KINGAZI BLOG: 05/08/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 8 May 2017

SEHEMU YA KWANZA MPAKA YA MWISHO YA HADITHI TAMU YA --NILAMBE HUMOHUMO (sehemu 1- 9)

Image result for nilambe humo humo sehemu ya nne

Nilambe Humo Humo - 1
CHOMBEZO: NILAMBE HUMOHUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SIMU: 0755 697335 
SEHEMU YA KWANZA 
Kidokezo
…ulikuwa mduara wa Segere kwa lugha isiyo rasmi. Au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa.
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu
vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda.
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa!
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani kwenye kiza. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipowatazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!.
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta, ambalo lilikuwa tayari likinishinikiza nasi tufanye mapenzi! Loh! My God ‘Gobbah…!’
Tembeeni muone.  
* * *
Naweza kusema nilikuwa na bahati mbaya maishani, ndio mwenyewe nilijiona kuwa na sura ya wastani isiyo mbaya sana wala nzuri sana.
Sura ambayo unaweza kumtongoza msichana huyu akakukatalia na yule akakukubalia! Lakini haikuwa kwangu. Kila niliyemtongoza alinikatalia, Kila niliyemtongoza!
Hali hii haikuanza leo wala jana, ilianza kitambo toka ningali kinda lisilojua adha wala starehe ya tendo hilo la ndoa. Wakati huo akili za utoto zikinifanya niamini kwamba sikuwa mtaalamu wa kupangilia vyema mashairi yangu wakati nilipotaka kufikisha ujumbe wangu kwa mlengwa.
Nilipoingia primary wewe iite shule ya msingi na tatizo hilo kujirudia tena, sikutilia maanani sana. Nilikuja kuadhirika mwishoni mwa kidato cha pili na mwanzoni mwa kidato cha tatu.
Nadhani kuathirika kwangu kisaikolojia kulitokana na ukweli kwamba kipindi hicho ndicho kilikuwa kipindi kipevu kwangu, kipindi cha masham sham na matamanio ya hamu. Kipindi cha mifadhaiko na majaribio, kipindi cha kupevuka.
Naam kilikuwa kipindi cha balehe. Kipindi cha kutoka utotoni na kuingia katika utu uzima. Ndugu yangu kipindi hiki kisikie hivyo hivyo, kama mwenzetu ulifanikiwa kukipita salama, hongera yako.
Lakini wale wenzangu na mimi tuliopelekwa na kupelekeshwa na kipindi hicho ambacho kila anayebahatika kupewa uhai na manani lazima akipitie, wanazielewa fika tamu na chungu za kipindi hiki hatari. 
Wakati huo mheshimiwa sana kule ikulu alikuwa akinisumbua vilivyo nyakati za usiku muda mfupi kabla ya kulala, kila wakati akitaka kukagua gwaride la heshima.
Hata hivyo bahati ilikuwa upande wangu mara nyingi usingizi uliponichukua ndoto nyevu ziliniokoa!
Ingawa shida za usiku hazikuwa za kupatiliza, adha nilizokuwa nikizipata mchana katika maeneo mbali mbali kila nilipokuwa nikikutana na mwanamke aliyeumbika vizuri, aliyevaa nguo za kubana sana, aliyevaa kimini na kitopu na hata wale waliovaa robo tatu uchi; hazikuwa na mfano.
Pengine ni hili lililoniingiza katika mkumbo waliopitia vijana wengi. Mkumbo wa kujichua! Potelea mbali kama unalegeza mishipa na kuathiri nguvu za kiume baadae!
Ndiyo, niliamua kufanya mapenzi na mikono yangu kwa msaada wa sabuni, mafuta au chochote nilichokiona kinafaa au kunirahisishia kazi. Hii ikaendelea kuwa mkombozi pekee kwangu katika masuala ya kupoza makali ya ukware!
Kumbe ningelifanyaje? hasa ukizingatia ukweli kwamba nilikuwa mwanafunzi nisiye na uwezo wowote kifedha, muoga wa kuwakabili viumbe hawa uzao wa Eva? Hakika hilo lilikuwa suluhisho kwangu.
Sikushauri uwe kama mimi, lakini mwenzako suluhisho hilo lilinifanya nihitimu elimu ya sekondari vizuri salama usalimini.
Sikupata alama nzuri ambazo zingeniwezesha kuendelea na masomo ya juu ngazi ya A – level, kidato cha tano na sita. Na hili nilitarajia kabisa. Unadhani? Ningewezaje kupata alama nzuri hali nikiona mguu uliojaziajazia chini ya sketi basi hata kama nilikuwa ninasoma na wenzangu ni lazima nitafute mahali nijichue kwanza ndipo mambo yaende sawa?
Wazazi wangu wakaamua kunipeleka Veta kuchukua mafunzo ya ufundi umeme! 
Kazi ambayo awali niliona inawastahili wanaume pekee, lakini nilipofika huko matokeo yakawa kinyume! Wanawake na labda niwaite wasichana walikuwa wamefurika isivyo kawaida katika darasa hilo.
Pongezi kwa wanaharakati wanaopigania usawa wa kijinsia, harakati zao zinazaa matunda ati! Kwa mujibu wa waalimu wa hapo, kipindi cha nyuma ilikuwa aghalabu kukuta wanawake wengi wakijitokeza katika fani kama hizi zilizoonekana kama zina harufu ya uume uume!
Wengi ungewakuta ama katika mafunzo ya ufundi wa ususi, urembaji mapambo, mabatiki, ushonaji nguo, upishi na aina zote zenye mwelekeo huo lakini sasa hali ni tofauti, tena tofauti sana.
Ni huko nilikokutana na rafiki yangu Akimu Yusuph, huyu alitokea kuwa rafiki wa kweli na mfariji mkuu wa maradhi yangu ambayo sina shaka kwamba sasa unayafahamu fika.
Halafu ilifika siku moja, siku isiyo na jina!
Siku ambayo hatukuwa na masomo hapo chuoni. Nadhani itapendeza zaidi nikiita siku ya mapumziko. Mchana wa siku hiyo ulinikuta katika grosari moja jirani na chuo chetu pale chang’ombe nikipata kinywaji laini cha baridi. Mimi sio mtumiaji wa vikali na ninaomba Mungu anisaidie nisijaribu kuvigusa, usiulize sababu tafadhali.
Mchana huo ukiendelea kuyoyoma taratibu sambamba na kinywaji changu, mkononi nilikuwa na gazeti la Ijumaa wikienda nikiendelea kupata elimu ya kutakata ya namna ya kuyafikia mafanikio toka kwa Brother Erick Shigongo.
“Hai Ibra?” Sauti nyembamba na laini ikaniharibia pozi.
Nikageuka taratibu kabla ya kujibu. Ni utaratibu nilio jiwekea toka enzi na enzi ili kuepuka kujibu salamu isiyonihusu na hivyo kumkwaza msalimiaji. Ndiyo! Kuna akina Ibra wangapi jijini?
Macho yangu yakakumbana na tabasamu zuri lililopachikwa kiufundi katika sura murua ya binti huyu mantashau. Hakuwa mgeni kwangu. Hili lilidhihirisha kwamba salamu ile ilikuwa yangu. Nami nikachanua tabasamu bomba kujibu tabasamu lake pamwe na salaam pia.
“Hai Shamsa! Mambo?”
“Kama mgambo kasoro kirungu!”
“Hivi bado hamjamuelewa Karl P tu? Kwanini hukujibu kama mgambo kasoro bunduki na pingu?”
Tukacheka.
Shamsa Nuhu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wenzangu tuliokuwa tukichukua mafunzo ya umeme pale VETA. Katika muziki Shamsa alikuwa akimpenda sana msanii Karl P, ingawa Karl P mwenyewe hayuko tena kwenye chati siku hizi .
Shamsa pia ni mmoja wa wasichana wachache walio kuwa wakiwapelekesha puta wanaume ndani na nje ya darasa letu.
Alikuwa na akili za kutosha, hilo lazima nilikiri. Masomoni alikula sahani moja na wale unaoweza kuwaita majiniazi. Kifedha pia alikuwa njema kiasi kile ambacho usingeweza kumrubuni akubaliane na wewe kwa kwa kumringishia vijisenti! Kama hujui vijisenti, usiniulize mimi; muulize Chenge!
Kwa uzuri sijui wengine, lakini kwangu alikuwa na uzuri ulio shinda malaika! Alikuwa na sura nzuri, tabasamu zuri, ‘dimples’ nzuri, shingo ya miraba miraba, umbo zuri, mzigo wa uhakika nyuma yake, usafiri mzuri na hata mwendo wake ulikuwa mzuri. wachilia mbali sauti, roho na vitendo vyake. Alikuwa mzuri hasa, mzuri fika.
Alikuwa mmoja kati ya wengi waliowahi kuumong’onyoa moyo wangu! Unadhani? Sio yeye tu, wako wengi waliowahi kupata hifadhi moyoni mwangu, lakini mimi nilipotaka kuingia katika mioyo yao wakagoma kunipa hifadhi!
Nilihofia kumueleza nilivyojisikia juu yake kutokana na ile hofu ya kawaida, hofu ya kukataliwa kwamba kama watu wanaoonekana; wenye akili zao darasani, fedha zao Benki na heshima zao katika jamii wamejaribu wameshindwa mimi mtoto wa msaka nyoka kama sio msaka tonge nitaweza kweli?
Niliendelea kuumia kwa muda mrefu mpaka siku fulani nilipopata ujasiri wa aina yake na kumkabili. Hii ilikuwa ni baada ya kujishauri sana na kuamua kwamba mwanaume anakufa siku moja. 
Aidha ilikuwa ni baada ya kujiuliza ni mara ngapi nimetongoza na kufaulu, nikagundua ni mara 0.05! Nikakubali kuishi siku moja kama simba kuliko kuishi siku mia moja kama inzi! Kwamba hata akinikatalia atakuwa tayari anajua ninampenda! Itatosha .
Nikamvaa!
Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo!
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda!
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma.
Ghafla akageuka na kunitazama.
Macho yetu yakagongana.  
***NILAMBE HUMO HUMO INAANZIA HAPA……Na itaendelea

‬: Nilambe  Humo Humo - 2
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA PILi 
Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo! 
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda! 
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la
maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma. 
Ghafla akageuka na kunitazama. 
Macho yetu yakagongana. 
Akatahayari, labda kwa vile alivyogundua kwamba alikuwa akitazamwa kifisifisi. Akageuza na kurudi kwa madaha akitumia hatua zilezile za miss Tanzania wa mwaka huu mpaka pale nilipokuwa nimesimama. Akaniangalia kwa muda kabla hajaniuliza kwa wasiwasi.
‘’Una nini Ibra?’’
“Sina kitu Shamsa!’’
‘’Kweli?’’ 
“Haki ya Mungu vile!’’
“Au nimekukatili?! Bado hujamaliza kiu yako ya maongezi na mimi?”
“Nilishamaliza kabisa. Amini nilitaka tu kujua kidogo kuhusu utendaji kazi wa Socket Bracker na vitambuzi vya Short, lakini jinsi ulivyonielekeza inatosha kabisa. Ahsante sana Da! Shamsa, Mungu akujaalie!”
“Amina” Akajibu akitabasamu, wasiwasi ukiondoka pole pole. Dimples zake zikabonyea na kukitonesha kidonda changu tena. Mshituko mdogo nilioutoa ambao nilijitahidi kuuficha asiuone, ukawa umeurudisha wasiwasi wake kwangu tena. 
‘’Sikiliza Ibra!’’ akaniambia kama aliyechoshwa na kitu fulani. 
“Mimi ni mwanadamu mwenye hisia timilifu kama wewe! Kama una lolote ambalo labda unahisi litahitaji msaada wangu we niambie tu. Acha kuteseka kipumbavu na njaa na wakati chakula unachodhani ni cha watu kipo karibu yako! Huwezi jua may be Mungu amepanga kukuokoa kwa chakula hicho.!” 
