KINGAZI BLOG: 01/04/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 4 January 2017

Ningekuwa Diamond nisingejiita simba – Darassa

Hit maker wa wimbo ‘Muziki’ Darassa ameweka wazi maana ya ule mstari wake wa “sio simba, sio chui, sio mamba” kwa kusema Diamond hakupaswa kujiita simba kwani simba ni mnyama ambaye anaweza kuuliwa anapozidiwa nguvu.

Darasa amedai Diamond ni msanii ambaye amehangaika sana kutoka kimuziki hivyo mafanikio yake na uwezo wake wa muziki alitakiwa ajiite jina lingine kwa kuwa Daimondi ni zaidi ya Simba kwa sasa kwani ni zaidi ya mnyama Simba.

“Ningekuwa Diamond nisingejiita simba,” Darassa alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV. “Ninavyomuona Diamond ni zaidi ya Simba, kuna watu wanaua simba, simba, kajichanganya, kaingia kijijini kapotea, Diamond kwa kitu anachofanya ni zaidi ya simba, angeweza kujiita jina lingine lolote kubwa, kafanya vitu vingi sana,”

Pia rapper huyo alidai wanyama wote ambao amewataja katika wimbo wake hawaogopi kwa kuwa ana kitu kikubwa ndani yake na yeye ni mwanaume na anajiamini kwa muziki wake anaofanya.

“Kwa upande wangu nimesema siyo simba, siyo chui siyo mamba, mamba ni mnyama anayetisha sana kwenye maji, simba anatisha sana porini, chui ni hunter mzuri, so katika vitu vyote ambavyo viko humo, mimi humo kote simo, ninacho kitu ambacho kinaweza kunifanya nikwambie aaaaah”. Amemalizia Darassa

Ziara Ya Rais Magufuli Kagera Yatumbua vigogo Watatu

Baada  ya Rais Dk. John Magufuli kuagiza watumishi wote wa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera waliohusika katika ukarabati wa majengo ya Shule ya Sekondari Omumwani ambayo yameonekana kutoendana na thamani ya fedha zilizotumika wachunguzwe, watumishi watatu wa manispaa hiyo wamesimamishwa kazi.

Watumishi hao walisimamishwa jana na Katibu Tawala, Mkoa wa Kagera, Diwani Athumani, baada ya kufanya ukaguzi wa miundombinu ya maji iliyomo katika majengo ya shule hiyo.

Shule hiyo ilikarabatiwa kuwapa hifadhi ya muda wanafunzi wa shule za sekondari Ihungo na Nyakato zilizoathiriwa na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera, Septemba 10, mwaka jana.

Baada ya ukaguzi huo, Athumani alimtaka Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Chibunu Lukiko, kumtajia majina ya watumishi waliohusika moja kwa moja katika usimamizi wa kila siku wa shughuli hiyo.

Katika maelezo yake, Athuman alisema aligundua ukarabati uliofanywa ulikuwa chini ya kiwango na hauendani na thamani ya Sh milioni 119 zilizotolewa na Serikali.

“Kwanini wakurugenzi hampendi kufuatilia miradi iliyo katika maeneo yenu? Kama mngefuatilia mapema, mngegundua ubadhilifu uliofanyika hapa na kuchukua hatua mapema.

“Kwa hiyo, naagiza kuanzia leo Januari 3 (jana), mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba uwasimamishe watumishi wote waliohusika ambao ni Mhandisi Kitengo cha Ujenzi wa Manispaa ya Bukoba, Andondile Mwakitalu, Mhandisi Msaidizi, Costane Felix na fundi Charles Kafumu.

“Hawa lazima wasimamishwe ili kupisha uchunguzi utakaofanyika kwa ajili ya kulinganisha kazi iliyofanywa na kiasi cha fedha kilichotumika kama vinaendana.

“Tatizo jingine nililoligundua ni kutokuwapo kwa usimamizi mzuri wa mradi huo kutoka kwa watumishi wa manispaa. Hao nao uchunguzi dhidi yao utafanyika kwa uwazi na ukweli na hatutamwonea mtu.

“Sitaki kusikia shughuli hii inasimama eti kwa sababu ya hawa watu wamesimamishwa, fanya makabidhiano na wale watakaokuwapo.

“Kaimu mkurugenzi hakikisha mnakabidhiana kila kitu, hata msumari usibaki na uchague watu wengine wa kuendelea na kazi ya kusimamia mradi huu ili ukamilike kwa muda uliopangwa,”alisema.

Naye Mhandisi Mwakitalu aliyesimamishwa, alisema majengo hayo yalikuwa katika hali mbaya na kwamba ukarabati wake unahitaji fedha nyingi ili yarudi katika hali yake ya kawaida.

 

Gallery

Popular Posts

About Us