KINGAZI BLOG: 05/03/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 3 May 2017

Hatimaye Serikali Imesikia Kilio cha Watumishi Waliosingiziwa kuwa na Vyeti Feki

DODOMA: Serikali imetoa nafasi kwa watumishi wanaodhani kuwa wameonewa, baada ya kutajwa kwenye orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi (feki) waandike barua ya kukata rufaa na kwa katibu mkuu wa wizara ya utumishi kuanzia kesho ili malalamiko yao yashughulikiwe haraka. 

Hatua hiyo imefikiwa leo Bungeni baada ya Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi, Rhoda Kunchela kuomba mwongozo wa spika kuhusiana na suala la baadhi ya watumishi kudai kuwa wameonewa kwenye sakata hilo. 

Akitoa mwongo huo, Kunchela amesema kuwa sakata la vyeti feki limeibua malalamiko mengi miongozi mwa watumishi waliokumbwa na suala hilo huku wengine wakidaiwa ‘kuchanganyikiwa’ na kupoteza mwelekeo wa maisha. 

Akitolea ufafanuzi suala hilo, Waziri wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki amelieleza Bunge kuwa, serikali imewapa nafasi watumishi wote wanaodhani kuwa wameonewa kwenye sakata hilo basi waandike barua za rufaa ya malalamiko yao na waiwasilishe kwa katibu mkuu wa wizara hiyo ili malalamiko yao yashughulikiwe mapema. 

“Kwa wale ambao wanafahamu kabisa kwamba vyeti vyao ni vya kugushi, wasithubutu kukata rufaa kwa kuwa ikibainika tena kwamba wamefoji, hatua kali zaidi zitachukuliwa.” Alisema Kairuki.

Kifungo cha maisha jela kwa kuchoma nyumba

MKAZI wa kijiji cha Kabita wilayani Busega mkoani Simiyu, Hezroni Mahila (28) amehukumiwa kutumikia kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kuchoma nyumba na kusababisha hasara ya Sh. 6,000,000.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa Simiyu, John Nkwabi, baada ya mtuhumiwa kukubali kutenda kosa hilo.

Awali kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Moses Mfuru, alieleza mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Februari 24, mwaka jana, saa 8:00 usiku kwa kuchoma nyumba mali ya Kapeji Sostenes.

Baada ya kusomewa shtaka lake, mshtakiwa alikiri kutenda kosa hilo na kuomba kupunguziwa adhabu kwa madai kuwa hakuisumbua mahakama lakini hakimu alimhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha maisha.

MAALIM Seif: Ni afadhali Nikae Meza Moja na CCM Kuliko Kukaa na lipumba.


Maalim Seif katika Mahojiano na Clouds asubuhi hii amesema kuwa hawezi kamwe kukaa meza moja na Profesa Lipumba.

Amesema ni bora akae na CCM kwani anawajua kabisa ni adui lakini si msaliti Lipumba na kusisitiza "Mimi siwezi kukaa na Msaliti"

Akaulizwa kuwa mbona hapo nyuma aliwahi kuwa na uhasama wa wazi kabisa na Sumaye lakini baadaye alikaa naye meza moja UKAWA?

Akasema uhasama wake na Sumaye ulikuwa wa tofauti za kichama na alimjua wazi kuwa ni adui kwani alikuwa CCM lakini kwa Lipumba ni tofauti kwani ni msaliti.

Maalim Seif: CUF kwa sasa inaendeshwa kwa pesa za michango ya wanachama. Matajiri hawaji CUF kwani wakiwajua TRA watawasumbua.

Unamzungumziaje Rais Magufuli?

Pamoja na kuwa ni mtu anayepigania haki, asiyependa Rushwa na Ubadhilifu lakini kuna watu hata wafanye nini hawachukulii hatua. Kwa nafasi yake hapaswi kuwa na double standards.

Unadhani kuna uhuru wa vyombo vya habari?

Hakuna uhuru wa vyombo vya habari. Sheria ya Habari ni mbaya kwa wanahabari. Si vema Waziri kupewa uwezo wa kufungia chombo cha habari.

Jecha alifuta uchaguzi kwa ubabe bila kushirikisha wenzake sababu hata katiba ya Zanzibar haimpi mamlaka ya kufuta uchaguzi

Lipumba si mwanachama wa CUF, na Magdalena Sakaya amesimamishwa uanachama, hivyo yote wanayofanya ni batili

Hakuna CUF ya Lipumba au CUF ya Maalim Seif, maamuzi yote ya chama yanafanywa na Baraza Kuu la chama

NACY MASOUND -MPENZI - New Official Audio || MP3 DOWNLOAD|| KINGAZI BLOG | Official Sites.

Download new official Audio From The Best Upcoming Artist in Tanzania NACY MASOUND
CLICK HERE
Image result for download

TANZANIAN NEWSPAPER OF TODAY MAY 2017


























Magazeti ya Leo Jumatano ya May 3



























 

Gallery

Popular Posts

About Us