Akazidi kunionyesha kwamba yuko tayari kwa lolote binti wa watu. Masikini laiti angelijua jinsi alivyozidi kuniweka mbali kwa kauli ile, asingeendelea.
“Da’ Shamsa, msaada niliouhitaji umekwisha nisaidia, tena umenisaidia kiukamilifu. Nikiwa na tatizo jingine nitakwambia tu. Naomba nawe usichoke kupokea miito yangu!”
‘’Usijali!’’ akaniwahi kwa pupa.
Ukapita ukimya mfupi tukiwa bado tumesimama hivyo hivyo tukiangaliana kwa zamu tena kwa wizi, mwishowe Shamsa akaniita tena.
‘’Ibra?” Sasa alinitulizia macho usoni moja kwa moja.
‘’Naam!’’ Nikaangalia pembeni, nikisugua vidole vyangu kama jinga vile
‘’Au… Au… Au unanipenda na unashindwa kuniambia?”
“Mmmm, mmmm!” Nikatikisa kichwa kushoto na kulia kukataa.
Shamsa akanipuuza na kuendelea “Kama umenipenda niambie tu. Niambie dia, niambie nijue! Hizi ni zama za ukweli na uwazi niambie usiogope!’’ 
Ooops! nikashusha pumzi ya faraja ndani kwa ndani, kwa namna ya mtu aliyeshusha mzigo mzito. Shamsa aliamua kuweka ile Msondo ngoma wanaita mambo hadharani. Ndiyo! Alikuwa amegusa mzizi, amegusa pale nilipotaka aguse.  

Pengine ingelikuwa wewe ilikuwa ni kiasi cha kuongeza maneno machache tu ndio ni kweli ninakupenda, lakini kutokana na uzuri wako, uwezo wako kiakili na kifedha nimekuwa nikihofia kukwambia kwa kuwa nilijua utanikataa na hivyo nitaaibika lakini ninakupenda sana na ninataka uwe mpenzi wangu please please naomba upokee ombi langu na kunipokea mimi mwenyewe, 
Lakini kwangu thubutu! Haikuwa hivyo nikajichekeshachekesha kiwazanga pale huku nikiona aibu kupindukia pengine kwa Shamsa kuligundua lile lililomo moyoni mwangu, nikaropoka. 
“Hapana Da’ Shamsa! Wewe ni dada yangu, kwamwe siwezi kukutamkia maneno kama hayo, nikiwa na mengine nitakwambia si hili!’’ Nilizidi kujiweka mbali na kujikaanga kwa mafuta yangu mwenyewe. 
Shamsa akaniangalia vizuri asiamini lile nililoongea, kutaka uhakika akaniuliza tena. ‘’Unasemaje?” 
Nikarudia nilichokisema awali mithili ya muigizaji aliyeiva vyema baada ya kumeza scripts kikamilifu. Nikaona Shamsa akiishiwa nguvu kwa staili ileile ya kukata tamaa, alipogundua nimemgundua katika hilo, haraka akajirekebisha na kusema. 
“Ok! Nafurahi kwa mawazo yako yaliyokwenda shule Ibra, laiti kama wanaume wote wangelikuwa kama wewe…! Ndio maana ninakupenda Ibra, wewe sio muhuni, hupendi mambo ya kipumbavu! 
Angelikuwa mwanaume mwingine, tayari angeisha nitongoza zamani. Lakini wewe akah! Keep it up. Keep it real Ibra. Endelea na moyo wako huo huo siku moja nitakuja kukupa tuzo. Bye!’’
Akaondoka bila kunipa nafasi ya kujibu tena, nadhani maneno yale aliyasema kwa uchungu kiasi cha machozi kumlenga na nilihisi aliondoka upesi akihofia kulia mbele yangu!
Kulia? Nikajiuliza kwa mshangao, kwa ajili yangu! Maana yake nini? Sikupata jibu! Niliendelea kumwangalia mpaka alipotoweka kwenye upeo wa macho yangu. Ndio kwanza nikapambazukiwa na ukweli wa kile nilicho kifanya. 
“Shit!” Nikaguta ghafla nikijipiga makonde ya nguvu kichwani. “Nimefanya nini sasa? Ama kweli mimi ndio mjinga wa wajinga No! Mwenyekiti wa wajinga. Mtoto tayari alishakaa katika laini namba moja, mie nimemrudisha line namba ziro! Tena ziro pointi ziro tano! Kamwe siistahili kusamehewa!” Nikajiambia nikizidi kujipiga makonde kichwani. 
‘’We vipi Ibra?’’ sauti niliyoifahamu sana ikanishtua kutoka nyuma yangu. Nikageuka haraka huku nikitahayari mithili ya mtu aliyefumaniwa, ni kweli rafiki yangu Yusuph alikuwa amenifumania, nikijipiga makonde kichwani kama chizi.
“Vipi nini?” Nikasaili kipumbavu nikizidi kuona hatia na kuongeza 
“Mbona mie mambo yangu yako safi? 
‘’Unahakika ni safi?’’ Akimu akanitulizia macho asiyapepese walau kiduchu. 
Nikazidi kuona soo. 
“Sikiliza Ibra, mimi ni rafiki yako wa damu, rafiki wa dhati rafiki wa kufa na kuzikana. Unaponificha jambo ni kama unajificha mwenyewe!”
‘’Hakuna Akimu! Hakuna kabisa. Nothing!”
‘’Kweli?’’
‘’Kweli tupu!
‘’Sasa mbona unajipigapiga makonde kichwani huku ukikita miguu chini utafikiri umepoteza kitu fulani kama sio kufeli mitihani!”
Eh! Hii kali! Nikawaza. Kumbe nilikuwa nikikitakita na miguu chini? Sekunde kadhaa zikapita huku Akimu akiniangalia na mimi nikiangalia chini kwa tahayari wakati huo kichwa changu kikizunguka kutafuta jambo la kumuongopea Akimu, sikulipata.
“Ukingali unajaribu kunificha Ibra! Any way haya ni maisha yako. Wewe ni mwamuzi wa mwisho kwayo. Ukiona ninastahili kuambiwa utaniambia, Ukiona sistahili usiniambie na sitolalamika kwaheri!”.
Akimu akamaliza na kuondoka kwa haraka kama alivyoondoka Shamsa. Nahisi nae aliongea kwa uchungu kwa kuwa tangu nianze masomo yeye ndio amekuwa rafiki na mwandani wangu mkuu. 
Sasa nitawakorofisha watu wangapi jamani? Kwa kule tu kukataa kwangu kusema ukweli! Kwa Shamsa naweza kustahimili kuishi bila ya kuwa na mahusiano nae mazuri. Lakini Akimu?! Itanichukua muda gani kutengeneza urafiki mzuri na bora kama yeye? 
Liwalo na liwe! Nikaanza kumkimbilia huku nikimwita, alikuwa amefika mbali kidogo, aliposikia akasimama na kugeuka .
‘’Unasemaje?” Akaniuliza nilipo mfikia.
“I am so sorry kaka!’’
‘’Samahani ya nini Ibra?! Si umesema hakuna kitu?”
‘’Nilikuwa wrong Akimu, nina tatizo! Tena tatizo kubwa!’’
‘’Tatizo la mapenzi sio? Linamuhusu Shamsa bila shaka!’’
Nikasikia moyo unafanya pah! Amejuaje? Nikatikisa kichwa chini na juu kuafiki,
’’Nilijua tu lipo tatizo, nikashangaa na kuchukia ulipotaka kunificha. Ulipotoka bwenini nilikuwa na shida na wewe, nikawa nimekufuatilia ili nikujuze shida yangu. Nikakukuta na Shamsa, na kutokea hapo nimeshuhudia kila lililojiri baina yenu ingawa sikuweza kusikia maneno mliyokuwa mkizungumza!’’
Unaona? Siku nyingine mtu unaweza kufungwa hivi hivi. Kumbe amenichora A to Z halafu mie nakomaa tu hakuna kitu, hakuna kitu! 
“Haya niambie ni tatizo gani? 
Nikabakia nikiumauma meno kwa muda nisijue nianzie wapi. Maana haya matatizo mengine wewe unaona tatizo, hali mwenzako haoni kama ni tatizo. Nikaamua kumweleza ukweli.
‘’Tatizo ni Shamsa Akimu, Nampenda sana, tena sana !’’
“Amekukataa? kwa kadiri nilivyoona na ninavyohisi kama sio kufahamu Shamsa nae anakupenda kupita kiasi, kwani bado haujamwambia kama unampenda?”
‘’Bado!’’
‘’Sasa tatizo liko wapi si ungemwita ukamwambia?! We mwambie tu Shamsa zungu yule hana tatizo!’’ 
“Tatizo lipo hapo kwenye kumwambia!”
“Unaogopa?”
‘’Naweza kusema hivyo, maana naweza kujipanga kwa sasa namwambia nikikutana nae tu nageuka zezeta kama sio bwege. Kujiamini kote kunatoweka na maneno yanakimbia kabisa!’’
Akimu akatabasamu.
‘’Wakati mwingine unapaswa kujiamini Ibra!’’
“Tatizo ni kwamba…” Nikamkumbusha kwa karaha, ’’Sio kwamba sijiamini, najiamini sana lakini ninapofika mbele yake tu ndipo hali hii inapo jitokeza! Unaweza kudhani Shamsa anadawa vile!’’
“Huko unakoenda mbali Shamsa hana dawa. Tatizo liko kwako tu tatizo ni kwamba hujiamini! Hilo tu. Lakini sio lazima umtongoze kwa kuongea nae, ziko njia nyingi za kufikisha ujumbe wako, 
Nikazibuka masikio. “Kama zipi?”
“Unaweza kumuandikia barua, ukamnunulia kadi za mapenzi, ukamtumia mauwaridi mazuri yenye ujumbe mzuri na hata kumwandikia sms za mapenzi na ujumbe ukafika, akaelewa na mkawa wapenzi. Shamsa hana ubavu wa kukukataa wewe Yule, sure am telling you!!
‘’Kumbe?!”
“Eeh!’’ Akakubali kwa msisitizo. Moyo wangu ukazizima kwa furaha nikajua naweza kutumia moja wapo kati ya njia hizo, mambo yakajipa na nikaweza kummiliki Shamsa Nuhu moja kwa moja. 
‘’Ila’’ Akimu akanizindua tena, “Itakubidi usubiri muhula huu wa mitihani uishe ili usichanganye mapenzi na masomo. Ukianza wewe kuvichanganya vyenyewe vitamalizia, na hupata zaidi ya hasara!’’
‘’Nitasubiri!” Nikamwambia
“Good!’’ Akashangilia baadae akaniambia lile alilokuwa akinitafutia, nami nikampa ushauri alioutaka. Mpaka tunaagana tabasamu lilikuwa bado limeupamba uso wake.itaendelea, usikose sehemu ya 3

‬: CHOMBEZO: NILAMBE HUMOHUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA NNE
Ukutani kulikuwa na picha kubwa za wanawake wa kizungu walio uchi ambao walikuwa wamelala kitandani katika namna ya kutamanisha kulikovuka mipaka, yule mheshimiwa akaanza fujo tena.
Jimama likaingia na kufunga mlango,
Likaondoa kanga kifuani na kile kijisketi kilichokuwa kimemsitiri kwa chini na kubaki kama lilivyozaliwa. Mwanga hafifu uliotoka katika balbu ukimpiga vilivyo katika mwili wake mtepe na kuufanya uwe mwekundu na kuvutia vitamu, jimama likapiga hatua za maringo na kuketi kitandani.
Mkono wake ukazama uvunguni na kuibuka na boksi la kondomu!
‘’Changamka! Hesabu haijatimia, nataka niendelee kula vichwa na kijua ndio hiki nisipouanika nitautwanga mbichi!’’ Nikaelewa nikavua shati, wakati najiandaa kuvua suruali akaniuliza
“Unataka kulala hapa hapa?”
‘’Hapana!’’
