KINGAZI BLOG: 05/27/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 27 May 2017

Nyuma ya Pazia kifo cha Mume wa Zari

 KAMPALA: Kifo cha aliyekuwa mume wa staa wa Uganda na Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Tycoon Ivan Semwanga ‘The Don’, raia wa Uganda, mwenye maskani yake Johannesburg na Pretoria, Afrika Kusini, kimeibua simulizi nzito nyuma ya pazia.

Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya familia ya Ivan iliyopo Muyenga jijini Kampala, kilichokaririwa na mitandao ya kuaminika nchini Uganda, katika siku za mwisho za maisha yake kabla ya kuripotiwa kupatwa na ugonjwa wa shambulio la moyo ambao kitaalam huitwa Coronary Artery Disease (CAD). Ilifahamika kuwa, ugonjwa huo ndiyo uliomsababishia kifo usiku wa kuamkia juzi.

Habari zilieleza kuwa, Ivan alionekana kwa mara ya mwisho kwenye Pati ya Blankets and Wine iliyofanyika huko Kampala, Uganda wiki mbili zilizopita. Ilielezwa kuwa, rais huyo wa Kundi la Rich Gang, mwenye umri wa miaka 39, alionekana aliyedhoofu na asiyekuwa na furaha kama kawaida yake huku akinywa soda na kula samaki, tofauti na alivyozoeleka kuwa ni mtu wa kupiga vinywaji vikali, tena vya bei mbaya. “Nyuma ya hali yake kiafya alionekana dhahiri mwenye matatizo yaliyosababisha hata kula yake kuwa ya kusuasua na kusababisha hali kuwa mbaya zaidi,” kilikaririwa chanzo hicho.

CHANZO CHA UGONJWA

Chanzo hicho kilidai kuwa, chanzo cha Ivan kupatwa na ugonjwa huo ni pale alipotokea Sauzi na kwenda kuangalia moja ya mali zake (mashamba makubwa) zilizopo Kampala na kukuta kuna watu wamebadilisha umiliki bila yeye kujua. Ilisemekana kuwa, kuna wakazi waliotengeneza nyaraka na hati za kumiliki ardhi ya jamaa huyo ambayo ilionesha walikuwa wamiliki wapya ilihali ni mali ya jamaa huyo.

Wakati watu hao wakifanya hivyo, Ivan hakujua kilichokuwa kikiendelea. Ilielezwa kwamba, ishu hiyo ilimsababishia Ivan mshtuko wa moyo na maumivu makali ya kichwa ambayo pia yaliathiri utendaji wake wa kazi wa kila siku.

Mbali na hilo, pia, kuliibuka taarifa za kuuzwa kwa nyumba yake na watu wasiojulikana ambapo alitumia nguvu kubwa kukanusha taarifa hizo na kueleza kuwa kwa utajiri alionao hawezi kuuza nyumba yake ya kifahari iliyopo Munyonyo, Kampala.

“Mwishowe, alipoona hali yake kiafya inakuwa mbaya kutokana na mshtuko uliotokana na mambo hayo, Ivan alichukua ndege na kwenda Afrika Kusini kisha kuripoti mwenyewe katika Hospitali ya Steve Biko Academy iliyopo Pretoria. “Vipimo vilionesha kuwa alipatwa na mshtuko wa moyo ambao ulisababishwa na kuganda kwa damu kwenye mishipa,” alisema sosi huyo wa jijini Kampala. Mwishoni mwa wiki iliyopita, baba huyo wa watoto watatu aliozaa na Zari alielezwa kuwa hali yake ilizidi kuwa mbaya zaidi hivyo kufanyiwa operesheni kubwa ya kichwa.

ZARI ATHIBITISHA

Kupitia ukurasa wake Mtandao wa Kijamii wa Instagram, Zari alithibitisha kifo cha mumewe ambapo aliandika
waraka wa simanzi: “Mungu huwapenda wale ambao ni maalum kwake ndivyo ulivyokuwa, umewagusa na kuwasaidia maelfu, ulifanya mengi ya kushangaza na nakumbuka maneno yako ‘maisha ni mafupi mno, acha tuishi kwa ukamilifu’. Hii ni saa ya giza, sasa naelewa kwa nini ulikuwa ukisema maneno hayo kwangu. “Kwa wanao, umekuwa shujaa -aina fulani ya superman. Mtu yeyote ambaye amewahi kuwa karibu yako anajua wewe ni mtu wa aina gani, anajua ucheshi wako.

