KINGAZI BLOG: 02/21/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 21 February 2017

JE UNA TATIZO LA KUTOPATA RAHA WAKATI WA TENDO LA NDOA.?? Soma hapa👇👇


Wapo ambao wakati wanapofanya mapenzi badala ya kupata raha, husikia maumivu, mwanaume katika uume lakini ni mara chache sana kulinganisha na wanawake. Mwanamke ndiye husumbuliwa zaidi na tatizo hili.

Mwanamke anaweza kukosa raha kabisa na matokeo yake kuumia wakati tendo linapoanza pale mwanzoni ukeni au kwa ndani zaidi. Maumivu haya pia yanaweza kugawanyika katika makundi mawili. Kwanza ni maumivu wakati wa tendo ambayo ndiyo hayo tuliyoyaona hapo juu na maumivu baada ya tendo.

Kuumia wakati wa tendo
Maumivu haya hutokea pale uume unapoanza kuingia ukeni na hutokana na uke kuwa mkavu.
Hili linaweza kusababishwa na maandalizi duni kabla ya tendo, matatizo katika mfumo wa homoni au kupoteza msisimko na hamu ya tendo.

Kubana kwa misuli ya uke pia huchangia ingawa tatizo hili zaidi ni la kisaikolojia kutokana na mwanamke kuwa na woga wakati wa tendo.
Kuwa na makovu ukeni kutokana na athari za kukeketwa, uwepo wa michubuko na vidonda au

maambukizi ukeni mfano fangasi ya muda mrefu na maambukizi mengine hasa magonjwa ya ngono.
Uvimbe ukeni au uwepo wa jipu na vipele, kuumia kwa kufanyiwa vipimo au baada ya kuzaa kwa njia ya kawaida endapo hukupona vizuri.

Kuhisi maumivu baada ya tendo
Maumivu haya hutokea muda mfupi baada ya tendo la ndoa. Mwanamke huhisi maumivu kwa ndani zaidi ukeni au chini ya tumbo. Maumivu huwa makali na huchukua muda mrefu.
Maumivu ya chini na ndani zaidi ukeni huleta hisia kama muwasho mkali wa pilipili au kama

unakatwakatwa na viwembe na ukinawa unazidi kupata maumivu.
Maumivu ya ndani zaidi ukeni wakati mwingine huambatana na hali ya kuhisi kama kuna kitu kinasukumwa wakati wa tendo na unapomaliza tendo ukinawa unahisi kitu kimevimba ndani ukeni

kama kigololi. Maumivu huwa chini ya tumbo na wakati mwingine husambaa kulia na kushoto ya mirija. Wengine huumwa na kiuno hata kutembea inakuwa shida mara tu baada ya kumaliza tendo.

Hali ikiwa mbaya mwanamke hutokwa na damu baada ya tendo, hali ambayo siyo dalili nzuri kwani hata saratani ya shingo ya uzazi nayo huonyesha dalili hii ya damu.
Hali ya maumivu pia huambatana na kutokwa na majimaji ukeni wakati mwingine yakiambatana na muwasho mkali na harufu. Hata wanaume wanaweza kutokwa na damu baada ya tendo badala ya manii.

Nini cha kufanya?
Tatizo hili ni kubwa na lina vyanzo vingi kama tulivyoona, hivyo ni vema kufanya uchunguzi kujua chanzo halisi ndiyo tiba ifuate.

Epuka kutumia dawa bila ya kujua chanzo halisi.
Uchunguzi hufanyika katika hospitali za mikoa, wilaya kwa madaktari wa magonjwa ya kinamama.
Ni vema uwahi hospitali.

LIKE FB PAGE INAITWA ...@HABARI ZOTE HAPA.

Hizi hapa Sifa za Mwanamke Asiyefaa Kuolewa Asilani

SUALA la kuoa lipo tu licha ya kwamba wapo wanaochelewa kuingia kwenye maisha hayo wakihisi inaweza kusitisha furaha ya maisha yao. Nasema hivyo kwa kuwa najua wapo wanaoamini kuoa ama kuolewa ni kujiingiza kwenye matatizo.