‘’Sasa unatoa nguo za nini?’’
‘Nikamshangaa ‘’si tunataka ku…ku…!’’
“Najua’’ akaniwahi kwa karaha ‘’Haina haja ya kuvua nguo shusha tu suruali kidogo kama huwezi kuipitisha hapo katika zipu! Halafu nipe hela yangu kabisa!”.
Nikatoa hela na kumpa nikimwambia “Lakini hapa hatuwezi…”
‘’Ukitaka starehe kamili kaoe! Mimi niko kazini na nilishakwambia hesabu haijatimia hivyo sitaki mizungu!’’ 
USIBONYEZE KAMA WEWE NI UNDER 18+ WAKUBWA TU.
Nikamtumbulia macho
Alipoona simuelewi akanisogelea pale akaivuta chini sarawili yangu na kumkamata jamaa aliyekuwa nusu akilia na nusu akitetemeka akamvisha koti la mvua na kumkaribisha uwanjani akague gwaride.
Hakukuwa na busu, sijui romance wala kunyonyana ndimi. Nikaanza kazi mara moja. Alikuwa fundi wa kuzungusha viuno na kunung’unika. unadhani nilichukua round basi!? dakika zangu mbili unusu tu, ikawa kitu na boksi! Akanitoa kunisukumia pembeni. Kazi ikawa imekwisha.
‘’Ukitaka kurudia je?” Nikamuuliza nikimwangalia kwa matamanio. Kusema kweli nilikuwa sijaridhika hata kidogo.
‘’Haturuhusu! Hapa goli moja, unatambaa!“
Nikamuelewa.
Dakika iliyofuata nikawa nje katika upande mwingine.
Elfu kumi niliyoichukua kwa kazi hii ilibaki elfu saba! Kwa bei ya elfu tatu ningeweza kupata wanawake wengine wawili na kubaki salio la elfu moja ambayo ningelitumia kama nauli na kurudi bwenini chuoni Chang’ombe.
Katika chumba hiki cha pili nikiwa na mwanamke mwingine tena nilikuwa nimeshakaa kifuani kwa zaidi ya dakika tano pasipo jibu kuonekana, ndipo mambo yalipoanza kwenda mrama.
‘’Changamka bwana muda wako umeisha!’’ Alinihimiza nikazidisha spidi. Dakika zingine tatu yule mama akanisukumia pembeni na kuliangalia koti la baridi alilonivika akidhani namuongopea.
‘’Alipokuta halijaloa akaniangalia vizuri na kunitwanga swali
“Umeshatoka kupata sehemu nyingine siyo?”
‘’Ndiyo!” Nikamjibu.
Akaachia mfyonzo mrefu uliotoka vizuri haswaa. Halafu akainuka kwa ghadhabu na kuvaa nguo zake, alipomaliza akaniambia “Haya toka!’’
‘’Lakini hatujamaliza bado!’’
‘’Tumemaliza umeniongopea kuwa hujapata kumbe umeshapata toka nakwambia!’’ Sasa alinifuata na kuniinua pale kitandani.
‘’Hatukuongea hivyo!’’
‘’Toka nitakupigia kelele za mwizi!’’ Sauti yake haikuwa ndogo, alikuwa akipayuka.
“Basi nipe chenji yangu nakudai elfu mbili, nimekupa elfu tano!’’
“Elfu tatu ni dakika tatu wewe umetumia kumi! Nikingali nakudai elfu tano!” Akabweka.
Nikachoka. “Haiwezekani!” Nami nikapandisha na kukomaa. “Lazima unipe chenji yangu’’
Akaufuata mlango na kuufungua nje kulikuwa na shehena ya kutosha ya watu, Baadhi wakitaka kujua kulikoni wengine wakipaza sauti nikomeshwe! “Betty mtoe fasta tumjeruhi!” Sauti kutoka nje ikaomba.
Akanivuta na kunisukumia nje akawageukia wale wanawake na kuwaambia “Alitaka kunitumia dabo dabo bila malipo!”
kufikia hapo moyo ulikuwa ukinipiga vibaya nikijua sasa ndio naadhirika. Kwa ajili ya ngono! Nikawaza kwa uchungu. Maana sikupewa hata nafasi ya kujieleza.
Pale nje nilipokelewa kama mpira wa kona, nikatukanwa matusi ya kila aina waloweza kunitia singi walinitia, walioweza kunipiga na viatu na makopo ya mkojo pia walifanya hivyo.
Mara wakatokea watoto kadhaa machokoraa wakanikwapua kama kipanga na kunipeleka mahala walipopaita Chakabovu! Kule wakanisachi na kunipokonya kila nilichokuwa nacho.
Simu, fedha kidogo, viatu, kofia! Halafu halafu wakaniambia nipotee!
Niliondoka roho ikiniuma na nikiwa nimewachukia wanawake wote wa Uwanja wa fisi. Niliwachukia isivyo kawaida. Kutoka pale Manzese Bahresa hadi magomeni makonda waliweza kunielewa na kunipa lifti.
Lakini kutoka Magomeni hadi Chang’ombe hawakunielewa ikanilazimu nitembee kwa mguu kutoka Magomeni baada ya kuona masaa yakiyoyoma bila kupata lifti. Nilifika chuoni usiku nikiwa hoi bin taaban.
Siku ya pili sikuingia darasani nikabaki bwenini nikijisomea na kuuguza majeraha madogo toka kwa wale machangu pamoja na machokoraa wao.
Jioni Akimu na Shamsa walikuja kunitazama na kunipa pole. Nikajisingizia ugonjwa. Shamsa akanisisitiza kwenda hospitali kuangalia afya pengine nina malaria
‘’Nitakwenda!’’ nikawaambia kuwapa moyo.
* * *
Miezi kadhaa baadae nilishaweza kuyasoma mazingira na kwenda nayo sawasawa. Niligundua kuwa uwanja wa fisi sio mahala pa’ kwenda na fedha nyingi, simu ya kifahari, mavazi mazuri sana na kadhalika.
Sio mahala pa’ kusema utapata bao mbili kwa mwanamke mmoja. Na muda wa kuwa na mwanamke kitandani usizidi dakika kumi,
Niligundua pia kuwa yako mamia kwa mamia ya wanaume wanaofuata ngono za bei raisi katika maeneo hayo kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es Salaam ambapo hapo hakuna haja ya kutongoza.
Hakuna pia kuombwa hela ya vocha, Saloon, hela ya mtindo mpya n.k pale ni mahala pa’ kulipa, kupata huduma utakayo na kutoweka! Mahala pa nipe nikupe.
Niligundua pia kwa siku moja pale mwanamke ambae mapato yake sio mazuri hulala na angalau wanaume kumi kwa siku na kupata elfu thelathini! Wale wenye mapato mazuri hupata wanaume kati ya ishirini na ishirini na tano kwa siku.
Hawa pato lao kwa mwezi lilifukuzia pato la mafisadi kwa karibu tu kwa vile ni kati ya milioni 1.2 na milioni 5, ambapo pia nao hulazimika kulala na wanaume 600 hadi 750!
Unashangaa nini? Wewe endelea tu kuhudhuria huko uwanja wa sifa kama ibada ujue hauko peke yako.
Niligundua mbali ya walevi, wanywa pombe na wabwia unga; wapo baadhi ya wanawake ambao wamelitumia pato hilo kwa kujenga makwao kusomesha watoto na n.k.
Niligundua tena kuwa wengi walikuwa ni waathirika wa ukatili wa kijinsia ambao uliwakumba katika familia zao na mikondo ya maisha waliokuwa wakiishi.
Wengine ndugu zao wa kiume walikuwa wamewadhulumu mali za urithi walioachiwa na wazazi wao, wengine walikuwa yatima walioondokewa na wazazi wao na kukosa mtu wa kuwaangalia! Wengine walikuwa wametupwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa wengine… wengine!
Basi ilimradi kulikuwa na mlolongo wa matatizo ambayo kwa hakika yalichusha na kuudhi.
Hofu ya ukimwi je?
Walikuwa nayo lakini wangefanyaje? Waliona bora waishi kwa furaha leo kwa kuwa hata kesho wasipokufa kwa ukimwi kama watajitunza, basi watakufa kwa njaa, umasikini na adha zingine kadha wa kadha.
Ugunduzi huu ukanifanya nisiwatizame kwa jicho baya tena, bali nikawaona kama wahanga fulani hivi!
Nikajitengenezea utaratibu mzuri wa kwenda pale na kuhudumiwa mara nne kwa wiki! ulikuwa utaratibu nilioupenda na kuufuatisha kama ibada, utaratibu mtamu kweli, mtamu haswaa. itaendelea

 MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA TANO
Wengine ndugu zao wa kiume walikuwa wamewadhulumu mali za urithi walioachiwa na wazazi wao, wengine walikuwa yatima walioondokewa na wazazi wao na kukosa mtu wa kuwaangalia! Wengine walikuwa wametupwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa wengine… wengine!
Basi ilimradi kulikuwa na mlolongo wa matatizo ambayo kwa hakika yalichusha na kuudhi.
Hofu ya ukimwi je?
Walikuwa nayo lakini wangefanyaje? Waliona bora waishi kwa furaha leo kwa kuwa hata kesho wasipokufa kwa ukimwi kama watajitunza, basi watakufa kwa njaa, umasikini na adha zingine kadha wa kadha.
Ugunduzi huu ukanifanya nisiwatizame kwa jicho baya tena, bali nikawaona kama wahanga fulani hivi!
Nikajitengenezea utaratibu mzuri wa kwenda pale na kuhudumiwa mara nne kwa wiki! ulikuwa utaratibu nilioupenda na kuufuatisha kama ibada, utaratibu mtamu kweli, mtamu haswaa.
* * *
Asubuhi kulipokucha, Akimu allikuja kunigongea, nikainuka na kufungua mlango.
‘’Mambo?’’ Akanisalimu akiingia ndani.
“Poa!’’
‘’Vipi mbona hivi, leo huendi?”
‘’Wapi?” Nikamuuliza kwa wasi wasi kidogo.
‘’Mara hii umesahau kuwa juzi tulikubaliana kwamba leo tutakuwa na round discussion kuhusu Utambuzi wa Short na mitihani ya mwisho inayokuja?
“My God!’’ Nikaguta. Nilishasahau kabisa, ukweli leo sikujisikia kujadili chochote mwenyewe nilikuwa nataka masaa yaende mbio jioni niende zangu uwanja wa miutamu.
‘’Sorry Akimu!’’ Nikamwambia Akimu “Sitaweza kuja katika discussion leo nataka nifue then nipumzike kabla sijajisomea kisha nitakwenda mahala!’’
‘’Lakini tulikubaliana utakuja!’’
“Ndio hivyo tena!’’
‘’Basi itakubidi umueleze Shamsa kabisa maana binti yule asipokuona hasomi sawa sawa!’’ Nikatabasamu “Nitamwambia!’’ nikajibu.
Wakati anataka kujibu akakiona kitabu cha gwiji wa riwaya nchini marehemu Eddie Ganzel ’Kijasho chembamba’, vile anavyopenda riwaya za Ganzel akainuka na kukitwaa.
Alipokiinua tu kadi za mapenzi, zenye picha nzuri na maua ya kuvutia pamoja na barua za mapenzi zikaonekana chini yake, akaniuliza maswali machache kuhusu nilikokipata kitabu kile, halafu akauliza
‘’Hivi haya maua na hizi kadi bado tu hujazipeleka kwa Shamsa?’’
“Bado!’’
Akimu akanitumbulia macho kwa mshangao!
Alikuwa na haki ya kushangaa, alikuwa nayo. Mosi ni
yeye aliyekuwa mwandani wangu, alifahamu vingi na mengi kunihusu, pili alikuwa shuhuda wa macho wa namna nilivyoathirika kwa kumpenda binti yule.
