KINGAZI BLOG: 09/10/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 10 September 2016

Rais Dkt. Magufuli awalilia waliofariki Kagera.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kufuatia vifo vya watu kadhaa vilivyotokea kufuatia tetemeko la ardhi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli
Katika salamu hizo Rais Dkt. Magufuli ameeleza kusikitishwa kwake kufuatia tukio hilo ambapo idadi kubwa ya watu wamepoteza maisha wengi kujeruhiwa na uharibifu wa mali.
Rais Magufuli amesema anaungana na familia ambazo zimepoteza ndugu jamaa na marafiki na anawaombea kwa Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani, Amen.

‘Kupitia kwako Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Mstaafu Mustafa Kijuu na wakuu wa Mikoa ya jirani yakoiliyokubwa na tukio hili natoa pole kwa familia ndugu jamaa na marafiki wote waliopoteza jamaa zao, nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape moyo wa subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu”Amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Dkt Magufuli amewaombea wote walioumia kufuatia tetemeko hilo wapone na kurejea katika hali yao ya kawaida na kuendelea na majukumu ya taifa.
Kwa taarifa ambazo zimethibitishwa kutoka mkoani Kagera watu 11 wamepoteza maisha na wengine 120 wamejeruhiwa.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kagera Augustine Olomi amethibitisha kutokea vifo hivyo na kusema zoezi la uokoaji linaendelea likihusisha taasisi ya Msalaba Mwekudu.

Rais Magufuli Kuwa wa Mwisho Kuhamia Dodoma

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Rais John Magufuli atakuwa wa mwisho kuhamia Dodoma na kupokewa na watumishi wa Serikali.

Rais Magufuli akihutubia Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM Julai 23 mwaka huu, mkoani hapa alitoa tamko la Serikali kuhamia Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa uamuzi ulitolewa mwaka 1973.

Akizungumza Jumatano wiki hii, katika kipindi cha Safari ya Dodoma kilichoandaliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Majaliwa alisema utaratibu wa kuhama umepangwa kutekelezwa kwa awamu sita.

Alisema awamu ya kwanza itaanza mwezi huu hadi Februari mwakani, ikiongozwa naye, mawaziri wote, makatibu wakuu, naibu katibu mkuu na idara angalau moja.

“Awamu ya pili itaanza Machi hadi Agosti, 2017. Katika kipindi hicho makatibu wakuu watapendekeza na kuomba fedha bungeni kwa ajili ya kazi hiyo,” alisema.

Kwa utaratibu wa Bunge, mikutano ya bajeti huanza Aprili hadi Julai ili kujadili na kuidhinisha mapato na matumizi ya Serikali ya mwaka mpya wa fedha.

Majaliwa alisema awamu ya tatu itaanza Septemba hadi Februari, 2018 na zitaendelea nyingine, ya mwisho ikiwa mwaka 2020.

Akizungumzia miundombinu, Majaliwa alisema Dodoma ina barabara za kutosha, nyingi zikiwa za lami na hata zisizo za lami zinapitika vizuri.

Majaliwa alisema kuna barabara ya kuunganisha mikoa mingine kama vile Singida, Morogoro na Iringa, hivyo kuwafanya watu kuingia na kutoka mjini hapa kwa urahisi. Kwa upande wa masoko, alisema yapo makubwa yenye vyakula vya kutosha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu), Jenista Mhagama hivi karibuni alisema ujenzi wa makazi, uzio na ofisi binafsi za waziri mkuu umekamilika.

Mhagama alisema kilichobaki ni kazi ya uboreshaji wa mandhari ya eneo la makazi hayo yaliyoko Mlimwa, mjini hapa na barabara za kuunganisha kati ya makazi hayo na nyingine kubwa.

Alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa

Dodoma, Jordan Rugimbana kuhakikisha mandhari ya eneo hilo yanaboreshwa ikiwa ni pamoja na kupanda maua.

Rugimba pia alipewa jukumu la kusimamia ujenzi wa barabara zinazounganisha makazi hayo na nyingine zilizopo maeneo hayo.

Kifaa cha Kuchemshia Maji Chateketeza Kiwanda, 15 Wafariki Duniua

 WATU 15 wamepoteza maisha nchini Bangladesh baada ya moto mkubwa uliosababishwa na mlipuko wa kifaa cha kuchemsha maji katika kiwanda kimoja.

Zaidi ya watu 70 wamejeruhiwa kwenye tukio hilo lililotokea pembeni mwa Mji Mkuu wa nchi hiyo, Dhaka, na inaarifiwa kwamba huenda idadi ya walioaga dunia ikaongezeka zaidi.

Polisi wanasema kwamba zaidi ya watu 100 walikuwa wakifanya kazi katika kiwanda hicho, na kwamba moto huo ulisambaa kwa kasi katika jengo hilo la ghorofa nne.

