KINGAZI BLOG: 04/15/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 15 April 2017

Miili Ya Askari 8 Waliouawa Mkoani Pwani Yaagwa Jijini Dar.......Mwigulu Nchemba Atangaza Kiama, IGP Atoa Onyo kwa Wanaoshabikia Mitandaoni

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amewatangazia kiama watu wote waliohusika kuwaua askari polisi nane Kibiti wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya askari hao jijini Dar es Salaam leo asubuhi Mwigulu alisema watu hao watakamatwa wote na kufikishwa kwenye mkono wa sheria. 

"Kitendo hiki cha mauaji kilichofanyika dhidi ya askari wetu hakivumiliki hata kidogo waliohusika tutawatafuta na kuwakamata" alisema Mwigulu.

Aliwaomba wananchi wa maeneo husika kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuwapata wahusika wa tukio hilo. 

Katika hatua nyingine Mwigulu ameitaka wizara husika kuhakikisha inatoa fidia kwa ndugu wa askari hao na majeruhi badala ya kuchukua muda mrefu kuitoa.

 "Naomba fidia kwa askari hawa tuliowapoteza wakitumikia taifa itolewa haraka bila kucheleweshwa" aliongeza Mwigulu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu alisema watuhumiwa wote waliohusika kufanya mauaji hayo ni lazima watafikiwa na mkono wa dola. 

Alisema wananchi wa eneo hilo wanawafahamu wahusika hivyo amewaomba washirikiane na polisi ili kuwapata vinginevyo nguvu itatumika.

Alisema linapotokea tukio kama hilo kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishabikia kupitia mitandao ya kijamii hivyo akatoa onyo kuwa watakao bainika na wao watakamatwa kwa kutenda kosa.

Askari waliopoteza maisha katika tukio hilo la kinyama wametajwa kuwa ni pamoja na Mkaguzi Msaidizi Peter Kiguu, Koplo Francis, PC Haruna, PC Jackson, PC Zakaria, PC Siwale, PC Maswi na PC Ayoub.


Makalio yamenipa ma 'dili' Sanchi.


MODO aliyejaaliwa kuwa na figa matata, Jane Ramoy ‘Sanchi’ amefunguka kuwa, shepu yake inampa madili ya kumuingizia mamilioni ya pesa hivyo kuweza kuyaendesha maisha yake bila presha.

Akizungumzia usumbufu anaopata kutoka kwa wanaume wakware kutokana na bambataa alilonalo, Sanchi alisema, hilo la usumbufu wa wanaume kwake wala siyo tatizo ila anachoshukuru ni kwamba figa yake inampatia pesa ndefu.

“Unajua kwa shepu hii niliyonayo, sitarajii wanaume wasini sumbue, kwa hiyo hilo kwangu wala siyo tatizo, ninachoshukuru ni kwamba napata madili ya kuwa modo kwenye video mbalimbali, matangazo na michongo mingine, kwa hiyo namshukuru Mungu kwa kunipa figa hii” alisema Sanchi.

Mchungaji Getrude Rwakatare ateuliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalum



Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Aman Ahukumiwa Kifungo cha cha Miezi 6

Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, imemuhukumu kifungo cha nje cha miezi sita na kulipa faini ya Sh1 milioni, Aman Mwasote baada ya kutiwa hatiani kwa kumwita mtoto wa miaka tisa kuwa mchawi.

 

Mwasote, ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za Injili alishtakiwa kwa kutoa kauli kuwa mtoto huyo huwaloga wanafunzi na walimu alipokuwa kwenye mkutano wa injili.

 

Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mkazi, Venance Mlingi aliyesema mahakama imeridhishwa na ushahidi uliotolewa na mashahidi wanne wa upande wa Jamhuri kwamba, Mwasote alitenda kosa hilo.

 

Awali, Wakili wa Serikali, Xaveria Makombe alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo Septemba 20, mwaka jana eneo la Shule ya Msingi Kalobe, akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Injili.

 

Hakimu Mlingi alisema mshtakiwa atatumikia kifungo cha nje kwa kufanya shughuli za kijamii na Aprili 20 atatakiwa kufika mahakamani ili apangiwe shughuli ya kufanya.

Mke wa Roma Aacha Gumzo Sakata la Mumewe.!


ya madai ya mumewe ambaye ni staa wa Hip Hop Bongo, Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kutekwa na kuteswa kisha kutelekezwa akiwa na wenzake watatu baada ya siku kadhaa, mke wa jamaa huyo aitwaye Nancy ameacha gumzo kufuatia ujasiri aliouonesha katika tukio hilo.

Kwa mujibu wa watu wa karibu na familia ya Roma, Nancy ambaye ni mama wa mtoto mmoja aliyezaa na Roma aitwaye Ivan, alionesha ujasiri wa aina yake kwani alikuwa halali badala yake alizunguka kila kona jijini Dar akimsaka mumewe, jambo ambalo baadhi ya wanawake wasingeweza kulifanya.

“Nancy siyo wa mchezomchezo, tangu mumewe alipotekwa alikuwa halali. Alichokifanya aliomba msaada kwa ndugu zake wa kumtafuta mumewe kila kona hadi alipopatikana.

“Unaambiwa alizunguka kila sehemu bila mafanikio akimtafuta mume wake tangu aliposikia taarifa za kutekwa usiku wa Jumatano (wiki iliyopita). “Nancy alianzia Studio za Tongwe Records (Masaki), baada ya hapo hakulala, alizunguka karibia vituo vyote vya polisi Dar.

Alituma watu hadi mochwari kumuulizia mumewe na wakati huohuo akiviomba vyombo vya habari kumsaidia hadi mumewe alipopatikana, tofauti na wanawake wengine ambao wangejifungia tu kusubiri taarifa.

“Unajua watu wengi walikuwa hawamjui Nancy ni mtu wa aina gani lakini tukio la Roma limemfanya awe gumzo sana kwa ujasiri aliounesha kwenye kipindi kigumu alichopitia,” alisema mtu huyo wa karibu wa familia ya Roma. Akizungumza na Amani juu ya ujasiri aliouonesha kwenye tukio hilo, Nancy alisema kuwa, tukio hilo lilimfanya achanganyikiwe na kujikuta akihangaika kwenye vituo vingi vya polisi jijini Dar. Alisema kuwa, kilichokuwa kinamfanya achanganyikiwe na kushindwa kupata usingizi ni kwamba, kabla, hakuwahi kumpatia taarifa yoyote kama anatafutwa na polisi achilia mbali kuwa na tatizo na mtu yeyote.

Hata hivyo, Nancy aliwashukuru wadau mbalimbali pamoja na Watanzania kwa ujumla kumuunga mkono katika jitihada za kumtafuta mume wake hadi alipopatikana na bado wameendelea kutoa pole hivyo kuonesha upendo mkubwa walionao kwa baba mtoto wake.

Jinsi mauaji ya Kutisha ya Polisi nane Yalivofanyika… Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 15



 

Gallery

Popular Posts

About Us