Na ni yeye aliyetoa ushauri wa kumpelekea zana hizo na kama vile haitoshi alikuwa amenisindikiza kuzinunua, kubuni maneno mazuri yaletayo faraja na kuyaandika juu ya kadi hizo, tena alikuwa amenitaka kumpelekea haraka iwezekanavyo ili kama kuna lolote tulijadili kwa pamoja.
Na sasa ulikuwa umepita mwezi na kidogo toka tulipoziandaa
“Kwanini hujazipeleka? Ibra usiniambie ulikosa ujasiri, maana nilikwambia wewe ukishindwa kumkabidhi nipe mimi nitamkabidhi!’’ Akatua kwa kila hali alikuwa na hasira, mimi nikatabasamu na kumjibu.
‘’Nimeona haina haja Akimu!’’
‘’Eti?!’’
‘’Enh! Hanisumbui tena nimesha muweka chini ya himaya yangu!’’ ikawa zamu yake kunitazama kwa mshangao, nusu akitabasamu nusu akitaka kushangilia.
‘’ Ina maana umeisha… umeisha….! Mungu wangu, mbona siamini!’’
‘’Sijafanya nae mapenzi wala hajanikubali niwe mpenzi wake! Ila nimemdhibiti, hanisumbui tena! Maelezo yangu yakazidi kumchanganya Akimu. Akanisaili tena.
‘’Unamaana gani Ibra?’’
‘’Nina maana kuwa kuna mahala ninapoupoza moyo wangu kwa maji baridi, maji ya ya mapenzi, maji ya uzima!’’
“Inamaana umepata mpenzi mpya unayempenda kuliko Shamsa?”
“Sijasema simpendi Shamsa!’’ Nikasema kwa karaha “Nikingali nampenda na nitaendelea kumpenda maisha yangu yote!”
‘’Basi nyoosha Kiswahili Ibra, hata hao wahenga misemo na mithali zao zilieleweka kwa urahisi!’’
“Nitakwambia!” Nikamwambia huku tabasamu likiwa limeupamba mdomo wangu “Nitakwambia rafiki yangu, tena nitakwambia ukweli mtupu naomba tu uniwie radhi kwa kukuficha!”
Nikakaa vizuri na kumueleza ugunduzi wangu wa kule Fisi. Nilimueleza kwa tuo pasipo kuacha hata tukio moja. Nilipo maliza Akimu alikuwa ameshika kichwa kama aliyepoteza kitu cha thamani sana!
‘’Ni kweli unielezayo Ibra?” Sasa machozi yalikuwa yakimlenga
‘’Ni kweli kabisa!’’
‘’Umepotea rafiki yangu, tena umepotea vibaya sana. Sio watu wale ni balaa!’’
‘’Tatizo lao liko wapi Akimu? Kama nilivyo kwambia nimewastadi vya kutosha kabla ya kuamua kuwa nao chanda na pete.
‘’Hawako salama wale! Kila mwaka wanakufa! Na wanakufa na idadi kubwa sana ya watu! Hii ni kwa vile wanafanya mapenzi na watu wengi sana, wengine hutembea mpaka na wanaume elfu sita na mia sita kwa mwaka hadi elfu saba na mia mbili.
Ni washenzi wa tabia wasio na utu walioamua pesa iwe yao kwa kila hali, ukiwa na pesa unaweza kumwambia akuuzie hata utumbo wake na akakuuzia! Zaidi na zaidi ni wabaya wazee na wasiovutia kwa chochote! Ndio maana nasema umepotea!”
Akiwa na jazba Akimu alitumia zaidi ya robo saa kuwaponda makwini wa fisi. Alipomaliza ndipo nami nilipoanza kum’bishia. Tulibishana sana na mwisho wa siku ikawa imeamuliwa mimi na yeye twende uwanja wa fisi wote akajionee, nae akasisitiza mimi nikajionee, tukaondoka mchana huo huo!
Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuingia uwanja wa fisi mchana. Eh! zaidi ya maajabu yalikuwa yakinisubiri
Wanawake karibuni wote waliokuwa wakiuza miili yao walikuwa watu wazima hasa, wazima kweli, umri umekwenda mno. Sura zao zilikuwa tisho jingine. Mbali ya kuwa zimekomaa kwa namna ya kuchusha, huo mkorogo waliojimwagia sikuwahi hata kuufikiria. Mkorogo hadi mapajani! Mkorogo hadi miguuni, hadi katika matiti!
‘’Niliwezaje kufanya mapenzi na watu hawa?” nikajiuliza nikitikisa kichwa kwa masikitiko. Nikajuta. Akimu akanikokota tukarudi chuoni nikiwa nimenyongea.
‘’Kwanini uliamua kuja huku Ibra?” Akanisaili kwa upole baadae.
‘’Msongo rafiki yangu! Mhemko! Nilihemkwa na kutamani ngono kupita kitu chochote! Nikaona huku ndio pa’ kuponea! Laiti ningelijua…,” Nikalia kimya kimya. Akimu akinifariji.
Kwa shinikizo lake niliweza kushiriki katika Round discussion ingawa nilipooza Kama ugali uliokosa moto wa kuuivisha sawa sawa. Shamsa alikuwepo na alifurahi kuniona, nikamtaka radhi kuwa sikuwa nikijisikia vizuri.
Mpaka tunamaliza majadiliano yetu sikuwa nimechangia lolote!
* * *
‘’Kanini umenileta huku Akimu? Nikamuuliza tukitembea kutoka sokoni, tulikuwa Songambele, kijiji kimoja kilichoko mkoani pwani ndani kabisa wenyewe walikuwa wamekibatiza jina la Gobba , ingawa jina lake la asili lilikuwa Songambele Sotele.
Kilikuwa kijiji ambacho Akimu alisomea elimu yake ya sekondari kabla hajafaulu vizuri, akakataa kuendelea na masomo ya juu na kuja kusomea umeme pale VETA. Hili lilijiri kwa kuwa Baba yake alikuwa fundi umeme aliyefanikiwa sana kimaisha kupitia kazi hiyo.
“Nimegundua rafiki yangu u’mhanga wa starehe! Starehe ya mapenzi. Huku utaburudika utastahali na kuneemeka vya kutosha. Na uzuri wanawake wa huku hawatokitoki hovyo nje ya vijiji vyao kwahiyo ni salama kwa kiasi kikubwa!”
Akanijibu. Angejua nilivyojiapiza kutofanya tena mapenzi tangu ulipojiri ule ugunduzi wa yaliyopo Uwanja wa fisi, wala asingejisumbua! Moyoni mwangu alibakia Shamsa pekee na vile tulibakiza miezi sita tuhitimu, nilijua nitamtamkia wakati huo na kitakachofuatia ni ndoa mara moja.
Nikiendelea kutembea, niliendelea kukiperuzi kijiji hiki cha Gobbah kuona kama kingeweza kunifariji. Hakikuwa na chochote cha kujivunia! Mifugo michache yenye siha na afya ya wastani, wakazi ambao mwonekano wao uliashiria umasikini uliotukuka na ardhi kubwa yenye rutuba ambayo haikuwa imelimwa, vilikuwa baadhi ya vitu vilivyoipamba Songambele Sotele a.k.a Gobbah.
Jioni tulikuwa baharini, tuliogelea na kufurahi pamoja na wenyeji wa eneo hilo ambao walikuwa na ukarimu unaovutia. Halafu tukaelekea mpirani. Usiku tulikuwa kwenye vijiwe vya kahawa ambapo tulipiga soga mpaka usiku ulipokomaa, tukaenda kulala.
Siku mbili zilizofuatia tuliishi katika mtindo huu.
Wakati nimeanza kuchoshwa na maisha haya katika siku ya tatu na nikiwa tayari kumwambia Akimu turudi Dar es salaam; ndipo lilipotokea lile ambalo ni miongoni mwa mambo matatu muhimu yalinifanya nishike peni na karatasi na kuandika mkasa wangu huu ambao Uncle Wamaywa ameamua kuuita chombezo.
‘’Jiandae Ibra,’’ Akimu Aliniambia kwa bashasha. ‘’Leo kuna ngoma! Watoto aina kwa aina wanakusanyika toka kata nzima. Hii hakuna kulala ni kutimbwirika hadi majogoo!”
Nikamtazama nisimuelewe! Ngoma ni miongoni mwa vitu ambavyo sikuwa na hobi navyo, Nikamuuliza taratibu hali nikiwa nimemkazia macho. ‘’Najua unajua kwamba mimi sipendi ngoma!”
‘’Najua sana, lakini hii tunaita ngoma kimazoea! Jina lake hasa ni mnanda!”
“Mnanda?!”
‘’Ndiyo!”
‘’Mnanda ni nini na Ngoma ni nini?!”
‘’Yanini tuandikie mate il-hali wino upo? mnanda unaanza saa kumi na mbili jioni na sasa ni saa kumi jioni subiria masaa mawili tu utapata majibu timilifu, majibu ya vitendo! Jiandae tu!”
Maswali yalikuwa mengi kichwani, lakini kila nilipomuuliza Akimu jibu lake lilikuwa moja tu. ‘’Jiandae, jiandae!’’
Nikajiandaa.
Kweli, jioni tukakusanyika mnandani watu aina na aina wakijisogeza na kumsherehekea binti huyu anayeolewa. Wasichana na niseme wanawake walikuwa wamejikwatua vilivyo na walikuwa wakijituma hasa pale dimbani.
Nikashangaa kwa kuwa sikuwa nimewaona kabla. Akimu akinijulisha kuwa nisingeweza kuwaona kwa kuwa ule ni mkusanyiko wa watu kutoka kata nzima na pengine tarafa.
‘’Mambo zaidi utayaona usiku!’’ akahitimisha wakati nikianza kusisimkwa! Ule uchezaji wao ulivutia kwa hakika, ulikuwa uchezaji ambao ungekulazimisha kuangalia huku mwili ukipatwa na joto ghafla.
****Nini kitajiri USIKU huu unaosemwa……IBRA tayari amesisimka….
Tukutane kesho tena/

‬: CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA SITA
Siku mbili zilizofuatia tuliishi katika mtindo huu.
Wakati nimeanza kuchoshwa na maisha haya katika siku ya tatu na nikiwa tayari kumwambia Akimu turudi Dar es salaam; ndipo lilipotokea lile ambalo ni miongoni mwa mambo matatu muhimu yalinifanya nishike peni na karatasi na kuandika mkasa wangu huu ambao Uncle Wamaywa ameamua kuuita chombezo.
‘’Jiandae Ibra,’’ Akimu Aliniambia kwa bashasha. ‘’Leo kuna ngoma! Watoto aina kwa aina wanakusanyika toka kata nzima. Hii hakuna kulala ni kutimbwirika hadi majogoo!”
Nikamtazama nisimuelewe! Ngoma ni miongoni mwa vitu ambavyo sikuwa na hobi navyo, Nikamuuliza taratibu hali nikiwa nimemkazia macho. ‘’Najua unajua kwamba mimi sipendi ngoma!”
‘’Najua sana, lakini hii tunaita ngoma kimazoea! Jina lake hasa ni mnanda!”
“Mnanda?!”
‘’Ndiyo!”
‘’Mnanda ni nini na Ngoma ni nini?!”
‘’Yanini tuandikie mate il-hali wino upo? mnanda unaanza saa kumi na mbili jioni na sasa ni saa kumi jioni subiria masaa mawili tu utapata majibu timilifu, majibu ya vitendo! Jiandae tu!”
Maswali yalikuwa mengi kichwani, lakini kila nilipomuuliza Akimu jibu lake lilikuwa moja tu. ‘’Jiandae, jiandae!’’
Nikajiandaa.
Kweli, jioni tukakusanyika mnandani watu aina na aina wakijisogeza na kumsherehekea binti huyu anayeolewa. Wasichana na niseme wanawake walikuwa wamejikwatua vilivyo na walikuwa wakijituma hasa pale dimbani.
Nikashangaa kwa kuwa sikuwa nimewaona kabla. Akimu akinijulisha kuwa nisingeweza kuwaona kwa kuwa ule ni mkusanyiko wa watu kutoka kata nzima na pengine tarafa.