Dhana hiyo haina mashiko kiviile, asikuambie mtu unapoingia kwenye ndoa na mtu anayekupenda na wewe unampenda kwa dhati, karaha hakuna licha ya kwamba kugombana kwa hapa na pale hakuwezi kukosekana.

Hata hivyo, nikiri tu kwamba, zipo ndoa ambazo ni ndoano. Yaani unakuta mtu kaingia kwenye ndoa na mtu ambaye hakuwa amedhamiria, matokeo yake kadiri siku zinavyokwenda anahisi ameingia chaka na anaishia kuomba ndoa isiwepo.

Leo nataka kuwazungumzia wanawake ambao ni majanga na ukijichanganya ukaingia nao kwenye maisha ya ndoa, utakiona cha mtemakuni.

10. Asiyeridhika na penzi unalompa
Wapo wanawake ambao wewe unaweza kujitahidi kumpatia mapenzi kadiri unavyoweza lakini yeye hatosheki. Anakuchukulia wewe ni dhaifu sana na wakati mwingine kuhisi yupo mwingine anayeweza kumpa zaidi ya kile unachompa, huyu ni tatizo.

9. Wivu kupindukia
Hatukatai, wivu ni muhimu sana kwenye suala la mapenzi lakini kuna ule wivu uliopindukia kiasi cha kuwa kero. Walio kwenye ndoa wananielewa namaanisha nini.

Kwa kifupi mtu mwenye mapenzi ya dhati na mwenziye lazima awe na wivu lakini ukiwa na ule wa kupinduki ni tatizo linaloweza kuitibua ndoa.

8. Anaona unamsaliti kila mara
Huku kunatokana na kutokujiamini tu. Ukioa mwanamke ambaye kila wakati unapokuwa mbali naye anahisi unamsaliti, huyo hakuamini na kamwe hamuwezi kudumu. Mara kadhaa mtakuwa mkigombana akihisi una mwingine kumbe hakuna ukweli katika hilo.

7. Anahisi amekosea kuwa na wewe
Wapo wanawake ambao wanapoingia kwenye ndoa baada ya muda wanahisi wamekosea kuolewa na mwanaume huyo. Unakuta mke wa mtu anahisi fulani ambaye zamani alikuwa kwenye uhusiano naye angekuwa sahihi zaidi baada ya kuona upungufu fulani kwa huyo aliyemuoa.

6. Yuko kimasilahi zaidi
Kuna wanawake ambao ukiwaoa wanakuwa na furaha na wewe ukiwa unazo tu, ukiishiwa wanaanza kununa na kuleta visirani vya hapa na pale. Hawa ni tatizo, mwanamke wa kweli ni yule anayeridhika kuwa na wewe kwenye shida na raha

5. Yuko tayari kuachana na wewe
Hivi hujawahi kumsikia mke wa mtu akimwambia mumewe; ‘Kama vipi tuachane, kwanza kwetu sijafukuzwa na nilikuwa nakula, nalala, navaa.” Mwanamke anayeweza kumtamkia mume wake maneno haya, huyo si mke na kamwe hawezi kukufanya uwe na furaha.

4. Hapendi ndugu zako
Waswahili wanasema ukipenda boga, penda na ua lake. Kama utatokea kuoa mwanamke ambaye anakupenda wewe tu lakini akija ndugu, rafiki au mtu mwingine wa karibu yako anabadilika, huyo ana matatizo kwani atakufanya utengwe na jamii yako.

3. Anajali mafanikio binafsi
Siku zote wawili waliotokea kupendana wakioana wanakuwa mwili mmoja hivyo lazima watakuwa wanawaza na kufanya maamuzi pamoja.

