KINGAZI BLOG: 02/26/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Sunday 26 February 2017

Taarifa Muhimu: TCU yatolea ufafanuzi uhakiki wa wanafunzi wasiokuwa na Sifa Vyuoni

Tume ya Vyuo  Vikuu  Tanzania (TCU)  inapenda kuuarifu umma kuwa, uhakiki wa ubora wa wanafunzi wa elimu ya juu

hufanyika kwa mujibu  wa Kifungu  5(1)(b)(c)  cha Sheria ya

Vyuo Vikuu Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania.

 

Katika kutekeleza jukumu hili Tume ilianza zoezi la uhakiki kuanzia mwezi Agosti 2016. Hadi kufikia Februari 2017 zoezi

hilo lilikuwa limekamilika kwa vyuo 67 kati ya 84 vinavyotoa shahada ya kwanza. 

Hii ni mara ya kwanza uhakiki wa sifa za wanafunzi wa vyuo  vyote nchini kufanyika kwa wakati mmoja.  Lengo  la uhakiki lilikuwa kujiridhisha kuwa wanafunzi waliopo vyuoni ni wale waliodahiliwa kwa mujibu wa  sheria na taratibu  na kwamba wanakidhi vigezo  stahiki.

 

Uhakiki ulifanyika kwa kulinganisha taarifa za TCU na zile zilizowasilishwa na vyuo.  Uhakiki huo  ulihusisha jumla ya wanafunzi 131,994 waliopo vyuoni kwa mwaka wa masomo 2016/17.

 

Baada ya kulinganisha orodha zilizowasilishwa na vyuo na ile ya TCU ilibainika kuwa wanafunzi 123,827 sawa na asilimia 93.8  wana sifa stahiki.  Aidha jumla ya wanafunzi 8,167 sawa na asilimia 6.2 tu walibainika kuwa na kasoro  katika taarifa za sifa zao.

Kufuatia hali hiyo, Tume ilitoa taarifa kwa umma kuwaomba wanafunzi kurekebisha dosari hizo  kwa kuthibitisha taarifa zao  kupitia vyuo  husika ifikapo  tarehe 28  Februari 2017  ili kuweka kumbukumbu sahihi za mwanafunzi.

 

Hata hivyo  imebainika kuwa taarifa hiyo  imepokelewa kwa mtazamo na hisia tofauti na hivyo kusababisha mkanganyiko vyuoni. Umma unaarifiwa kwamba haikuwa nia wala lengo la Tume kusababisha mkanganyiko huo.

 

Kwa kuwa uhakiki wa sifa za wanafunzi ni kazi endelevu ya Tume na kutokana na maombi ya wadau  mbalimbali,  Tume sasa  itaendelea kuwasiliana moja kwa moja na vyuo  katika kukamilisha zoezi hilo. 

Hivyo  wanafunzi wote waliokuwa wameorodheshwa katika taarifa iliyotolewa awali wanaombwa kuwa watulivu  na kuendelea na masomo  yao kama kawaida.

 

Aidha ifahamike kuwa wanafunzi waliokuwa wameorodheshwa siyo kwamba wamethibitika kuwa hawana sifa stahiki bali kuna dosari katika taarifa zao. Ndiyo sababu Tume iliwaomba kuthibitisha taarifa zao  ili kuondoa dosari hizo.

 

Imetolewa na

Kaimu Katibu Mtendaji

24 Februari 2017

Je, ulikuwa ukiyajua haya kabla??

UMEWAHI ONA HII...

💞chumvi ikizidi kwenye wali weka kiazi mviringo katikati kikiwa kimemenywa chumvi itapungua.

💞kama choo chako, kina harufu, ya mkojo na huna dawa washa kiberiti chooni harufu itakwisha

💞chukua ganda la limao lichome na vipisi vya karafuu weka kila pembe ya chumba mbu utawasikia kwa jirani

💞kutoa harufu kwenye wali uliongua weka kipande cha mkaa harufu ya kuungua itakata

💞km umepika mchuzi upo maji maji yaani mwepesi labda maji yamezidi chukua kiazi kikune na cha kukunia nyanya weka chuzi litakuwa rost

💞kuivisha maharage faster chukua maji yalochemka tia maharage weka kwenye chupa ya chai funga kesho mimina kwenye sufuria pika nusu saa harage litakuwa lishaiva

💞ukipika mchuzi vitunguu vikiungua weka sukari kidogo harufu ya kuungua haitasikika

💞Ukiamaliza kuosha vyombo still wire iweke kweny maji haiharibiki utaendelea kutumia kesho

💞big g ikiganda kwenye nguo weka kweny friza ikiganda itatoka kirahisi

💞kuondoa harufu ya uvundo kwenye fridge weka baking soda kwenye kikombe na maji kidogo weka kwenye fridge

Ukiipenda mpe au share na mwenzio

Mađãda poa Dar waanza kushughulikiwa

MKUU wa wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Ali Hapi, ametoa onyo kwa wamiliki wa baa wanaowahifadhi watu wanaojihusisha na biashara ya ngono ‘Machangudoa’ kuwa watafutiwa leseni.

Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kata ya Kijitonyama waliodai kuwa kuna baadhi ya baa zimekuwa zikiwahifadhi wanaouza miili, hali ambayo ni hatari kwa mazingira na makuzi ya watoto.

Hapi amesema haiwezekani serikali iwe inapambana na biashara hiyo haramu lakini kuna baadhi ya baa zinawafuga machangudoa.

"Tutashughulika na changudoa na tutashughulika na wenye baa zinazowahifadhi machangudoa, kwa sababu hili ni suala lililo kinyume cha sheria, serikali inapambana na hili tatizo halafu mwingine analikumbatia, hilo haliwezekani, tutawachukulia hatua za kisheria," amesema.

Awali, akitoa malalamiko yake kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Mama Salma Kikwete, mkazi wa Kijitonyama alidai kuna baa zilizogeuka kero kwao.

Ameitaja baa iitwayo Kona ya Sinza imekuwa ikiwahifadhi machangudoa hivyo kuhatarisha makuzi ya watoto kwa kuwa wanaweza kuiga tabia zisizofaa.

"Hii baa iko hapo Afrika Sana, machangudoa wako pale wanajiuza hadharani, sasa kwa kweli hii ni kero kubwa kwetu, watoto wanaweza kuiga na matokeo yake tutakuwa na kizazi kibaya ," amesema mwananchi huyo.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI YA TAREHE 26 / 2 / 2017



































 

Gallery

Popular Posts

About Us