Watu watakumisi na kukumbuka sana kwa namna nyingi…Ulikuwa IVAN DON.

Baadhi ya mastaa wa Uganda walieleza ni namna gani walivyoshtushwa na kifo cha Ivan. Bebe Cool –Natoa rambirambi zangu za dhati kwake na familia yake. RIP kaka IVAN. Jose Chameleone -Mungu anaumba na kuchukua kilicho chake! Mungu akurehemu rafiki yangu na kuimarisha familia yako na sisi rafiki zako. Pumzika kwa amani Ivan. Ed Cheune –Ulieneza furaha miaka yote ulipokuwa nasi wote, sasa ni zamu ya Mungu kukupa furaha yote katika kurudi kwako kwake.

Pumzika kwa amani ndugu yangu mpendwa Ivan Semwanga. Baadhi ya mastaa wa Kibongo walioandika mitandaoni kumlilia Ivan ni pamoja na Wema Isaac Sepetu, Emmanuel Mbasha, Ali Kiba, Ester Kiama, Shilole na wengine wengi kutokana na ukaribu wake na wao. Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, bado utaratibu wa mazishi ulikuwa haujawekwa wazi. Ivan alipata umaarufu Afrika Mashariki kutokana na biashara zake kubwa ikiwemo umiliki wa vyuo mbalimbali nchini Afrika Kusini huku akisifika kwa kusaidia shughuli za kijamii nchini Uganda.


Wakristo 23 wa kanisa la Coptic wauawa wakienda kanisani kwa maombi Misri

Watu takriban 23 wameuawa na wengine 25 kujeruhiwa baada ya watu wenye silaha kufyatulia risasi waumini wa kanisa la Coptic waliokuwa wakisafiri kwa kutumia basi katikati mwa Misri, vyombo vya habari vya serikali ya nchi hiyo vimesema.

Kisa hicho kilitokea katika mkoa wa Minya, takriban kilomita 250 (maili 155) kusini mwa Cairo, basi hilo lilipokuwa linawasafirisha kwenda kanisani.

Kumetokea visa kadha vya waumini wa kanisa la Coptic kushambuliwa, mashambulio ambayo kundi la Islamic State limedai kuhusika.

Mashambulio mawili ya mabomu ya kujitoa mhanga katika makanisa Tanta na Alexandria mnamo 9 Aprili yalisababisha vifo vya watu 46.

Waumini hao waliuawa walipokuwa wakisafiri kwenda kanisa la Mtakatifu Samuel kuomba.
Basi lao lilikuwa katika msafara mdogo wa magari na taarifa zinasema gari hilo lilisimamishwa na watu kati ya wanane na kumi waliokuwa wamevalia sare za kijeshi.

Watu hao wenye silaha walifyatulia risasi basi hilo kwa kutumia bunduki za rashasha kisha wakatoroka kwa kutumia magari matatu ya 4x4.

Afisa Mkristo kutoka Minya Ibram Samir ameambia gazeti la New York Times kwamba kulikuwa na watoto kwenye basi hilo na ni miongoni mwa waliofariki.

Gavana wa Minya Essam al-Bedawi amesema maafisa wa usalama walifika eneo hilo na wanaweka vizuizi kwenye barabara hiyo ya kulekea kanisa la Mtakatifu Samuel pamoja na kufanya msako mkali.

Wakristo wa Coptic hujumuisha asilimia 10 ya raia wote 92 milioni wa Misri.
Mashambulio ya mwezi jana yalimfanya Rais Abdul Fattah al-Sisi kutangaza hali ya hatari ya miezi mitatu kote nchini humo na kuahidi kuchukua hatua kukabiliana na wapiganaji wa Kiislamu, wengi ambao hutoka maeneo ya kaskazini ya Sinai.

Lakini wengi wa waumini wa Coptic wamekuwa wakilalamika kwamba serikali haifanyi juhudi za kutosha kuwalinda, anasema mwandishi wa BBC aliyepo Cairo Orla Guerin.

Kwa sasa kuna hali ya wasiwasi miongoni mwa Wakristo ambao wanahisi kwamba wanawindwa, anasema.

Kanisa la Coptic ni gani?
Kanisa la Coptic ni la Kiothodoksi na ndilo kanisa kuu la Kikristo nchini Misri.
Ingawa wengi wa waumini wa Coptic huwa Misri, kanisa hilo lina waumini karibu milioni moja nje ya nchi hiyo.

