KINGAZI BLOG: 02/25/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 25 February 2017

Picha ya pamoja zari na wema sepetu.

Hii ni picha iliyo sambaa mtandao ikimuonesha mzazi mwenza wa Mwanamuziki Diamond platnumz na ex-girlfriend wake Wema sepetu katika picha ya pamoja 
Swali ni Je picha hii ni ya kweli au editing???
Tupe Maoni yako hapo chini!!!

STEVE Nyerere Kakerwa na Kitendo cha Kurekodiwa na Mama yake Wema Sepetu..Kasema Wema Sepetu Hadai Chochote CCM

Baada ya sauti zilizosambaa zikimuhusisha Mwigizaji Steve Nyerere na Mama wa mwigizaji Wema Sepetu wakizungumza huku akitaja baadhi ya viongozi mbalimbali aliodili nao kwenye sakata la Wema kushikwa na Polisi, leo Steve Nyerere ameita Waandishi wa habari na kuongea nao.

Steve Nyerere amesema kuwa hakuna msanii hata mmoja ambaye anakidai Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema mambo ambayo anasema Weme Sepetu kuwa anakidai chama hicho ni uongo na uzushi mtupu.

Amesema katika wasanii mbalimbali ambao huenda walilipwa pesa nyingi zaidi ni Wema Sepetu pamoja na yeye na kusema wao pamoja na wasanii waliokuwa wanaendesha kampeni ya 'Mama ongea na mwanao' ni wasanii ambao walilipwa vizuri sana na Chama Cha Mapinduzi kuliko wasanii wengine wowote wale.

Steve Nyerere anasema katika mkataba walioingia na Chama Cha Mapinduzi hakuna sehemu mkataba huo unasema ukikamatwa na madawa ya kulevya, bangi  chama hicho kitakuja kukusaidia.

Pia Steve Nyerere anakiri wazi kuwa sauti ambayo inazunguka kwenye mitandao ya kijamii ni kweli ni sauti yake na alikuwa akiongea vile ili kumridhisha mama yake na Wema Sepetu kwani wakati huo jambo hilo lilikuwa ngumu kwake.

==> Fuatilia maongezi yake ya moja kwa moja hapo chini

1.Nimewaiteni hapa kama msanii wa tasnia ya filamu pia kama kada wa chama cha mapinduzi

2.Kulikuwa na maongezi ya simu kati ya mimi na mama Sepetu, mimi ndio nilikuwa naogea na mama Sepetu yasipindishwe

3.Nilichofanya ni kutumia sanaa yangu na ujuzi kumtoa mama kwenye hali ambayo anasema anataka kujitoa hata kwenye chama"

4.Mama alikuwa anaamini naweza kumtoa Wema, nilikuwa natumia ujuzi wa akili yangu kumlidhisha mama, kumbe yeye ananirekodi

5.Kwenye kampeni tulilipwa hakuna aliyefanya kazi bila kulipwa, kundi la mama ongea na mwanao mimi ndio nilikuwa mwenyekiti

6.Maneno niliyoyasema ktk simu na Mama Wema na kutaja viongozi ni UONGO, ilibidi nifanye hivyo maana sikuwa na jinsi...

7.Uwezo wa kuwaambia Wabunge au kuwaelekeza cha kufanya sina, sina ujanja huo.... namuomba radhi Spika Job Ndugai"

8.Mimi na Wema ndio tuliwafuata CCM kwamba tuna wazo la mama ongea na mwanao, na tukalipwa

9.Namuomba radhi Rais Magufuli na Chama changu cha CCM, yanaongelewa mengi ninayasikia, naomba radhi familia pia, niliteleza

10.Nia yangu haikua mbaya, wakati naongea na Mama niliamini ni mama mzazi... ile audio ina siku 5, kwanini iachiwe juzi?

