KINGAZI BLOG: 11/07/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 7 November 2016

(18+)JAMAAANI!!! HEBU CHEKI PICHA HIZI ZA KUSTAAJABISHZITAKUACHA MDOMO WAZI



Image result for BIG BOOTY EBONY

HIZI NI MOJA YA SANAMU ZA AJABU ZILIZO CHONGWA NA KUWEKWA KATIKA MOJA YA MTAA 

HUKO UGHAIBUNI,  

Image result for BIG BOOTY EBONY

HEBU TOA COMMENT YAKO HAPO CHINI


CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO ====8

CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA nane
“Mimi ni miongoni mwa watu wachache sana wasiopenda kuwakwaza wenzao hasa wewe! Kuendelea kunilaumu kana kwamba nimeua bila kunieleza nilililolifanya, hunitendei haki Shamsa! Unaniweka katika kimuhemuhe ambacho kinanifanya nishindwe kujua nastahili kuwemo katika fungu gani kati ya wastaarabu na washenzi. Tafadhali niambie, niambie tu usihofu!’’
Shamsa akashusha pumzi na kuzivuta tena akauliza
“Kwa hiyo hujafanya kitu?’’
‘’Kitu gani? kwa kadiri ninavyokumbuka na kufahamu, sijafanya lolote la kumchukiza mtu yeyote! Na kama nilivyokwambia sipendi kumkwaza mtu!’’
‘’Kweli!?’’
‘’Kabisa!’’
‘’Sasa kule Chuoni ulikuwa unalia nini?”
Akili ikazibuka.
Macho yakazibuka pia na fahamu kufunguka. Masikio, moyo na hata vinyweleo vya mwili ambavyo wakati huu vilikuwa vikikiruhusu kijasho chembamba kupenya na kuteleza juu ya paji la uso wangu, juu ya mashavu, juu ya mikono, juu ya kila mahali, sasa nikaelewa! Kwamba Shamsa alikuwa akizungumzia kufeli kwangu.
‘’Machozi yakafurika upya katika macho yangu. Shamsa alikuwa amenitonesha donda. Amegusa mahali ambapo sikutaka paguswe. Halafu kilio kidogo kikanianguka. Nilijitahidi kukizuia mpaka nikafaulu.
‘’Mapenzi Shamsa!” Nikasema huku nikipenga kamasi na kufuta machozi
‘’Mapenzi?!” Shamsa hakuamini!.
“Yeah, Mapenzi! Naweza kusema ni mapenzi kwa kila hali ndiyo yaliyonifanya nifeli. Ukweli huu huniumiza zaidi. Huniumiza kwa vile ni ukweli unaoashiria upumbavu ulikithiri nilionao. Ni upumbavu tu maana ujinga unatibika, upumbavu hautibiki!”
‘’Bado sijakuelewa!’’ Alikuwa Shamsa kwa upole kabisa.
‘’Ni mapenzi Shamsa, nilikupenda sana mfano wa maua, ninakupenda hata sasa na nitaendelea kukupenda daima!’’
‘’Kunipenda huko ndio kukakufanya ufeli?’’
Nikatikisa kichwa juu na chini kukubali.
‘’Si kweli!’’ Akasema kwa sauti thabiti nae akitikisa kichwa kushoto na kulia kukataa ‘’Si kweli hata kidogo!‘’ Akaongezea na kuendelea ‘’Nahisi unajaribu kunificha kama sio kunichezea shere. Naomba uniambie ukweli Ibra, ili niangalie namna ya kukusaidia tafadhali!’’
Sikujua nimwambie ukweli upi
‘’Mbona hata mie ninakupenda sana na nimefaulu vizuri tu? Mbona nilikuwa nikikufikiria na kutamani kuwa nawe mahala kama hapa nikila raha na kustarehe na wewe? Mimi nina nini niweze na wewe una nini ushindwe? Hapana niambie ukweli Ibra’’
Akatua. Furaha na bashasha vikiuvaa moyo akili na mwili wangu kwa zamu. Shamsa ananipenda! Ulikuwa ukweli ulionitoa machozi ya furaha, machozi ya upendo! Upendo wa dhati. Upendo uliotukuka!
‘’Shamsa’’ Nikaita nisiamini masikio yangu, “Ni kweli unanipenda?!’’
“Ni kweli Ibra, nakupenda sana! Nakupenda mno! Nakupenda kuliko unavyofikiria. VETA nzima watu wa Compass wanajua jinsi nilivyokufa na kuoza juu yako, Najua hata wewe unanipenda tu ila hujiamini na pengine unanipenda kupita kiasi, kiasi umekuwa kama unaniogopa uongo?’’
Akasuta! Ulikuwa ukweli, ukweli halisi. Ukweli Original kama alitegemea kunisuta kule kungenifanya nione haya kama sio aibu, alikosea! Badala yake nilitahayari na kuinamisha uso kwa fedheha, nilipoinua bado alikuwa akinitazama. Nikanong’ona.
“I love you Shamsa!’’
‘’I love you too Ibra!’’
Moyo wangu ukachanua kwa raha, akili ikapigwa dafrao na furaha huku mate ya uchu kama sio utamu yakijaa mdomoni. Nikamsogelea akanisogelea! Tukakutana katikati na kukumbatiana kwa nguvu na kudumu katika hali hiyo kwa muda.
Hatimaye! Nikawaza kwa furaha nikingali nimekishikilia kifua chake Hatimaye Shamsa ameanguka mikononi mwangu, Ananipenda! Kwa mara ya kwanza nimepata hifadhi katika moyo wa mwanamke!’
Ilikuwa ajabu na kweli.
