KINGAZI BLOG: 03/30/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Thursday 30 March 2017

Jukwaa la Wahariri Latoa Tathmini ya iki moja ya Kususia Habari Makonda

Bodi ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) imekutana jijini Dar es Salaam leo Machi 30, 2017. Pamoja na mambo mengine imejadili mwenendo wa vyombo vya habari ndani ya wiki moja tangu tulipotoa msimamo wa kutotangaza habari za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Bodi imepitia habari za Mkuu wa Mkoa zilizochapishwa tangu ulipotolewa msimamo wa kumfungia. Bodi inapenda kawapongeza wahariri wote waliotekeleza kwa usahihi msimamo wa kutochapisha habari za Mkuu wa Mkoa kwa wiki nzima.

Bodi inapenda kusisitiza kuwa wahariri katika vyombo vya habari; magazeti, radio na televisheni waendelee na msimamo wa kususia habari za Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, hadi atakapotimiza takwa la kuomba radhi kwa tukio la kuvamia kituo cha Clouds.

Aidha, Bodi inatoa wito kwa viongozi wa mitandao ya kijamii kuunga msimamo huu. Bodi inapenda kufafanua kuwa Mhe. Makonda amewekewa vikwazo Maalum (Smart Sanction) kwa mikutano atakayoiandaa au matukio atakayoyaongoza habari zake hatutazichapisha.

Wakati huo huo, kituo cha Clouds kimepongezwa kwa kumsimamisha kazi mtangazaji aliyekiuka msimamo wa kutotangaza habari za Makonda.

Bodi pia imewasiliana na Uongozi wa UTPC na kukubaliana kwamba msimamo huu uendelee.

Theophil Makunga,

Mwenyekiti TEF

Imetolewa Leo,

Machi 30, 2017

Shilawadu nawaona . inasemekana eti Mama Wema Atuhumiwa Kudendeka na Alex Msama,Ubuyu Wote Uko Hapa..!!!


 Hatari! Mama mzazi wa muigizaji mkubwa wa filamu Tanzania, Wema Sepetu, Miriam Sepetu anadaiwa kuitikisa ndoa ya mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Msama, Risasi Mchanganyiko limepewa mchongo mzima.

ANA KWA ANA NA CHANZO Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho karibu na ishu hiyo, mtikisiko huo mkubwa ulitokea ndani ya familia ya muandaaji huyo wa matamasha ya Injili baada ya mkewe kukuta ujumbe mfupi wa maneno katika simu ya mumewe, hivyo kusababisha mtafaruku.

“Sijui hasa nini kilitokea, lakini nilicho na uhakika nacho ni kuwa ndoa ya wawili hao ilikuwa katika majaribu makubwa wakati huo, maana kulionekana kuwepo kwa mawasiliano ya mara kwa mara baina ya Msama na Mama Wema, kitu ambacho mkewe alishindwa kuelewa. “Msama alijitahidi sana kupooza mambo kwa kujaribu kumuweka sawa mkewe, lakini bado ikawa ngumu hadi baadhi ya marafiki wa karibu wa pande

WAANDISHI WETU, RISASI zote mbili walipoingilia kati na kuliweka sawa jambo hilo na hivyo kupoa,” kilisema chanzo hicho. Chanzo hicho kilisema wakati mmoja katika mtafaruku huo, wanandoa hao walikuwa hawazungumzi, kitu ambacho kilitishia sana uhai wa ndoa hiyo. Baada ya kupata taarifa hizo, Risasi Mchanganyiko lilifanya juhudi kubwa za kuwatafuta wawili hao, likifika ofisini na nyumbani kwa nyakati tofauti lakini mara zote likiambulia patupu. Hata hivyo, mwishoni mwa wiki iliyopita, Msama alipatikana kupitia simu yake ya mkononi.

HUYU HAPA ALEX MSAMA

“Ni kweli, ndoa yangu ilipata mtikisiko mkubwa sana kwa sababu ya Mama Wema, mke wangu alikuta mawasiliano baina yangu na yule mama kwenye simu, akaja juu. Alikuwa akiniuliza huyu ni nani na kwa nini nawasiliana naye mara kwa mara.

“Nilikuwa nawasiliana naye mara kwa mara kwa sababu nilikuwa na biashara naye. Unajua kuna kipindi nilitaka kununua nyumba yake, nikawa wakati mwingine ninampa hela kidogokidogo, sasa katika biashara kubwa kama ile ni lazima mtakuwa mnawasiliana mara kwa mara.

“Mke wangu alipokuwa anaona meseji nyingi kutoka kwake, akawa anahisi kuna kitu, lakini nilijitahidi kumweleza kuwa ni kwa sababu ya biashara tu, hatimaye alinielewa, mambo yakaisha na sasa kila kitu kiko vizuri,” alisema Msama. Mke wa Msama ni mtangazaji wa kituo kimoja cha Redio, kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

VIPI KUHUSU PESA ZAKE?

