IMEBAINIKA..Kumbe Robert Mugabe Huwa Halali Bali Hupumzisha Macho tuu | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 12 May 2017

IMEBAINIKA..Kumbe Robert Mugabe Huwa Halali Bali Hupumzisha Macho tuu

Msemaji wa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kiongozi huyo huwa anapumzisha macho tu na si kulala wakati wa mikutano kama wanavyoamini watu wengi.Kiongozi huyo amekuwa akionekana kusinzia katika mikutano mingi."Rais huwa anasumbuliwa na mwanga mkali," George

Charamba amenukuliwa akisema na gazeti la serikali la Herald.Rais huyo kwa sasa yupo nchini Singapore akipokea matibabu maalum kwenye macho yake.Bw Mugabe, 93, anapanga kuwania tena urais katika uchaguzi mkuu mwaka ujao.

"Huwa najihisi kama mtu ambaye amekosa kutekeleza kazi yake vyema ninaposoma (kwenye vyombo vya habari na mtandaoni) kwamba rais alikuwa anasinzia katika makongamano - la hasha," Bw Charamba amesema.Alilinganisha tatizo la Bw Mugabe na matatizo ya macho ambayo yalikuwa yanamsibu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Bw Mandela alikuwa anatatizwa na mwanga mkali na wapiga picha hawakuruhusiwa kutumia mwanga wa kamera wakati wanapiga picha katika hafla zake.Matatizo ya Bw Mandela yalitokana na kufanya kazi kwa muda mrefu katika timbo na pia kufungwa jela muda mrefu Robben Island.

miliki ya pichaAFPImage captionMacho ya Robert Mugabe hutatizwa na mwanga, msemaji wake amesema. Hapa Mugabe anaonekana akiwa Bamako Januari 13, 2017.Safari za Bw Mugabe za mara kwa mara nje ya nchi zimekuwa zikishutumiwa sana na wakosoaji wake.Sekta ya afya nchini Zimbabwe imedorora na wahudumu wa afya hulalamika kwamba huwa hawalipwi vyema.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us