‘’Mambo zaidi utayaona usiku!’’ akahitimisha wakati nikianza kusisimkwa! Ule uchezaji wao ulivutia kwa hakika, ulikuwa uchezaji ambao ungekulazimisha kuangalia huku mwili ukipatwa na joto ghafla.
Wachezaji walio wengi walikuwa akina mama ambao walikuwa na kanga mbili tu, moja kifuani na nyingine kiunoni. Ile ya kiunoni ilikunjwa kiustadi ikaweza kufunika matiti na tumbo kwa kiasi kidogo.
Ile ya kiunoni ilifungwa kinamna kiasi cha kuweza kuonyesha shanga za kutosha zilizosheheni pale kiunoni. Wachezaji walijenga duara kwa mirindimo yao na katikati ya duara hilo kulikuwa na meza iliyojengwa mfano wa jukwaa na kuwekwa nguzo katikati yake.
Kadiri ngoma ilivyokuwa ikinoga, ndivyo mwanamke mmoja alivyochepuka kutoka katika mduara na kuiparamia ile stage ya meza, akainama na kuishikilia ile nguzo kama nyenzo ya kumfanya asianguke!
Hapa tena atayabinua makalio yake ambayo hayakuwa na kitu ndani zaidi ya ile khanga iliyofungwa chini kidogo ya shanga. Halafu angeanza kuzungusha kiuno katika namna ambayo usingetamani aache.
Mwingine midadi ilipomzidia kabla mwenzie hajashuka basi angeinama tu na kumwaga vitu, atamwaga vitu kweli kweli. Mara mbili ngoma ilizimwa, mpiga ngoma akasikilizwa.
Ni katika wakati huu nilipogundua kuwa Akimu hayupo! Unadhani nilimtafuta? Thubutu, ule uchezaji ulishanikamata na kunifanya mateka kabisaa! Akimu nitamtafuta baadae! Nilijiambia nikiendelea kuufuatilia muziki ule wa asili.
Naam huu ulikuwa mduara orijino wa Segere au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa.
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda.
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa!
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipo watazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta ambalo nalo lilikuwa tayari likinishinikiza tufanye mapenzi! Vile nilivyokuwa na ukata wa mwanamke, vile ambavyo jimama yule alikuwa amenihamasisha vya kutosha sikujivunga mwanaume! Nikampa kitu na box!
Tukaneng’eneka kisawa sawa.
‘’Ngoma ilipoanza kupigwa tena ishara ya kuwaita watu warejee ngomani, mimi na yule jimama hatukurudi. Tulikuwa tumeianza ngwe ya pili. Ngwe ambayo ilikuwa na urefu usiochusha wala kuudhi, urefu mtamu.
Ufundi wote aliouonyesha katika ngoma sasa aliuonyesha mbele yangu juu ya nyonga yangu. Nilifaidi hasa, nilifaidi mno! Nilifaidi ukweli wa kufaidi. Mpaka tunafika tamati na kumwaga mizigo yetu ya kuni pale, kila mmoja wetu alikuwa ameridhika.
‘’Ahsante anti!’’ Nikamshukuru
‘’Asante nawe! U’ngangari na unayaweza kwa hakika!’’ akajibu yule jimama.
‘’Sikushindi wewe!’’
‘’Ahsante’’
Ukimya mfupi ukapita
‘’Unaitwa nani?”
‘’Havijawa! Havijawa Mawimbe! Na wewe?’’
‘’Ibra! Ibrahim Semkee Kinara! Ni mgeni hapa nimetokea Dar es salaam!”
‘’Najua kama umetokea Dar!’’
‘’Eeh?”
‘’Ndiyo!’’
“Umejuaje?’’
‘’Pale ulipofikia yupo anti Hidaya, Hidaya ametujuza kila kitu kuwahusu, kuwa mmekuja huku kuburudisha mioyo akili na mawazo! Na manta hofu Ibrahim, hapa hamtaburudisha mioyo tu, bali na miili pia!‘’ Akanambia, nikabaki hoi.
Nikamuuliza maswali kadhaa kuhusu mnanda, akanieleza mengi ambayo sikuyajua, mengi mno!. Nilipoagana nae tukawa tumeachiana namba za simu.
Kesho yake tulipoonana na Akimu nyumbani kila mtu alikuwa na kitu cha kumuhadithia mwenzake. Nae yalimkuta kama yangu! Tulikaa Gobbah kwa siku kadhaa halafu tukarejea Dar.
Ambacho Akimu hakukijua ni kuwa mie niliendelea kuwasiliana na Havijawa na nikawa mgeni wa Gobah kila baada ya siku kadhaa. Minanda nikaizoea, nikawa mzaramo hasa.
Vile Havijawa alikuwa akijuana na wale wapiga ngoma ambao walikuwa wakimpa ratiba ya kazi. Wiki hii tutapiga kijiji X, mwezi ujao tutamtoa na kumfunda mwali kijiji Y!
Ngoma zote nikawa nahudhuria! Mara nyingi nikiwa na Havijawa.
* * *
‘’Leo jioni kuna ngoma!” Sauti nyembamba niliyoifahamu fika ikapenya masikioni mwangu. Nikasisimkwa furaha ikinitawala nusu nusu.
‘’Unasema?’’ Nikauliza tena.
‘’Nasema hivi…,” akarudia kwa msisitizo tunaoweza kuuita wa herufi kubwa “Leo kuna ngoma, nyumbani kwetu!’’
‘’Eti?!’’
‘’We bwana ni kiziwi au kitu gani? Leo kuna ngoma bwana! ‘mnanda!’ nyumbani kwetu!’’
‘’Kwa hiyo nije?’’
‘’Unauliza majibu? Njoo!’’
Nikaenda. Niliyoyakuta yalinitoa jasho! Havijawa alikuwa amenipokea vizuri japokuwa hakutaka kuwa karibu na mimi, kila niliposema nimsogelee aliongea na mimi kwa mkato mkato tu kabla ya kunitaka radhi na kutoweka!
Una nini leo? Nilikuwa nimekumbuka kumuuliza hivi kwenye sms kupitia simu ya mkononi mara kadhaa, pasipo kupata majibu. Ngoma ilipozimwa kwa mara ya kwanza na watu kwenda kupoza makoo mie nilibakia mpweke nikitandikwa na baridi.
Ilipozimwa mara ya pili hali kadhalika.
Mara ya tatu nikiwa nimeanza kupandwa na ghadhabu ndipo yule mpiga ngoma mmoja ambae nilikuwa nimekaa karibu naye na ambae alianza kuwa rafiki yangu aliponiambia kitu kilichoniogopesha kama sio kunitisha. Hii ilikuwa baada ya yeye kuniuliza, nami kumtajia Havijawa.
“Kaka bora utafute mwanamke haraka sana!’’
‘’Mmh hilo nalijua, ndio maana namsubiria Havijawa’’
‘’Huyo hakufai kwa sasa hivi huyo ni moto!’’
Nikashtuka na kumuuliza kwa pupa ‘’Una maana gani?!”
‘’Havijawa ni mke wa mtu!’’
‘’Eti?” Nikasikia nanga zinapaa.
‘’Enhe na mwenyewe keshajua kuwa kuna doezi linalomuibia mali zake ambalo ni lilevi la ngoma ingawa sio lizaramo! Kwa taarifa yako Ngoma hii ni mtego! Mnasubiriwa wewe na Havijawa tu mwende mkaneng’eneke mkamatwe wewe ugeuzwe asusa, baadae mshikaki ili liwe fundisho kwa wengine, ndio maana nakwambia tafuta mwanamke mwingine!’’
Yakaniingia! Nikaweza kuunganisha moja na moja na kupata mbili, baadae kama mpelelezi niliyefundwa vyema, nikafanya mbili na mbili na kupata nne. Havijawa alijua huu ni mtego na hakutaka kunitosa ndio maana akawa mbali.
Akashindwa hata kujibu meseji zangu. Sikujua yuko wapi kwa sasa na sikujua yuko katika hali gani. May be yuko katika kibano kilichopatiliza, na kama hivyo ndivyo basi hata simu yangu kuendelea kuwa hewani ni kosa, nikaizima.
Nikamdodosa rafiki yangu mila na taratibu za pale nae akanifahamisha kuwa adhabu ya ugoni ni kifo. Nikazidi kuogopa ngoma ikiendelea yule bwana akazidi kuwa rafiki yangu.
Ilipozimwa kwa mara ya nne na ya mwisho, Havijawa akatokea! Hakuwa na furaha na bashasha kama ilivyo ada yake. Sura yake ilisawijika na kupoteza nuru, yaelekea alikuwa akilia kwa muda mefu.
Nikijua mtego ndio unakaribia kufyatuka, sikumgusa!
Badala yake nilikwapua mwanamke mwingine nikatokomea nae migombani na kwenda kuneng’eneka nae, Nikamuacha Havijawa pale pale uwanjani. Mwanamke niliyemchukua hakuwa haba, alikuwa bora kwa kila hali.
Nikamuuliza kama ameolewa akasema bado, nikamuomba niwe mgeni wake kwa siku hiyo akakubali. Sikurudi uwanjani nikaenda kulala kwa mwanamke huyu mpya.
**Ni mambo juu ya mambo katika NILAMBE HUMOHUMO……..nini kitajiri…….HAVIJAWA!!!!!!
[5/7, 22:38] ‪+255 753 879 215‬: chombezo: nilambe humohumo
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA SABA
Nikijua mtego ndio unakaribia kufyatuka, sikumgusa!
Badala yake nilikwapua mwanamke mwingine nikatokomea nae migombani na kwenda kuneng’eneka nae, Nikamuacha Havijawa pale pale uwanjani. Mwanamke niliyemchukua hakuwa haba, alikuwa bora kwa kila hali.
Nikamuuliza kama ameolewa akasema bado, nikamuomba niwe mgeni wake kwa siku hiyo akakubali. Sikurudi uwanjani nikaenda kulala kwa mwanamke huyu mpya.
Asubuhi na mapema nilikuwa ndani ya gari nikielekea Daresalaam.
Ukawa mwisho wa kuwasiliana na Havijawa. Ikawa mwanzo wa mawasiliano na yule mpiga ngoma, nikaendelea kuhudhuria katika ngoma hata iwe wapi. Ni hapa nilipojua ni kwanini ngoma inapendwa sana uzaramuni.
Nami nikawa mfuasi mtiifu na mkamilifu wa ngoma!.
* * *
Naam, niliyainua tena macho yangu na kuutazama ubao wa matangazo No! Ubao wa matokeo. Nao haukunidanganya. Uliniambia tena kama unaonidhihaki. Kwamba nilipata alama F katika mitihani yangu ya mwisho pale chuoni.
Kwa sekunde kadhaa niliduwaa nikiwa siuoni ubao huo wa matokeo sawasawa. Akilini niliona kama kitu cha kawaida huku nikitabasamu kiwazanga kama niliyefurahishwa na matokeo yale. Wenzangu wachache niliofeli pamoja nao walikuwa wakilia. Wengine wakisikitika.
Wachache waliokuwa na roho ya paka wakaniangalia kwa mshangao.
‘’He Ibra anacheka!” Mmoja aliropoka ’’Wakati amefeli vibaya!” mwingine akadakia ‘’Lazima kuna analotarajia sio bure!” Mwingine akahitimisha.
Shamsa alikuwa miongoni mwa wanafunzi wachache waliofanya vizuri sana kiasi cha kupata A+. Wakati huu alikuwa hajiwezi kwa furaha machozi yakimtoka hovyo asiyaamini macho yake.
Wengine wakashangaa, aliyefeli anacheka, aliefaulu analia! Akimu alikuwa mbali sana, alikuwa na alama za wastani hazikuwa mbaya wala nzuri sana alipata grade C, yeye pia alikuwa akisononeka. Alitaka apate grade A!