Ogopa sana mwanamke anayependa kutumia kipato chake kufanya mambo binafsi tena kwa siri. Kwa mfano kusaidia kwao, kujenga nyumba kwao, kuanzisha miradi yake bila kukushirikisha.

2. Eti akizaa utamzeesha
Hili kwa wale wanaopenda kuoa masistaduu. Wapo ambao wakitajiwa suala la kuzaa mara baada ya kuingia kwenye ndoa wanagoma wakidai eti watazeeshwa hivyo waachwe kwanza wale ujana. Wakati huo unaweza kukuta mwanaume anataka mtoto ili apate ile heshima, mke anagoma kwa sababu hiyo isiyo na msingi, hili ni tatizo.

1. Anataka awe na sauti
Mwanaume siku zote atabaki kuwa kiongozi wa familia lakini wapo baadhi ya wanawake hawataki kukubaliana katika hilo. Wengi wanalazimisha usawa na wengine wakitaka wao ndiyo wawe na sauti kuliko.

CHOMBEZO: NILAMBE HUMO HUMO == 5

                                    BOFYA

Image result for WAKUBWA TU BONYEZA HAPA

MTUNZI: HUSSEIN WAMAYWA
SEHEMU YA TANO
Wengine ndugu zao wa kiume walikuwa wamewadhulumu mali za urithi walioachiwa na wazazi wao, wengine walikuwa yatima walioondokewa na wazazi wao na kukosa mtu wa kuwaangalia! Wengine walikuwa wametupwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa wengine… wengine!
Basi ilimradi kulikuwa na mlolongo wa matatizo ambayo kwa hakika yalichusha na kuudhi.
Hofu ya ukimwi je?
Walikuwa nayo lakini wangefanyaje? Waliona bora waishi kwa furaha leo kwa kuwa hata kesho wasipokufa kwa ukimwi kama watajitunza, basi watakufa kwa njaa, umasikini na adha zingine kadha wa kadha.
Ugunduzi huu ukanifanya nisiwatizame kwa jicho baya tena, bali nikawaona kama wahanga fulani hivi!
Nikajitengenezea utaratibu mzuri wa kwenda pale na kuhudumiwa mara nne kwa wiki! ulikuwa utaratibu nilioupenda na kuufuatisha kama ibada, utaratibu mtamu kweli, mtamu haswaa.
* * *
Asubuhi kulipokucha, Akimu allikuja kunigongea, nikainuka na kufungua mlango.
‘’Mambo?’’ Akanisalimu akiingia ndani.
“Poa!’’
‘’Vipi mbona hivi, leo huendi?”
‘’Wapi?” Nikamuuliza kwa wasi wasi kidogo.
‘’Mara hii umesahau kuwa juzi tulikubaliana kwamba leo tutakuwa na round discussion kuhusu Utambuzi wa Short na mitihani ya mwisho inayokuja?
“My God!’’ Nikaguta. Nilishasahau kabisa, ukweli leo sikujisikia kujadili chochote mwenyewe nilikuwa nataka masaa yaende mbio jioni niende zangu uwanja wa miutamu.
‘’Sorry Akimu!’’ Nikamwambia Akimu “Sitaweza kuja katika discussion leo nataka nifue then nipumzike kabla sijajisomea kisha nitakwenda mahala!’’
‘’Lakini tulikubaliana utakuja!’’
“Ndio hivyo tena!’’
‘’Basi itakubidi umueleze Shamsa kabisa maana binti yule asipokuona hasomi sawa sawa!’’ Nikatabasamu “Nitamwambia!’’ nikajibu.
Wakati anataka kujibu akakiona kitabu cha gwiji wa riwaya nchini marehemu Eddie Ganzel ’Kijasho chembamba’, vile anavyopenda riwaya za Ganzel akainuka na kukitwaa.
Alipokiinua tu kadi za mapenzi, zenye picha nzuri na maua ya kuvutia pamoja na barua za mapenzi zikaonekana chini yake, akaniuliza maswali machache kuhusu nilikokipata kitabu kile, halafu akauliza
