KINGAZI BLOG: 01/06/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 6 January 2017

Madhara ya Kiafya Kuhusu Wanaojichora Tattoo

Tafiti nyingi za kitabibu pia zinaonesha kwamba, wino au rangi za tattoo zinaweza kusababisha uambukizo wa bakteria aina ya Mycobacterium cholonae.

Bakteria hawa wanaweza kusababisha magonjwa ya ngozi na nyama za mwili, matatizo ya njia ya mkojo, mfumo wa kupumua, magonjwa ya uambukizo kwenye mifupa na nyama za moyo.

Michoro hiyo pia huweza kusababisha homa ya uti wa mgongo na tatizo la macho.

Vilevile, vifaa vinavyotumiwa kuchora mapambo hayo hutumika kwa watu mbalimbali kwa wakati mmoja bila utaalamu sahihi wa kuvisafisha.

Hali hiyo huweza kusababisha vibebe vimelea vya magonjwa mbalimbali na kuyahamishia kwa wengine.

Hali hii inaweza kusababisha uambukizo wa magonjwa yatokanayo na virusi hatari kama vile virusi vya Ukimwi, virusi ninavyosababisha homa ya ini (Hepatitis B na C) au virusi vya malengelenge (herpes simplex virus).

Kumbuka, wakati wa kuchora tattoo, ngozi hutobolewa kwa mashine au sindano hadi kuifikia sehemu ya ndani kabisa. Hii ni hatari kwa afya yako.

Ajinyonga kwa kunyimwa na mkewe samaki mbichi

MKAZI mmoja wa kijiji cha Kalundi kilichopo kata ya Kipande wilayani Nkasi, Vedast Kazumba (51) amejiua kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa alighadhabika, baada ya mkewe kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha tukio hilo.

Alisema ni la usiku wa mkesha wa Mwaka Mpya na kwamba Kazumba alifikia uamuzi huo mgumu kwa kujinyonga akitumia kamba ya katani .

Alieleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na polisi kuhusu tukio hilo na uchunguzi wake unaendelea . Habari kutoka kijijini humo, zinaeleza kuwa chanzo cha Kazumba kujinyonga ni kukasirishwa na kitendo cha mkewe, Antoniata Mwisua kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

“Mke wa marehemu aitwae Antoniata alimwandalia mumewe huyo chakula cha usiku, kitoweo chake kikiwa ni samaki mbichi alimkomba samaki huyo kisha akamwomba amwongezee kitoweo kingine cha samaki, lakini mkewe alimweleza kuwa kitoweo hicho kimekwisha. Ndipo mumewe alipokasirika akidai kuwa mkewe amemnyika kwa makusudi kitoweo hicho ndipo alipochukua hatua ya kuzira kula“ alieleza mmoja wa mashuhuda kwa masharti ya kutoandikwa gazetini.

Akizungumzia mkasa huo , Mwenyekiti wa Kijiji cha Kalundi , John Kalasa alidai kuwa marehemu wakati wa uhai wake alikuwa ni mtu mwenye kujawa na ghadhabu ambapo mara kadhaa alisikika akitishia kujinyonga.

 

Gallery

Popular Posts

About Us