KINGAZI BLOG: 10/16/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Sunday 16 October 2016

SIMULIZI TAMU INAYOITWA = NILAMBE HUMO HUMO-1

Image result for booty ebony

Nilambe Humo Humo - 1
CHOMBEZO: NILAMBE HUMOHUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SIMU: 0755 697335

SEHEMU YA KWANZA

Kidokezo
…ulikuwa mduara wa Segere kwa lugha isiyo rasmi. Au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa. 
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu
vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda. 
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa! 
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani kwenye kiza. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipowatazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!.
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta, ambalo lilikuwa tayari likinishinikiza nasi tufanye mapenzi! Loh! My God ‘Gobbah…!’ 
Tembeeni muone. 

* * * 
Naweza kusema nilikuwa na bahati mbaya maishani, ndio mwenyewe nilijiona kuwa na sura ya wastani isiyo mbaya sana wala nzuri sana. 
Sura ambayo unaweza kumtongoza msichana huyu akakukatalia na yule akakukubalia! Lakini haikuwa kwangu. Kila niliyemtongoza alinikatalia, Kila niliyemtongoza! 
Hali hii haikuanza leo wala jana, ilianza kitambo toka ningali kinda lisilojua adha wala starehe ya tendo hilo la ndoa. Wakati huo akili za utoto zikinifanya niamini kwamba sikuwa mtaalamu wa kupangilia vyema mashairi yangu wakati nilipotaka kufikisha ujumbe wangu kwa mlengwa.
Nilipoingia primary wewe iite shule ya msingi na tatizo hilo kujirudia tena, sikutilia maanani sana. Nilikuja kuadhirika mwishoni mwa kidato cha pili na mwanzoni mwa kidato cha tatu. 
Nadhani kuathirika kwangu kisaikolojia kulitokana na ukweli kwamba kipindi hicho ndicho kilikuwa kipindi kipevu kwangu, kipindi cha masham sham na matamanio ya hamu. Kipindi cha mifadhaiko na majaribio, kipindi cha kupevuka.
Naam kilikuwa kipindi cha balehe. Kipindi cha kutoka utotoni na kuingia katika utu uzima. Ndugu yangu kipindi hiki kisikie hivyo hivyo, kama mwenzetu ulifanikiwa kukipita salama, hongera yako.
Lakini wale wenzangu na mimi tuliopelekwa na kupelekeshwa na kipindi hicho ambacho kila anayebahatika kupewa uhai na manani lazima akipitie, wanazielewa fika tamu na chungu za kipindi hiki hatari.

Wakati huo mheshimiwa sana kule ikulu alikuwa akinisumbua vilivyo nyakati za usiku muda mfupi kabla ya kulala, kila wakati akitaka kukagua gwaride la heshima. 
Hata hivyo bahati ilikuwa upande wangu mara nyingi usingizi uliponichukua ndoto nyevu ziliniokoa!
Ingawa shida za usiku hazikuwa za kupatiliza, adha nilizokuwa nikizipata mchana katika maeneo mbali mbali kila nilipokuwa nikikutana na mwanamke aliyeumbika vizuri, aliyevaa nguo za kubana sana, aliyevaa kimini na kitopu na hata wale waliovaa robo tatu uchi; hazikuwa na mfano.
Pengine ni hili lililoniingiza katika mkumbo waliopitia vijana wengi. Mkumbo wa kujichua! Potelea mbali kama unalegeza mishipa na kuathiri nguvu za kiume baadae! 
Ndiyo, niliamua kufanya mapenzi na mikono yangu kwa msaada wa sabuni, mafuta au chochote nilichokiona kinafaa au kunirahisishia kazi. Hii ikaendelea kuwa mkombozi pekee kwangu katika masuala ya kupoza makali ya ukware! 
Kumbe ningelifanyaje? hasa ukizingatia ukweli kwamba nilikuwa mwanafunzi nisiye na uwezo wowote kifedha, muoga wa kuwakabili viumbe hawa uzao wa Eva? Hakika hilo lilikuwa suluhisho kwangu.
Sikushauri uwe kama mimi, lakini mwenzako suluhisho hilo lilinifanya nihitimu elimu ya sekondari vizuri salama usalimini. 
Sikupata alama nzuri ambazo zingeniwezesha kuendelea na masomo ya juu ngazi ya A – level, kidato cha tano na sita. Na hili nilitarajia kabisa. Unadhani? Ningewezaje kupata alama nzuri hali nikiona mguu uliojaziajazia chini ya sketi basi hata kama nilikuwa ninasoma na wenzangu ni lazima nitafute mahali nijichue kwanza ndipo mambo yaende sawa?
Wazazi wangu wakaamua kunipeleka Veta kuchukua mafunzo ya ufundi umeme!