‘’Hivi haya maua na hizi kadi bado tu hujazipeleka kwa Shamsa?’’
“Bado!’’
Akimu akanitumbulia macho kwa mshangao!
Alikuwa na haki ya kushangaa, alikuwa nayo. Mosi ni
yeye aliyekuwa mwandani wangu, alifahamu vingi na mengi kunihusu, pili alikuwa shuhuda wa macho wa namna nilivyoathirika kwa kumpenda binti yule.
Na ni yeye aliyetoa ushauri wa kumpelekea zana hizo na kama vile haitoshi alikuwa amenisindikiza kuzinunua, kubuni maneno mazuri yaletayo faraja na kuyaandika juu ya kadi hizo, tena alikuwa amenitaka kumpelekea haraka iwezekanavyo ili kama kuna lolote tulijadili kwa pamoja.
Na sasa ulikuwa umepita mwezi na kidogo toka tulipoziandaa
“Kwanini hujazipeleka? Ibra usiniambie ulikosa ujasiri, maana nilikwambia wewe ukishindwa kumkabidhi nipe mimi nitamkabidhi!’’ Akatua kwa kila hali alikuwa na hasira, mimi nikatabasamu na kumjibu.
‘’Nimeona haina haja Akimu!’’
‘’Eti?!’’
‘’Enh! Hanisumbui tena nimesha muweka chini ya himaya yangu!’’ ikawa zamu yake kunitazama kwa mshangao, nusu akitabasamu nusu akitaka kushangilia.
‘’ Ina maana umeisha… umeisha….! Mungu wangu, mbona siamini!’’
‘’Sijafanya nae mapenzi wala hajanikubali niwe mpenzi wake! Ila nimemdhibiti, hanisumbui tena! Maelezo yangu yakazidi kumchanganya Akimu. Akanisaili tena.
‘’Unamaana gani Ibra?’’
‘’Nina maana kuwa kuna mahala ninapoupoza moyo wangu kwa maji baridi, maji ya ya mapenzi, maji ya uzima!’’
“Inamaana umepata mpenzi mpya unayempenda kuliko Shamsa?”
“Sijasema simpendi Shamsa!’’ Nikasema kwa karaha “Nikingali nampenda na nitaendelea kumpenda maisha yangu yote!”
‘’Basi nyoosha Kiswahili Ibra, hata hao wahenga misemo na mithali zao zilieleweka kwa urahisi!’’
“Nitakwambia!” Nikamwambia huku tabasamu likiwa limeupamba mdomo wangu “Nitakwambia rafiki yangu, tena nitakwambia ukweli mtupu naomba tu uniwie radhi kwa kukuficha!”
Nikakaa vizuri na kumueleza ugunduzi wangu wa kule Fisi. Nilimueleza kwa tuo pasipo kuacha hata tukio moja. Nilipo maliza Akimu alikuwa ameshika kichwa kama aliyepoteza kitu cha thamani sana!
‘’Ni kweli unielezayo Ibra?” Sasa machozi yalikuwa yakimlenga
‘’Ni kweli kabisa!’’
‘’Umepotea rafiki yangu, tena umepotea vibaya sana. Sio watu wale ni balaa!’’
‘’Tatizo lao liko wapi Akimu? Kama nilivyo kwambia nimewastadi vya kutosha kabla ya kuamua kuwa nao chanda na pete.
‘’Hawako salama wale! Kila mwaka wanakufa! Na wanakufa na idadi kubwa sana ya watu! Hii ni kwa vile wanafanya mapenzi na watu wengi sana, wengine hutembea mpaka na wanaume elfu sita na mia sita kwa mwaka hadi elfu saba na mia mbili.
Ni washenzi wa tabia wasio na utu walioamua pesa iwe yao kwa kila hali, ukiwa na pesa unaweza kumwambia akuuzie hata utumbo wake na akakuuzia! Zaidi na zaidi ni wabaya wazee na wasiovutia kwa chochote! Ndio maana nasema umepotea!”