Guardiola amzima Mourinho Old Trafford


TIMU ya Manchester City leo imeshinda mabao 2 – 1 dhidi ya Manchester United  katika mchezo mkali uliopigwa Uwanja wa Old Trafford. Mabao yote yalifungwa kipindi cha kwanza, wafungaji kwa upande wa Man City ni De Bruyne aliyetupia dakika ya 15 kisha Iheanacho akaongeza la pili dakika ya 36, bao pekee la wenyeji Man United liliwekwa kimiani na Zlatan Ibrahimovic dakika ya 42.

MANCHESTER UNITED: De Gea, Valencia, Bailly, Blind, Shaw, Pogba, Fellaini, Mkhitaryan (Herrera), Rooney, Lingard (Rashford), Ibrahimovic 
Subs: Mata, Martial, Smalling, Romero, Schneiderlin
Booked: Bailly, Fellaini, Ibrahimovic
Scorer: Ibrahimovic 
MANCHESTER CITY: Bravo, Sagna, Stones, Otamendi, Kolarov, De Bruyne (Zabaleta), Fernandinho, Silva, Sterling (Sane), Iheanacho (Fernando), Nolito 
Subs: Caballero, Jesus Navas, Clichy, Garcia
Booked: Silva
Scorers: De Bruyne, Iheanacho

Kevin De Bruyne (kulia) akishangilia baada ya kufunga bao la kuongoza dhidi ya Manchester Utd leo katika Uwanja wa Old Trafford.

De Bruyne akipiga shuti ambalo ndilo lilizaa bao la kwanza kwa Man City, huku kipa  wa Manchester United, David de Gea (kulia) akijitahidi kutaka kuokoa lakini alishindwa.

Mourinho (kushoto) na  Guardiola wakifuatilia mechi hiyo.

Wachezaji wa Man City wakishangilia.

Ibrahimovic akishangilia baada ya kuifungia Man Utd bao.

Kocha wa Man Utd, Mourinho akitoa maelezo kwa wachezaji wake (hawapo pichani) baada ya mchezaji wake kufanyiwa faulo.

Tetemeko kubwa la Ardhi laikumba mikoa ya Mwanza na Kagera..

Mchana wa  leo Mikoa ya Kanda imekumbwa na tetemeko la ardhi ambapo nyumba kadhaa zimebomoka na inadaiwa kuna vifo kadhaa




Mtangazaji wa Clouds Tv ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Wilaya

Leo Septemba 10, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya 11, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji 1 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa 1 ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika Halmashauri hizo.

Miongoni mwa Wakurugenzi wa Halmashauri walioteuliwa, yumo pia mtangazaji wa kipindi cha Clouds 360 cha Clouds Tv kinachorushwa kila siku kuanzia jumatatu hadi Ijumaa.

Hudson Stanley Kamoga ameteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara.

Hii sio mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kuteua watangazaji kushika nyadhifa mbalimbali kwani alimteua aliyekuwa Mtangazaji wa ITV, Godwin Gondwe kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni.

Wakurugenzi wengine walioteuliwa leo ni pamoja na;-

Mwailwa Smith Pangani – Halmashauri ya Wilaya ya NsimboGodfrey Sanga – Halmashauri ya Wilaya ya MkalamaYusuf Daudi Semuguruka – Halmashauri ya Wilaya ya UlangaBakari Kasinyo Mohamed – Halmashauri ya Wilaya ya NachingweaJuma Ally Mnwele – Halmashauri ya Wilaya ya KibondoButamo Nuru Ndalahwa – Halmashauri ya Wilaya ya MoshiWaziri Mourice – Halmashauri ya Wilaya ya KaratuFatma Omar Latu    – Halmashauri ya Wilaya ya BagamoyoGodwin Emmanuel Kunambi – Manispaa ya DodomaElias R. Ntiruhungwa – Mji wa TarimeMwantumu Dau – Halmashauri ya Wilaya ya BukobaFrank Bahati – Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Rosa Robert wa Navy Kenzo: Nyimbo Zangu Natungia Toilet




 
    
KAMA kawa, kama dawa leo Mpaka Home imemleta kwenu mrembo anayefanya Muziki wa Hip Hop ambaye ni zao la Kundi la Navy Kenzo, Rosa Robert ‘Rosa Ree’.

Mrembo huyo anaishi Mapinga Wilaya ya Bagamoyo. Anaishi na dada yake na shemeji yake. Twende pamoja chini ili uweze kujua mengi zaidi kumhusu yeye anapokuwa nyumbani:



Ni kitu gani hapendi kukifanya na anachokipenda akiwa nyumbani?

“Napenda sana kupika lakini kuna kitu ambacho sikipendi japokuwa nakifanya kwa kuwa ni lazima nikifanye ni kuosha vyombo, bora nipike kuanzia asubuhi mpaka jioni.