Wengi wa waumini wa kanisa hilo huamini kwamba asili ya kanisa lao ni mwaka 50 AD (Baada ya kuzaliwa kwa Kristo) pale Mtume Mark alipozuru Misri.

Mkuu wa kanisa hilo huitwa Papa na huchukuliwa kuwa mrithi wa Mtakatifu Mark.
Kanisa hilo lilijitenga na Madhehebu mengine ya Kikristo katika Mkutano wa Chalcedon (451 AD) baada ya mzozo kuhusu sifa za utu na umungu za Yesu Kristo.

Klabu ya Everton Yathibitisha Kutua Tanzania Kucheza na Simba na Yanga..!!!


Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter wa klabu ya soka ya Everton, umethibitisha kuwa klabu hiyo kuwasili nchini mwezi Julai na itakuwa ni timu ya kwanza inayoshiriki Ligi kuu nchini Uingereza kucheza na timu za Afrika mashariki.

Ujio wa Everton ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi, Vilabu vinavyo tarajiwa kunufaika na ujio huo ni vile ambavyo vipo chini ya udhamini wa kampuni ya Michezo ya kubashiri ya SportPesa. Kwa hapa nchini mpaka sasa kampuni hii imeingia mkataba na klabu tatu ambazo ni Simba SC, Yanga SC pamoja na Singida United .

Kwa mujibu wa Kampuni ya SportPesa, wameandaa ligi ijulikanayo kama SportPesa  Super Cup , inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi tarehe 5  / 6 / 2017, kwa kushirikisha jumla ya timu 8  kutoka mataifa mawili, Tanzania na Kenya, na mshindi wa mashindano hayo atacheza na timu inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza.

Mshindi wa michuano hiyo mikubwa atapata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu thelathini (USD 30,0000) na mshindi wa pili wa michuano hiyo anatarajia kupata kiasi cha Dola za kimarekani Elfu kumi (USD 10,000).

Kutokana na kuthibitisha kwa klabu ya Everton bilashaka mshindi wa mashindano hayo atacheza na klabu hiyo kongwe iliyoanzishwa  mwaka 1978.

Watu 1,945 Wafariki Katika Ajali ya Pikipiki Ndani ya Miaka Miwili..!!!


Jumla Watu 1,945 wamefariki dunia katika ajali za bodaboda 5,418 tangu mwaka 2015 hadi Februari mwaka 2017 hivyo serikali imeanzisha mikakati kabambe ya kupunguza ajali hizo ambazo zinapoteza nguvu kazi ya taifa licha ya kutoa ajira nyingi kwa vijana

Akitoa mikakati ya Serikali jana Bungeni Mjini Dodoma Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, amesema kati ya mikakati hiyo ni kupitishwa kwa kanuni ya leseni ya pikipiki na bajaji pamoja na kutoa elimu ya usalama barabarani mashuleni pamoja na vyombo vya habari.

Mhe. Mwigulu amesema kuwa mikakati mingine ni kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa waendesha bodaboda, kuimarisha usimamizi wa sheria za barabarani pamoja kusisitiza matumizi ya kofia ngumu ili kupunguza madhara pindi ajali zinapotokea.

Aidha Waziri wa Mambo ya Ndani amesema kuwa Serikali kupitia wadau mbalimbali nchini pia wanaendesha semina mbalimbali kwa waendesha bodaboda hao ili kupunguza ajali lakini pia amelitaka suala hilo lianzie kuelimishwa kuanzia ngazi ya jamii ili kulidhibiti kabisa.

TLS chini ya Lissu Kama Kweli Wanaitakia Mema Tanzania Waungane Kuzima Wizi wa Acacia

Tumesikia mengi kuhusu Acacia kutuibia Watanzania kwa kutumia mikataba, tena iliyoandaliwa na Watazania wenzetu. Kama taifa, hatuwezi kuendelea kulalamika na kunyoosheana vidole, ni lazima tuchukue hatua. Sheria sio Misahafu. Sheria zimewekwa na binadamu na zinaweza kufutwa au kurekebishwa na binadamu pia.

Pamoja na nguvu ya kifedha waliyonayo Acacia Watanzania wakiungana tutashinda hii vita ya kiuchumi. Sasa, TLS kama kweli wanaitakia mema Tanzania waungane na kusimamia mabadiliko ya sheria ili kufuta vifungu vya kinyonyaji na kuhakikisha kila kinachovunwa kwenye ardhi ya Tanzania kinalipiwa kwa haki, na sio kutumia huu ujanja wa 'commercially viable'.