11.fikifria ile audio ina siku tano, inakuja kutolewa juzi na watu wamehama tayari chama, nafikiri walifanya hivyo kunichafua

12.Ile audio imekuja kuachiwa juzi wakati watu wanahama chama, kwanini nirekodiwe? naamini wamefanya hivyo makusudi

13.Nimetaja viongozi ktk ile audio alafu unakuja kuisambaza nimetaja viongozi wa Nchi, Mama alichofanya kuisambaza ni mauaji

14.Si kweli nilishinkiza wabunge wamjadili Wema, mtoto anapotaka kuchomwa Sindano kuna vitu anaambiwa, ndio hivyo nilivifanya

15.Watanzania wenzangu usimuamini binadamu yeyote, Mama Wema alitaka kuniharibia maisha yangu, Mama kanikosea.. namuachia Mungu

16.Mimi na Makonda hatujawahi kwenda alikokutaja Mama, ilibidi niitikie kama zoba, Waandishi naomba mkaseme NAOMBA RADHIII

17.Sina ugomvi na Makonda na ninamuomba msamaha na hakuna ukweli kwamba siongei nae.... Paul ni kaka yangu, tunawasiliana

18.Naliomba radhi bunge tukufu na Spika Ndugai kwa kauli ya kusema nimeshinikiza bunge, nilifanya hivyo kutaka asitoke ndani ya CCM

19.Uwezo wa kuwashinikiza wabunge sina na wala mamlaka hiyo sina

20.Hii kesi kila mtu alirudi nyuma.. ni maulizo tu inaendeleaje? tunamuombea kwa Mungu tu, CCM ni kama bahari wametoka wangapi?

21.Mimi kama mtu wa karibu na familia nilitakiwa nitoe maneno matamu na ndio hayo

22.Kwenye project ya kampeni ya uchaguzi mkuu 2015 MAMA ONGEA NA MWANAO hatuidai CCM hata senti tano

23.Alichofanya mama kunirekodi huo ni uuaji, kuna watu wananitegema nyuma ya Steve alitaka anigombanishe na marafiki


UHEARD!!..MAHAKAMA Yabariki Kuvunjika Kwa Ndoa ya Flora Mbasha na Mumewe...Sasa Kugawana Mali

Baada ya msuguano wa miezi kadhaa, hatimaye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni imeridhia kuvunja ndoa ya Mwanamuziki wa Injili, Flora na mumewe Emmanuel Mbasha kisha kugawana mali walizochuma pamoja. Chanzo makini kimefunguka kuwa, Flora aliyekuwa akiidai talaka hiyo ili aweze kuolewa na mwanaume wake mpya, alifanikiwa azma yake hiyo hivi karibuni baada ya mahakama kuridhia.

“Si unajua Flora ameshapata bwana mpya yule Daud Kusekwa na vikao nasikia vimepamba moto. Hivyo alikuwa anapambana kwelikweli kuhakikisha anapewa talaka na mimi ninayo nakala yake kama vipi niwatumie.

“Sasa amefanikiwa, wamegawana mali na mahakama imewapa masharti juu ya malezi ya mtoto wao aitwaye Eliza kwamba Flora ndiye atakayempa mahitaji yote ya msingi,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Si unajua wale kuna mali walichuma pamoja? Basi zote wamezipiga pasu. Kuanzia zile zilizokuwa kwenya akaunti ya pamoja na hata ile nyumba yao iliyopo Tabata Kimanga.”

Risasi Jumamosi baada ya kuipata nakala ya hukumu hiyo ya talaka, lilimvutia waya Flora ili kumsikia anazungumziaje hatua hiyo lakini simu yake haikupatikana hewani.

Kwa upande wake Mbasha, alikiri ndoa yao kuvunjika mahakamani na kusema hayuko tayari kuzungumzia mgawanyo wa mali zao. “Wewe elewa tu tumeshaachana, talaka imetoka mahakamani.

Hayo mambo mengine mimi siwezi kuyazungumzia,” alisema Mbasha. Wawili hao kwa sasa kila mmoja ameshampata mwenzi. Flora anatarajia kuolewa Aprili 30, mwaka huu wakati Mbasha bado haijajulikana kama atamuoa mchumba wake wa sasa au la.

