KINGAZI BLOG: 05/12/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 12 May 2017

IMEBAINIKA..Kumbe Robert Mugabe Huwa Halali Bali Hupumzisha Macho tuu

Msemaji wa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kiongozi huyo huwa anapumzisha macho tu na si kulala wakati wa mikutano kama wanavyoamini watu wengi.Kiongozi huyo amekuwa akionekana kusinzia katika mikutano mingi."Rais huwa anasumbuliwa na mwanga mkali," George

Charamba amenukuliwa akisema na gazeti la serikali la Herald.Rais huyo kwa sasa yupo nchini Singapore akipokea matibabu maalum kwenye macho yake.Bw Mugabe, 93, anapanga kuwania tena urais katika uchaguzi mkuu mwaka ujao.

"Huwa najihisi kama mtu ambaye amekosa kutekeleza kazi yake vyema ninaposoma (kwenye vyombo vya habari na mtandaoni) kwamba rais alikuwa anasinzia katika makongamano - la hasha," Bw Charamba amesema.Alilinganisha tatizo la Bw Mugabe na matatizo ya macho ambayo yalikuwa yanamsibu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Bw Mandela alikuwa anatatizwa na mwanga mkali na wapiga picha hawakuruhusiwa kutumia mwanga wa kamera wakati wanapiga picha katika hafla zake.Matatizo ya Bw Mandela yalitokana na kufanya kazi kwa muda mrefu katika timbo na pia kufungwa jela muda mrefu Robben Island.

miliki ya pichaAFPImage captionMacho ya Robert Mugabe hutatizwa na mwanga, msemaji wake amesema. Hapa Mugabe anaonekana akiwa Bamako Januari 13, 2017.Safari za Bw Mugabe za mara kwa mara nje ya nchi zimekuwa zikishutumiwa sana na wakosoaji wake.Sekta ya afya nchini Zimbabwe imedorora na wahudumu wa afya hulalamika kwamba huwa hawalipwi vyema.

Ofisi ya Rais yakanusha taarifa inayosambazwa mitandaoni kuhusu vigezo vya utoaji ajira



Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma afariki dunia leo

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu amefariki dunia leo saa nne asubuhi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Mdogo wa marehemu, Shaibu Mwambungu amesema kaka yake alifariki dunia leo asubuhi baada ya hali yake kubadilika ghafla akiwa hospitalini hapo.

Shaib amesema taratibu za mazishi zitatolewa baadaye ambapo kwa sasa anajiandaa kusafiri kutoka Songea kuja jijini Dar es salam kwa ajili ya mazishi.


TUHUMA za Mateso Dhidi ya Wafanyakazi wa Ndani Oman, Mtanzania Afunguka Makubwa


Wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Wafilipino peke yao ni wengi mara nyingi sana kuliko Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman.

Wapendwa waungwana na wapenda ukweli. Siku hizi za karibuni kumekuwako na upotoshwaji mkubwa wa habari za wafanyakazi wa ndani nchini Oman. Jamani waungwana, Waswahili husema kunya anye kuku akinya bata huambiwa kaharisha. Hizo habari za mayaya Oman ni za fitina na uchochezi uliokithiri na hazitamsaidia mtu yoyote, maana sisi ndio wahitaji zaidi wa hizo ajira nje ya nchi yetu.

Nchi za GCC zimekuwa na utaratibu wa miaka mingi kuajiri wafanyakazi kutoka nchi za Asia. Kwa kuzingatia msemo “mfae nduguyo kwanza” ndipo Waomani wakawa pia na utaratibu wa kuwaajiri wafanyakazi kutoka Afrika Mashariki, kwa kuwa kuna historia ya muda mrefu na ya kidugu baina yao. Sasa imekuwa balaa kila kukicha ni matusi yasiyokuwa na maana ila kutapakaza fitina na chuki kwenye mitandao ya kijamii na hata baadhi ya vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.

Bora nitangulize kusema kitu kimoja ambacho mtu yeyote mwenye akili zake timamu na kupenda kusikia ukweli hawezi kukikataa, nacho ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo haina watu wema na pia watu waovu. Mambo ni kuzidiana tu. Wala hakuna nchi yenye matajiri wenye kuajiri wafanya kazi pasitokee wenye kudhulumu na wenye kudhulumiwa. Kwa vile nazijua vizuri nchi mbili hizi — Tanzania na Oman — naweza pia kusema kwa uhakika kuwa baina ya Tanzania na Oman, utakuta kuwa dhulma wanazotendewa wafanyakazi wa majumbani Tanzania ni kubwa zaidi ukilinganisha na Oman.

