KINGAZI BLOG: 09/16/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 16 September 2016

TCU YAONGEZA MUDA WA UDAHILI WA VYUO VIKUU MEAKA 2016/17.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imeongeza muda wa udahili wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mwaka wa masomo 2016/2017 ili kuwapa fursa  waombaji ambao wana sifa lakini hawakupata vyuo kutokana na ushindani wa vyuo na kozi walizozichagua.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mtendaji wa TCU Prof. Eleuther Mwageni alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya mwenendo mzima wa udahili kwa mwaka wa masomo 2016/2017, leo  Jijini, Dar es Salaam.
“ Tume imekamilisha awamu ya kwanza ya udahili kwa waombaji wenye sifa ya kidato cha 6, ambapo jumla ya waombaji wote ilikuwa 55,347, waombaji wenye sifa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3 ya waombaji wote. Katika waombaji hao wenye sifa waliopata vyuo ni 30,731 sawa na asilimia 65 na waombaji 16,472 ambao wana sifa sawa na asilimia 35 hawajapata vyuo hadi sasa, waombaji waliokosa sifa ni 8,144,” alifafanua Prof. Mwageni.

Amesema kuwa Tume imeamua kuongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 mpaka Septemba 23, 2016 ili kuwapa nafasi waombaji wenye sifa, fursa ya kuomba tena vyuo na kozi zenye nafasi kutokana na  wengi wao kuomba vyuo na kozi za aina moja.

Prof. Mwageni alivitaja vyuo ambavyo vimeombwa na waombaji wengi na tayari vimeshajaa kuwa ni Chuo cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afya na Sayansi Shirikishi, Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba Kilimanjaro(KCMUCo) na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.

Pia alizitaja kozi ambazo zimechaguliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo kuwa ni kozi ya Ualimu, Udaktari wa Binadamu, Ufamasia, Uhandisi, Sayansi ya Uthamini wa Ardhi na Sheria. Alitoa mfano wa kozi ya Ualimu Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000.

Hivyo amewashauri waombaji waliokosa nafasi kuomba vyuo na kozi zisizo na ushindani ili waweze kupata nafasi kwa awamu hii ya pili.

Aidha Tume hiyo imepunguza viwango vya udahili kwa waombaji wenye sifa ya stashahada kutoka GPA 3.5 mpaka 3.0. Hivyo wamewataka waombaji wenye vigezo hivyo kuomba vyuo na kwa wale waliomba awamu ya kwanza hawatatakiwa kuomba tena bali kusubiri matokeo ya waombaji wenye sifa ya stashahada.

NEWS: TAMISEMI YATOA TAMKO HILI KUHUSU AJIRA ZA UALIMU,UHAMISHO NA KUPANDISHA MADARAJA 2015/2016


Hivi karibuni kumezuka tabia za utapeli unaofanywa na wanaojisadikisha kuwa ni watumishi wa Umma au Mawakala wa kusimamia uhamisho wa Watumishi kuhama kutoka Mkoa mmoja kwenda Mkoa mwingine na pia kujihusisha  na kutoa taarifa za uongo kwa   kugushi nembo za Ofisi ya Rais.

– TAMISEMI kuhusu ajira, kupandisha madaraja ya walimu.

Yamekuwepo Malalamiko mengi kutoka kwa wahanga/waathirika wa tabia hiyo kwa nyakati tofauti ambayo watumishi wamehadaiwa kuwa watasaidiwa kuhamia sehemu yoyote wanayoihitaji baada ya kulipa kiwango cha fedha ambacho hupangwa na wahalifu hao. Miongoni mwa taarifa batili wanazosambaza ni Uhamisho na Ajira za Walimu.

Matangazo hayo pia yameonekana katika mbao za matangazo za baadhi ya Halmashauri. Mara nyingi watu hao huweka namba zao za simu kwa ajili ya kupokea fedha za uhamisho kutoka kwa watumishi pamoja na kuweka anuani za barua pepe zinazosadikiwa kutumika katika kukusanya barua za maombi ya uhamisho.

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) inapenda kuchukua fursa hii, kutoa taarifa hii kwa lengo la kuujulisha Umma wa Watanzania juu ya kuwepo kwa uhalifu huu ili waweze kujiepusha nao.

Ofisi ya Ras –TAMISEMI haitasita kuchukua hatua za Kisheria kwa wale wote watakaobainika kujihusisha na uhalifu wa aina hii.

Tunasisitiza kuwa wananchi wafuate taratibu na pia watambue kuwa hakuna malipo yoyote yanayotakiwa ili kuhamisha mtumishi. Wananchi wanaombwa kutoa taarifa pale watakapoona kuna utapeli unaoendelea katika masuala ya ajira na uhamisho.

Watumishi wanaweza kufahamishwa juu ya taratibu za uhamisho katika Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri na pia kupitia tovuti ya Ofisi ya Rais -TAMISEMI  (www.tamisemi.go.tz).

Ofisi ya Rais TAMISEMI haijatoa matangazo yoyote yanayohusiana na Ajira za Ualimu katika kipindi hiki.

Imetolewa na:-

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Ofisi ya Rais,

Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,

15 Septemba, 2016.

MASTAA WALIVYOKARIBISHWA BUNGENI DODOMA LEO KABLA YA KUPIGA SHOW YA TIGO FIESTA LEO



September 16 2016 historia nyingine itaandikwa ndani ya viwanja vya makao makuu ya nchi Dodoma ambapo burudani ya FIESTA 2016 inatarajia kudondoshwa hapo kutoka kwa wasanii mbalimbali wa bongo.
Asubuhi ya leo baadhi ya wasanii na wafanyakazi wa Clouds media walipata nafasi ya kutembelea bunge ili kujionea utendaji kazi unavyofanyika na hapa nimekuzogezea picha 13 za mastaa hao kuanzia nje hadi ndani.

Baadhi ya wafanyakazi wa Clouds media na wasanii wakiwa nje ya bunge

Wasanii G Nako na Jux wakiwa nje ya bunge

Joh Makin

Mtangazaji wa XXL B 12 pamoja na wasanii wengine ndani ya bunge

Kutokea kushoto Chege, Snura, B 12

Kutoka kushoto Maua sama, Mr Blue, Adam Mchomvu




Update: Watanzania Wenzetu Waliokuwa Wametekwa huko DRC Congo Wameokolewa

Madereva wa malori kutoka Tanzania waliokuwa wametekwa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hatimaye wameokolewa na vikosi vya jeshi la nchi hiyo.

Waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo amezungumza na shirika la utangazaji la BBC na kusema wote wameokolewa   na wako salama

Taarifa iliyotolewa jana  na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilieleza kuwa watekaji hao ni kikundi cha waasi cha MaiMai ambao baada ya kuyateka magari 8 toka Tanzania , waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Bw. Dewji.

Waasi hao walioa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia.

HIZI HAPA NAFASI NA VIGEZO VYA SCHOLARSHIPS ZA OMAN KWA MWAKA 2016/2017

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI FORM 6 WALIOCHAGULIWA MARIAN UNIVERSITY 2016/2017-FIRST BATCH

 

Gallery

Popular Posts

About Us