KINGAZI BLOG: 04/08/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 8 April 2017

UMEIPATA HII??Mkuu wa Freemason Duniani Kutua Tanzania na Mafreemason zaidi 300


Mazishi ya mkuu Sir Andy chande (88 years) aliyefariki huko Nairobi Kenya yanatarajiwa kufanyika Jumanne ijayo kwa mwili wake kuchomwa moto mpaka kuteketea wote (cremation.)

Wageni zaidi ya 300 kutoka nje ya nchi wakiongozwa na Freemason mkuu watahudhuria mazishi yatayofanyika hapa Dar. Booking za guest watazofikia wageni mashughuli wa freemason zinaendelea kufanyika kwa kasi ya ajabu hapa jiji zina la dsm.

Kumbuka Sir Andy chande alikuwa kiongozi wa Freemason, mmiliki wa shule ya shaaban Robert, Ashawahi kuwa mkuu wa makumbusho ya Taifa (mkabala na IFM).

Baada ya post ya Gwajima, Diamond Platnumz amuandikia ‘chondechonde’

Hazijafika saa 72 toka mwimbaji wa Bongofleva Diamond Platnumz aachie wimbo mpya ambao unagusia yanayoendelea sasa hivi Tanzania ambapo baada ya Askofu Gwajima kuusikia, alitumia time yake kupost kwenye Instagram yake haya maneno hapa chini.

Baada ya Diamond Platnumz kuona post hiyo ya Askofu Gwajima ameyaandika yafuatayo >>> “Yala! Yala! Jamani Mwenzenu nimeyatimba….. lakini mi nafkiri watu wanatakiwa waiskilize hii nyimbo kwa umakini sana tena sana na wataelewa nini ilikuwa maana yangu haswa… Hususani kama kipengele nilichomtaja mzee wangu@Bishopgwajima

“Nilisema: “mara nasikia vya aibu Konda na Gwajima eti ugomvi umekolea….ila kuchunguza kwa karibu ni kuna binti mmoja tu ndio kwa mitandao anachochea…” point yangu ni kwamba licha ya kweli kuna yaliyojiri nyuma lakini kwa busara zao ninazoamini wamejaaliwa na Mwenyez Mungu muda si mref wangekaa chini na kumaliza na wote kufurahi kwa pamoja

“Lakini kwakuwa kuna dada mwingine alikua anachochea hawa ndugu zetu wazidi kufarakana…ikapelekea hadi kufikia hapa…asa hapo kosa langu mie liko wapi? chondechonde mzee wangu@Bishopgwajima usinigeuze maji kesho , mana nakujua ukimuamulia mtu…. naweza jumapili ya kesho nikaiona chungu Mwaka mzima

Kamanda aahidi Siro Kumsaka Roma na wenzake popote walipo!!

JESHI la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limeazimia kumtafuta msanii wa muziki wa Bongo Hip Hop Ibrahim Mussa, (Roma) wa wenzake.

Roma , Monii (msanii),(Bin Raden mtayarisha muziki wa studio hiyo) na emmanuel  walitekwa na watu wasiojulikana siku ya tarehe 5 Aprili mwaka huu usiku wa kuamkia alhamis kwenye kwenye makoa ya studio hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamshna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Simon Sirro ,amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi linamsaka Roma na wenzake pamoja na kuunda timu maalamu.

Kamanda Sirro amesema kuwa amesema kuwa jeshi hilo linaendelea na Upelelezi na kwamba tayari jarada wa uchunguzi wa tukio hilo tayari umeshaundwa.

Amewasisitiza wananchi kuliamini jeahi hilo na kuwa wavumilivu jeshi hilo likiwa linafanya uchunguzi.

Hata hivyo jeshi hilo  limewataka wananchi kuwa na imani na jeshi hilo

Umeisikia Kauli ya Makonda kuhusu akina Roma.?? SOMA HAPA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, ameahidi Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wengine wawili watapatikana Jumapili hii baada ya wasanii hao kutekwa na watu wasiojulikana Jumatano hii wakiwa Tongwe Record.