Hapa Tanzania wapo wafanyakazi wanaoteseka kila siku na jamaa zao wenyewe kwa mshahara wa shilingi 20,000 au 40,000 kwa mwezi. Sio hilo tu la mshahara, bali hata siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili au zile sikukuu za kitaifa, hawapewi. Haya ni ya ukweli kabisa na wala sio siri. Ukitaka kumtoa mtu kijiti jichoni mwake, kwanza jiangalie kama jicho lako halina boriti.

Hapa Tanzania wafanyakazi wana kila mateso lakini wanavumilia tu. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa haya ya uchochezi uliojaa fitina unatokana na kundi fulani ambalo hawapendelei pawe na masikilizano mema baina ya Waarabu na Waafrika. Na lengo lao hasa hata si Waarabu. Ukipeleleza kwa makini utagundua kuwa wanachokichukia kweli ni dini waliyoileta Waarabu, nayo ni Uislamu.

Katika siku za hivi karibuni kuna sauti zinatumwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hasa WhatsApp na Instagram, zikidai kuwa kuna wafanyakazi wa majumbani nchini Oman wanateswa vibaya hadi kusema kuwa wanauawa kwa makusudi na wengine wanapangiwa njama za kuuliwa ili wawe mihanga kwa majini ya Kiomani. Mojawapo ni sauti ya mama mtu mzima ambaye dhahiri kabisa inaonekana kuwa alitumwa kusudi kutukana dini ya Kiislamu.

Hilo ndilo lengo lao hasa, maana hakuwa na haja ya kutaja maneno kama vile kuwa watu wanasali sala tano kila siku halafu wanatesa watu. Hiyo haikuhusu kabisa. Ikiwa sala tano zinawaudhi basi wataumia sana. Mimi binafsi nimeishi na Mlokole wa Kanisa la Efatah, (mlokole) ni wale wanaojiita wasafi kwa jina la Yesu, huyo mama kila mwezi au wiki tatu hubadilisha mfanyakazi au wanaacha kazi kwa mateso yake. Sasa jee huyu mlokole anashinda kanisani kusali mpaka ndoa zinavunjika, hivyo tumuweke kundi gani? Mbona hawasemi “wanasali siku nzima na makelele mtaani na ni hao hao wanatesa wafanyakazi!” Jamani tuishi kwa kusema ukweli kuwa fitina za uzushi ni mbaya na haupiti muda huwarudia mwenyewe.

Kuna na mwengine ambaye anasema ni Mkenya anayedai kuwa alitaka kuuliwa na waliomuajiri Oman ili akawe kafara kwa mizimu ya Oman. Naye huyu ni mzushi mkubwa na unauona uzushi wake mara moja ukiwa si mtepetevu wa akili na unaweza kupima anayoyasema. Hebu hapa tutumie akili zetu kuchambua aliyoyasema:

Kwanza, anatuambia anakijua Kiarabu vizuri sana bila ya kututolea ushahidi. Lakini, tumkubalie kwa hili.

Pili, eti amewasikia waajiri wake wakipanga njama za kumuuwa ili kumtoa muhanga na akawasikia vizuri; hivyo kweli waajiri hao wapange njama zao mbele yake naye anawasikia!?

Tatu, eti ameingia chumbani kwake na akafungua ‘air condition’ na kupanga mito kama kuwa yeye amelala na kutoroka asije akauliwa na kutolewa muhanga! Tunajuaje kama huu ni uwongo? Jawabu: Waarabu hawakuwa na mila ya kumtoa binadamu muhanga hata katika siku hizo za ujahiliya kabla ya Uislamu, itakuwa leo!? Hii ni mila yao wenyewe baadhi ya Waafrika na anataka kuipandikiza kwa Waarabu! Tafuteni uzushi mwingine, huu hautafaa.

Nne, eti ametaka ubalozi wa Kenya kumsaidia na hawakumsaidia. Wakatae kumsaidia kwa sababu gani? Anasema haya ili tukitaka kuujua ukweli kutokana na Ubalozi tusiweze kuupata. Kwa nini? Kwa sababu anayoyasema si ya kweli kwani kesi zote zinazofikishwa balozini kokote duniani husajiliwa na hatua huchukuliwa na ubalozi. Huyu mzushi sura zake tumeshaziona, sasa na atuoneshe paspoti yake na mihuri ya kuingia na kutoka Oman na viza yake ya kufanya kazi Oman kama mkweli, tutaifuatilia kesi yake.

