KINGAZI BLOG: 03/03/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 3 March 2017

Diamond atoa kauli kuhusu wimbo wa ‘Salome’ kujaa matusi

Maoni ya baadhi ya wadau wa muziki kuwa kila wanapousikiliza ‘Salome’ wa Diamond na RayVanny wanapata picha ya matusi, yamekutana na majibu ya Boss huyo wa WCB.

Akifunguka jana kwenye kipindi cha Ngazi Kwa Ngazi kinachorushwa na EATV, Diamond alisema kuwa ‘Salome’ haina matusi bali imebeba lugha ya mahaba mazito.

“Ukiangalia wimbo wa Salome, hauna matusi, ila una maneno ya kimahaba,” alisema Mond.

“Unapozungumzia wimbo wa kimahaba, matusi yanatokea pale. Matusi yapo kwenye mahaba. Unapokuwa unaelezea masuala ya kimahaba utaonekana kama unatukana. Lakini sisi tumejitahidi kadri ya uwezo wetu mahaba yale kuyazungumza katika lugha ambayo ni ngumu sana mtu kuielewa,” alifafanua.

Kwa upande wake Ray Van, alisema kuwa pamoja na yote yanayosikika kwenye wimbo ule, wamejitahidi kutumia tafsida kuyaficha na ndio sababu wimbo ule unapendwa na watu wa rika zote na unaweza kusikilizwa hata katika jumuiya ya watu wanaoheshimiana.

Salome ni wimbo uliochukua mahadhi ya wimbo wa zamani wa Saida Kalori ‘Chambua Kama Karanga’ na umepata nafasi na mafanikio makubwa katika vituo vya runinga vya kimataifa na kuweka rekodi ya aina yake kwenye mtando wa YouTube.

Video ya Salome imeangaliwa zaidi ya mara milioni 13 na laki 7 kwenye YouTube.


Elimu ya Makonda Kaa la Moto,Mawaziri Waogopa Kuzungumzia..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 3/3/2017..!!!



Breaking News...Makonda Afunguka Kuhusu Elimu Yake,Atoa Majibu Haya Kwa Wanaoshinda Mitandaoni Wakimsema..!!!


KUHUSU ELIMU YAKE

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amefunguka tuhuma zinazozushwa kupitia mitandao ya kijamii na watu mbalimbali kuhusu elimu yake na zinazoeleza kuwa amefoji cheti cha mtu mwingine.

Akizungumza kwenye kikao cha kamati ya ushauri wa Mkoa (RCC) RC Makonda ameeleza kuwa kinachogombaniwa siyo Makonda bali ni kiti alichokalia (UKUU WA MKOA), hivyo ameeleza kuwa nafasi yake ya ukuu wa Mkoa amepewa na Mungu.

Na kufafanua kuwa hatakama angepata sifuri au daraja la kwanza katika masomo yake, Mungu angetaka awe Mkuu wa Mkoa angekuwa tu, kwani Mungu ndiye anapanga kila kitu na kuongeza kuwa yupo imara kuliko alivyokuwa jana.

KUTISHWA KWA WAZAZI WAKE

Pia RC Makonda amefunguka kuhusu kutishwa kwa baba yake mzazi, pia kuna watu walikwenda eneo analoishi baba yake na mama yake mzazi na kupiga picha, ili wakaoneshe nyumba anayoishi mzazi wake.

KUHUSU KUITWA SHOGA NA MGUMBA

RC Makonda ameeleza kuwa watu wamekuwa wakimtolea lugha chafu kuhusu uzazi wake na kumuita mgumba kwa kuwa hana mtoto na wengine wamekuwa wakimuita shoga, amefunguka na kusema kuwa haoni tusi jipya.

RC Makonda amesema ipo siku watu wataulizwa kuhusu matendo wanayoyafanya duniani kilasiku, hawana budi kuwa makini na matendo yao.

KUHUSU DAWA ZA KULEVYA

RC Makonda ameeleza kuwa tangu aianze vita ya dawa za kulevya yameibuka mengi na kusisitiza kuwa hatoacha ataendelea kwani wapo wanaoshukuru kuanza kwa vita hiyo na kuhoji kwanini haikuanza mapema kwani imeokoa maisha ya wengi, kuhusu maendeleo ya vita hiyo RC Makonda amesema kuwa mashamba ya bangi yanateketezwa kila uchwao, siku mbili zilizopita wamekamatwa watu 100 na kete 400 za dawa hizo pia zimekamatwa.

 

Gallery

Popular Posts

About Us