Alisema hayo jana akiwa nyumbani kwake Masaki jijini Dar es salaam, muda mchache baada ya kutembelewa na wasanii ambao walimtaka mkuu huyo kuwasaidia kupatikana kwa wasanii hao.

Akiongea na waandishi mbele ya wasanii hao, RC Makonda alisema kila mtanzania ana nafasi ya kumtafuta Roma na wenzake kwa kuwa hakuna anayejua watu hao wako wapi.

“Natoa pole kwa ndugu pamoja na marafiki, hakuna mtu ambaye anaweza kupotelewa na mtu akawa na furaha na bahati mbaya tunahangaika kujua wapi waliko. Nitumie fursa hii kuwaambia wananchi wa mkoa wa Dar es salaam kwamba tunapopotelewa na ndugu zetu katika mazingira ambayo hatuyafahamu sio wakati ya kuyarusha rusha maneno na kufika hatua tunapoteza ushahidi,” alisema RC Makonda.

Alisema tayari ameliagiza jeshi la polisi kufuatia suala hilo kwa ukaribu zaidi ili kupata ufumbuzi mapema huku akiahidi mpaka Jumapili hii watu wao watakuwa wamepatikana.

Imefichuka !!! Kumbe Hiki ndicho kilichomuua Bosi wa Freemason Tanzania

MWILI wa aliyekuwa Kiongozi wa Jumuiya ya Freemason Tanzania na Afrika Mashariki, Sir Jayantilal Keshavji Chande (89) ‘Andy’ Chande, umewasili juzi kutoka jijini Nairobi nchini Kenya alipokuwa akipatiwa matibabu.

Akizungumza na MTANZANIA mmoja wa wafanyakazi wa Sir Chande ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini, alisema kiongozi huyo aliyefariki juzi alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya tumbo.

“Mwili wake umeshawasili tangu jana (juzi) saa 2:30 usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) na wamerudi wote pamoja na familia yake yaani mkewe na watoto watatu waliokuwa wakimuuguza,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alisema kwa sasa mwili huo umehifadhiwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam, ukisubiri maziko yatakayofanyika Jumanne ijayo.

Mbali na hilo pia alishangazwa na kusambaa kwa taarifa za kifo hicho kwa haraka juzi kwa kuwa familia hadi jana mchana ilikuwa haijapata taarifa rasmi.

“Mzee ni mtu mkubwa si Tanzania tu hata India, Marekani wote wameandika habari zake baada ya kusikia katika mitandao, lakini bado watu hawajaanza kuja kutoa pole, wengi wanapiga simu kuuliza tu kama ni kweli sisi tumeshangaa taarifa hizi mmezitoa wapi wakati hakukuwa na mtu aliyetoa habari  kutoka katika familia jana,” alisema mfanyakazi huyo.

Alisema Sir Chande ambaye anatarajiwa kuchomwa Jumanne katika eneo la Makumbusho, aliugua tumbo kwa kipindi cha wiki moja wakati ugonjwa wake mkubwa uliokuwa ukimsumbua ulidaiwa kuwa ni shinikizo la damu.

Alisema vikao vya familia bado vinaendelea na kwamba wageni kutoka nchi mbalimbali wanatarajiwa kuingia kuanzia Jumapili kuhudhuria mazishi hayo.

Aidha, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana jioni na msemaji wa familia ya Sir Chande ambaye ni mtoto wake, maziko ya kiongozi huyo yatafanyika Jumanne saa nne asubuhi katika makaburi ya Makumbusho jijini Dar es Salaam.

“Taratibu za kuaga mwili wa Sir Chande zitafanya siku hiyo hiyo kuanzia saa 2.30 asubuhi nyumbani kwake,” ilieleza taarifa hiyo.