Wabongo kwa kutoridhika? Mie niliyepata mswaki je?
Kadiri muda ulivyokuwa ukipita ndivyo nami nilivyokuwa nikipambazukiwa na ukweli, ukweli kwamba nimefeli vibaya! Ukweli kwamba miaka yangu mitatu pale chuoni ilikuwa bure, bure kabisa! Bure kwa maana ya kwenda na maji.
Nikawafikiria wazazi wangu waliopoteza mamilioni kwa malaki ya shilingi kunisomesha mwana wao. Kunisomesha nisihangaike na maisha kwa namna itakayoikwaza mioyo yao na kuwasononesha.
Kunisomesha ili nije niwatunze wao mara nguvu zitakapowaishia. Kunisomesha ili nije nitimize wajibu wangu kama binadamu wa kuisaidia jamii kupata unafuu katika sekta fulani. Kunisomesha… kunisomesha…! Niliendelea kutafakari pasipo kupata majibu.
Sikuwa nimewahi kufeli kwa mtindo huu toka nilipoanza elimu ya Awali, chekechea kwa maana halisi. Nikafuatia ile ya msingi hadi sekondari! Lakini leo… My God nitawaambia nini wazazi wangu?
Chozi la uchungu likateleza na kuanguka shavuni.
Roho na moyo vikaniuma kwa pamoja na kuufanya mwili wangu kuwa handaki la mateso kwa muda.
Nikiwa katika hali hii mwili ulitikisika na kutetemeka kwa nguvu wakati mawimbi ya kilio yakitoka kifuani mwangu na kunifanya nitoe mlio mithili ya gari ndogo yenye mzigo mkubwa inayopanda mlima na kushindwa kuumaliza.
Nililia na kulia na kulia! ’’Hatimae mapenzi yameniliza!” Niliwaza kwa uchungu nikiendelea kulia kwa nguvu.
‘’Ibra… Ibra… Ibra!’’
Sauti nzuri nzuri ikapasua anga, ikakizidi kilio changu na kuzifikia mboni za masikio yangu, mwito huu ulienda sambamba na mtikiso wa bega langu la kushoto. Sio siri ulikuwa mguso wa faraja. Nikainua uso na kumwangalia huyu aliyeingia chumbani kwangu bila hodi na kujipa mamlaka ya kuniita.
Ana kwa ana na Shamsa Nuhu, msichana wa maisha yangu!
”Pole!’’ Akaniambia kwa upole hali akinihurumia.
Huruma hii ikanifanya niangue kilio upya. Kilio cha nguvu, kilio cha simanzi. Nililia haswa, nililia mno. Ukweli nililia kweli kweli. Shamsa alijaribu kunibembeleza kwa muda mfupi akashindwa na kuniacha nilie. Nadhani aliniacha nafasi nimalize machungu niliyo nayo moyoni.
Na niliyamaliza.
Ilikuwa baadae sana niliponyamaza na kupitiwa na usingizi moja kwa moja. Shamsa aliniamsha jioni kabisa nikaamka! Alikuwa ndani ya vazi la usiku! Mwili wake mzuri ulionekana vizuri zaidi ndani ya vazi lile la kulalia.
‘’Amka ukaoge!’’ Akaniambia, nikamtazama kwa matamanio.
‘’Nataka nikutoe out!‘’ Akaongezea akitabasamu alipoona namwangalia tu pasipo kuinuka. Nikainuka, nikajinyoosha nikatwaa taulo, mswaki pamwe na sabuni na kuelekea bafuni.
Nilipotoka yeye, akaingia.
Akanichagulia nguo za kuvaa alipotoka bafuni, nae akavaa za kwake ambazo zilikuwa katika mkoba aliokuja nao. Tulipokuwa tayari akainua simu akabofya nambari kadhaa na kuipeleka sikioni. Akatamka neno moja tu
“Unaweza kuja!’’ Halafu akakata simu.
“Huyo ni Tax Drive ambae huwa anapaki gari lake hapo nje. Anaitwa Sudi’’ akaniambia. Nilimjua vizuri sana dereva huyo na nilikuwa nikimtumia sana mara kwa mara katika harakati zangu.
‘’Hutaki nikutoe out?’’ akaniuliza tena
‘’Hata kama sitaki unafikiri mbele yako nitakuwa na ubavu wa kukataa?’’ Nikamwambia kiutani, akatahayari na kunikabili tena.
‘’Ina maana hutaki?’’
‘’Hapana nataka sana, fursa hii nimeililia kitambo, nasikitika imekuja wakati mbaya! Wakati nimefeli!’’
‘’Usijali, kupanda na kushuka ni mojawapo ya safari za kimaisha, na ili mwanadamu ukamilike kabla hujaumbika haswa ni lazima uzipitie!‘’ Akatua. Nikamuuliza.
“Kuumbika haswa?! Unamaana gani?”
‘’Umesahau ule msemo?”
‘’Msemo gani?’’
‘’Hujafa hujaumbika!’’
‘’Naufahamu, kwa hiyo una maana kuumbika hasa ni kufa siyo?’’
‘’Yes!’’
Akajibu kwa bashasha. Nikatabasamu naye akatabasamu. Tukatengeneza njozi mbili adimu sana. Nilipotaka kusema kitu, akaangalia simu na kuniambia “Sudi yuko nje!”
‘’Mie nipo tayari!”
Akaukwapua mkoba wake toka pale sofani na kuutia begani, nikauchukua ufunguo wa chumba nikafunga mlango na kutoka.
‘’Kwa nini uliniuliza vile?’’ Nikamuuliza tukitoka nje.
‘’Vipi?!”
‘’Kwamba sitaki nikutoe out?’’
‘’Ulionekana kuwa na fikara sana Ibra. Sijui ulikuwa ukifikiria nini’’
Tukaifikia gari, tukaingia nyuma na kumsalimia Sudi, akawasha gari na kumuuliza Shamsa ‘’Haya niambie wapi Shamsa?’’
‘’Sudi bwana, unakuwa kama sio Born Town?! Nimekwambia sehemu yoyote tulivu!’’
“Sehemu tulivu ziko nyingi Shamsa! Kuna hoteli za kitalii, majumba ya kifahari na makumbusho, fukwe na n.k.!”
Ukazuka mjadala mfupi wa wapi atupeleke kutokea pale chang’ombe. Mjadala ambao ulimalizika kwa kuamuliwa atupeleke Coco beach. Hii ni kwa vile watu wangekuwa wachache sana kwa kuwa sio mwisho wa wiki. Hivyo iliaminika kule tungeweza kupata utulivu wa haja.
Tukaondoka.
Njiani nilimwambia Shamsa kuwa chanzo cha fikara zangu kule bwenini ni kumfikiria yeye, kwamba aliwezaje kuingia katika bweni la wanaume, akapata hadi ujasiri wa kubadili na kuvaa night dress achilia mbali kuniandalia maji kana kwamba nilikuwa mpenzi kama sio mume wake!
Shamsa akatabasamu kabla hajaniambia kuwa aliamua kuhamishia kambi katika chumba changu kwa muda kabla ya kunitoa out ili awe pamoja na mimi katika kipindi hiki kigumu.
Ilitosha! Alikuwa kama amenitonesha donda upya. Sura yangu ikasawijika na kupoteza nuru, alipoligundua hili akabadili mada haraka na niliporejea katika mood yangu, hatukuzungumza tena hadi tulipofika Coco Beach.
* * *
‘ ’Katika mambo yote, hili sikulitarajia!’’ Shamsa alianza taratibu mara tu tulipochagua mahala patulivu pa’ kuketi pale Coco Beach na kufungua vinywaji vyetu vya kopo, ‘’Naapa hili sikulitarajia kabisa!”
Sauti yake ilikuwa ndogo yenye mchanganyiko wa mizizimo ya upendo wa dhati, huruma pamoja na uchungu. Machozi pia yalikuwa yakitafuta njia katika kingo za macho yake. Kwa kila hali alikuwa katika majonzi!
‘’Ibra niliyekuamini, Ibra niliyekuthamini, Ibra niliyekutegemea ukweli wa kukutegemea! Bado siamini dear! Kwanini ukafanya hivi? Enhe kwa nini Ibra?’’
Machozi yakamtoka.
Moyo wangu ukazizima kwa simanzi ingawa nilihisi nitakuwa namuumiza, nikajikakamua na kumuuliza
‘’Kufanya nini Shamsa?”
Akageuka na kuniangalia kwa mshangao, akafuta machozi na kuniuliza,
‘’Bado hujui tu? Hujui ulichofanya?! My God are you serious Ibra?”
‘’Sijui!” Nikajibu na kuapia
“Mungu mmoja sijui!! Ningejua nisingeuliza!” Nikatua.
Akaendelea kunitazama nikaona kama hanielewi, nikamsogelea na kumshika mkono kwa upendo uliotukuka, “Shamsa?” Nikaita taratibu nikingali nimeushikiria mkono wake
“Mimi ni miongoni mwa watu wachache sana wasiopenda kuwakwaza wenzao hasa wewe! Kuendelea kunilaumu kana kwamba nimeua bila kunieleza nilililolifanya, hunitendei haki Shamsa! Unaniweka katika kimuhemuhe ambacho kinanifanya nishindwe kujua nastahili kuwemo katika fungu gani kati ya wastaarabu na washenzi. Tafadhali niambie, niambie tu usihofu!’’
Shamsa akashusha pumzi na kuzivuta tena akauliza
“Kwa hiyo hujafanya kitu?’’
‘’Kitu gani? kwa kadiri ninavyokumbuka na kufahamu, sijafanya lolote la kumchukiza mtu yeyote! Na kama nilivyokwambia sipendi kumkwaza mtu!’’
‘’Kweli!?’’
‘’Kabisa!’’
‘’Sasa kule Chuoni ulikuwa unalia nini?”
Akili ikazibuka.
Macho yakazibuka pia na fahamu kufunguka. Masikio, moyo na hata vinyweleo vya mwili ambavyo wakati huu vilikuwa vikikiruhusu kijasho chembamba kupenya na kuteleza juu ya paji la uso wangu, juu ya mashavu, juu ya mikono, juu ya kila mahali, sasa nikaelewa! Kwamba Shamsa alikuwa akizungumzia kufeli kwangu.
ITAENDELEA

CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA nane
“Mimi ni miongoni mwa watu wachache sana wasiopenda kuwakwaza wenzao hasa wewe! Kuendelea kunilaumu kana kwamba nimeua bila kunieleza nilililolifanya, hunitendei haki Shamsa! Unaniweka katika kimuhemuhe ambacho kinanifanya nishindwe kujua nastahili kuwemo katika fungu gani kati ya wastaarabu na washenzi. Tafadhali niambie, niambie tu usihofu!’’
Shamsa akashusha pumzi na kuzivuta tena akauliza
“Kwa hiyo hujafanya kitu?’’
‘’Kitu gani? kwa kadiri ninavyokumbuka na kufahamu, sijafanya lolote la kumchukiza mtu yeyote! Na kama nilivyokwambia sipendi kumkwaza mtu!’’
‘’Kweli!?’’
‘’Kabisa!’’
‘’Sasa kule Chuoni ulikuwa unalia nini?”
Akili ikazibuka.
Macho yakazibuka pia na fahamu kufunguka. Masikio, moyo na hata vinyweleo vya mwili ambavyo wakati huu vilikuwa vikikiruhusu kijasho chembamba kupenya na kuteleza juu ya paji la uso wangu, juu ya mashavu, juu ya mikono, juu ya kila mahali, sasa nikaelewa! Kwamba Shamsa alikuwa akizungumzia kufeli kwangu.
‘’Machozi yakafurika upya katika macho yangu. Shamsa alikuwa amenitonesha donda. Amegusa mahali ambapo sikutaka paguswe. Halafu kilio kidogo kikanianguka. Nilijitahidi kukizuia mpaka nikafaulu.
‘’Mapenzi Shamsa!” Nikasema huku nikipenga kamasi na kufuta machozi
‘’Mapenzi?!” Shamsa hakuamini!.