Risasi Mchanganyiko lilimuuliza Msama hatima ya fedha zake za maudhiano ya nyumba ambazo hivi karibuni alilazimika kutumia Polisi ili kumkamata, baada ya kudai kuwa mama huyo alichukua fedha, lakini badala yake akamuuzia mtu mwingine.

“Hapa ni lazima niwe mkweli, siwezi kukubali huyu mama achukue tu fedha zangu kirahisi atoweke, ninasikia faili lake tayari limeshafika kwa Mwendesha Mashtaka wa serikali, ninachotaka mimi ni vyombo vya sheria kufanya kazi yake ili haki itendeke.

“Sitakubali mazungumzo, maana watu kama hawa wapo wengi sana hapa mjini, wanafanya mambo makusudi, wakitegemea huruma, siwezi kuwa na huruma na mtu ambaye anadhani udanganyifu ni jambo zuri, suala hilo ninataka limalizike mahakamani,” alisema Msama ambaye pia ni mmiliki wa Kampuni ya Habari ya Msama Media Group.

MSAKO WA MAMA WEMA

Mbio za kumsaka Mama Wema zilishika kasi na kulifikisha Risasi Mchanganyiko hadi nyumbani kwake, Sinza Mori, lakini msichana aliyefungua mlango alisema mwanamama huyo, aliyegonga vichwa vya habari wiki chache zilizopita kufuatia sakata lake na Steve Nyerere, hakuhitaji kuonana na mtu yeyote kwa wakati huo.

Kuona hivyo, waandishi wetu walimtumia ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu yake ya mkononi, lakini licha ya kuonyesha kuwa ujumbe huo ulifika na kusomwa, hakurudisha majibu.

TUJIKUMBUSHE

Alex Msama na Miriam Sepetu wamejikuta wakiingia katika mtafaruku baada ya kushindwa kuelewana katika suala lao la mauziano ya nyumba ya mama huyo iliyopo Sinza Lion.

Taarifa za awali zilizoandikwa na gazeti hili, zilisema mama huyo alitaka kuiuza nyumba hiyo kwa Msama, lakini mfanyabiashara huyo alichelewesha malipo na kumfanya aiuze kwa mtu mwingine. Hadi anafikia uamuzi wa kufanya biashara na mtu mwingine, inadaiwa kuwa tayari alikuwa ameshachukua kiasi cha shilingi milioni 16 kutoka kwa Msama.

Mama Yake Hamisa Mobeto Amtolea povu Zari the Boss Lady,Amtaka Akome Kumtajataja Mwanae Mitandaoni.


DAR ES SALAAM Skendo ya mjini iliyotapakaa mjini na kwenye mitandao ya kijamii inamgusa modo maarufu Bongo, Hamisa Mobeto akidaiwa kujichora ‘tatuu’ ya mwanamuziki maarufu Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, ishu iliyosababisha mwandani wa jamaa huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kumporomoshea matusi.

Kuhusu sakata hilo, mama mzazi wa Mobeto ameshindwa kujizuia na kujikuta akimtolea povu Zari juu ya mwanaye huyo. Akizungumza na gazeti hili kwa uchungu alipoulizwa kuhusu sekeseke hilo la mwanaye, mama Mobeto alisema kuwa, hakuna wakati mgumu kama kuona mtoto wake huyo anazungumziwa vibaya kila wakati katika mitandao ambapo wakati mwingine siyo jambo la kweli zaidi ya kumchafua tu.

“Jamani mimi kama mzazi, sidhani kama kuna mzazi yeyote anayeweza kuvumilia kuona mwanaye kila mara yuko kwenye midomo ya watu au kuongelewa vibaya kwenye mitandao ya kijamii kwa vitu ambavyo hajafanya,” alisema mama Mobeto. Alifunguka kuwa, habari ambayo imesambaa kuhusu mwanaye kujichora tatuu ya Diamond, anaona ni mambo ambayo hayana msingi wowote zaidi ya kumchafua na kumdhalilisha mwanaye.

“Unajua unapomuona Hamisa (Mobeto) amenyamaza, kila wakati wanatafuta kumuwekea jambo baya,  kitu ambacho siyo sahihi, mimi sijawahi kuiona hiyo tatuu wanayosema zaidi ya kuona kuwa wanampandikizia maneno tu ya kumchafua, sipendezwi kabisa na tabia hiyo,” alisema mama Mobeto.