FAMILIA YAMWELEZEA

Katika taarifa, familia yake pia ilimwelezea Kiongozi huyo kama mtu aliyekuwa na hekima ambapo mara nyingi alikuwa anaisaidia Serikali na Watanzania na watu wengine duniani kote kwa kujihusisha na shughuli za kijamii, uchumi na misaada ya kibinadamu.

“Katika kutambua hilo, Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza alimtunuku medali ya heshima ya kuwa Commander of the Civil Division of the Most Excellent Order of the British Empire (KBE),” ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, wakati akitoa maoni ya tuzo hiyo alisema anashangilia kushuhudia Mtanzania aliyestahili kutunukiwa ‘Order of Knighthood in the British Empire’.

Familia yake pia imesema Chande aliwahi kupewa tuzo ya heshima ya Pravasi Bharatiya Samman kutoka kwa Rais wa India ambayo inatambulika kwa kiasi kikubwa nchini India kama mwanachama wa Diaspora.

Mwaka 2004, Chande alichapisha hotuba zake pamoja na mafundisho na habari kuhusu Freemason katika kitabu kinachoitwa Whither Directing Your Course na mwaka 2011 alichapisha kitabu kingine cha Transitions of a Life na kingine  ‘A Knight in Africa: Journey From Bukene.

Vitabu vyake viligusa maeneo mbalimbali ikiwemo historia, biashara, mazingira, elimu na mambo ya kijamii.

Taarifa hiyo ya familia pia imeelezea namna Sir Chande alivyoshiriki katika harakati za ukombozi na uhuru nchini.

Inaelezwa uzalendo wa Sir Chande katika taifa kwa mara ya kwanza ulijitokeza mwaka 1967 katika harakati za maazimio ya Arusha wakati wa biashara ya familia yake, kiwanda cha Chande Industries Limited kilitaifishwa kwa Serikali Februari 7, 1967.

Hayati Mwalimu Nyerere alimwalika Chande kusaidia kuanzishwa kwa Shirikisho la viwanda vya kusaga na kuchakata (National Milling companies).

Alikubali kwa uaminifu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa National Milling Corporation kwa miaka mitano, baada ya kustaafu alitumikia kama mshauri wa Bodi ya Wakurugenzi.

Kati ya mwaka 1958 hadi 1961 kabla ya uhuru wa Tanzania, Sir Chande inaelezwa alitumikia katika nafasi ya mwanachama wa Legislative Council (LEGICO ).

Mwaka 1959, alipata nafasi ya kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Katibu Mkuu wa Serikali ya Uingereza, Ian McLeod, kuhusiana na mapendekezo ya Uingereza kutoa uhuru wa kujitawala kwa Tanganyika.

Baada ya uhuru, Chande inaelezwa alishiriki katika shughuli mbalimbali nchini hasa za kijamii na kiuchumi.

Kwa nyakati tofauti aliwahi kuwa Mwenyekiti au kama mwanachama wa Bodi ya Wakurugenzi wa makampuni kadhaa ya umma na binafsi ikiwa ni pamoja na Benki ya Barclays Tanzania na Uganda na pia mashirika mbalimbali ya Serikali ikiwa ni pamoja na Shirika la Reli la Afrika Mashariki na East African Harbors Corporation.

Kufuatia kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977, Sir Chande, aliteuliwa kuwa mwanzilishi na Mwenyekiti wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na baadaye Mwenyekiti wa Mamlaka ya Bandari Tanzania na wa Tanzania Railways Corporation.

Inaelezwa pia Chande alikuwa anajishughulisha na masuala ya kisiasa na kidiplomasia, wakati mmoja aliwahi kuwa mshauri wa Wizara ya Kamati ya Umoja wa Afrika ambayo inashughulikia masuala ya migogoro ya mafuta nchi za Waarabu.

Nyumbani kwake Masaki

Mazingira ya nyumbani kwa Sir Chande,  Masaki hayaonyeshi eneo hilo kama kuna tukio lolote kubwa kutokana na ukimya uliokuwepo jana.