Tulipoachiana matendo halisi ya mapenzi yalifuatia. Tulilishana, tukacheza na kuogelea pamoja. Tulipotosheka tukarudi mchangani tena. Shamsa akaniita kwa upendo uliotukuka. Sauti yake ilikuwa tamu vibaya sana
“Ibra mpenzi?”
‘’Naam!’’
‘’Bado hujanishibisha dear!’’
‘’Lakini biskuti, Chocolate na Ice cream hazishibishi!’’
Akatabasamu, vishimo vikatokea hapa na pale katika mashavu yake na kidevuni.
“Unanielewa vizuri sana Ibra! Ni kuhusu kufelishwa na mapenzi! Hebu niambie ukweli!’’
‘’Ni ukweli mpenzi!’’
Nikamwambia, kabla sijaanza kumsimulia safari ya maisha yangu toka Shule ya Msingi, Sekondary, hadi pale VETA. Nikamwambia jinsi nilivyokuwa nampenda na namna nilivyoshindwa kumkabili licha ya yeye kunionyesha dalili za waziwazi.
Nikamwambia pia namna nilivyopateua uwanja wa fisi kama mahala mbadala, ushauri niliopewa na Akimu baadae ambapo nilijikuta nikianguka tena katika ngoma za kizaramo. Nikashindwa kujisomea, kufuatilia masomo na kuendekeza ngono, mpaka ninamaliza kusimulia, Shamsa alikuwa bado ana hamu ya kunisikiliza.
“Huo ndio mkasa wangu Shamsa! Unadhani kitu gani naweza kusema kimenifelisha kama sio mapenzi?”
“Duh! Pole sana Ibra una bonge la mkasa! Mkasa ambao umeusisimua moyo wangu katika namna inayonifanya nikuogope! Nikuulize swali jingine?”
‘’Uliza tu laaziz!”
‘’Mbona siku ile nilipokuuliza kama unanipenda ulikataa kata kata?”
Nikatabasamu, “Mbona hilo umeshalijibu katika maelezo yako? Shamsa mpenzi nilikuwa sijiamini, nilikuwa nakuogopa! Akili zako, uzuri na uwezo wako kifedha vilinifanya niufyate, nikawa nakufa kiofisa tai shingoni!”
Akacheka. Nami nikacheka. Ikawa raha juu ya raha
‘’Siku nyingine usiogope ukubwa wa samaki! Uliza bei!’’ Akasema kati kati ya kicheko, tukacheka zaidi.
‘’Lakini kufeli kwako hakutokani na mapenzi! Naweza kusema hivyo!’’ akaniambia baadae kwa uhakika kabisa.
‘’Kumbe kunatokana na nini na au nikuiteje?”
‘’Kunatokana na tamaa kali ya ngono na niite tu umalaya, kwa sababu hata ngoma unazozizingizia huzifuati zenyewe! Hii ni kwa vile hujui kucheza kabisa, unayo ifuata ni ile mijimama na kile kipindi muhimu cha kuzima ngoma uongo?”
Nikashindwa kumjibu.
“Mapenzi ya kweli ni zaidi ya ngono Ibra! Unadhani ni kwanini mimi imeniuma wewe kufeli? Kwanini nilikuja kukufariji katika bweni lenu? kwanini nimekuleta huku?! Sababu ni moja tu Ibra wangu. MAPENZI! Ni mapenzi ya dhati niliyo nayo kwako, hilo tu!” Akahitimisha.
Alikuwa sahihi.Image result for BIG BOOTY EBONY
Tuliendelea kufurahi na kula maisha pale ufukweni hata msiba wote wa kufeli ukaondoka. Nilichogundua tu ni kuwa Shamsa alikuwa mwangalifu sana wakati huu. Hakujiachia sana kama alivyokuwa akijiachia wakati ule kabla sijampa full story yangu.
Jioni tuliondoka na kuelekea mabwenini.
Siku ya pili yake tulikuwa kwenye hoteli moja ya kitalii huko baada ya maongezi yetu ya kawaida ndipo alipo nitwanga swali..
‘’Sasa Ibra Chuo ndio tumemaliza, baada ya kutunukiwa shahada zetu yatupasa kuondoka. Mwenzangu una mipango gani? Mie mwenzio Mzee ameniunganishia Tanesco na mwakani nitaajiriwa!’’
Swali zito. Nikachoka kabisa, dakika zikayoyoma pasipo kujibu
“Sikiliza Ibra, kufeli masomo sio kufeli maisha. Kwa hiyo usifikirie sana kuhusu hilo, mimi nina ushauri mzuri kwako!’’ Akatua na kunitazama.
‘’Enhe upi?’’
‘’Kwanza nataka mimi na wewe tuoane unasemaje?”
Sura yangu ikachanua mithili ya maua katika jua la asubuhi. Nikamwambia, “Sina kipingamizi Shamsa nakupenda mno!”
Naye akatabasamu kufuatia kauli yangu hii. Akasema.
‘’Basi kama hivyo ndivyo, huna budi kujifunza udereva haraka sana, ili nimwambie mzee akuajiri katika kampuni yake. Nitamshauri akulipe mshahara mzuri sana unaonaje?”
‘’Nitashukuru kupita kiasi!” Nikasema haraka nikiwaza hata kama Lady Jay dee ataniita mwanaume kama binti na Bushoke kuniita Mume bwege shauri yao! Nitafanyaje hali nimesha ulowanya?” Nikakubali.
Lakini kabla haya hayajafanyika inakubidi uanze taratibu za uchumba na kwa hili hatuna budi kwenda kupima afya zetu kwanza ili ulete barua ya posa wakati huo huo ukianza Driving School! Sawa mpenzi?!”Image result for BIG BOOTY EBONY
***HE MAMBO YA KUPIMA TENAAA…….IBRA ANALOOOO!!!!

