KINGAZI BLOG: 11/25/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 25 November 2016

Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso) Watoa Tamko Kali Kwa Bodi ya Mikopo

Dar es Salaam. Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso) imevikumbusha vyuo vikuu nchini mambo wanayotakiwa kufanya ikiwamo kuelewa mikataba na nafasi ya wanafunzi katika masuala ya malipo ya ada vyuoni mwao.

Katika waraka wake uliotolewa kwa vyombo vya habari, Tahliso walilaani vikali kitendo cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kutangaza kuwazuia wanafunzi kufanya mahafali kwa kisingizio cha ada.

“Tahliso tumepokea malalamiko yenye kusikitisha kutoka kwa wanafunzi wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) - MWANZA ambao wamehitimu katika mwaka wa masomo 2015/2016” amesema  Stanslaus Kadugalize, Mwenyekiti wa Tahliso

Waraka huo umesema Mkataba wa malipo ya ada ni kati ya vyuo hivyo na HESLB na kuwa zipo taratibu zinazotumika kulipana ada hizo kati ya vyuo na Serikali kupitia HESLB;

“Wanafunzi hawajawahi kushiriki katika kupanga ada hizo, kufuatilia malipo ya ada hizo wala kutafuta fedha za kulipa ada hizo.” umesema waraka huo na kuongeza:

“Kwa sababu hizo, TAHLISO tunapinga vikali hatua hiyo iliyochukuliwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino na kuwataka wakuu wa taasisi za elimu ya juu nchini kutozuia wanafunzi kuhitimu masomo yao.”

Katika waraka huo Tahliso ilizitaka taasisi za elimu ya juu ambazo zinadai ada kutoka HESLB, kufuata utaratibu uliopo ambao umezoeleka wa kuidai HESLB na sio kuwaadhibu wanafunzi wahitimu.


UDAKU SPECIAL BLOG

PICHAZ++HUYU NDIO MWANAUME ALIYEKUWA AKIYEJIGEUZA HUKU AKIJIFANYA MWAKAMKE NA KUTAPELI WATU

Mwanaume mmoja nchini Uganda aliyefahamika kwa jina la Ivan Bebeto amekamatwa na Polisi akidaiwa kuwa amekuwa akijifanya yeye ni mwanamke na kuwatapeli wanaume.

Mwanaume huyo anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Katwe jijini Kampala akidaiwa kuwa hujifanya mwanamke ambapo huvalia mavazi ya kike na kujiweka kama mwanamke kisha kuwatapeli wanaume. Taarifa kutoka nchini humo zimeeleza kuwa mtuhuiwa huyo amekuwa akifanya ujanja huo kwa muda mrefu sasa hasa katika miji ya Nairobi, Kampala na Bujumbura.


Akiwa katika muonekano wa kike, mtuhumiwa huyo hujiita Queen.

Aidha, siku ya tukio hilo alikamatwa baada ya mwanamume mmoja aliyekuwa tayari amekubaliana nae kuanza kumtilia mashaka baada ya Bebeto kukataa kwenda nyumba ya kulala wageni kama walivyokuwa wamekubaliana kabla ya kupewa malipo.


Baada ya hali hiyo, mwanaume huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja alipiga simu Polisi na ndio Bebeto akakamatwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Novemba 25




 

Gallery

Popular Posts

About Us