KINGAZI BLOG: 02/15/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 15 February 2017

Ridhiwani Kikwete atoa kauli hii kuhusu sakata la dawa za kulevya

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete, amefunguka kuhusu sakata la dawa za kulevya na kuipongeza serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa kuanzisha vita hiyo na kutaka wahusika wachukuliwe hatua.

Kikwete amefunguka hayo leo katika kipindi cha East Africa Breakfast cha EA Radio, kinachoruka kila siku saa 11:00 alfajiri hadi saa 3:00 asubuhi.

Ametumia nafasi hiyo kuishauri serikali kuifikisha mwisho vita hiyo, ili kulimaliza kabisa tatizo hilo kwa kuwa limepoteza vijana wengi wenye uwezo mkubwa na mchango katika taifa, huku akitolea mfano uwezo wa msanii wa Bongo Fleva, Langa ambaye kwa sasa ni marehemu ikidaiwa kuwa alipoteza maisha kutokana na dawa hizo, pamoja na shida alizokuwa akizipata msanii Ray C, za kutafuta dawa hizo hata usiku wa manane.

Ameitaka mamlaka mpya wa dawa za kulevya kuwachunguza watu 97 ambao majina yake yamekabidhiwa hivi karibuni na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, na yeyote atakayethibitika kuhusika, achukuliwe hatua, huku akionesha imani kubwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Dkt Rogers William Sianga.

Alichokipost Diamond Baada ya Kukamatwa na Polisi.

Eric Omondi airudia muvi ya Adam na Eva wakiwa kwenye bustani ya Eden.


DOWNLOAD
Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi amekuwa na utundu wa  kuzirudia na kuziigiza movie na nyimbo za mastaa mbalimbali ambapo wakati huu ameirudia sehemu ya movie ya Adam na Eva wakiwa kwenye bustani ya Eden.
DOWNLOAD

AGNES MASOGANGE NAYE AKAMATWA NA POLISI AKIHUSISHWA NA SAKATA LA DAWA ZA KULEVYA.

Image result for masogange agnes

Habari zilizoenea ni kwamba maarufu kwa sababu ya Umbo lake , anayefahamika kaama Agness Masogange tayari amekamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu madawa ya kulevya na tayari yupo kituo kikuu cha polisi ya Central kwa mahojiano ambayo yamedumu kwa saa 10 na bado akishikiliwa kwa uchunguzi na polisi.

Ikimbukwe kuwa Mrembo huyo alishawahi kukamatwa katika uwanja wa ndege wa Oliver tambo South Afrika kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya alizokutwa nazo kwenye mizigo aliyokuwa nayo na yeye kujitetea kuwa yeye hajui lolote ila huo ni mzigo aliyoagizwa na mtu asiyemfahamu kwa jina ila anamfahamu kwa  Sura. 

Kukamatwa kwake kunatokana  kampeni nzito inayoongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda akishirikiana na Jeshi la polisi kutokomeza dawa za kulevya pamoja na biashara hiyo kwa ujumla hapa Tanzania

Hivi ndivyo makalio ya kichina yanavyotengenezwa

DOWNLOAD

(DOWNLOAD)YAMOTO BAND__ KICHECHE (NEW OFFICIAL SONG)



Image result for YAMOTO BAND

Ngoma mpya kutoka kwa yamoto band baada ya kukaa kimya kwa muda.

 

Gallery

Popular Posts

About Us