Mwandishi wa gazeti hili ambaye alifika nyumbani hapo mchana, alishuhudia wana ndugu wachache pamoja na watoto waliokuwa ndani.

Ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na waombolezaji wapatao watano waliokuwa wakionekana sebuleni huku baadhi ya wana ndugu wakitajwa kuwa eneo la juu la nyumba hiyo wakiendelea na kikao cha kupanga taratibu za mazishi.

Sir Chande alizaliwa Mei 7, mwaka 1928 nchini Mombasa, Kenya ameacha mjane Jayalaxmi na watoto watatu.

Hatua kwa hatua atakavyochomwa

Baada ya mwili wa marehemu kuingia ndani ya jengo lakuchomea maiti, Wahindi huvunja nazi tatu katika kaburi lililo karibu kabisa na lango kuu.

Baada ya hapo mwili huletwa katika tanuru lenyewe na hupangwa kuni juu ya tanuru hilo ambalo limeundwa mithili ya kitanda cha chuma.

Kuni hupangwa kwa ustadi mkubwa na zile za ukubwa kiasi hupangwa katika umbile la reli na magogo makubwa manne hupangwa kushoto, kulia Magharibi na Mashariki ya tanuru hilo ambapo kuni zinakuwa nyingi.

Kabla ya kuchoma maiti

Kabla ya kuuweka mwili katika tanuru huuzungusha mara nne kulizunguka tanuru hilo.

Baada ya hapo, mwili wa marehemu ukiwa na sanda huwekwa katikati ya kuni hizo, kichwa kikielekezwa Magharibi.

Kabla ya uchomaji wenyewe kuanza, mila za Wahindu hutaka kuhakikisha iwapo kweli ndugu yao amefariki.

Ndugu mmoja wa marehemu hutakiwa kuhakiki kwa kuchukua kipande kidogo cha kuni chembamba kilichoshika moto, kisha humchoma marehemu katika unyayo mara nne huku akilizunguka tanuru.

Hatua inayofuata ni kuchukua moto kwa kutumia makoleo maalumu, kisha kuuchanganya moto huo na mafuta ya samli.

Mwili wa marehemu hupakwa mafuta ya samli kuanzia usoni mpaka miguuni kabla ya kuwasha moto, baada ya hapo moto huwashwa na unakuwa moto mkali zaidi ya gesi.

Mafuta ya samli pamoja na mafuta ya marehemu mwenyewe husaidia moto kuwa mkali kuliko kawaida.

Wakati moto unaendelea kuwaka kwa kasi, mbegu za ufuta hurushwa juu ya mwili unaoendelea kuungua na ndugu za marehemu ambao wanakuwa wamelizunguka tanuru.

Uchomaji mwili kawaida huchukuwa saa mbili au mbili na nusu kumalizika au kuteketea kabisa.

Baada ya mwili kuungua na kwisha kabisa, kinachotakiwa kubaki ni vipande vya mifupa, lakini wakati mwingine moto huweza kwisha kabisa na wakati huo mwili bado haujamalizika.

Baada ya mwili kuchomwa na kwisha, ndugu mmoja wa marehemu huchukua chungu maalumu kilichojazwa maji na kukiweka katikati ya miguu, kisha anatakiwa kutazama Magharibi akiyapa kisogo mabaki ya mwili huo wakati huo waombolezaji wote wanageuka pia.

Anachofanya ndugu huyo wa marehemu akiwa amesimama ni kuchukua jiwe na kukipiga chungu hicho kwa nguvu hadi kivunjike na maji yamwagike kuelekea lilipo tanuru.

Baada ya tukio hilo yeye pamoja na umati wote wa waombolezaji hutakiwa kuondoka bila kugeuka nyuma.

Kwa upande mwingine baada ya mwili kuchomwa na moto kumalizika kabisa, mabaki ya mwili hutolewa kama vipande vya mifupa ya mwili na fuvu, vilivyochanganyika na majivu na mkaa kutoka tanuruni.