WIZARA YA AFYA INATANGAZA NAFASI ZA KUSOMESHA/UFADHILI WA WANAFUNZI WA AFYA WALIOCHAGULIWA CHETI NA DIPLOMA 2016/2017

Image result for serikali ya tanzania 

KUSOMA TANGAZO HILO 

Jeshi la Canada lachunguza kelele za ajabu kutoka bahari ya Arctic


Kelele hizo ziliripotiwa na watu wa eneo hilo kwamba zimewatisha wanyama na kuwafanya wakimbie mbali katika kipindi cha miezi michache iliyopita.

Jeshi la Canada limechunguza kelele za ajabu zenye mlio mkali zinazotoka kwenye sakafu ya bahari katika eneo lisiloweza kufikiwa kwa urahisi la kanda ya Arctic, maafisa wameiambia BBC
Kelele hizo za ajabu ziliripotiwa na watu wa eneo hilo kwamba zimewatisha wanyama na kuwafanya wakimbie mbali katika kipindi cha miezi michache iliyopita.

Ndege ya kijeshi imefanya msako wa aina mbali mbali wa kunasa sauti hizo, wamesema maafisa siku ya Ijumaa.

Hata hivyo jeshi hilo la Canada limesema hadi sasa haliwezi kuelezea sababu ya "sauti hizo za ajabu".

" Mhudumu wa ndege hiyo amesema hawakuweza kubaini kitu chochote cha ajabu kwenye uso wa bahari ama chini ya uso wa bahari ," imesema taarifa ya jeshi iliyotolewa kwa BBC.

" Kile ambacho alikiona ni makundi mawili ya nyangumi na sili wa bahari wenye pembe sita katika eneo lililochunguzwa''

Msemaji wizara ya usalama wa taifa mjini Ottawa amesema kuwa sababu ya kelele hizo - amazo wakazi wanasema zinaweza kusikika hata kupitia kuta za maboti zimesalia kuwa vigumu kutambuliwa.

Eneo ambalo llimekumbwa na kelele za ajabu

Sauti hizo ambazo zimekuwa zikisika katika kipindi chote cha majira ya joto katika maeneo ya baridi, mbunge Paul Quassa ameiambia CBC, yapata kilomita 120 kaskazini-magharibi mwa kijiji kidogo cha Igloolik.