Ni wazo tu
By Hekima Kwanza

Je Mdau Unaonaje Hapo?

Nina Kipaji cha Kukomolewa Kwenye Mapenzi – Wolper

Malkia wa filamu, Jacqueline Wolper amefunguka kueleza moja na sababu ya mahusiano yake na wanaume wengi kushindwa kudumu kwa muda mrefu.

Muigizaji huyo ambaye ameachana na msanii Harmonize miezi kadhaa iliyopita, amedai kuna baadhi ya wasichana wanaingilia mapenzi yake ili kumkomoa.

“Mimi ni kama nina kipaji cha kukomeshwa kwenye mapenzi kwa sababu kipaji ninachokivumbua mimi wenzangu wanataka wapite hapo hapo ili kunikomoa. Ni kwamba nina kipaji cha kukomeshwa lakini huyo anayenikoa unakuta hajui mimi nimepambana vipi kumtengeneza mtu anipendae” alisema Wolper.

Licha ya Wolper na Harmonize kutoweka wazi sababu ya kuachana, lakini stori ambazo ziko mtaani zinadai Harmonize amemuacha muigizaji huyo baada ya kupata mwanamke wakizungu.

Wasanii Watatu Wanao Amini Mambo ya Waganga na Ushirikina Watajwa.

Meneja wa wasanii wa bongo fleva maarufu kwa jina la Meneja Maneno, amefunguka na kusema wapo wasanii wengi Bongo wanaamini ushirikina na kukiri kuwa wapo wasanii wengine ambao yeye mwenyewe aliwapeleka kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kuroga.
.
.
Meneja Maneno aliyewahi kuwa meneja wa Diamond Platnumz, Rich Mavoko, Sam wa Ukweli na Nay wa Mitego, amefunguka hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kuwataja wasanii ambao aliwahi kuwapeleka kwa waganga na ambao wanaamini sana ushirikina kuwa ni pamja na Rich Mavoko, Sam wa Ukweli huku akisema katika wote Diamond Platnumz ndiyo zaidi yao. "Ndele ni sehemu ambayo baadhi ya wasanii waliiamini sana lakini Mungu akisema 'Yes' ni 'Yes' tu kwa hiyo nakumbuka wasanii ambao nilikwenda nao kwa waganga kuroga ni pamoja na Rich Mavoko tena tulienda mbali kabisa huko Kigamboni ndani ndani huko tumeenda ndugu yangu, nilisharusha nazi katikati yaani usiku ule unajifanya chizi kama umevurugwa" alisema Meneja Maneno.
.
.

Meneja Maneno aliendelea kutoa orodha ya wasanii hao ambao kwao shiriki ni kitu ambacho wanakiamini na kukiri kwenda nao huko na kufanya mambo hayo "Hata Sam wa Ukweli siwezi kukataa, ni watu ambao imani yao iliwapeleka huko lakini mimi nakumbuka kazi yangu niliyokuwa nafanya sikutaka kwenda kwa waganga.... ila sasa huyu Mondi sasa nimepata taabu naye, mara leo twende kwa mjomba, tunapeleka unga, leo tunapeleka mchele na mganga alivyo mshenzi hajawahi kuagiza samaki, yeye ni jogoo, mbuzi" alisisitiza Meneja Maneno .
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Kagame Atangaza Kuachia Madaraka ya Urais Rwanda..Awataka Wanyarwanda Kufikiria Mtu Sahihi Ili Kuziba Nafasi Yake..!!!


Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Rwanda unaotarajiwa kufanyika Agosti 3 mwaka huu, Rais wa Rwanda Paul Kagame ameeleza kinaga ubaga kuwa ukomo wake wa kutawala ni mwaka 2024.

Rais Kagame amethibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wa Jeune Afrique kuwa awamu hii ya miaka saba ndiyo ya mwisho na Wanyarwanda wanatakiwa waanze kufikiria mtu mwingine atakayewaongoza baada ya mwaka 2024.

“Inawezekana natakiwa niliangazie suala hili katika siku chache zijazo nitakapoanza mbio za urais. Kuna aina ya makubaliano kati yangu mimi na RPF-Inkotanyi kwa upade mmoja, na raia wa Rwanda kwa upande mwingine“,alisema Kagame na kuendelea kuweka wazi kuwa

“Raia, kupitia kura ya maoni ya Disemba 2015, waliniomba niendelee kuwaongoza nikakubali, ila muda mwafaka wa kupumzika umewadia na waomba waanze kufikiri nje ya mimi baada ya miaka saba“,alisema Kagame kwenye mahojiano yake na mtandao wa Jean Afrique.