Akiwa na jazba Akimu alitumia zaidi ya robo saa kuwaponda makwini wa fisi. Alipomaliza ndipo nami nilipoanza kum’bishia. Tulibishana sana na mwisho wa siku ikawa imeamuliwa mimi na yeye twende uwanja wa fisi wote akajionee, nae akasisitiza mimi nikajionee, tukaondoka mchana huo huo!
Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuingia uwanja wa fisi mchana. Eh! zaidi ya maajabu yalikuwa yakinisubiri
Wanawake karibuni wote waliokuwa wakiuza miili yao walikuwa watu wazima hasa, wazima kweli, umri umekwenda mno. Sura zao zilikuwa tisho jingine. Mbali ya kuwa zimekomaa kwa namna ya kuchusha, huo mkorogo waliojimwagia sikuwahi hata kuufikiria. Mkorogo hadi mapajani! Mkorogo hadi miguuni, hadi katika matiti!
‘’Niliwezaje kufanya mapenzi na watu hawa?” nikajiuliza nikitikisa kichwa kwa masikitiko. Nikajuta. Akimu akanikokota tukarudi chuoni nikiwa nimenyongea.
‘’Kwanini uliamua kuja huku Ibra?” Akanisaili kwa upole baadae.
‘’Msongo rafiki yangu! Mhemko! Nilihemkwa na kutamani ngono kupita kitu chochote! Nikaona huku ndio pa’ kuponea! Laiti ningelijua…,” Nikalia kimya kimya. Akimu akinifariji.
Kwa shinikizo lake niliweza kushiriki katika Round discussion ingawa nilipooza Kama ugali uliokosa moto wa kuuivisha sawa sawa. Shamsa alikuwepo na alifurahi kuniona, nikamtaka radhi kuwa sikuwa nikijisikia vizuri.
Mpaka tunamaliza majadiliano yetu sikuwa nimechangia lolote!
* * *
‘’Kanini umenileta huku Akimu? Nikamuuliza tukitembea kutoka sokoni, tulikuwa Songambele, kijiji kimoja kilichoko mkoani pwani ndani kabisa wenyewe walikuwa wamekibatiza jina la Gobba , ingawa jina lake la asili lilikuwa Songambele Sotele.
Kilikuwa kijiji ambacho Akimu alisomea elimu yake ya sekondari kabla hajafaulu vizuri, akakataa kuendelea na masomo ya juu na kuja kusomea umeme pale VETA. Hili lilijiri kwa kuwa Baba yake alikuwa fundi umeme aliyefanikiwa sana kimaisha kupitia kazi hiyo.
“Nimegundua rafiki yangu u’mhanga wa starehe! Starehe ya mapenzi. Huku utaburudika utastahali na kuneemeka vya kutosha. Na uzuri wanawake wa huku hawatokitoki hovyo nje ya vijiji vyao kwahiyo ni salama kwa kiasi kikubwa!”
Akanijibu. Angejua nilivyojiapiza kutofanya tena mapenzi tangu ulipojiri ule ugunduzi wa yaliyopo Uwanja wa fisi, wala asingejisumbua! Moyoni mwangu alibakia Shamsa pekee na vile tulibakiza miezi sita tuhitimu, nilijua nitamtamkia wakati huo na kitakachofuatia ni ndoa mara moja.
Nikiendelea kutembea, niliendelea kukiperuzi kijiji hiki cha Gobbah kuona kama kingeweza kunifariji. Hakikuwa na chochote cha kujivunia! Mifugo michache yenye siha na afya ya wastani, wakazi ambao mwonekano wao uliashiria umasikini uliotukuka na ardhi kubwa yenye rutuba ambayo haikuwa imelimwa, vilikuwa baadhi ya vitu vilivyoipamba Songambele Sotele a.k.a Gobbah.
Jioni tulikuwa baharini, tuliogelea na kufurahi pamoja na wenyeji wa eneo hilo ambao walikuwa na ukarimu unaovutia. Halafu tukaelekea mpirani. Usiku tulikuwa kwenye vijiwe vya kahawa ambapo tulipiga soga mpaka usiku ulipokomaa, tukaenda kulala.