Eneo hilo ni njia ya vijito vya maji katika Nunavut, eneo ambalo ni makazi mapya , makubwa na yenye kukaliwa na idadi ndogo ya watu nchini Canada, karibu na Greenland.

" Ni moja ya maeneo maarufu zaidi kwa shughuli za uwindaji nyakati za majira ya joto na baridi kwasababu ni eneo pana zaidi la maji lililozingirwa na barafu ambayo ina wanyama wengi wa baharini ," Amesema Bwana Quassa.

" Na wakati huu, majira haya ya joto, kulikuwa hakuna mnyama yoyote. Na hili likawa suala la kushangaza."

Maelezo mbali mbali kuhusu sauti hizo za kushangaza yamekuwa yakiwasilishwa katika vyombo vya habari nchini Canada.

TB Joshua atabiri nani kuwa Rais wa Marekani



Muhubiri maarufu wa vipindi vya Televisheni nchini Nigeria TB Joshua amesema ametabiri " kwamba Hillary Clinton atamshinda Donald Trump" katika uchaguzi wa urais wenye ushindani mkali tarehe 8 Novemba mwaka huu.

Katika ujumbe alioutuma kwenye ukurasa wake wa Facebook TB Joshua amesema kuwa Bi Clinton atashinda kwa ushindi mdogo, lakini atakabiliwa na changamoto nyingini - likiwemo jaribio la kupiga kwa kura ya kutokuwa na imani dhidi yake.

"boti ya rais mpya itakuwa imefungwa," aliongeza.

TB Joshua ni mmoja wa viongozi wa kidini wenye ushawishi na utata barani Afrika, huku wengi wa wafuasi wake wakiamini kuwa "utabiri " wake ni wa uhakika.

DIAMOND PLATNUMZ ASHINDA TUZO TATU KWA 'MKUPUO' AFRIMMA

Diamond Platnumz ameibuka na ushindi wa nguvu kwenye tuzo za Afrima 2016 zilizotolewa Jumapili hii jijini Lagos, Nigeria. Muimbaji huyo ameshinda tuzo tatu, Song of The Year – Utanipenda, Best Artist/Duo/Song Of The Year Utanipenda na Best Male Artist in Eastern Africa.

Pamoja na ushindi huo, Diamond pia alitumbuiza wimbo alioimba na Papa Wemba, msanii aliyetunukiwa tuzo ya heshima.

Wasanii wengine waliotumbuiza ni pamoja na Patoranking, P-Square, Falz, Eddy Kenzo, Avril, Simi, Darey, Phyno, Seyi Shay na wengine.

Chini ni orodha ya washindi kwenye tuzo hizo pamoja na picha za ndani ya ukumbi na red carpet:

Artist of the Year 
Wizkid

Song of The Year
Utanipenda – Diamond

Album of the Year
Ahmed Soultan

Revelation of the year
Falz

Video of the Year
Dogo Yaro – Vvip

Best African Collaboration
Eddy Kenzo ft Niniola – Mbilo Mbilo (Remix)

Best African Group

VVip

Best African Jazz

Jimmy Dludlu

Best Artist/Duo/Song Of The Year 
Diamond – Utanipenda

Best Artist/Duo/Group in African Rock
Mvula

Best Artist/Duo/Group African Ragga & Dancehall
Patoranking

Best Artist/Duo/Group African RnB
Henok and Mehari Brothers

Best Artist/Duo/Group African Hiphop
Stanley Enow

Favourites Award
Phyno

Song writer of the year

Unique Muziki – Uganda

Most Promising Artiste
AmineAub

Artiste/Dou/GroupBand in African Contemporary

Flavour

Best female Artiste in Inspirational music
Naomi Achu

Best Male Artiste Western Africa
Flavour

Best female artiste Western Africa
Aramide

Best male artiste Northern Africa
Dj Van

Best male artiste S/Africa

BlackCoffee

Best female artiste S/Africa

Bruna Tatiana

Best Male Artiste Eastern Africa
Diamond Platnumz

Best Female Eastern Africa

Cindy Sanyu

Taarifa Rasmi: Aliyekuwa Spika wa Bunge Samwel Sitta Afariki Dunia

Aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo wakati akipatiwa matibabu nchini Ujerumani.

Kiongozi huyo inadaiwa alifikwa na mauti saa 7:30 kwa muda wa nchini Ujerumani alikokuwa akitibiwa.

Rais Magufuli amtumia Spika wa Bunge salama za rambirambi kufuatia kifo cha Spika Mstaafu Mhe. Samwel Sitta.




Habari kuu kwenye Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Novemba 7

























 

Gallery

Popular Posts

About Us