Kamanda aahidi Siro Kumsaka Roma na wenzake popote walipo!! | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 8 April 2017

Kamanda aahidi Siro Kumsaka Roma na wenzake popote walipo!!

JESHI la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limeazimia kumtafuta msanii wa muziki wa Bongo Hip Hop Ibrahim Mussa, (Roma) wa wenzake.

Roma , Monii (msanii),(Bin Raden mtayarisha muziki wa studio hiyo) na emmanuel  walitekwa na watu wasiojulikana siku ya tarehe 5 Aprili mwaka huu usiku wa kuamkia alhamis kwenye kwenye makoa ya studio hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamshna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Simon Sirro ,amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi linamsaka Roma na wenzake pamoja na kuunda timu maalamu.

Kamanda Sirro amesema kuwa amesema kuwa jeshi hilo linaendelea na Upelelezi na kwamba tayari jarada wa uchunguzi wa tukio hilo tayari umeshaundwa.

Amewasisitiza wananchi kuliamini jeahi hilo na kuwa wavumilivu jeshi hilo likiwa linafanya uchunguzi.

Hata hivyo jeshi hilo  limewataka wananchi kuwa na imani na jeshi hilo

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us