Tano, kwa vile waajiri wameshafikwa na mengi kutokana na waajiriwa, kuna walioibiwa dhahabu za kina mama, makarani waliofyeka pesa benki na kadhalika na kadhalika, ndio maana waajiri hao huchukua paspoti na kuziweka wao na kumpa mfanyakazi anapotaka kusafiri kihalali; mfanyakazi huwa na kadi tu. Sasa huyo mzushi, paspoti ya kusafiria aliipata wapi? Tiketi alimlipia nani?

Sita, hapana shaka, hata angelikuwanayo paspoti, hapana shaka ilichukua muda kabla ya kuweza kusafiri, hivyo siku ya pili asubuhi waajiri wake walipokuwa hawamuoni, unafikiri nini wangefanya awali? Si wangelipiga ripoti polisi kuwa mtumishi wao haonekani! Unafikiri polisi hufanya nini? Si hupeleka habari katika kila kituo cha usafiri. Na wakishapiga ripoti na popote atakapotaka kuondokea lazima wangelimzuia na wangelimuhoji na kama ana kesi ya kuwashitaki waajiri wake, basi kesi ingelifunguliwa na waajiri kushtakiwa. Sasa huyu mzushi ameondoka vipi Oman!

Nimekuandikieni haya kwa muhtasari tu. Mkifikiria vizuri mtagundua kuna hoja nyinginezo zinalifanya porojo hili kuwa la ki-paukwa pakawa. Hivyo basi, mkipanga njama zenu wazushi wa fitina tumieni akili, kama mnazo!

Mwishoni nasema kuwa wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Idadi ya Wafilipino peke yake ni kubwa kwa mara nyingi sana kuliko ya Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman. Waomani hawana shida ya wafanyakazi. Wala hawatapungukiwa wala kuharibikiwa iwapo wafanyakazi kutoka Tanzania watazuiliwa kwenda kufanya kazi Oman. Sasa kazi kwetu. Kusuka au kunyoa.

WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya



Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.

Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.

Tuliwapa ofisi.

Tulwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng'ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.

Mahusiano na yadumu. 

Afrika ni moja na itabakia kua moja .

By Chiwinga A.

Rufaa Dhidi Ya Mbunge Wa Bunda Mjini Ester Bulaya Yafika Mahakama Ya Rufaa Jijiji Dares Salaam

Aliyekuwa  kuwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Steven  Wassira  akiwa katika jengo la Mahakama ya Rufaa jijiji Dares Salaam akizungumza jambo na baadhi ya mawakili kabla ya kusikiliza kwa Rufaa ya kesi yake dhidi ya Mbunge wa Bunda mjini Ester Bulaya.  Katika kesi hiyo jopo la majaji watatu  wa Mahakama ya Rufaa limepanga kuendelea na kesi hiyo Jumatatu ijayo ya Aprili 15, mwaka huu. Uamuzi huo umetolewa  leo  Aprili 11, mwaka huu katika Mahakama hiyo  baada ya  Pande zote mbili  kutoa maelezo  ya sababu za rufaa. 

 Wakili wa Mbunge  wa Jimbo la Bunda Mjini, Tundu Lissu  akizungumza  jambo na mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya. 

Wakili  Constantine  Mutalemwa  akifafanua  jambo kwa baadhi  ya waandishi  wa habari  mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.

WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya



Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.

Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.

Tuliwapa ofisi.

Tulwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng'ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.

Mahusiano na yadumu. 

Afrika ni moja na itabakia kua moja .

By Chiwinga A.

TUHUMA za Mateso Dhidi ya Wafanyakazi wa Ndani Oman, Mtanzania Afunguka Makubwa


Wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Wafilipino peke yao ni wengi mara nyingi sana kuliko Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman.

Wapendwa waungwana na wapenda ukweli. Siku hizi za karibuni kumekuwako na upotoshwaji mkubwa wa habari za wafanyakazi wa ndani nchini Oman. Jamani waungwana, Waswahili husema kunya anye kuku akinya bata huambiwa kaharisha. Hizo habari za mayaya Oman ni za fitina na uchochezi uliokithiri na hazitamsaidia mtu yoyote, maana sisi ndio wahitaji zaidi wa hizo ajira nje ya nchi yetu.

