KINGAZI BLOG: 04/11/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 11 April 2017

Picha za Mrembo maarufu wa Kenya Anayeozea Gerezani Ghana Baada ya Kunaswa na Madawa ya Kulevya


Huyu dada anaitwa Pesh, ni mrembo maarufu sana Kenya lakini hivi sasa anaozea Gerezani Kenya.Huyu dada inadaiwa alikuwa na mpnz wake aliyekuwa anaishi Ghana ambaye ndie aliyemuingiza kwenye hii biashara.
==>Safisha macho kw picha zake hapo chini
tangaz

Roma:Hii Sio Kiki, Tumeteswa Jamani..!!!


NYOTA wa miondoko ya Hip Hop nchini, Roma Mkatoliki amejitokeza hadharani na kusema kuwa, kilichowakumba kwa kutekwa na watu wasiojulikana si kitendo cha kusaka kiki ama limetengenezwa kisiasa, bali ni la kweli na wameteswa.

Roma aliyetekwa pamoja na wenzake wawili katika studio za Tongwe Records, aliyasema hayo katika mkutano wake na wanahabari ambao ulihudhuriwa pia na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.

Msanii huyo aliyeonekana mnyonge alieleza kuwa tukio la kutekwa kwao sio kiki ama lililotengenezwa kwa kutumiwa kisiasa ila jambo lililotokea kweli na limewapa hofu kubwa kwa sababu hawakuwahi kuhisi litakuja kuwakumba.

"Kuna watu wanasema hii ni kiki, hawa watu wanafikiri tunafanya na wengine wameenda mbali sana kwamba tunatumika kisiasa. Wengine wanaenda mbali zaidi kusema kana kwamba wanajua zaidi," alisema Roma na kuongeza;

"Kuna watu wamesema tumepewa hela tufanye hivi, inaumiza sana kuna wasanii wengine wamesema kwamba tumepewa hela, si kweli. Sisi ni maskini na tunaishi maisha ya kawaida sana, hatuwezi kurisk (hatarisha) maisha yetu kwa sababu hiyo. Tunahisi itamtokea mwingine na tutakuwa katika nafasi mbaya sana."

Msanii huyo alifunguka namna walivyofuatwa na watu hao na kisha kuwapeleka kwenye gari kabla ya kuwafunga macho kwa vitambaa na kuanza kuwahoji, huku wakiwatesa mpaka walipotolewa kwenye gari na kutelekezwa wakiwa hoi.

"Ilikuwa ni usiku sana nilijitahidi kujifungua kitambaa na kamba. Nilifanikiwa na kuwafungua wenzangu tukaanza kutembea pasipo kujua Tunaenda wapi hadi tulipokikuta kibao kimeandikwa mahaba Beach ndipo tukagundua ni Ununio, baada ya hapo tukapata msaada wa polisi mpaka polisi Central," alisema.

Roma aliwashukuru wote wakiwamo wasanii kwa ushirikiano walioonyesha kiasi cha kuweka mbali itikadi zao kipindi chote alipokuwa haonekani, lakini akisisitiza kuwa hali ni mbaya na lazima serikali iwasaidie wasanii kuwa salama.

Alisema yeye na wenzake wamekuwa na hofu ya usalama wao, kwa namna hali ilivyowabadilikia wakati waliamini studio waliokuwa wakifanyia muziki ilikuwa salama kwao kabla ya kukumbwa na kisanga hicho, huku akieleza alivyoteswa kiasi fulana yake kuwa nyakanyaka kwa damu zilizomtoka, ingawa hakufafanua zaidi.

"Kama alifanyiwa daktari akaja akafanyiwa mwingine usishtuke kesho akafanyiwa daktari au yoyote. Wito wangu kuhusu hili kwa serikali tunaomba waziri atulinde bado hatuna Amani tangu juzi kuna picha inaingia bado tunahitaji ulinzi, watu wapaze sauti ili wasikie wengine kusaidia," alisema Roma Waziri Mwakyembe alisema ameshtushwa sana aliposikia taarifa hizi nilishtuka na kujiuliza kila chombo cha dola kimekiuka utaratibu wake wa kuwasiliana naye kwa tatizo lolote la wasanii.

"Ni lazima tujue nani amewafikisha wasanii wangu hapa, tunaomba ushirikiano wenu wote tumeshtushwa hili siyo jambo la kawaida kwa Watanzania. Siwezi kukubali tukachezea chezea watu hawa waliofanya kitendo hiki kwa sasa tumeunda vyombo vya upepelezi kupata majibu ya kina sana," alisema Waziri.