Hivi karibuni Zari alimtolea matusi Mobeto kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii akimtahadharisha juu ya habari zilizozagaa kuwa, huwa anachepuka na Diamond kwa siri hasa mwanamama huyo anapokuwa nyumbani kwake, Afrika Kusini na kumwacha baba watoto wake huyo jijini Dar.

Kimenukaa Clouds Media..Mfanyakazi Asimamishwa Clouds kwa Kutangaza Habari ya Paul Makonda, TEF Yaitaka Mitandao Iunge Mkono..!!!


Bodi ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) imekutana jijini Dar es Salaam leo Machi 30, 2017. Pamoja na mambo mengine imejadili mwenendo wa vyombo vya habari ndani ya wiki moja tangu tulipotoa msimamo wa kutotangaza habari za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Bodi imepitia habari za Mkuu wa Mkoa zilizochapishwa tangu ulipotolewa msimamo wa kumfungia. Bodi inapenda kawapongeza wahariri wote waliotekeleza kwa usahihi msimamo wa kutochapisha habari za Mkuu wa Mkoa kwa wiki nzima.

Bodi inapenda kusisitiza kuwa wahariri katika vyombo vya habari; magazeti, radio na televisheni waendelee na msimamo wa kususia habari za Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, hadi atakapotimiza takwa la kuomba radhi kwa tukio la kuvamia kituo cha Clouds.

Bodi inatoa wito kwa viongozi wa mitandao ya kijamii kuunga msimamo huu. Bodi inapenda kufafanua kuwa Mhe. Makonda amewekewa vikwazo Maalum (Smart Sanction) kwa mikutano atakayoiandaa au matukio atakayoyaongoza habari zake hatutazichapisha.

Bodi inakipongeza Kituo cha Clouds kwa kumsimamisha kazi mtangazaji aliyekiuka msimamo wa kutotangaza habari za Makonda. Bodi pia imewasiliana na Uongozi wa UTPC na kukubaliana kwamba msimamo huu uendelee.

Theophil Makunga,

Mwenyekiti TEF

Imetolewa Leo,

Machi 30, 2017

"Tutaipinga bajeti bungeni kwa sababu haitekelezeki"- Freeman Mbowe.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema wataipinga bungeni bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2017/18 kwani haina msaada wowote kwa wananchi wa hali ya chini na wanaamini fedha hizo hazitapatikana kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mbowe amesisitiza mwaka jana wabunge wa kambi ya upinzani walieleza wazi kuwa bajeti ya mwaka huu isingetekelezeka na ndio kilichotokea kwani mpaka sasa asilimia 34 pekee ya pesa zote za maendeleo ndizo zimetolewa.

Makubwaaa!!!Mchungaji ashinda Mochwari akisubiri mkewe afufuke

 Mchungaji Githumba kutoka Kenya jana alishinda katika chumba cha kuhifadhi maiti  akisubiri mke wake aliyefariki Jumapili afufuke siku ya 3.


CREDIT. MUUNGWANA BLOG

BREAKING NEWS: Mahakama kuu imetengua hukumu ya Mbunge wa Chadema aliyefungwa miezi 6 jela


Mahakama Kuu Dar es Salaam imetengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya W/Kilombero dhidi ya Mbunge Peter Lijualikali, amekutwa hana hatia.


January 2017, Mahakama ya wilaya ya Kilombero ilimuhukumu kwenda jela miezi sita Mbunge wa jimbo la Kilombero, Peter Lijualikali (30) kwa kosa la kufanya fujo na kusababisha taharuki katika maeneo ya ukumbi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.

Mwendesha mashtaka inspekta wa Polisi Dotto Ngimbwa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa, akiwa mshtakiwa namba moja pamoja na mwenzie Stephano Mgata (35) walitenda kosa hilo machi mosi mwaka 2016 kwenye kikao cha Baraza la Madiwani katika eneo la Kibaoni ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero.

Kufuatia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, Hakimu mkazi katika mahakama ya wilaya ya Kilombero Timothy Lyon aliwatia hatiani washtakiwa hao walipatikana na makosa. Aidha, Hakimu alisema kuwa mshtakiwa wa kwanza ambaye ni Mbunge ambaye alikuwa na kesi tatu huko nyuma atatumika kifungo cha miezi sita jela kwa kuwa anaonekana kuwa mkosaji mzoefu.

Hata hivyo Mahakama hiyo iliona kwa kuwa mshtakiwa wa pili Stephano Mgata (35), hili ni kosa lake la kwanza amehukumiwa kifungo cha miezi sita nje ambapo ndani ya kipindi hicho cha miezi sita hatotakiwa kutenda kosa lolote la jinai.

Saa tatu za makonda kwenye kitimoto.....Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya March 30 2017





Saa tatu za makonda kwenye kitimoto.....Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya March 30 2017





 

Gallery

Popular Posts

About Us