Mifupa hiyo huwekwa katika mifuko maalumu na hatua ya mwisho ni ndugu kwenda kuyatupa baharini.

Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond Platnumz ameachia wimbo wake mpya kwa kushtukiza uitwao ‘Acha Nikae Kimya.’ Wimbo unazungumzia masuala mengi yanayotokea sasa ikiwemo hofu iliyotanda baada ya Roma na wenzie kutekwa.

Wimbo huo hata hivyo umepokelewa kwa hisia tofauti.

Hizi ni sababu zake kwanini ameamua kuuachia:

Ili Nchi ipate maendeleo inahitaji Upendo na Ushirikiano wa Wananchi na Serikali..Na Nikiwa kama Msanii, jukumu langu ni kuhakikisha natumia Hekma na busara kukemea jambo nilionalo haliko sawa ili lirekebishwe, lakini pia panapokuwa hakuna maelewano jukumu langu pia ni kupatanisha ili kwa pamoja tujenge nchi yetu kusudi wazazi wetu, watoto pamoja na familia zetu waishi kwa Upendo Amani na kufurahia nchi yetu…Na ndiomaana kwenye nyimbo nakwambia “MI NA WEWE WA TAIFA MOJA…KAMBARAGE BABA MMOJA….SASA TOFAUTI ZA NINI TUSHIKAMANE TUKAIJENGE TANZANIA”… Unatakiwa utambue kuwa kila kiongozi ni Binadamu na kama wote tujuavyo, Binadamu hatujakamilika… hivyo katika nchi yoyote lazma wakati mwingine kuna jambo linaweza likawa haliko sawa, ila sisi kama wananchi tunatakiwa tutumie Hekima na Busara kwenye kufikisha ujumbe ama hoja zetu ili viongozi walieke sawa…Busara na Hekima itafanya viongozi watuelewe kirahisi na pengine mengi tuyatakayo tutimiziwe kirahisi… mfano mzuri, juzijuzi kupitia kipindi cha Clouds360 cha clouds Tv nlipopata bahati ya kuongea na Mh Raisi nilimuomba atufungulie Mabanda ya Chipsi na Bodaboda ziruhusiwe kufanyakazi hadi asubuhi maana zilikuwa nwisho saa 4 ama 5 usiku…kwakuwa nilitumia Hekima na busara kwenye Kufikisha hoja ama Ombi langu..alikubali na tukapewa ruksa na sasa hivi maeneo mengi ya Chipsi na Bodaboda yanafanya kazi hadi usiku mnene… hivyo tusikubali tu kulishwa Sumu za kuleta ugomvi kati yetu wenyewe kwa wenyewe eti Mara Tutukane mara sijui fanyeni hiki, wakati hata baadhi ya wanaochochea mambo hayo hawaishi Tanzania wanaishi Ulaya / Marekani / kifupi nje ya nchi…ikija kutokea bahati mbaya kimenuka wao watakuwa wanakula kuku kwa mrija huko walipo…halafu sisi na familia zetu ndio tutateseka na kuhaha kunusuru roho zetu usiku kucha.. Hatutaki makelele ya Uchonganishi mitandaoni, kama mtu kweli anauchungu na nchi na kweli akisemacho anamaanisha aje, na kwa pamoja twende sehemu husika kupeleka malalamiko sio kukaa kitandani kupost kuchochea Ugomvi kumbe anatuchora na kutufanya kama sie mataahira wake, anatupeleka mara kushoto mara kulia… Akikaa pekeake anatucheka kuwa sie wajinga wake katueka mkononi…

Kimenuka !!!!.MANGE Kimambi Amvaa Diamond Platnumz baad ya kuhisi kamtaja kwenye wimbo mpya!!