CHOMBEZO - KIDUKU CHA MGUU MMOJA

Image result for masogange agnes

>>>>> BOFYA HAPO KUONA KIONJO CHA VIDEO HII 18+ onl

“Mambo vipi kaka Eddy mzima wewe, samahani kaka sijui unakumbuka ulichoniahidi???…..najua haukumbuki lakini mimi nitakukumbusha ni kuhusu kunifundisha kucheza mziki” aliongea maneno hayo mwanadada Yasmin kupitia simu ya mkononi akimwambia Eddy, ambaye ndio kwanza alikuwa ametoka usingizini.
Eddy kwa hali ya kawaida alikuwa amesahau kabisa kuwa aliwahi kumuahidi mwanadada Yasmin kuwa atamfundisha kucheza mziki katika staili tofauti tofauti. Hiyo ilikuwa baada ya Yasmin kumwambia kuwa anatamani sana siku moja aweze kucheza mziki
“Aaah!!! Ok! Nimekumbuka sasa tufanye lini na wapi?? Samahani jamani” aliuliza Eddy huku akiomba radhi
“Mama amesafiri kaenda Pemba kumpeleka mdogo wangu kutembea kwa bibi yaani nimebaki peke yangu hapa nyumbani kwa hiyo sitaweza kutoka hapa labda uje wewe jamani samahani eeh!!” alijibu kwa sauti nyembamba ya kike mwanadada huyu.
Jibu hilo lilimtia Eddy nguvu sana na kumfungua akili yake. “Mama hayupo na baba hayupo kifuatacho???” alijisemea kimoyo moyo huku akiyakariri maneno ya Yasmin. 
“Basi nitakuja, ulisema unataka staili gani vile nimesahau maana na wewe unapenda staili nyingi sana”
“Mdogo wangu ananicheka eti sijui kucheza kiduku na mimi nataka nijue halafu na kucheza mapanga yale ya TMK ya Wanaume Family….” Alijibu Yasmin huku sauti yake ikimuumbua kuwa alikuwa na aibu
“Ah!! Mapanga ya kizamani hayo nitakufundisha kiduku sawa dada….”
“Yaani nitafurahi kweli kikitoka huko Pemba nitakiringishia kweli” alijibu tena kwa furaha binti huyu kutoka familia bora sana aliyekuwa anaishi maeneo ya “masikini hajengi” ya Kidichi Spice mjini  Zanzibar.
“Kwa hiyo lini nije” aliuliza Eddy
“Siku yoyote saa yoyote unayotaka chamsingi mimi nijue kucheza kiduku, si nitajua upesi eeh!!….”
Baada ya maongezi marefu na kufikia muafaka wa lini waonane Eddy alikata simu na baada ya muda akaongezewa muda wa maongezi wenye thamani ya shilingi elfu moja kutoka kwa Yasmin. Pale pale Eddy akajiunga huduma maarufu ya vijana wasiokuwa na pesa za kupiga simu yaani “Epic Nation ya Tsh 500/=” pale akawa ameunganishwa moja kwa moja na huduma ile ambapo alijinyakulia sms 300 na dakika 15 za Zantel kwenda Zantel, na kuanza kuchat na Yasmin.
Eddy: hivi Yasmin utaweza kucheza kiduku kweli
Yasmin: ntaweza kwani wanaoweza wana nini?? Kwani  ni kigumu sana eenh??
Eddy: Unajua staili ngapi za viduku?? Eddy akawa ameanza ualimu wake
Yasmin: Mi huwa nasikia kiduku kujiremba, kiduku mcharuko, kiduku cha kukuna nazi na cha kuendesha mtumbwi
Eddy: mh!! Hayo maviduku ya zamani kweli mimi nitakufundisha mpya kabisa hata watu hawaijui
Yasmin: Kinaitwaje hicho jamani yaani natamani hata ungekuja leo ili nijifunze upesi kabla dogo halijarudi.
Eddy: kinaitwa ‘kiduku cha mguu mmoja’ mdogo wako anakiweza hicho!!!
Yasmin:mh! Sijawahi kumsikia akisema hakiwezi hicho labda ndo maana hasemi, anavyopenda sifa angekuwa keshanambia
Eddy: sasa nitakuja leo jioni kukufundisha sawa?
Yasmin: usiache Eddy
Akili ya Eddy ilijizungusha haraka haraka na kuamini huu ulikuwa muda muafaka wa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na Yasmin kwa kutumia fursa hii ya kumfundisha kucheza kiduku.
Ni siku nyingi sana alikuwa anajaribu kumjengea mazingira ya kimapenzi lakini hata hisia za Yasmin hazikuonekana wazi kwake na yeye Eddy alishindwa kumtamkia.

