KINGAZI BLOG: 12/25/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Sunday 25 December 2016

FARU John Huyu Hapa, Lindo lake lilikuwa Sh215,000 Kwa Kila Siku

Wakati Waziri Mkuu ameagiza kaburi la Faru John lifukuliwe na kuchukuliwa vipimo vya vinasaba kuthibitisha kama pembe alizopelekewa ni zake, mabaki yanayoaminika kuwa ni ya mnyama huyo (pichani) yameonekana yakiwa porini katika eneo la Grumeti, wilayani Serengeti alipofia.

Vilevile, gazeti hili limebaini kuwa kabla ya kifo chake, Faru John alikuwa analindwa kwa gharama ya Sh225,000 kila siku.

Faru John alihamishiwa Grumeti, Desemba 17, mwaka jana na kufa Agosti 18, mwaka huu katika mazingira yanayodaiwa kuwa tata.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Disemba 25




UTAFITI: Mitandao ya Kijamii Inaweza Kusababisha Magonjwa ya Akili

Je, unapenda kufungua mitandao mbalimbali ya jamii kama Facebook, Tweeter, Instagram, Google Plus, Snapchat, LinkedIn, Youtube na mingineyo kila siku?

Kama jibu ni ndiyo, basi uko hatarini kupata tatizo la msongo wa mawazo na wasiwasi.

Utafiti mpya uliofanywa na Chuo Kikuu cha Pittsburgh cha Pennsylvania nchini Marekani mwaka 2014 na kuzinduliwa mwaka huu, unaonyesha kuwa matumizi ya mara kwa mara ya mitandao ya jamii yanaweza kusababisha magonjwa ya akili, ukiwamo msongo wa mawazo na wasiwasi.

Wakati kukiwa na tatizo hilo, inakadiriwa kuwa asilimia 71 ya vijana duniani kote hutembelea mitandao tofauti ya jamii kila siku huku simu za mikononi zinazowezesha kupatikana mitandao hiyo kirahisi zikizidi kubuniwa na kuboreshwa.

 

Gallery

Popular Posts

About Us