Mange Kimambi hajapendezwa na Wimbo mpya wa Diamond "Acha nikae Kimya" Amemshukia Diamond Kama Ifuatavyo:
"We pumbu unatumika vibayaaaaaa.Hiyo kitu ya kuwatishia watanzania na vita sijui ukosefu wa amani CCM washaitumia for many years kuwatisha watanzania.Watu wakitaka mabadiliko gia Yao ya kwanza ni kuwatishia kuwa amani itapotea. Acha ipoteeee, Amani ya kisenge ya nyinyi wachache kutajirika kujenga mastate house sijui ushenzi gani Huku wengine wanasaga meno tumeichoka.wewe Dai umeshashiba huoni shida ya wengine lazma utake Amani, kamuulize anaeshinda mlo mmoja kama kuna Amani Tz?
You call this Amani? Amani ya vyama vya siasa kunyimwa kufanya mikutano ya hadhara, Amani ya Wa Bunge wa upinzani kufungwa jela kila siku? Amani ya vyombo vya habari kuvamiwa kwa mitutu? Amani ya wananchi kutajwa kama wauza unga ili waibiwe mali zao? Amani ya watz kutishiwa kuuwawa sababu ya kuandamana kitu ambacho kinaruhusiwa kikatiba?Amani ya wasaniii kutekwa sababu kiongozi anatafuta Kiki za kisenge, Hiyo Amani ya kisenge hatuitaki. Dai Ungemsikilzia mamako na unyamazeeee.Ndio sisi watz tulio nje ya Tz ndo tunaongea sana , hilo tu ni ushahidi tosha kuwa Tz hakuna Amani kwanini walioko ndani waogope kusema tuseme sisi tulioko nje?
Dai embu tuliza pumbu hizo! Kama umekosa cha kufanya kamtie Mimba Zari mfanye arobaini maana ndo kiki ulizobakiza siku hizi.Kwenye issue za msingi usilete pumbu zako. Fala wewe!" Mange Kimambi

ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII  TUTAENDELEA KUKUHABARISHA ....SHARE NA MARAFIKI ZAKO



Haya Ndio Madhara Sita Ya Kutoa Mimba

Kutoa mimba ni nini? Hii ni hali ya mwanamke kwa hiari yake mwenyewe kuharibu mimba iliyoingia ndani ya kizazi chake.

Kutokana kuongezeka kwa idadi ya mahusiano duniani na kutotumia njia za uzazi wa mpango kwa watu wengi walioko kwenye mahusiano, wasichana wengi kwa sasa wanatoa mimba.
Utafiti nilioufanya mwenyewe nimegundua kwamba zaidi ya asilimia tisini ya wasichana wanaokua kwenye mahusiano na wanaume zaidi ya mwaka mmoja kabla ya ndoa hutoa mimba na asilimia tano tu ya wote ndio wanaamua kuzaa. Sio ajabu kusikia mtu ameolewa akiwa ametoa mimba nne mpaka tano. Sasa unajiuliza bado kuna mtu humo au mfu?

Hata hivyo hao wanaozaa pia hujikuta wamebeba mimba zingine wakati watoto wao wakiwa wadogo na kulazimika kuzitoa. Najua watu wengi wanatoa mimba kukwepa aibu, kutokua tayari kisaikolojia na kadhalika lakini ni bora kutumia njia za uzazi wa mpango kama condomu kuzuia mimba na kama kondomu huiwezi basi tumia njia zingine kama sindano na vijiti kwasababu wengi wenu mkishalewa pombe au kondomu isipokuepo ndio basi tena.

Hebu tuyaangalie madhara ya kutoa mimba kama ifuatavyo…

Uwezekano mkubwa wa kufa:
Utafiti uliofanywa na madaktari wa finland mwaka 1997 umegundua kwamba wanawake wanaotoa mimba wanauwezekano wa kufa mara nne zaidi kuliko ambao hawatoi mimba. Vifo hivyo vimekua vikisababishwa na kujiua wenyewe kutokana na kujuta kwa maamuzi yao na madhara ya mda mrefu ya kimwili yatokanayo na kutoa mimba. Vifo ndani ya wiki moja baada ya kutoa mimba hutokana na kuvuja damu sana, madhara ya dawa za usingizi, mabonge ya damu kwenye mishipa ya damu na mimba iliyotunga nje ya uzazi. Utafiti pia uliongeza kutoa mimba moja uwezekano wa kufa unakua 45%, mimba mbili 114%, mimba tatu 192%.