“Yeah, Mapenzi! Naweza kusema ni mapenzi kwa kila hali ndiyo yaliyonifanya nifeli. Ukweli huu huniumiza zaidi. Huniumiza kwa vile ni ukweli unaoashiria upumbavu ulikithiri nilionao. Ni upumbavu tu maana ujinga unatibika, upumbavu hautibiki!”
‘’Bado sijakuelewa!’’ Alikuwa Shamsa kwa upole kabisa.
‘’Ni mapenzi Shamsa, nilikupenda sana mfano wa maua, ninakupenda hata sasa na nitaendelea kukupenda daima!’’
‘’Kunipenda huko ndio kukakufanya ufeli?’’
Nikatikisa kichwa juu na chini kukubali.
‘’Si kweli!’’ Akasema kwa sauti thabiti nae akitikisa kichwa kushoto na kulia kukataa ‘’Si kweli hata kidogo!‘’ Akaongezea na kuendelea ‘’Nahisi unajaribu kunificha kama sio kunichezea shere. Naomba uniambie ukweli Ibra, ili niangalie namna ya kukusaidia tafadhali!’’
Sikujua nimwambie ukweli upi
‘’Mbona hata mie ninakupenda sana na nimefaulu vizuri tu? Mbona nilikuwa nikikufikiria na kutamani kuwa nawe mahala kama hapa nikila raha na kustarehe na wewe? Mimi nina nini niweze na wewe una nini ushindwe? Hapana niambie ukweli Ibra’’
Akatua. Furaha na bashasha vikiuvaa moyo akili na mwili wangu kwa zamu. Shamsa ananipenda! Ulikuwa ukweli ulionitoa machozi ya furaha, machozi ya upendo! Upendo wa dhati. Upendo uliotukuka!
‘’Shamsa’’ Nikaita nisiamini masikio yangu, “Ni kweli unanipenda?!’’
“Ni kweli Ibra, nakupenda sana! Nakupenda mno! Nakupenda kuliko unavyofikiria. VETA nzima watu wa Compass wanajua jinsi nilivyokufa na kuoza juu yako, Najua hata wewe unanipenda tu ila hujiamini na pengine unanipenda kupita kiasi, kiasi umekuwa kama unaniogopa uongo?’’
Akasuta! Ulikuwa ukweli, ukweli halisi. Ukweli Original kama alitegemea kunisuta kule kungenifanya nione haya kama sio aibu, alikosea! Badala yake nilitahayari na kuinamisha uso kwa fedheha, nilipoinua bado alikuwa akinitazama. Nikanong’ona.
“I love you Shamsa!’’
‘’I love you too Ibra!’’
Moyo wangu ukachanua kwa raha, akili ikapigwa dafrao na furaha huku mate ya uchu kama sio utamu yakijaa mdomoni. Nikamsogelea akanisogelea! Tukakutana katikati na kukumbatiana kwa nguvu na kudumu katika hali hiyo kwa muda.
Hatimaye! Nikawaza kwa furaha nikingali nimekishikilia kifua chake Hatimaye Shamsa ameanguka mikononi mwangu, Ananipenda! Kwa mara ya kwanza nimepata hifadhi katika moyo wa mwanamke!’
Ilikuwa ajabu na kweli.
Tulipoachiana matendo halisi ya mapenzi yalifuatia. Tulilishana, tukacheza na kuogelea pamoja. Tulipotosheka tukarudi mchangani tena. Shamsa akaniita kwa upendo uliotukuka. Sauti yake ilikuwa tamu vibaya sana
“Ibra mpenzi?”
‘’Naam!’’
‘’Bado hujanishibisha dear!’’
‘’Lakini biskuti, Chocolate na Ice cream hazishibishi!’’
Akatabasamu, vishimo vikatokea hapa na pale katika mashavu yake na kidevuni.
“Unanielewa vizuri sana Ibra! Ni kuhusu kufelishwa na mapenzi! Hebu niambie ukweli!’’
‘’Ni ukweli mpenzi!’’
Nikamwambia, kabla sijaanza kumsimulia safari ya maisha yangu toka Shule ya Msingi, Sekondary, hadi pale VETA. Nikamwambia jinsi nilivyokuwa nampenda na namna nilivyoshindwa kumkabili licha ya yeye kunionyesha dalili za waziwazi.
Nikamwambia pia namna nilivyopateua uwanja wa fisi kama mahala mbadala, ushauri niliopewa na Akimu baadae ambapo nilijikuta nikianguka tena katika ngoma za kizaramo. Nikashindwa kujisomea, kufuatilia masomo na kuendekeza ngono, mpaka ninamaliza kusimulia, Shamsa alikuwa bado ana hamu ya kunisikiliza.
“Huo ndio mkasa wangu Shamsa! Unadhani kitu gani naweza kusema kimenifelisha kama sio mapenzi?”
“Duh! Pole sana Ibra una bonge la mkasa! Mkasa ambao umeusisimua moyo wangu katika namna inayonifanya nikuogope! Nikuulize swali jingine?”
‘’Uliza tu laaziz!”
‘’Mbona siku ile nilipokuuliza kama unanipenda ulikataa kata kata?”
Nikatabasamu, “Mbona hilo umeshalijibu katika maelezo yako? Shamsa mpenzi nilikuwa sijiamini, nilikuwa nakuogopa! Akili zako, uzuri na uwezo wako kifedha vilinifanya niufyate, nikawa nakufa kiofisa tai shingoni!”
Akacheka. Nami nikacheka. Ikawa raha juu ya raha
‘’Siku nyingine usiogope ukubwa wa samaki! Uliza bei!’’ Akasema kati kati ya kicheko, tukacheka zaidi.
‘’Lakini kufeli kwako hakutokani na mapenzi! Naweza kusema hivyo!’’ akaniambia baadae kwa uhakika kabisa.
‘’Kumbe kunatokana na nini na au nikuiteje?”
‘’Kunatokana na tamaa kali ya ngono na niite tu umalaya, kwa sababu hata ngoma unazozizingizia huzifuati zenyewe! Hii ni kwa vile hujui kucheza kabisa, unayo ifuata ni ile mijimama na kile kipindi muhimu cha kuzima ngoma uongo?”
Nikashindwa kumjibu.
“Mapenzi ya kweli ni zaidi ya ngono Ibra! Unadhani ni kwanini mimi imeniuma wewe kufeli? Kwanini nilikuja kukufariji katika bweni lenu? kwanini nimekuleta huku?! Sababu ni moja tu Ibra wangu. MAPENZI! Ni mapenzi ya dhati niliyo nayo kwako, hilo tu!” Akahitimisha.
Alikuwa sahihi.
Tuliendelea kufurahi na kula maisha pale ufukweni hata msiba wote wa kufeli ukaondoka. Nilichogundua tu ni kuwa Shamsa alikuwa mwangalifu sana wakati huu. Hakujiachia sana kama alivyokuwa akijiachia wakati ule kabla sijampa full story yangu.
Jioni tuliondoka na kuelekea mabwenini.
Siku ya pili yake tulikuwa kwenye hoteli moja ya kitalii huko baada ya maongezi yetu ya kawaida ndipo alipo nitwanga swali..
‘’Sasa Ibra Chuo ndio tumemaliza, baada ya kutunukiwa shahada zetu yatupasa kuondoka. Mwenzangu una mipango gani? Mie mwenzio Mzee ameniunganishia Tanesco na mwakani nitaajiriwa!’’
Swali zito. Nikachoka kabisa, dakika zikayoyoma pasipo kujibu
“Sikiliza Ibra, kufeli masomo sio kufeli maisha. Kwa hiyo usifikirie sana kuhusu hilo, mimi nina ushauri mzuri kwako!’’ Akatua na kunitazama.
‘’Enhe upi?’’
‘’Kwanza nataka mimi na wewe tuoane unasemaje?”
Sura yangu ikachanua mithili ya maua katika jua la asubuhi. Nikamwambia, “Sina kipingamizi Shamsa nakupenda mno!”
Naye akatabasamu kufuatia kauli yangu hii. Akasema.
‘’Basi kama hivyo ndivyo, huna budi kujifunza udereva haraka sana, ili nimwambie mzee akuajiri katika kampuni yake. Nitamshauri akulipe mshahara mzuri sana unaonaje?”
‘’Nitashukuru kupita kiasi!” Nikasema haraka nikiwaza hata kama Lady Jay dee ataniita mwanaume kama binti na Bushoke kuniita Mume bwege shauri yao! Nitafanyaje hali nimesha ulowanya?” Nikakubali.
Lakini kabla haya hayajafanyika inakubidi uanze taratibu za uchumba na kwa hili hatuna budi kwenda kupima afya zetu kwanza ili ulete barua ya posa wakati huo huo ukianza Driving School! Sawa mpenzi?!”
***HE MAMBO YA KUPIMA TENAAA…….IBRA ANALOOOO!!!!

MTUNZI: HUSS EIN WAMAYWA
SEHEMU YA MWISHO
‘’Nitashukuru kupita kiasi!” Nikasema haraka nikiwaza hata kama Lady Jay dee ataniita mwanaume kama binti na Bushoke kuniita Mume bwege shauri yao! Nitafanyaje hali nimesha ulowanya?” Nikakubali.
Lakini kabla haya hayajafanyika inakubidi uanze taratibu za uchumba na kwa hili hatuna budi kwenda kupima afya zetu kwanza ili ulete barua ya posa wakati huo huo ukianza Driving School! Sawa mpenzi?!”
Nikasikia kama nimepigwa na nyundo kichwani! Ule msururu wa wanawake niliotembea nao toka Uwanja wa fisi, Songambele, Gobbah Sotele, Msangule, Msanga na vijiji vingine hamsini kidogo utanisalimisha kweli?
‘’Mbona hivyo Ibra?” Shamsa akanigundua “Au hukuvaa kondomu vizuri? Si umeniambia ulihakikisha unajilinda?’’
‘’Ni kweli! Nikajibalaguza, sura yangu ikavaa tabasamu bandia.
“Nilikuwa makini mno!’’ Nikaongezea.
‘’Sasa mbona unaogopa?’’
‘’Siogopi nina hofu kidogo tu! Unajua tena kuna Saloon, Hospital, Ajali na kadhalika. Kote huko unaweza kuambukizwa!’’
“Jiamini Ibra!” Akasema kwa karaha, “Kumbuka kutojiamini huko ndio kumekufanya ufeli na kuharibu ndoto zako!’’
‘’Kwa… kwa… kwani nilazima sana kupima? Si ningeleta tu hiyo barua ya posa na … na …!” Uoga ulinisumbua. Wale wanawake wa kule fisi afadhali, lakini kule katika ngoma, thubutu! Nilitumia kondomu mara chache sana!
‘’Ni lazima Ibra!” Shamsa akanikata kalmia na kuendelea.
“Mimi na wewe tunataka kufunga pingu za maisha zitakazofunguliwa na kifo, tunataka kutengeneza familia bora yenye afya furaha na amani, tunataka kuanza kuyaona maisha katika mwanga bora, na hii inaanza na kujua afya zetu Ibra. Ujue mimi na wewe tumekutana VETA, huko nyuma kila mtu amekuwa na majangusho yake, na katika majangusho hayo, lolote laweza kuwa limetokea. Hapana Ibra, kupima ni lazima dia!”
Sikuwa na jinsi. Kwa kila hali nilikuwa nimeshikwa. Kadiri nilivyotaka kuruka viunzi ndivyo alivyonibana kwa hoja hata nikakosa la kusema. Mwishoe nikaamua, “Acha niende nikajue moja kama kusuka au kunyoa,
Nikamkubalia, akafurahi na kunipongeza kwa kunikumbatia.