Ni kitu gani kinachompa furaha na amani nyumbani?

“Napata sana amani na furaha nikiwa karibu na ndugu zangu kwa sababu wao wananipa sapoti kubwa ya kila kitu kwenye harakati zangu ni watu wanaonitia moyo sana wa kuzidi kusonga mbele na kufanya mambo yangu yaende sawa.

Mlo wake wa kila siku upoje?

“Unaweza kucheka, hivi sasa nipo kwenye diet na pia utashangaa kwa nini nafanya hivyo wakati sina mwili kabisa lakini hii ni sababu ya kutaka kufanya mwili wangu kuwa na afya bora siyo bora afya, hivyo nakula vitu vya kujenga mwili kama matunda na mboga za majani kwangu ndiyo mpango mzima.


Nini anapendelea kukifanya akiwa toilet?

“Huwa napenda kufanya mazoezi ya kuimba, nyimbo zangu nyingi natungia toilet. Ndiyo kuna utulivu mzuri. Ukiwa unaendelea na mambo, mistari inapanda kwelikweli. Ndiyo sehemu pekee ambayo naona kwangu inakuwa ya private zaidi ambayo naweza kufikiri mambo yangu na kuimba nyimbo ninazozifikiria.


Miaka 10 baadaye anafikiria kuwa nani?

“Nitakuwa mwanamuziki mkubwa sana siyo Tanzania pekee mpaka nje ya nchi na ninaamini ndoto hiyo itakamilika kabla hata ya hiyo miaka kwa sababu najikubali sana na nina amini ninachokifanya.


Anapenda wageni wa aina gani, anawaandalia nini?

“Sichagui mgeni mradi tu awe wa nia nzuri na pia ukiniambia unakuja kwangu sifikirii mara mbili najua chakula cha wengi ni pilau hicho ni kitu muhimu sana kwa wageni wangu na ninatumaini kila mtu anapenda chakula hicho.”


UKAWA Watibuana Tena na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson


Mvutano umeibuka kati ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na wasemaji wa kambi ya upinzani walipokuwa wakisoma maoni yao kuhusu miswada iliyowasilishwa bungeni baada ya kusoma utangulizi uliokuwa nje ya hoja.

Katika Bunge la Bajeti lililoisha Juni mwaka huu, upande wa Kambi ya Upinzani Bungeni uliingia kwenye mgogoro na Dk Tulia, hali iliyosababisha wabunge kutoka vyama vinavyounda Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi) kutoka bungeni kila Naibu Spika alipokuwa akiendesha vikao.

Jana, ilikuwa mara ya kwanza tangu wabunge wasusie vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia kukubali kuwapo ndani ya Bunge, hatua iliyotokana na viongozi wa dini kuingilia kati sakata hilo.

Tangu kuanza kwa Mkutano wa Nne wa Bunge la 11, imepitishwa miswada miwili huku wapinzani wakisoma utangulizi wa maoni kueleza jinsi wanavyobanwa kufanya shughuli za siasa.

Hata hivyo, jana ilikuwa ni tofauti baada ya Dk Tulia kuwabana wawasilishaji wa miswada ya Sheria ya Uanzishaji wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, ambao ulisomwa na Dk Godwin Mollel na aliyesoma Muswada wa Uanzishaji Baraza la Watalaaluma wa Kemia ni Ester Matiko.

Katika maoni yao, Matiko na Dk Mollel walieleza jinsi Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanavyowapiga na kuwakamata wananchi wanaojadili masuala ya siasa. Dk Mollel alipinga watu kunyimwa haki ya kutoa maoni, kufanya mikutano ya hadhara na maandamano. “Tupinge unyama unaondelea dhidi ya Watanzania wenzetu,” alisema Dk Mollel.

Hata hivyo, kabla ya kumaliza kile alichokuwa akitaka kusema Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu), Dk Abdallah Posi aliomba mwongozo kwa kutumia kifungu namba 68 (1) akitaka msemaji kujielekeza katika hoja kama kinavyotaka kifungu 86.

Baada ya Dk Tulia kutoa mwongozo wa kutaka kuacha kusoma maneno ya utangulizi huo, Dk Mollel alitii na kuendelea na hoja iliyokuwa mezani. 

Hali ilizidi kuwa mbaya baada ya Matiko kuingia kusoma maoni ya kambi hiyo kuhusu Muswada wa Sheria ya Uanzishwaji wa Baraza la Wanataaluma wa Kemia.

“Watanzania wote wenye mapenzi mematupinge vyombo vya dola vinavyotumika kufanya shughuli za siasa,” alisema Matiko.

Licha ya Dk Possi kuomba mwongozo wa Spika, Matiko aliendelea kusoma maneno ya utangulizi ambayo aliambiwa asiyasome.