Ugumba kwa wanawake wengi:
Miaka hii ya karibuni wanawake wengi ambao wanalia kutopata watoto wana historia za kutoa mimba miaka iliyopita, na wengi wao nilionana nao wanajuta sana kwa maamuzi yao. Hii inatokana na madhara makubwa waliyoyapata kwenye mfuko wa uzazi baada ya mimba kutoka.

Mimba kutunga nje ya kizazi:
Mfuko wa uzazi una utando maalumu amaboa hufanya mimba iliyotungwa kwenye mirija iitwayo fallopian kuwezesha yai kushuka hadi kwenye mifuko ya uzazi. Lakini utoaji wa mimba huambatana na magonjwa ya mirija hiyo na kupoteza utando huo na kusababisha mimba kukulia huko.matibabu ya tatizo hili ni kukata mrija husika tu hivyo kuongeza hatari ya ugumba..

Kuzaa watoto wasio na akili nzuri:
Utoaji wa mimba kuharibu mlango wa mfuko uzazi kushindwa kushika vizuri na matokeo yake mwanamke huyu hujikuta akizaa kabla ya mda husika akibeba mimba nyingine. Lakini pia watoto hawa wanaozaliwa kabla ya muda maalumu  na viungo ambavyo havijakomaa hupata shida ya ubongo na kua wagonjwa wa akili maisha yao yote.

kansa ya mlango wa uzazi
Wanawake wanaotoa mimba wana hatari kubwa ya kupata kansa ya mlango wa uzazi kuliko wengine ambao hawajatoa mimba. Hii ni kwasababu ya kusumbuliwa kwa mlango huo kwa dawa za kutoa mimba, vifaa vya kutoa mimba na mabadiliko ya ghafla ya homoni za uzazi.

Kuathirika kisaikolojia;
Hakuna mwanamke ambaye hatakaa ajutie maamuzi yake ya kutoa mimba siku za usoni hata kama hakupata madhara yeyote hii itamfanya aishi kama ana deni Fulani maisha yake yote na itakua inamuumiza usiku na mchana. Zingine ni kukosa hamu ya kula, kusikia sauti ya mtoto anayelia wakati hayupo, kua na hasira sana…

Mwisho
kumbuka kila mwaka wanawake 70000 wanakufa kwa kutoa mimba...maumivu ya kukosa mtoto ni makali sana kuliko aibu ya kuzaa nje ya ndoa. Hawa wanaozaa sasa hivi unawaona malaya ipo siku utawakumbuka utakapo ambiwa na daktari kwamba labda itokee miujiza ndo utazaa.Kama hutaki mimba tumia njia za uzazi wa mpango kwani kuendelea kutoa mimba kutakupa adhabu ya kukosa mtoto ambayo adhabu hiyo utaitumikia maisha yako yote

Maagizo Aliyoyatoa Waziri Nchemba Kwa Polisi Kuhusu Kutekwa kwa Msanii Roma

Msanii wa hip hop Roma Mkatolikia alikamatwa April 5 usiku ambapo taarifa zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kuwa alikamatwa studio za Tongwe Records  na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na wakapelekwa  kusikojulikana.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba ambaye ndio anahusika na usalama wa raia, ametumia ukurasa wake wa instagram kuonesha kuguswa na tukio la kutekwa kwa Roma Mkatoliki na Moni.

Waziri Nchemba ameeleza kuwa amewaagiza polisi kufuatilia na kutoa taarifa kwa umma.