Majira ya saa kumi na mbili jioni Eddy mtoto wa Mboriborini uswahilini alikuwa akipata juisi baridi ya embe katika sebule pana iliyopulizwa na kiyoyozi wakati wote, Yasmin alikuwa amevalia pensi iliyokuwa imembana na ilionekana dhahiri hakuwa na hakuwa na kitu chochote ndani.
Mate ya uchu yalimjaa mdomoni Eddy na kwa jicho la wizi wizi aliweza kuchungulia cheni iliyong’ara kutokea kiunoni mwa Yasmin. Maungo yake yakamsisimka!!!
“Yasmin usiku unaingia, nenda ukavae nguo za kuchezea Kiduku cha mguu mmoja” Eddy alimwambia.
“Ndio zikoje hizo mwalimu wangu unadhani mimi nazijua basi…..” alijibu Yasmin huku akimkata jicho la mahaba Eddy. Eddy nae  akakwepesha macho!!!
“Kavae kanga na kitop nadhani hapo itakuwa sawa” alijibu huku akiona haya kidogo kwa jambo alilotamka.
“Haya Mwalimu wangu…..” alijibu huku akiondoka
“pia usisahau kuweka hii Cd wimbo namba tatu…” alisisitiza Eddy.
Baada ya dakika kumi Yasmin alirejea, kama Eddy alivyoagiza Yasmin alikuwa amevaa kanga moja pekee na kitop kilichoachia kitovu chake nje kidogo.
Kwa mwendo wa kunyata aliisogelea redio na kuweka ile Cd kisha akachagua wimbo namba tatu, ulikuwa wimbo wa taarabu uitwao ‘mama nipe radhi’. Eddy aliangalia kwa wiziwizi upande wa nyuma wa Yasmin akatamani kumrukia, kwa kitendo cha haraka haraka bila Yasmin kugundua Eddy alitumbukiza mkono wake katika suruali yake akaweka mambo sawa asije kuaibika!!
Eddy akamsogelea Yasmin pale alipokuwa na kuizungusha mikono yake katika kifua cha Yasmin.
“Sasa inatubidi tuanzie kiduku cha kawaida halafu cha mcharuko kisha tutamalizia kiduku cha mguu mmoja. Yasmin hakuwa na pingamizi lolote alikubali kila kitu alikuwa na hamu kubwa ya kujua kucheza kiduku!!!, mikono ya Eddy ilivyogusa kifua cha vuguvugu cha Yasmin alihisi kuishiwa pumzi zake, alijaribu kufundisha lakini somo lilikuwa haliendi, kwa ujasiri mkubwa alipandisha mikono yake katika chuchu ndogo za Yasmin na ni wakati huo huo ulikuwa umemalizika wimbo wa Mama nipe radhi na kuingia wimbo wa marehemu Nasma Khamis Kidogo uitwao
‘SABALKHERI’ (wale wapenzi wa muziki wanautambua wimbo huu wa chombezo) Katika taarabu za asili ni wimbo huo uliomkosha sana Eddy na alikuwa amekariri mashairi yaliyokuwa yakiimbwa na mwanaume hivyo alishindwa kujizuia kuigiza sauti ile na bila kutegemea alishangaa mashairi ya Nasma Khamis Kidogo yakijibiwa kiustadi kabisa na Yasmin ambae wakati huo pumzi zake zilipishana kwa kasi tofauti na mwanzo
Eddy: Sabalkheri mpenzi waonaje hali yako
Yasmin: albanur azizi hali yangu kama yako
Eddy: wawaonaje wazazi nyumbani utokeapo
Yasmin: kawanusuru mwenyezi hali hofu yao juu yako,hebu nitoe majonzi unijuze shida yako.
Eddy:Shida yangu sijiwezi,dawa yangu sura yako.
 Mwingine we achomozi nakupenda peke yako
Yasmin:Daima nitakuenzi silitupi pendo lako
Yasmin: usiingie simanzi sura yangu mali yako
Eddy: nakuikosa siwezi sikia langu tamko
Yasmin: mwingine we hachomozi nakupenda peke yako
Eddy: nimefanya uchunguzi nakiri maneno yako, Naiona waziwazi ishara ya pendo lako.
Yasmin: milele nitakuenzi natoa ahadi kwako………
Eddy: kibaya sikivumbuwi ndani ya maungo yako
Yasmin: na mimi simtambui mwenye sifa kama zako……………..wallah sijitambui mgonjwa kwa raha zako
Waliendelea kujibishana maneno yale kwa sauti za chini wakati huo kanga ikiwa tayari imeanguka chini na Eddy akihesabu idadi ya cheni alizokuwa amevaa mwanadada Yasmin zilikuwa nne na shanga tatu!!!!, mwanga wa taa nyekundu pale ndani uliwapa hamasa zaidi hadi wakajikuta wote wapo uchi wa mnyama pale pale sakafuni wakati huo ukilindima wimbo wa mwanamziki  aliyejizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania Ommy Dimpoz uitwao “Baadae” tayari Eddy alikuwa juu ya kifua cha Yasmin na kilichokuwa kinaendelea pale ni “KIDUKU CHA MGUU MMOJA”, wakati miguu miwili ikiwa imetulia tuli mguu mmoja uliosalia ulikuwa bize ukicheza kiduku.
“Kumbe unakiweza kiduku dah!!!” Eddy alimsifu Yasmin aliyekuwa anaona haya wakati akivaa nguo zake

