KINGAZI BLOG: 03/02/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Thursday 2 March 2017

Aunt Ezekiel Afunguka Juu ya Mimba Alizowahi kutoa.


Msanii wa filamu Aunt Ezekiel amefunguka kwa kudai kuwa ameshawahi kutoa mimba kadhaa lakini hajui ni ngapi

Muigizaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja aitwae Cookie, akijibu swali la shabiki wake kupitia Kikaango cha EATV aliyetaka kujua idadi ya mimba ambazo amewahi kutoa, Aunty alisema hawezi kusema uongo kuwa hajawahi kutoa mimba, lakini kitu ambacho hakumbuki ni idadi ya mimba alizowahi kutoa.

“Kutoa nishawahi, nikisema sijawahi nitakuwa muongo, ila kukumbuka ni mimba ngapi ndiyo tatizo,”alisema staa huyo wa filamu.

Muigizaji huyo ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano na dansa wa Diamond Platnumz, Mose Iyobo, amesema kwa sasa anatamani zaidi kupata mtoto wa kiume atakamuita jina la Greyson ambalo ni jina la babu yake.

Rais Magufuli Amteua Mama Salma Kikwete Kuwa Mbunge

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 01 Machi, 2017 amemteua Mhe. Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Salma Kikwete ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Salma Kikwete ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zitakazotangazwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

RC Makonda Yamkuta Juu ya Elimu Yake..ni moja ya Habari Katika Magazeti ya Leo alhamisi march 2



Inasikitisha Sana..Wamchoma Moto Hadi Kifo kwa Kisingizio cha Kumtoa Mapepo...!!!


MWANAMKE mkazi wa Managua, amekufa baada ya kufungwa kamba na kurushwa kwenye moto na watu wanaodhaniwa wafuasi wa dhehebu la dini kwa lengo la kuteketeza mapepo.

Watu wa familia yake wameviambia vyombo vya habari kuwa, Vilma Trujillo (25) alishambuliwa na watu wanne wakiongozwa na mtu aliyetajwa kuwa ni mhubiri.

Mhubiri huyo, Juan Rocha amekusha tuhuma za kumuua mwanamke huyo kwa kumchoma moto.

Amedai kuwa, Trujillo amekufa kwa kuwa pepo wabaya walimchukua mwanamke huyo na kumrusha motoni.

Mwili wa mwanamke huyo ulipatikana ukiwa na majeraha makubwa ya moto.

Maofisa wa polisi walimkamata Rocha na watu wengine wanaohusishwa na tukio hilo la kumchoma kwa moto Trujilo.

Mume wa mwanamke huyo, Reynaldo Perlata Rodriguez amesema mkewe alichukuliwa na kupelekwa kanisani wiki iliyopita wakati wafuasi wa kanisa hilo walipodai ana mapepo baada ya kujaribu kuwashambulia watu kwa panga.

"Hatuwezi kuwasamehe kwa kile walichotufanyia, alinukuliwa akisema. Walimuua mke wangu mama wa watoto wangu wawili. Nitawaambia nini watoto wangu?" amesema.

 

Gallery

Popular Posts

About Us