Kazi ambayo awali niliona inawastahili wanaume pekee, lakini nilipofika huko matokeo yakawa kinyume! Wanawake na labda niwaite wasichana walikuwa wamefurika isivyo kawaida katika darasa hilo. 
Pongezi kwa wanaharakati wanaopigania usawa wa kijinsia, harakati zao zinazaa matunda ati! Kwa mujibu wa waalimu wa hapo, kipindi cha nyuma ilikuwa aghalabu kukuta wanawake wengi wakijitokeza katika fani kama hizi zilizoonekana kama zina harufu ya uume uume!
Wengi ungewakuta ama katika mafunzo ya ufundi wa ususi, urembaji mapambo, mabatiki, ushonaji nguo, upishi na aina zote zenye mwelekeo huo lakini sasa hali ni tofauti, tena tofauti sana. 
Ni huko nilikokutana na rafiki yangu Akimu Yusuph, huyu alitokea kuwa rafiki wa kweli na mfariji mkuu wa maradhi yangu ambayo sina shaka kwamba sasa unayafahamu fika. 
Halafu ilifika siku moja, siku isiyo na jina!
Siku ambayo hatukuwa na masomo hapo chuoni. Nadhani itapendeza zaidi nikiita siku ya mapumziko. Mchana wa siku hiyo ulinikuta katika grosari moja jirani na chuo chetu pale chang’ombe nikipata kinywaji laini cha baridi. Mimi sio mtumiaji wa vikali na ninaomba Mungu anisaidie nisijaribu kuvigusa, usiulize sababu tafadhali.
Mchana huo ukiendelea kuyoyoma taratibu sambamba na kinywaji changu, mkononi nilikuwa na gazeti la Ijumaa wikienda nikiendelea kupata elimu ya kutakata ya namna ya kuyafikia mafanikio toka kwa Brother Erick Shigongo. 
“Hai Ibra?” Sauti nyembamba na laini ikaniharibia pozi.
Nikageuka taratibu kabla ya kujibu. Ni utaratibu nilio jiwekea toka enzi na enzi ili kuepuka kujibu salamu isiyonihusu na hivyo kumkwaza msalimiaji. Ndiyo! Kuna akina Ibra wangapi jijini?
Macho yangu yakakumbana na tabasamu zuri lililopachikwa kiufundi katika sura murua ya binti huyu mantashau. Hakuwa mgeni kwangu. Hili lilidhihirisha kwamba salamu ile ilikuwa yangu. Nami nikachanua tabasamu bomba kujibu tabasamu lake pamwe na salaam pia. 
“Hai Shamsa! Mambo?” 
“Kama mgambo kasoro kirungu!” 
“Hivi bado hamjamuelewa Karl P tu? Kwanini hukujibu kama mgambo kasoro bunduki na pingu?” 
Tukacheka.
Shamsa Nuhu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wenzangu tuliokuwa tukichukua mafunzo ya umeme pale VETA. Katika muziki Shamsa alikuwa akimpenda sana msanii Karl P, ingawa Karl P mwenyewe hayuko tena kwenye chati siku hizi .
Shamsa pia ni mmoja wa wasichana wachache walio kuwa wakiwapelekesha puta wanaume ndani na nje ya darasa letu. 
Alikuwa na akili za kutosha, hilo lazima nilikiri. Masomoni alikula sahani moja na wale unaoweza kuwaita majiniazi. Kifedha pia alikuwa njema kiasi kile ambacho usingeweza kumrubuni akubaliane na wewe kwa kwa kumringishia vijisenti! Kama hujui vijisenti, usiniulize mimi; muulize Chenge!
Kwa uzuri sijui wengine, lakini kwangu alikuwa na uzuri ulio shinda malaika! Alikuwa na sura nzuri, tabasamu zuri, ‘dimples’ nzuri, shingo ya miraba miraba, umbo zuri, mzigo wa uhakika nyuma yake, usafiri mzuri na hata mwendo wake ulikuwa mzuri. wachilia mbali sauti, roho na vitendo vyake. Alikuwa mzuri hasa, mzuri fika. 
Alikuwa mmoja kati ya wengi waliowahi kuumong’onyoa moyo wangu! Unadhani? Sio yeye tu, wako wengi waliowahi kupata hifadhi moyoni mwangu, lakini mimi nilipotaka kuingia katika mioyo yao wakagoma kunipa hifadhi!
Nilihofia kumueleza nilivyojisikia juu yake kutokana na ile hofu ya kawaida, hofu ya kukataliwa kwamba kama watu wanaoonekana; wenye akili zao darasani, fedha zao Benki na heshima zao katika jamii wamejaribu wameshindwa mimi mtoto wa msaka nyoka kama sio msaka tonge nitaweza kweli? 
Niliendelea kuumia kwa muda mrefu mpaka siku fulani nilipopata ujasiri wa aina yake na kumkabili. Hii ilikuwa ni baada ya kujishauri sana na kuamua kwamba mwanaume anakufa siku moja.

Aidha ilikuwa ni baada ya kujiuliza ni mara ngapi nimetongoza na kufaulu, nikagundua ni mara 0.05! Nikakubali kuishi siku moja kama simba kuliko kuishi siku mia moja kama inzi! Kwamba hata akinikatalia atakuwa tayari anajua ninampenda! Itatosha . 
Nikamvaa!
Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo! 
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda! 
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma. 
Ghafla akageuka na kunitazama. 
Macho yetu yakagongana. 