“Nimeshtushwa kwa kutokuonekana kwa Msanii Roma na Wenzake mpaka sasa. Nimeshtuka zaidi nilipofuatilia na kuambiwa hakuna kituo chochote cha polisi kinachowashikilia. Nimeelekeza Polisi wafuatilie kwa karibu kujua undani wa tukio hili na hatima yao na kutoa taarifa kwa umma”

Wema sepetu atoa povu kwa bongo movies Sakata la Roma.......Ray Amtolea Uvivu na Kumjibu

Baada ya wasanii Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wenzao kuchukuliwa na watu wasiofahamika tangu usiku wa kuamkia juzi  wasanii mbalimbali wamekuwa wakitumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kupost juu ya kusikitshwa na kitendo hicho, Wema Sepetu akiwa moja kati yao.

Lakini post ya Wema Sepetu ambayo aliiandika kupitia ukurasa wake wa Instagram imeonesha kutokumfurahisha muigizaji mwenzake Ray Kigosi ambaye amepost pia katika ukurasa wake wa instagram na kueleza kutokufurahishwa na namna Wema alivyoandika kuhusu ishu hiyo.

==> Wema Sepetu aliandika hivi;

"This Is Scary… Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla… Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino…. Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake…

"Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa…??? Oh God help Us Please… Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu Tumejawa sana Unafki…!!! All in All namuonea sana huruma Nancy…

"Our prayers are with u mama… Inshallah mumeo atapatikana… Tuzidi kumuomba Mungu…..🙏🏼🙏🏼🙏🏼…. Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani….!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino…?? 🙄🙄🙄 SMH.. "

This Is Scary... Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla... Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino.... Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni...??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake.... Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa...??? Oh God help Us Please... Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu... Tumejawa sana Unafki...!!! All in All namuonea sana huruma Nancy.... Our prayers are with u mama... Inshallah mumeo atapatikana... Tuzidi kumuomba Mungu.....🙏🏼🙏🏼🙏🏼.... Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani....!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino...?? 🙄🙄🙄 SMH...

A post shared by Wema Sepetu (@wemasepetu) on Apr 7, 2017 at 6:31am PDT


==>Ray Kigosi  hakuipenda post hii, hivyo akajibu;

NAFIKIRI NI VEMA MTU KUELEZA HISIA ZAKE JAPO SIO BUSARA KWA MWENYE HISIA HIZO KUZIELEZA BILA WEREDI NAWASIHI WASANII WENZANGU KUPOTEA KWA ROMA ISIWE SABUNI YA KUTAKATISHA UCHAFU WA MTU SOTE TUMESIKITISHWA NA JAMBO HILO NA TUMEONYESHA KWA VITENDO. MIMI NIMEPOST INSHU YA ROMA TANGU JANA USIKU WEMA SEPETU WEWE ULIKUWA HUJAPOST CHOCHOTE TUSEME ULIKUWA HUNA UCHUNGU? ALAFU LEO UNAANDIKA KUWA BONGO MOVIE HAWAPO PAMOJA NA TUKIO LA ROMA HUKU NI KUTUGOMBANISHA NA WANANCHI WANAOTUAMINI. SISI BONGO MOVIE MARA NYINGI SANA TUNAKUWA PAMOJA KWENYE MATUKIO YA BONGE FLEVA TOFAUTI NA WAO. KAMA UNA UGONVI NA MTU HAYO NI MAMBO YAKO BINAFSI ILA USITUFANYE SISI TUONEKANA WABAYA MBELE YA JAMII UTAKUWA KICHAA KAMA USIPOPATA MAUMIVU KWA TUKIO LA ROMA NIMESIKITISHWA SANA POST YAKO @wemasepetu KAMA UNADHANI HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUTAFUTIA POINT KATIKA TUKIO LA ROMA MKATOLIKI UMEFELI HILI NI JANGA LETU SOTE. @wemasepetu #(KINA ROMA WAKO WAPI?).

Mtuhumiwa wa Mil.7 kila dakika awaponza vigogo TRA.... Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 8 2012



 

Gallery

Popular Posts

About Us