kusuka njia mbili ndefu za kuacha mkia ukining’inia na kwa upande wa mastaa wa kiume, pande zote za pembeni hunyoa na katikati husuka njia mbili ama tatu kisha huzifunga kwa nyuma.
 Post Malone
Staa huyu wa muziki nchini Marekani ambaye pia ni rafiki mkubwa wa Justin Bieber, amekuwa akibadili staili ya nywele zake mara kwa mara.
Ukicheki baadhi ya video zake za hivi karibuni alizofanya na wakali kama Young Thug, 50 Cent na Kanye West kichwani kwake utamuona katika muonekano wa Ki-dutch.
 The Game
Mei mwaka huu, kupitia ukurasa wake wa Instagram, kwa mara ya kwanza rapper The Game aliitambulisha staili hii ya Duth kwa mashabiki wake.
Rapa huyu kutoka Los Angeles, Marekani aliiweka picha mtandaoni akiwa saluni katika matengenezo ya staili ya Dutch na baada ya hapo alipewa shavu la kutosha kutoka kwa mashabiki.
 Chris Brown
Mkali huyu wa R&B kwa miaka mingi amekuwa hatabiriki katika staili zake za nywele lakini baada ya staili hii kuteka mastaa wengi naye amekuwa miongoni mwao.
Chris ambaye ni baba wa mtoto mmoja, Royalty amekuwa akitupia picha zake mitandaoni zikimuonesha katika muonekano wa Ki-dutch lakini kwa staili mbalimbali.
Jux
Kuonesha kuwa mastaa wa Bongo hawapitwi na kitu katika kukopi na kupesti, staa wa Ngoma ya Wivu, Jux amekuwa miongoni mwa mastaa Bongo waliotekwa na staili hii.
Jux ameonekana kula sahani moja na Chris Brown. Mara ya kwanza Chris alitengeneza staili hii ya Dutch kizamani kwa kuning’iniza nywele mbili mbele na nyuma kubana, Jux alipoona akakopi na kupesti.
Chris akabadili staili hiyo na kunyoa za pembeni, nyuma akizibana. Jux kuona hivyo naye akaiga tena ambayo ndiyo anayo hadi sasa.
Harmonize
Staa huyu anayebamba na Ngoma ya Matatizo, baada ya kuongeza michoro kadhaa mwilini mwake (tattoo), ameamua kubadili na staili ya nywele.
Alichokifanya kichwani kwake, amejaribu naye kukopi na kupesti staili ya Dutch ambapo kwa sasa amekuwa akitupia picha nyingi na vipande vya video akiinamisha kichwa ili mashabiki wake waione staili hiyo mpya ya nywele.
Romy Jones
Hivi karibuni, binamu na DJ wa staa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond, Romy Jones katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Next Door, jijini Dar aliingia na sapraizi kichwani kwake akiwa katika muonekano wa Ki-dutch.
Kama ulivyo muonekano wa nywele kwa sasa wa Omario, Chris Brown na The Game kwa Rommy hakuna tofauti yoyote kwani naye amekopi na kupesti tu.

SHKODRAN MUSTAFI ALIITOSA CITY, AKABANIWA NA MOYES SASA YUPO NA WENGER

Na Athumani Adam

Tetesi zimekuwa kweli mapema wiki hii pale Arsene wenger alipokamilisha usajili wa beki Shkodran Mustafi. Usajili wa beki huyo Mjerumani mwenye miaka 24 kutoka klabu ya Valencia ya kule nchini Hispania utasaidia kuziba nafasi zilizopo kwenye safu ya ulinzi ya Arsenal ukizingatia Per Mertesacker bado anasumbuliwa na majeraha

Ikiwa bado mashabiki wa Arsenal wana furaha ya ujio wa Mustafi, makala hii inakupa historia fupi kabla ya kuja Arsenal

HISTORIA

Shkodran Mustafi alizaliwa tarehe 17 April 1992 kule Bad Hersfeld nchini Ujerumani. Wazazi wake ni raia wa Albania wenye asili ya Marcedonia. Mwaka 2006 alijiunga na timu ya vijana ya Hamburger SV

AKATAA OFA YA MAN CITY NA NEWCASTLE

Mwaka 2009 klabu za Man City pamoja na Newcastle United zilitaka kumsajili Mustafi lakini akataa na kuelekea zake kule Merseyside kwenye klabu ya Everton

