KINGAZI BLOG: 04/03/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 3 April 2017

9 pictures : Corazon Kwanboka is one of Kenya’s most curvaceous model and socialite. See more photos of her below..

Corazon Kwanboka is one of Kenya’s most curvaceous model 
and socialite. See more photos of her below..
















MAAJABU YA MWAKA HAYA ....Jamaa anayeatamia mayai ya kuku Ufaransa

Msanii kutoka Ufaransa Abraham Poincheval anaendelea kuatamia mayai ya kuku akiwa na matumaini kwamba  yataangua vifaranga. Jamaa anatumia joto kutoka kwenye mwili wake kuatamia mayai hayo 10. Poincheval ambaye hufanya uigizaji wa kuigiza mambo ya ucheshi lakini ya hatari alishahi kuishi wiki mbili ndani ya dubu na mengine mengi ya kushangaza.

Jamaa atakuwa katika chumba maalum ambacho anatamia mayai ambapo watalii wanaweza kumtazama katika makumbusho ya Palais de Tokyo mjini Paris na anatarajia kuatamia mayai hayo kwa siku 21 hadi 26.

Badala ya kuatamia mayai hayo kwa kuchuchumaa juu yake moja kwa moja, anatumia kiti maalum ambacho kina mfuko eneo lake la kukalia, hapo ndipo mayai hayo yamewekwa.

Poincheval amejifunga blanketi kuzuia joto kupotea aidha anapanga kula vyakula vinavyoongeza sana joto mwilini, kama vile tangawizi. Wakati wa haja atatumia kijisanduku kidogo kilichomo mvunguni mwa kiti chake. Unaambiwa jamaa hatakiwi kuondoka zaidi ya dakika 30 kwa si

Kampuni ya The Guardian Inayochapisha Magazeti ya Nipashe Imetoa Tamko Hili Kuhusu Taarifa za Kufilisika kwake.


Kampuni ya uchapishaji magazeti The Guardian Limited ambayo huchapisha magazeti ya The Guardian, Nipashe na Lete Raha, imekanusha taarifa za uzushi zilizosambaa mtandaoni kuwa inaifunga kutokana na ukata.

Hii ni taarifa yake:


Taarifa hiyo ya uzushi ilisema:

Management ya The Guardian Chini ya General Manger, Ndg Srinivas imewatangazia wafanyakazi wa IPP- The Guardian kusudio la kufunga kampuni kutokana na ukata unaoikabili kampuni hiyo. The Guardian ni miongoni mwa kampuni kubwa za Magazeti wachapishaji wa Gazeti la kila siku la The Guardian, Nipashe, Lete Raha.  


Wafanyakazi wa The Guardian wanaishi/Kupita katika kipindi kigumu hawajalipwa mshaara miezi 4 toka January 2017 wafanyakazi hawajalipwa mshahara. Frelencer na correspondence reporter hawajalipwa toka August 2016.  


Media Solution (Wachapishaji wa Gazeti la Kulikoni na ThisDay) ambayo ni kampuni Dada wa The Guardian lilifungwa Rasmi mwezi February 2017. Wafanyakazi zaidi ya 200 wa Media Solution Ajira zao zilisitishwa mwezi uliopita. “Kimsingi hali ni Mbaya,  


kama Mzee Mengi anaisoma number inabidi tujitafakari kama Nchi tunaelekea wap?” Alinukuliwa mfanyakazi mmoja wa The Guardian akilalamika kwa uchungu.
Kufungwa kwa The Guardian kutasababisha wafanyakazi zaidi ya 350 kupoteza kazi.


Aliyetumbuliwa na Rais Magufuli Dk Mwele Malecela Ateuliwa Kuwa Mkurugenzi Shirika la Afya Duniani (WHO)..!!!


Salamu za pongezi zimeendelea kumiminika kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr), Dk Mwele Malecela baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika vya Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika.

Pia, Dk Mwele  aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Mpango wa Maalumu wa WHO wa kutokomeza magonjwa yasiyopewa kipaumbele (Espen) na sasa atahamia kituo chake cha kazi Congo-Brazaville. 

Mradi wa Espen ulianza kutekelezwa mwaka 2016 hadi 2020, una lengo la kumaliza magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwa kutoa vifaa tiba, elimu na dawa. 

Magonjwa yasiyopewa kipaumbele ni pamoja na matende, mabusha, kichocho, minyoo ya tumbo na usubi. 

Miongoni mwa waliomtumia pongezi ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Sikika, Irenei Kiria ambaye aliandika katika ukurasa wake wa Twitter: “Hongera Mwele kwa kupata nafasi hiyo ina maana ulipangwa kulisaidia Taifa letu ukiwa nje.”

 Mwingine ni Mhadhiri wa Saikolojia wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kitila Mkumbo aliyeandika katika ukurasa wake wa twitter akisema: “Nina furaha kwa uteuzi wa Dk Mwele kuwa Mkurugenzi wa WHO.Nahisi kusamehewa kwa kuikosoa Serikali baada ya kumuondoa Nimr.” 

Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile yeye aliandika katika ukurasa wake akimpongeza Dk Mwele na kusema, “Nimezidiwa na furaha baada ya kupata taarifa kuwa umepata kazi kubwa katika ogani ya kimataifa. Mlango mmoja ukifungwa mwingine hufunguliwa. Katumikie vyema.” 

Dk Mwele aliondolewa kuwa Mkurugenzi wa Nimr na Rais John Magufuli Desemba 17 mwaka jana. 

Kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kulifanyika siku moja baada ya kutoa ripoti ya utafiti wa magonjwa, ndani yake ikiwamo taarifa ya virusi vya ugonjwa wa Zika katika maeneo ya Morogoro, Geita na Magharibi mwa Tanzania. 

Taarifa ya Dk Mwele, ilieleza kuwa kati ya watu 533 waliopimwa, asilimia 15.6 walibainika kuwa na virusi hivyo. 

Siku moja baada ya kutoa takwimu hizo, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa na Dk Mwele aliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hizo kwamba ugonjwa huo bado haujaingia nchini.

Jinsi Ya Kumshawishi Mwanamke Mtandaoni na ukaweza kumpata kiurahisi zaidi




Kama kuna sehemu moja hapa duniani ambayo unaweza kujiachilia na kuwa wewe mwenyewe na kupata wanawake wakupende, bila shaka hio sehemu ni mtandaoni.
Hii ndio sababu kuu ya wanaume wengi kujiingiza katika Internet ili kujaribu mizare yao ya kuwavutia na kuwashawishi wanawake sikuhizi. Habari njema ni kwamba wanaume wengi hufanikiwa katika azma yao. Kuingia katika mitandao ya kijamii na kujaribu kuwashawishi wanawake inaweza kuwa jambo gumu kiasi na wakati mwingine likawa ni rahisi. Wengine hutumia fursa ya kutumia mitandao kama mazoezi ya washawishi mademu huku wengine wakifanikiwa kupata wachumba ambao wanakuwa nao katika maisha yao ya kawaida. Well, kama hujawahi kutongoza mwanamke online, ama unapata vigumu kutongoza then hapo chini kuna mbinu mwafaka ambayo itakuwezesha wewe kumtongoza yeyote yule katika mitandao ya kijamii kiurahisi.

1. Mtongoze
Kama maisha ya kawaida, kumtongoza mwanamke akiwa online ni lazima kama ibada. Itakuwa bora zaidi ukichanganya mitindo spesho ya kutongoza mara kwa mara, Mnyeshee kwa kumsifu siku moja halafu unakuwa mfidhuli siku nyingine. Jambo muhimu hapa ni utambue kuwa lazima unafaa kumfanya awe ametulia wakati unapochat nayeye. Pia lazima awe anajiskie yuko huru kabisa wakati mnapoongea. Hii itahakikisha kuwa anapenda na kufurahia kutaka kukujua zaidi na labda siku moja atatamani muweze kukutana ana kwa ana.

2. Tafuta maneno ya kwako
Usithubutu kutafuta mistari ya papo kwa papo kwani kawaida haifaulu katika mitandao. Kile unachohitajika kufanya ni kuhakikisha umepanga conversation yenu vizuri ili isiweze kukwama mbeleni. Pia hakikisha kuwa unaingiza maneno ambayo yataleta hisia za kucheka na furaha. Hii itamfanya amakinike zaidi na wewe.

3. Mfanye Acheke
Ok najua si kila mtu ana talanta ya kumfanya mwanamke yeyote acheke kama vile mzee Majuto lakini unafaa angalau utumie maujanja uliozaliwa nayo ili kumfanya mwanamke acheke. Nasema hivi kwa sababu wanawake wengi kawaida hupenda wanaume wacheshi. Ukitumia mbinu hii utamfanya akiwa offline ama online, fikra zake zitakuwa kwako.

4. Usimwambie kila kitu chako
Ukiwa unachat na mwanamke online, hakikisha humwambii kila kitu chako kwa wakati mmoja. Hakikisha ya kuwa kama mnachat unamfungulia moyo wako pole pole. Hii itamfanya yeye kuwa na shauku ya kutaka kukujua zaidi. Ukiweka baadhi za siri zako kikapuni, lazma ataingiwa na tamaa ya maswali hivyo kutaka kuongea na wewe zaidi na zaidi.

5. Kutana na yeye uso kwa uso.
Mwisho wa siku -baada ya kumtongoza na kumjua nje na ndani -unafaa kumuuliza kama atatoka out na wewe. Kumbuka hii ni level nyingine kubwa sana katika chat ya online hivyo kabla hujamuagiza mukutane uso kwa uso, lazima ujipange vilivyo

Habari katika Magazeti ya leo tar 3 April 2017




























 

Gallery

Popular Posts

About Us