Siku mbili zilizofuatia tuliishi katika mtindo huu.
Wakati nimeanza kuchoshwa na maisha haya katika siku ya tatu na nikiwa tayari kumwambia Akimu turudi Dar es salaam; ndipo lilipotokea lile ambalo ni miongoni mwa mambo matatu muhimu yalinifanya nishike peni na karatasi na kuandika mkasa wangu huu ambao Uncle Wamaywa ameamua kuuita chombezo.
‘’Jiandae Ibra,’’ Akimu Aliniambia kwa bashasha. ‘’Leo kuna ngoma! Watoto aina kwa aina wanakusanyika toka kata nzima. Hii hakuna kulala ni kutimbwirika hadi majogoo!”
Nikamtazama nisimuelewe! Ngoma ni miongoni mwa vitu ambavyo sikuwa na hobi navyo, Nikamuuliza taratibu hali nikiwa nimemkazia macho. ‘’Najua unajua kwamba mimi sipendi ngoma!”
‘’Najua sana, lakini hii tunaita ngoma kimazoea! Jina lake hasa ni mnanda!”
“Mnanda?!”
‘’Ndiyo!”
‘’Mnanda ni nini na Ngoma ni nini?!”
‘’Yanini tuandikie mate il-hali wino upo? mnanda unaanza saa kumi na mbili jioni na sasa ni saa kumi jioni subiria masaa mawili tu utapata majibu timilifu, majibu ya vitendo! Jiandae tu!”
Maswali yalikuwa mengi kichwani, lakini kila nilipomuuliza Akimu jibu lake lilikuwa moja tu. ‘’Jiandae, jiandae!’’
Nikajiandaa.
Kweli, jioni tukakusanyika mnandani watu aina na aina wakijisogeza na kumsherehekea binti huyu anayeolewa. Wasichana na niseme wanawake walikuwa wamejikwatua vilivyo na walikuwa wakijituma hasa pale dimbani.
Nikashangaa kwa kuwa sikuwa nimewaona kabla. Akimu akinijulisha kuwa nisingeweza kuwaona kwa kuwa ule ni mkusanyiko wa watu kutoka kata nzima na pengine tarafa.
‘’Mambo zaidi utayaona usiku!’’ akahitimisha wakati nikianza kusisimkwa! Ule uchezaji wao ulivutia kwa hakika, ulikuwa uchezaji ambao ungekulazimisha kuangalia huku mwili ukipatwa na joto ghafla.
****Nini kitajiri USIKU huu unaosemwa……IBRA tayari amesisimka….
Tukutane kesho tena/


                                 WAKUBWA TU BONYEZA HAPA

Mbowe tayari Kaachiwa Huru baada ya Kuhojiwa na Kupekuliwa Usiku

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe ameachiwa saa saba na robo usiku wa kuamkia leo baada ya kuhojiwa na kupekuliwa na Jeshi la Polisi.

 

Mbowe alikamatwa jana Jumatatu jioni wakati akienda kujisalimisha polisi na kupekuliwa nyumbani kwake kabla ya kuhojiwa hadi alipoachiwa usiku wa manane.

 

Ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene amethibitisha  taarifa za kuachiwa mwanasiasa huyo kuwa ni za kweli.

 

Hata hivyo, taarifa iliyosambazwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu kupitia mitandao ya kijamii imesema kuwa chama hicho kitatoa taarifa zaidi juu ya tukio hilo leo.

 

“Tunawashukuru wote kwa sala, maombi na subira na hivyo kuhitimisha salama saa kumi za mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam,” Mwalimu amesema.

 

Gallery

Popular Posts

About Us