A-Z ya Mkasa mzima!!!.. Roma Asimulia Ilivyokuwa Baada ya Kutekwa..!!! SOMA HAPA


Hatimaye rapper Roma amesimulia mkasa wa kutekwa akiwa na wenzake watatu kuanzia Jumatano iliyopita hadi Ijumaa. Tumekuandikia kile alichosimulia.

Wakati naendelea na shughuli zangu, walifika watu ambao sikuweza kuwafahamu mbaya zaidi walikuwa na silaha za moto na amri yao ya kwanza ilikuwa ni ingia ndani ya gari. Baada ya kuingia tu ndani ya gari, nakumbuka wale watu walitufunga usoni na vitambaa na kutuamuru tuiname chini kwa order ya kwamba inama chini na usiinuke na wakiwa wameshika silaha za moto. Hofu yetu ikatufanya wote tuiname chini na gari ikaanza kuondoka maeneo ya studio na ikaelekea ambako sisi hatukupajua.

Tulipofika hiyo sehemu ambayo hatuijui tukiwa tumefungwa usoni, na walitufunga na pingu. Tukaenda sehemu ambayo hatuijui, kwa kuhisi tu hujui chochote na ndio sehemu ambayo tulikaa kwa siku zote tatu kwasababu ilikuwa ni Jumatano, Alhamis, tunakuja kupata sisi usalama ilikuwa ni Ijumaa usiku kuamkia Jumamosi. Kwahiyo siku zote watu kilichokuwa kinaendelea huko ambako tupo na hatupafahamu, kuna mahojiano yalikuwa yanaendelea baina yetu na wale watu, mahojiano yenyewe ndio hizo details ambazo nasema tumesharipoti katika vyombo vya dola wanaendelea na upelelezi, wakimaliza upelelezi, wao wenyewe wataongea watatoa taarifa.

Lakini mahojiano hayo yaliendana na vipigo ambavyo nimeonesha majereha. Kila mtu alipata majereha, kila mtu alipigwa, kwahiyo mahojiano yalikuwa yanaendelea na hizo torture mpaka siku ya Ijumaa usiku sababu hatukuwa tunaweza kugundua ni saa ngapi. Tulitolewa hapo tulipokuwepo na kuingizwa ndani ya gari na safari ilipoanza hapo tukiwa tumefungwa vilevile lakini safari hiyo tulifungwa na mdomo, tukafungwa na miguu tukiwa ndani ya gari tukaenda umbali ambao hatukuweza kujua ni wapi mpaka kufika eneo ambalo tukatupwa tukiwa katika hali hiyo wote wanne.

Ilikuwa ni usiku sanam hatukuweza kujua ni wapi lakini tulifikiri ni kwenye dimbwi tu la maji tumetupwa. Niliweza kujifungua mimi wa kwanza nikawafungua na wenzangu, hatukujua ni maeneo gani lakini yalikuwa maeneo ya baharini, tulikuwa na maumivu sana. Nilivyoweza kuwafungua wenzangu tukajikuta tuko salama, tukaanza kutembea kwa muda kiasi na baada ya muda tukakutana na kibao fulani kimeandikwa mahaba beach tukagundua kuwa pale ni maeneo ya Ununio. Tulitembea kwa umbali mrefu sana mpaka tulipoweza kupata msaada baada ya hapo tukaenda kuripoti maelezo yote katika kituo cha polisi.

ALIPOFIKA NYUMBANI

Tulipofika Mbezi mimi nagonga mlango, ndani hakuna mtu, nikazunguka mlango wa nyuma nikavunja mlango wa nyumbani kwangu. Kuingia ndani familia hakuna, hilo lilikuwa pigo jingine kwangu sababu sikujua familia yangu nayo imeenda wapi. hiyo ikawa hofu nyingine, kwahiyo tulichokifanya nikawaambia tubadilishe nguo nikachukua nguo nikawa wenzangu, tutokea katika zile nguo za matatizo. Nikawaambia kama familia haipo nadhani hapa si salama, ilikuwa inaelekea alfajiri saa kumi saa kumi na moja ikabidi tutoke tutafute bajaji tukiwa katika mavazi salama ikawa ni nafuu kwetu. Tulipotafuta bajaji tukaomba namba ya simu ya bajaji kumpigia mtu. Na mtu wa kwanza kumpigia ni bosi wetu J-Murder, hakutuamini kwamba ni sisi kwasababu ya kile alichokuwa anajua kinaendelea uraiani.

Ukweli Kuhusu Kutekwa kwa Roma Huu Hapa... Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 11


























 

Gallery

Popular Posts

About Us