KINGAZI BLOG: 11/22/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 22 November 2016

JAMAA ATAMANI KURUDIA UANAUME BADA YA KUJIBADILI NA KUWA MWANAMKE

A transs3xual who had a £10,000 s3x change on the NHS to become a woman now wants the taxpayers to foot the bill for a further £14,000 of surgery so she can become a man again.

According to DailyMail, Chelsea Attonley, 30, who was born a boy and called Matthew, said she now finds being a woman

‘exhausting’, is tired of putting on make-up and wearing heels, and now accepts that she should always have stayed a man.

Chelsea said she had struggled with her identity while growing and as a child she would dress up in

women’s clothes. In her twenties she became a drag queen known as Miss Malibu, drawing on glamour model Katie Price’s look for inspiration. An initial bid for a s3x change to become a woman was turned down by a doctor, sending Chelsea into a spiral of depression, she said.

MREMBO JODIE MARSH AACHIA PICHA ZA NUSU UTUPU MTANDAONI




Taarifa ya Mugabe kustaafu urais Zimbabwe

Kwa mara ya kwanza rais mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe adokezea kuhusu kustaafu kwake .

.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na gazeti linalomilikiwa na serikali la Sunday Mail ni kuwa  rais alisema "Nitastaafu ipasavyo."

Rais Mugabe alisema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano na washirika wa vita mjini Harare .

Hata hivyo neno 'Ipasavyo' kama alivyotumia katika kauli yake halikueleweka vizuri.

Vile vile Robert Mugabe ameripotiwa kusema kuwa naamini kuwa ameshinda serikali za Uingereza na Marekani .

Wakati huo huo televisheni ya habari za taifa ya ZBC ilitangaza kuwa mikoa mingi ya chama cha ZANU PF imeunga mkono Robert Mugabe kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2018 .

PICHAZ+++ MCHUNGAJI ANAYEOMBEA WATU NA KUWAPILIZIA DAWA YA MBU



Nafahamu hii inaweza kukushtua sana, imetokea nchini Afrika Kusini kumuhusu mchungaji Lethebo Rabalago wa Kanisa la Mountzion General Assembly lililopo mji wa Limpopo, ambaye amekutwa akiwapulizia dawa ya kuua wadudu kwa madai kwamba itawaponya matatizo yao.

Mchungaji wa Limpopo Afrika Kusini awa gumzo, ni baada ya picha kusambaa akiombea watu kwa kuwapulizia dawa ya Mbu kanisani kwake Mount Zion



Mchungaji aliyezua gumzo kwa kuwaombea watu kwa kuwapulizia dawa ya Mbu South Africa aliwahi kusema chochote kinafaa kwa uponyaji akitamka.

Kupitia picha alizozishare kwenye ukurasa wake wa Facebook, ameonekana akiwapulizia dawa hizo waumini kwenye sehemu mbalimbali za mwili na kueleza kwamba yeye kwake kila kitu anaweza kukifanya kuwa baraka za uponyaji.

Sasa muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa na picha za Mchungaji huyo akitumia dawa ya kuua wadudu kuwapulizia waumini kanisani kwake, Kampuni inayotengeneza dawa hizo iitwayo Doom imetoa tamko lake na kumuonya mchungaji huyo kuacha mara moja kutumia bidhaa zake kwa matumizi ya aina hiyo.


Nimekuwekea picha hapa chini.


 
 
 

Baba Wa Kambo Atiwa Mbaroni kwa Kumnajisi Hadi Kufa Mtoto wa Miaka Mitatu

Mtoto  mdogo mwenye umri wa miaka mitatu mkazi wa Kijiji cha Nyamihaga Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma amekufa baada ya kunajisiwa na baba yake wa kambo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui alisema jana kwamba wamemtia mbaroni mtuhumiwa Hamimu Saidi (27) mkazi wa kijiji hicho cha Nyamihaga.

Akitoa maelekezo kuhusu mkasa huo, Kamanda Mtui alisema mtuhumiwa alitekeleza dhamira yake hiyo wakati mama wa mtoto huyo ambaye alikuwa mke wa mtuhumiwa alipokwenda kisimani kuchota maji.

Alisema baada ya mwanamke huyo kurejea nyumbani kutoka kisimani alimshuhudia mtoto wake akilalamika sana wakati akitaka kujisaidia haja ndogo na ndipo alipomchunguza akagundua kwamba mtoto huyo alikuwa ameingiliwa na kujeruhiwa kwenye sehemu zake za siri.

Kamanda Mtui alisema baada ya kugundua hilo, mama huyo wa mtoto alimchukua mtoto huyo na kumpeleka Hospitali ya Mkoa ya Maweni kwa matibabu, ambako iligunduliwa kuwa mtoto huyo alikuwa amenajisiwa na alikuwa amebanwa shingo wakati akifanyiwa kitendo hicho hivyo alikosa pumzi wakati akifanyiwa unyama huo.

Kamanda huyo alisema hata hivyo mtoto huyo alifariki katika Hospitali ya Mkoa ya Maweni alipokuwa akitibiwa na kwamba baada ya uchunguzi wa kidaktari na uchunguzi wa Polisi, mwili wa mtoto huyo ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya maziko.

“Kwa sasa mtuhumiwa Hamimu Saidi anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi mjini Kigoma wakati upelelezi ukiendelea ili taratibu za kumfikisha mahakamani zifanyike na kwamba anatarajia kufikishwa mahakamani wakati wowote upelelezi huo utakapokamilika,” alieleza Kamanda Mtui.

HABARI KUU KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOV 22



























 

Gallery

Popular Posts

About Us