Wakati mvutano huo ukiendelea, baadhi ya wabunge wa upinzani walisimama kupinga uamuzi wa Dk Tulia wakitaka wasemaji hao kuendelea kusoma utangulizi.

Hata hivyo, Dk Tulia aliwataka kukaa chini huku akimtaja Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee kwa zaidi ya mara mbili akimsihi kukaa hali aliyokubaliana nayo.

Mwimbaji Linah Amnyakuwa Idriss Sultan Kutoka Kwa Wema Sepetu...Yadaiwa Amelipiza Kisasi

Kipindi cha Nyuma Linah sanga aliingia Bifu zito baada ya Kuibiwa Bwana na Wema Sepetu ambapo alilalamika sana kwenye vyombo vya habari hasa Radioni... Hivi karibuni Linah na Mpenzi wa Wema Sepetu Idriss Sultan wanaonekana kuwa na ukaribu usio wa kawaida kiasa kwamba inasemekati eti ni wapenzi wanapika na kupakuwa kitendo ambacho kinaonyesha ni kama kulipa kisasi kwa Wema....!! Haya Tuache Movie liendeleeee tutawajuza zaidi kinachoendelea.......






UKAWA Watibuana Tena na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson


Mvutano umeibuka kati ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na wasemaji wa kambi ya upinzani walipokuwa wakisoma maoni yao kuhusu miswada iliyowasilishwa bungeni baada ya kusoma utangulizi uliokuwa nje ya hoja.

Katika Bunge la Bajeti lililoisha Juni mwaka huu, upande wa Kambi ya Upinzani Bungeni uliingia kwenye mgogoro na Dk Tulia, hali iliyosababisha wabunge kutoka vyama vinavyounda Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi) kutoka bungeni kila Naibu Spika alipokuwa akiendesha vikao.

Jana, ilikuwa mara ya kwanza tangu wabunge wasusie vikao vinavyoendeshwa na Dk Tulia kukubali kuwapo ndani ya Bunge, hatua iliyotokana na viongozi wa dini kuingilia kati sakata hilo.

Tangu kuanza kwa Mkutano wa Nne wa Bunge la 11, imepitishwa miswada miwili huku wapinzani wakisoma utangulizi wa maoni kueleza jinsi wanavyobanwa kufanya shughuli za siasa.

Hata hivyo, jana ilikuwa ni tofauti baada ya Dk Tulia kuwabana wawasilishaji wa miswada ya Sheria ya Uanzishaji wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, ambao ulisomwa na Dk Godwin Mollel na aliyesoma Muswada wa Uanzishaji Baraza la Watalaaluma wa Kemia ni Ester Matiko.

Katika maoni yao, Matiko na Dk Mollel walieleza jinsi Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanavyowapiga na kuwakamata wananchi wanaojadili masuala ya siasa. Dk Mollel alipinga watu kunyimwa haki ya kutoa maoni, kufanya mikutano ya hadhara na maandamano. “Tupinge unyama unaondelea dhidi ya Watanzania wenzetu,” alisema Dk Mollel.

Hata hivyo, kabla ya kumaliza kile alichokuwa akitaka kusema Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu), Dk Abdallah Posi aliomba mwongozo kwa kutumia kifungu namba 68 (1) akitaka msemaji kujielekeza katika hoja kama kinavyotaka kifungu 86.

Baada ya Dk Tulia kutoa mwongozo wa kutaka kuacha kusoma maneno ya utangulizi huo, Dk Mollel alitii na kuendelea na hoja iliyokuwa mezani. 

Hali ilizidi kuwa mbaya baada ya Matiko kuingia kusoma maoni ya kambi hiyo kuhusu Muswada wa Sheria ya Uanzishwaji wa Baraza la Wanataaluma wa Kemia.

“Watanzania wote wenye mapenzi mematupinge vyombo vya dola vinavyotumika kufanya shughuli za siasa,” alisema Matiko.

Licha ya Dk Possi kuomba mwongozo wa Spika, Matiko aliendelea kusoma maneno ya utangulizi ambayo aliambiwa asiyasome.

Wakati mvutano huo ukiendelea, baadhi ya wabunge wa upinzani walisimama kupinga uamuzi wa Dk Tulia wakitaka wasemaji hao kuendelea kusoma utangulizi.

Hata hivyo, Dk Tulia aliwataka kukaa chini huku akimtaja Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee kwa zaidi ya mara mbili akimsihi kukaa hali aliyokubaliana nayo.

TAZAMA PICHA ZA NUSU ALIZOZIACHIA MARIAH CAREY MTANDAONI


46-year-old singer and mother -of-two, Mariah Carey puts her body on display in sexy new photos...

Vi

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Septemba 10



 

Gallery

Popular Posts

About Us