Nchi za GCC zimekuwa na utaratibu wa miaka mingi kuajiri wafanyakazi kutoka nchi za Asia. Kwa kuzingatia msemo “mfae nduguyo kwanza” ndipo Waomani wakawa pia na utaratibu wa kuwaajiri wafanyakazi kutoka Afrika Mashariki, kwa kuwa kuna historia ya muda mrefu na ya kidugu baina yao. Sasa imekuwa balaa kila kukicha ni matusi yasiyokuwa na maana ila kutapakaza fitina na chuki kwenye mitandao ya kijamii na hata baadhi ya vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.

Bora nitangulize kusema kitu kimoja ambacho mtu yeyote mwenye akili zake timamu na kupenda kusikia ukweli hawezi kukikataa, nacho ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo haina watu wema na pia watu waovu. Mambo ni kuzidiana tu. Wala hakuna nchi yenye matajiri wenye kuajiri wafanya kazi pasitokee wenye kudhulumu na wenye kudhulumiwa. Kwa vile nazijua vizuri nchi mbili hizi — Tanzania na Oman — naweza pia kusema kwa uhakika kuwa baina ya Tanzania na Oman, utakuta kuwa dhulma wanazotendewa wafanyakazi wa majumbani Tanzania ni kubwa zaidi ukilinganisha na Oman.

Hapa Tanzania wapo wafanyakazi wanaoteseka kila siku na jamaa zao wenyewe kwa mshahara wa shilingi 20,000 au 40,000 kwa mwezi. Sio hilo tu la mshahara, bali hata siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili au zile sikukuu za kitaifa, hawapewi. Haya ni ya ukweli kabisa na wala sio siri. Ukitaka kumtoa mtu kijiti jichoni mwake, kwanza jiangalie kama jicho lako halina boriti.

Hapa Tanzania wafanyakazi wana kila mateso lakini wanavumilia tu. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa haya ya uchochezi uliojaa fitina unatokana na kundi fulani ambalo hawapendelei pawe na masikilizano mema baina ya Waarabu na Waafrika. Na lengo lao hasa hata si Waarabu. Ukipeleleza kwa makini utagundua kuwa wanachokichukia kweli ni dini waliyoileta Waarabu, nayo ni Uislamu.

Katika siku za hivi karibuni kuna sauti zinatumwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hasa WhatsApp na Instagram, zikidai kuwa kuna wafanyakazi wa majumbani nchini Oman wanateswa vibaya hadi kusema kuwa wanauawa kwa makusudi na wengine wanapangiwa njama za kuuliwa ili wawe mihanga kwa majini ya Kiomani. Mojawapo ni sauti ya mama mtu mzima ambaye dhahiri kabisa inaonekana kuwa alitumwa kusudi kutukana dini ya Kiislamu.

Hilo ndilo lengo lao hasa, maana hakuwa na haja ya kutaja maneno kama vile kuwa watu wanasali sala tano kila siku halafu wanatesa watu. Hiyo haikuhusu kabisa. Ikiwa sala tano zinawaudhi basi wataumia sana. Mimi binafsi nimeishi na Mlokole wa Kanisa la Efatah, (mlokole) ni wale wanaojiita wasafi kwa jina la Yesu, huyo mama kila mwezi au wiki tatu hubadilisha mfanyakazi au wanaacha kazi kwa mateso yake. Sasa jee huyu mlokole anashinda kanisani kusali mpaka ndoa zinavunjika, hivyo tumuweke kundi gani? Mbona hawasemi “wanasali siku nzima na makelele mtaani na ni hao hao wanatesa wafanyakazi!” Jamani tuishi kwa kusema ukweli kuwa fitina za uzushi ni mbaya na haupiti muda huwarudia mwenyewe.

Kuna na mwengine ambaye anasema ni Mkenya anayedai kuwa alitaka kuuliwa na waliomuajiri Oman ili akawe kafara kwa mizimu ya Oman. Naye huyu ni mzushi mkubwa na unauona uzushi wake mara moja ukiwa si mtepetevu wa akili na unaweza kupima anayoyasema. Hebu hapa tutumie akili zetu kuchambua aliyoyasema:

Kwanza, anatuambia anakijua Kiarabu vizuri sana bila ya kututolea ushahidi. Lakini, tumkubalie kwa hili.

Pili, eti amewasikia waajiri wake wakipanga njama za kumuuwa ili kumtoa muhanga na akawasikia vizuri; hivyo kweli waajiri hao wapange njama zao mbele yake naye anawasikia!?