***NILAMBE HUMO HUMO INAANZIA HAPA……Na itaendelea

HAYA HAPA MAJINA YAWALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU ST.AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA-SAUT 2016/2017- FIRST AND SECOND ROUND











SAUT


KUONA MAJINA 


<<BONYEZA HAPAYOTE >>

MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA ( IAA ) BARCHELOR DEGREE 2016/17


Kuona majina ya waliochaguliwa kujiunga na chuo cha Uhasibu Arusha ( INSTITUTE OF ACCOUNTANCY ARUSHA - IAA) Bofya hapa chini.... 

                       BOFYA HAPA KUONA MAJINA

HAYA HAPA MAJINA YA DIPLOMA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU UDOM 2016/17 BATCH 1

Logo

KUONA MAJINA

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU MARIAN UNIVERSITY(THIRD ROUND) 2016/2017

KUONA MAJINA YOTE 

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAJI UBUNGO WALIOPATA MKOPO 2016/2017

Names of WTF Loan Beneficiaries 2016-17

ATTENTION TO THE WTF LOAN APPLICANTS
The Board of The Registered Trustees of Water Technicians Fund (RTWTF) hereby wishes to inform all loan applicants that by applying and meeting the loan allocation criteria, eighty eight (88) applicants have qualified to be beneficiaries of the loan
for the academic year 2016/2017. The Board likewise disqualified some of the applicants for not adhering to the instructions laid in the form as well as not putting either valid certificates or the required attachments. The board went further to verify the information provided by applicants.The list of successful applicants can be viewed on this website underPublications.

KUONA MAJINA HAYO 

MAGAZETI YA TANZANIA YALICHOANDIKA LEO JUMAPILI YA TAREHE 16 OCTOBA





BODI YA MIKOPO YAPITISHA WANAFUNZI 7, 904 KUPATA MKOPO KWA AWAMU YA KWANZA.


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetangaza awamu ya kwanza ya majina ya wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu nchini watakaopewa mkopo kugharimia masomo yao.

 

Idadi ya wanafunzi ambao tayari wamepitishwa kupata mkopo ni 7,904, hata hiyo imeelezwa kiwango hicho kitaendelea kubadilika kwa kuwa mchakato unaendelea.

Taarifa iliyotolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Stella Manyanya ilibainisha kuwa bodi imekamilisha uchambuzi wa majina ya waombaji ambao wana sifa zinazotakiwa na majina ya wanufaika wapya ambayo yameanza kutangazwa kupitia tovuti ya bodi hiyo.

 “Kwa kuzingatia mpango mkakati, pia mwongozo wa utoaji mikopo kwa mwaka 2016/17, Serikali imetoa vigezo vitakavyozingatiwa katika utoaji mikopo,”alisema Manyanya.

Alitaja vigezo vilivyotumika kuwa ni pamoja na vipaumbele vya kitaifa vinayoendana na mpango wa maendeleo wa Taifa wa miaka mitano, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na mafunzo ambayo yatazalisha wataalamu wanaokidhi mahitaji ya kitaifa katika fani za kipaumbele.

Manyanya alizitaja fani zilizopewa vipaumbele kuwa ni sayansi za tiba na afya, ualimu wa sayansi na hisabati, uhandisi wa viwanda, kilimo, mifugo, mafuta na gesi asilia, sayansi asilia na mabadiliko ya tabianchi, sayansi za ardhi, usanifu majengo na miundombinu.

Katika taarifa yake, Manyanya alisema pia mchakato wa kuwapata wenye sifa za kukopa uliangalia uhitaji wa waombaji, hususan wenye mahitaji maalumu kama walemavu na yatima, ufaulu wa waombaji katika maeneo ya vipaumbele na umahiri. 

“Kuanzia mwaka huu wa masomo, wanufaika wote wa mikopo (wapya na wanaoendelea na masomo) watakopeshwa kulingana na uwezo wao katika vipengele vyote vya mikopo,”alisema.

Akizungumzia mchakato huo, mkurugenzi mtendaji wa bodi hiyo, Abdul Badru alisema unaendelea kufanywa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na timu ya bodi imejigawa katika vikundi ili kuhakikisha mipango inakwenda jinsi inavyotakiwa.

 “Timu ipo kazini na inafanya kazi yake kwa umakini. Kwa sasa majina ya waliochaguliwa kutokana na vigezo yamewekwa, lakini ni wahusika wenyewe au walezi na wazazi ndiyo wanaweza kuyaona kupitia namba zao za usajili wa kidato cha nne. Lakini siku chache zijazo tunaweza kuwataja wakaonekana kwa kila anayehitaji kuyaona,” alisema Badru.

==>Bofya    <<HAPA>>   Kuona  Majina  Wa  Waliopata  Mkopo  Awamu  ya  Kwanza

HAYA HAPA MAELEKEZO YA JINSI YA KUHAMA CHUO ULICHOPANGIWA NA TCU NA KUHAMIA KINGINE MWAKA 2016/17

Official VIDEO | Jah Prayzah - Mdhara Vachauya | Watch/Download

 

Gallery

Popular Posts

About Us