Hatukwenda kupima mara moja tu, zilipita siku za kutosha mpaka tukahitimu na kutunukiwa. Baadae alinipeleka kwao na kunitambulisha kwa wazazi wake kuwa nilikuwa Boy friend wake,
Wazee wake walikuwa na uwezo kweli, yale mandhari na ile nyumba yao mpaka sasa sijaiona mfano wake. Tena walikuwa wakarimu kweli. Tukajadiliana nao sana kuhusu maisha na mafanikio.
Siku iliyofuata ndio tukaenda Angaza
Tulikutana na akina dada wazuri wakatupa ushauri wa kutosha wa Ukimwi. Wenyewe wanaita ushauri nasaha. Tuliposema tumeelewa, tukaingia ndani na kupimwa!
Kabla ya kupewa majibu, tukapewa ushauri nasaha mwingine! Ushauri wa kina. Tuliposema tuko tayari, tukapewa majibu yetu. Ikawa kitu na box!! Naam! Nilikuwa nimeathirika wakati Shamsa alikuwa amesalimika.
‘’Shamsa hakuyaamini masikio yake ingawa mimi niliyatarajia hayo, akauliza mara mbili mbili kama daktari alikuwa amekosea au lah! Jibu alilopata lilikuwa lile lile! Akavunjika moyo vibaya,
Akageuka na kuniangalia kwa majonzi, machozi yakateleza juu ya mashavu yangu. Akanisogelea na kunifuta, bado yaliendelea kunitoka. Moyo ukinidhihaki kwamba huu ulikuwa mwisho wa kila kitu baina yangu na Shamsa, mwisho wa ahadi! Mwisho wa mikakati ya kuelekea katika nchi ya maziwa na asali! Kwanini machozi yasinitoke? Kwanini?!
Shamsa akaniinua taratibu, tukatoka nje huku nikiwa sina nguvu hata moja . Naam! Malipo ya ngono ni ukimwi.
Hatua chache kabla ya kutoka nje ya jengo hilo, nikashindwa kabisa kutembea! Nikauegemea ukingo wa nguzo, Shamsa akalitambua hilo, akajua ninahitaji faraja faraja ya kweli
‘’Taratibu akajivuta maungoni mwangu na kunikumbatia kwa nguvu huku maneno ya faraja yakimtoka ‘’Huu sio mwisho wa maisha Ibra!’’ akasema mara nyingi na kuongeza “Wapo watu waliokuwa na matatizo lukuki na bado wakafaulu, usife moyo…! ’’
Kana kwamba hiyo haitoshi, akaanza kunipapasa hapa na pale huku pia akiruhusu mikono yangu itembee katika kiuno chake na nyonga kwa ujumla.
Tukaendelea kuchezeana pale kwa muda huku kucha za vidole vyake zikitambaa katika shingo yangu na kunipa faraja iliyo pitiliza, kutahamaki mikono yangu ikarukia katika matiti yake, ‘
Akaguna.
Akaacha kunichezea shingoni na kurudi kunikumbatia kwa nguvu tena. Mikono yangu ikashindwa kufanya chochote maana ilibanwa barabara katikati ya kifua changu na cha Shamsa.
Nyuso zetu zilibakiza sentmita chache sana kukutana, wakati huu tulikuwa tukibadilishana pumzi. Hata mapigo ya mioyo yetu tuliweza kuyahisi. Kila mmoja aliyahisi ya mwenzake,
Nikafunua mdomo kumuomba anipe ulimi!
Akanielewa. Akasogea taratibu, ikiwa imebaki sentmita tatu hivi midomo yetu iungane na ndimi kusalimiana, Shamsa akashituka na kurudi nyuma ,
‘’I m so sorry Ibra, Samahani mpenzi! Akanong’ona akinikumbatia kwa nguvu.
‘’Najua!’’ nikasema kwa jazba ‘’Najua kama nimeathirika lakini kidogo tu!’’
‘’Haitawezekana Ibra! Unaweza kuniambukiza, kumbuka nina watu wanaonitegemea wazazi na ndugu zangu waliojikusuru na kunilipia kozi yangu yote ili nije kuwa msaada kwao . Niamini dear kama sio hilo ningekuruhusu tu unilambe humo humo mdomoni!’’
‘’Shamsa ajue mimi ni wa kufa tu kwa sasa nahitaji faraja, tafadhali mara moja tu ukimwi hauambukizwi kwa kunyonyana ndimi!’’
‘’Sio kweli Ibra, asilimia kadhaa ya virusi hivyo huishi kwenye mate pia!’’
‘’Kwa hiyo unananinyanyapaa Shamsa?” Nikafoka nikishindwa kuidhibiti akili yangu “Wote waninyanyapae, hata wewe Shamsa? Nani basi atakayenipa upendo! Nani atakaye nijali, nani atakayenifariji nani atakaye…Oooh! Mungu wangu mbona umeniacha?!!’’ Nililia kwa uchumgu msisimko wote ulioletwa na Shamsa ukitoweka.
‘’Hapana Ibra!” Alikuwa Shamsa kwa sauti thabiti, sauti yenye mamlaka, sauti inayobembeleza, kusihi na kushawishi. Sauti tamu ajabu! Akaendelea.
“Hapana mpenzi wangu! Hapana! Amini kwamba ninakupenda kwa dhati, ninakupenda ukweli wa kukupenda, tena ninakupenda kwa moyo wangu wote.
Na ili kulinda heshima yako sitaolewa wala kuwa na mpenzi mwingine maishani ila wewe tu, potelea mbali kama hatutafanya mapenzi daima nitaishi maisha ya kitawa mpaka hapo muumba atakaponichukua! Nakuahidi hilo na ninakuapia hii ni ahadi ya dhati kabisa toka moyoni hasa!”
Nikamtazama na kutabasamu, akanifuta machozi.
Nilijua hii ni kauli tu kama kauli zingine. Kauli za wanasiasa, kauli ya faraja, kauli kutoka kwa aliyesalimika, kwenda kwa aliyeathirika. Hata siku moja sikutaka kuyaamini kwamba atayatekeleza yote aliyonihubiria! Ili tu kunilindia heshima! Heshima gani niliyo nayo kwake? kwa thamani ipi? Kwa kipi cha ajabu nilichomfanyia hata anikumbuke hivyo?
‘’Nimempa nini hata ayafanye hayo eti tu kumlindia heshima mtu ambae miaka mitatu kama sio minne ijayo atakuwa chini ya ardhi futi saba huku tani kadha wa kadha za mchanga zikiwa tele juu yake.
Nikazipokea! Kumbe ningefanya nini? Na ili kutomvunja moyo nikamwambia, “Nitafurahi sana ikiwa utatimiza hayo uyanenayo!’’ Shamsa akaniangalia tena na kutabasamu.
‘’Tabasamu zuri ajabu akaniambia.
‘’Kwa uwezo wa mola Hakika nitayatimiza!’’
Akashuka ngazi kabla hatujajipakia kwenye taxi ya Sudi na kutokomea!
MWISHO.

 SOMA STORY FUPI YA MAPENZI YA KUHUZUNISHA YENYE MAFUNZO KWENU HASA HASA WAKINA DADA. NI STORY YA KWELI KABISA
"Nilipoingia katika mahusiano naye nilimuamini, nikampa kila kitu nilichoweza. Nakumbuka enzi zile 
nyumbani tulikuwa tuna ng’ombe, niliiba maziwa kila siku na kumpelekea kwao. Akanenepa!! Penzi letu 
likawa huru alipoanza maisha yake mwenyewe. Sikuwa najua lolote kuhusu mapenzi. Alinifundisha.
Nikaegemeza maisha yangu yote kwake. Akanifanya nikawa mtumwa wa ngono kila nikienda chumbani 
kwake. Kama haikutosha sasa akaanza kunifundisha kunywa pombe. Niliamini kuwa ndiye mume wangu 
mtarajiwa, kwa nini nikatae? Nilimkubalia kila kitu.
Alinilazimisha ngono hata nilipokuwa katika siku zangu. Kweli nilikuwa msomi na niliyajua madhara ya 
kufanya hivyo lakini sikutaka kumuudhi huyo niliyeamini kuwa ni mume wangu. Nilipenda tutumie kinga 
lakini aliipinga sana. 
Nikapata mimba ya kwanza!! Hakuwa na pesa lakini alinilazimisha niitoe. Nikaiba pesa nyumbani 
nikafanyaalivyotaka. Kwa mara yakwanza nika toa mimba. Haikuniuma sana!! Niliamini kuwa ni yeye 
atakuja kunioa na atanifichia aibu hii.
Nilitegemea sasa tutaanza kutumia kinga. Lakini hapana haikuwa hivyo. Aliendelea kunilaghai. Tayari 
aliujua udhaifu wangu. Alinishika hapa na pale. Nikishtuka tayari amefanya anavyojua. Pombe kidogo 
na nyingine kidogo. Nikazoea lakini nikawa na wahi kulewa. Akautumia udhaifu huu kunifanyia jambo 
baya lililonifanya niandike haya kwako. Akaniingilia kinyume na maumbile. Alinilawiti!! Nilishindwa 
kumshtaki popote. Nikavumilia kwa kuwa alikuwa mume wangu mtarajiwa. Mume asiyejulikana hata kwa 
wazazi.
Mchezo ule ukaendelea. Akajitetea eti hataki nipate mimba tena, hivyo hiyo ni mbinu mbadala. Najuta 
kumuamini!! Lakini huyo alikuwa mume wangu. Miaka ikapita, ule urembo wangu niliozoea kuuona 
katika kioo ukatoweka, simu za mara kwa mara kutoka kwake zikatoweka, akawa mkali sana kwangu. 
Hakutaka niende kwake. Wakati huo nilikuwa nasoma chuo. Pesa ya mkopo ikitoka ananitafuta na 
tunakuwa marafiki tena. Anasema ananipenda na atanioa. Ananilewesha na kunitumia kinyume na 
maumbile. Pesa ikiisha na mapenzi yanaisha nabaki mwenyewe katika msoto.
Sasa akaanza kubadilisha wasichana waziwazi. Ningesema nini mimi? Ninajua alishindwa kusema neno 
moja tu. Tuachane!! Nilijuatayari ameniacha!!! Afya yangu ikadolola sana, nikalazimika kwenda kupima 
hospitali. Sikuwa na virusi. Nikapewa ushauri nikautumia.
Siku zikasonga nikampata mwanaume mwingine. Huyu alikuwa ananijali sana. Nikaanza kumsahau yule 
aliyenitenda. Nilipomaliza chuo akajitambulishanyumbani na alitaka kunioa. Akanioa kweli. Maisha 
yakaanza. Mwaka wa kwanza, mwaka wa pili na hadi wa tatu. Sikuwa nabeba mimba. Mume wangu 
alikuwa mvumilivu sana, hakuwahi kunilaumu. Lakini niliumizwa na mawifi. Nikaamua kwenda hospitali.
Nikaambiwa kizazi changu kiliharibiwa kwa kutoa mimba mara kwa mara. Pia mapenzi ya kinyume na 
maumbile yamenivuruga kabisa.Nililia sana huku nikimkumbuka yule aliyeuleta uchungu huu kwangu. 
Dunia haikuwa mahali pangu sahihi. Nimekuandikia baruahii mdogo wangu. Uisome mwenyewe!! Lakini 
uwasimulie wengi baada ya kifo changu.
Uwasimulie bila kuchoka wasichana wa kileo wanaodanganyikanakufanya mambo magumu 
kuwaridhisha wapenzi wao. Waambie watakufa kwa mateso kama mimi. Wasipokusikiliza usijisikie 
vibayamaana hata mimi nilikuwa siwasikilizi watu waliponambia lolote kuhusu yule mume mdanganyifu. 
Sitajiua lakini nitakufa kabla ya wakati!!!
Nimekuandikia wewe kwa kuwa u mwandishi. Japo kwa sasa u mtoto mdogo najua utaipata nafasi siku 
moja ya kuwafikishia wasichana hawa. Usilie kwa sababu nitakufa. Lia kwasababu mwanaume 
mwenzako 
AMENITENDA HIVI!!! 
 

Gallery

Popular Posts

About Us