Tatu, eti ameingia chumbani kwake na akafungua ‘air condition’ na kupanga mito kama kuwa yeye amelala na kutoroka asije akauliwa na kutolewa muhanga! Tunajuaje kama huu ni uwongo? Jawabu: Waarabu hawakuwa na mila ya kumtoa binadamu muhanga hata katika siku hizo za ujahiliya kabla ya Uislamu, itakuwa leo!? Hii ni mila yao wenyewe baadhi ya Waafrika na anataka kuipandikiza kwa Waarabu! Tafuteni uzushi mwingine, huu hautafaa.

Nne, eti ametaka ubalozi wa Kenya kumsaidia na hawakumsaidia. Wakatae kumsaidia kwa sababu gani? Anasema haya ili tukitaka kuujua ukweli kutokana na Ubalozi tusiweze kuupata. Kwa nini? Kwa sababu anayoyasema si ya kweli kwani kesi zote zinazofikishwa balozini kokote duniani husajiliwa na hatua huchukuliwa na ubalozi. Huyu mzushi sura zake tumeshaziona, sasa na atuoneshe paspoti yake na mihuri ya kuingia na kutoka Oman na viza yake ya kufanya kazi Oman kama mkweli, tutaifuatilia kesi yake.

Tano, kwa vile waajiri wameshafikwa na mengi kutokana na waajiriwa, kuna walioibiwa dhahabu za kina mama, makarani waliofyeka pesa benki na kadhalika na kadhalika, ndio maana waajiri hao huchukua paspoti na kuziweka wao na kumpa mfanyakazi anapotaka kusafiri kihalali; mfanyakazi huwa na kadi tu. Sasa huyo mzushi, paspoti ya kusafiria aliipata wapi? Tiketi alimlipia nani?

Sita, hapana shaka, hata angelikuwanayo paspoti, hapana shaka ilichukua muda kabla ya kuweza kusafiri, hivyo siku ya pili asubuhi waajiri wake walipokuwa hawamuoni, unafikiri nini wangefanya awali? Si wangelipiga ripoti polisi kuwa mtumishi wao haonekani! Unafikiri polisi hufanya nini? Si hupeleka habari katika kila kituo cha usafiri. Na wakishapiga ripoti na popote atakapotaka kuondokea lazima wangelimzuia na wangelimuhoji na kama ana kesi ya kuwashitaki waajiri wake, basi kesi ingelifunguliwa na waajiri kushtakiwa. Sasa huyu mzushi ameondoka vipi Oman!

Nimekuandikieni haya kwa muhtasari tu. Mkifikiria vizuri mtagundua kuna hoja nyinginezo zinalifanya porojo hili kuwa la ki-paukwa pakawa. Hivyo basi, mkipanga njama zenu wazushi wa fitina tumieni akili, kama mnazo!

Mwishoni nasema kuwa wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Idadi ya Wafilipino peke yake ni kubwa kwa mara nyingi sana kuliko ya Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman. Waomani hawana shida ya wafanyakazi. Wala hawatapungukiwa wala kuharibikiwa iwapo wafanyakazi kutoka Tanzania watazuiliwa kwenda kufanya kazi Oman. Sasa kazi kwetu. Kusuka au kunyoa.

Mvua Sababisha Maporomoko ya Mawe Tanga..Barabara ya Dar Arusha Yafungwa

Jeshi la Polisi mkoani Tanga imefunga barabara ya kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha kufuatia eneo la Mombo mkoani Tanga kuangukiwa na maporomoko ya mawe pamoja na matope na kusababisha athari kwa baadhi ya magari

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani humo Benedict Wakuyamba  amesema, maporomoko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani humo na maeneo mbalimbali nchini

"Hali ya mvua imeendelea kunyesha na kufukia barabara eneo la Mombo kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha ambapo matope na miti vimesombwa na kukwama barabarani hali iliyokwamisha magari makubwa kwa madogo kusafiri kupitia eneo hilo..Niwaombe abiria au wananchi kwa ujumla kama hawana ulazima wa kusafiri kwenda mikoa ya Kaskazini ni vizuri wakatulia kwa siku mbili tuone hali inakwendaje kwa ajili ya usalama wao". Alisema Kamishna Msaidizi Benedict

Kwa upande mwingine Kamishna huyo amesema TANROADS na Jeshi la Polisi mkoani humo wanaendelea kusaidia kuondoa magogo na tope zilizosakama katika barabara ili kunusuru hali ya usafiri

 

Gallery

Popular Posts

About Us