ACHEZA GAME MMOJA TU EVERTON

Tangu ajiunge na Everton hadi anaondoka mwaka mwaka 2012, Mustafi alicheza mechi moja tu.   Mechi ambayo Mustafi alicheza ilikuwa dhidi ya Bate Borisov michuano ya Europa League.  Ilikuwa kwenye uwanja wa Goodson Park December 16, 2009 mchezo ambao Everton ililala 1-0

Baada ya kuona hapati nafasi ya kutosha kucheza, mustafi alimwomba kocha David Moyes kuhama Everton na kulelekea kwenye klabu ya Sampdoria.

AFUNGA GOLI LAKE LA KWANZA SAMPDORIA (MECHI 53, GOLI 1)

Mustafi alifunga goli lake la kwanza kama mchezaji “professional” kwenye mechi ya Serie A dhidi ya Atlanta October 2013. Sampdoria ilikuwa imepanda daraja kutoka Serie B tangu iliposhuka mwaka 2011. Mbali na Mustafi pia Samporia walikuwa na wachezaji vijana  Simon Zaza na Mauro Icardi

DAU LA USAJILI LAWA SIRI VALENCIA (MECHI 78, GOLI 6)

Mustafi alijiunga na Valencia mwaka 2014 akitokea Sampodria bila dau la usajili kuwekwa wazi. Zipo tetesi kwamba japo haikuwekwa wazi, lakini Mustafi alitua kwa Euro milioni 8. Ndani ya Valencia Mustafi alicheza mechi 78 na kufunga goli 6.

ALIKUWEPO WORLD 2014, EURO 2016

Mustafi alikuwepo kwenye kikosi cha Ujerumani kilichotwaa kombe la dunia kule nchini Brazil mwaka 2014. Alipata kuitwa kwenye kikosi na kocha Joackim Low baada ya kuumia kiungo Marco Reus. Mustafi aliingia kutokea sub kwenye mechi dhidi ya Portugal na Ghana. Bahati mbaya aliuumia wakati mashindano yanaendelea

Mbali na kombe la dunia pia mustafi alikuwepo kwenye mashindano ya euro 2016 kule nchini Ufaransana.

Pichaz: Hatimaye Drake na Rihanna Wapeana Mahaba Hadharani

Image result for rihanna and drake Couple inayoendelea ku "make" headlines za dunia imezidi kupamba moto baada ya DRAKE NA RIHANNA  kuonesha ulimwengu kuwa mapenzi yao kwa sasa hayafichiki hebu ona pichja hizi hapa














STERLING AJA KIVINGINE, CITY YALA VYA KUCHINJA

Ni kama vile Guardiola anatengeneza timu ambayo itakuwa tishio sana katika ligi kuu ya Uingereza kwa namna ambayo amekuwa akipangilia kikosi chake na namna ambavyo wachezaji wamekuwa wakitoa matokeo kwa klabu hiyo.
Timu imeongeza kujiamini kwa ujumla na pia baadhi ya wachezaji wamepanda kiwango huku majukumu kwa baadhi pia yakiwa yamebadilika na kuwa tofauti kiasi. Sergio Kun Aguero anaonekana kupunguziwa mzigo wa ufungaji na ndio maana sio ajabu kuona watu kama Raheem Sterling na Nolito wakiwa tayari wameona wavu zaidi ya mara mbili.
Uhuru uliopo kati ya Kevin De Bryune na Silva unawapa City sababu nyingine ya kucheza vyema wanapokuwa wanaelekea eneo la ushambuliaji huku pia Fernandinho akiweza kupatia vyema mfumo wa kucheza kama kiungo pekee wa chini na mkabaji huku akiwa jirani zaidi na John Stones.
Jumapili dhidi ya West Ham United, klabu ya Man City iliendeleza ushindi wake wa asilimia 100 kwa kushinda kwa jumla ya mabao 3-1. Mabao mawili ya Raheem Sterling (7, 90+2) pamoja na lile la Fernandinho yaliwabeba City huku Michail Antonio akifunga bao pekee a West Ham ambao hawajaanza vyema msimu kutokana na majeruhi wengi kikosini.
HIGHLIGHTS

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Agosti 29


 

Gallery

Popular Posts

About Us