“Kumbe hicho ndo kiduku cha mguu mmoja?????” alihoji Yasmin, Eddy hakumjibu bali aliachia tabasamu tu!!!!!

Kiduku cha mguu mmoja kikawa kimechezwa katika mazingira ya ajabu.


Swali likabaki kwa Yasmin je atajisifia kwa mdogo wake kuwa anaweza kucheza Kiduku cha MGUU MMOJA????.





MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI YA TAR 25 FEBRUARY 2017.


Wema Sepetu Alivyoihama CCM na kuingia  Chadema.


Msanii wa filamu nchi Tanzania Wema Sepetu ametangaza rasmi kukihama Chama cha Mapinduzi CCM na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Akizungumza na waandishi wa habari leo  akiwa ameambata na mama yake mzazi nyumbani kwao Sinza Jijini Dar es Salaam, Wema amesema sababu kubwa ya kuhamia CHADEMA ni ili kupata nafasi ya kupigania demokrasia anayodai kuwa inapotea nchini Tanzania.

Sababu nyingine aliyoieleza Wema ni kutelekezwa na CCM licha ya kujitolea kutoa mchango wake kwa chama hicho wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kiasi cha kuwa hatarini kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar.

"Kuanzia sasa mimi siyo tena mwanachama wa CCM, na muda mfupi ujao nitachukua kadi yangu ya CHADEMA... Nimeamua kuingia CHADEMA kwa sababu nataka kupigania demokrasia, laiti ningejua, ningeingia zamani sana, najua nimewahi kusema kuwa nitakufa nikiwa CCM, lakini sikujua kama itakuwa hivi, laiti ningejua mapema basi nisingesema vile na ningejiunga CHADEMA muda mrefu sana".Amesema Wema Sepetu

Amesisitiza kuwa hajaamia CHADEMA kwa sababu ya pesa kama ambavo imekuwa ikidaiwa, bali ni kwa ajili ya kupigania demokrasia, na kuweka wazi kuwa kuanzia sasa ameingia kwenye mapambano ya kupigania demokrasia akiwa kwenye chama ambacho anaamini kuwa ni chama peke chenye uwezo wa kurejesha demokrasia inayopotea.

"Sijachukua pesa yoyote kutoka CHADEMA, kama nimechukua hata shilingi 10,000 ya CHADEMA basi kaburi la baba yangu huko Zanzibar litikisike" - Amesema Wema

Wema pia amejibu kuhusu baadhi ya wasanii kuidai CCm ambapo amesema "Ni kweli kuna madeni mengi wasanii tunaidai CCM, lakini kila wakati tukidai tunaambiwa tukamdai JK" - Wema Sepetu

Baada ya Wema kukabidhi kadi ya CCM, mama yake pia amerudisha kadi ya CCM na kusema "Tutatembea Tanzania nzima kuinadi CHADEMA".Kauli hiyo ilikuja baada ya mama huyo kueleza jinsi ambavyo CCM haikumtendea haki

Kuhusu sauti zilizosambazwa mitandani zikionesha Mama Wema akiongea na Steve Nyerere, mama Wema amesema "Kuhusu sauti zinazosemwa kuwa ni mimi na Steve Nyerere, siwezi kulizungumzia hilo maana sijazisikia" 

 

Gallery

Popular Posts

About Us