Kwa sasa hakuna shaka yoyote kuwa Rais Kagame atashinda uchaguzi wa urais mwaka huu na ni ushindi ambao umekuwa ukitabiriwa kwa muda mrefu na Wanyarwanda.

Mwaka 2015 Wanyarwanda wapatao milioni 4 ambao ni zaidi ya asilimia 70% ya wapiga kura, walipaza sauti zao kulitaka Bunge lirekebishe katiba ili Kagame apate nafasi ya kuendelea kutawala.

Bunge lilifanya hivyo ili limruhusu rais huyo ambaye ana umri wa miaka 59 kuwania awamu zingine mbili hadi mwaka 2024.

JPM Kutikisa Tena Baraza la Mawaziri..Miongoni mwa Hawa Huenda Akamrithi Prof Muhongo Kwenye Wizara ya Nishati na Madini..!!!


UAMUZI wa Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa rafiki yake, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ni wa tatu tangu aunde Serikali, sasa analazimika kukuna kichwa kuteua waziri mwingine kushika nafasi hiyo.

Wakati hilo likisubiriwa, wanasiasa na wasomi wameeleza kuwa hakuna waziri atakayeteuliwa na kusalimika katika wizara hiyo, kwa madai kwamba inazungukwa na rushwa kubwa za kimataifa, mikataba mibovu na kuingiliwa uamuzi na Ikulu.

“Ndiyo maana tumekuwa tukipendekeza kugawanywa kwa wizara hii kwa maana ya kuwa na wizara mbili; ya Nishati na ya Madini,” alisema Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema.

Mei 20 mwaka jana, kwa mara ya kwanza Rais alitengua uteuzi wa rafiki yake mwingine wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga na nafasi yake kuzibwa na Mwigulu Nchemba, ambaye awali alikuwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, huku Mbunge wa Buchosa, Dk Charles Tizeba akiteuliwa kuchukua mikoba ya Mwigulu.

Mabadiliko ya pili ya Baraza la Mawaziri yalifanyika Machi 23, baada ya mkuu huyo wa nchi kumteua Dk Harrison Mwakyembe kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuchukua nafasi na Nape Nnauye ambaye aliachwa.

Katika mabadiliko hayo, Profesa Palamagamba Kabudi ambaye awali aliteuliwa na Rais kuwa mbunge, alipewa Wizara ya Katiba na Sheria ambayo kabla ya mabadiliko hayo ilikuwa ikiongozwa na Dk Mwakyembe.

Rais hakusubiri Profesa Muhongo ajitathmini, baada ya kupokea taarifa ya uchunguzi wa sakata la kiwango cha madini kwenye kontena, alikiri kuwa na urafiki na Mbunge huyo wa Musoma Vijijini na hilo halikumfanya asite kumwajibisha, kwani baada ya kuisoma ripoti hiyo, Ikulu ilituma taarifa kwa vyombo vya habari ikieleza kuwa Rais ametengua uteuzi wa mtaalamu huyo wa miamba.

Mara zote mbili alizofanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, Rais Magufuli amekuwa na utaratibu wa kuhamisha mawaziri kutoka wizara moja kwenda nyingine au kuteua wabunge na kuwapa wizara.

Katika mabadiliko hayo mawili aliyofanya, ni Dk Tizeba pekee ambaye aliteuliwa kuwa waziri kutoka miongoni mwa wabunge wa majimbo.

Iwapo Rais Magufuli atazingatia utaratibu wa mtangulizi wake Jakaya Kikwete kuteua waziri kutoka mkoa ambao waziri aliyeondoka anatoka, huenda nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Muhongo ikajazwa na wabunge kutoka mkoa wa Mara.

Baadhi ya wabunge wa CCM kutoka mkoani Mara ni Boniface Getere (Bunda Vijijini), Nimrod Mkono (Butiama), Vedastus Mathayo (Musoma Mjini), Kangi Lugola (Mwibara) na Lameck Airo (Rorya).

Pia, kauli ya CCM jana kwamba imechoshwa na mauaji yanayotokea kila uchwao mkoani Pwani, ni sawa na kutuma ujumbe kwa Rais Magufuli kwamba kuna tatizo katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuchochea ukubwa wa mabadiliko.

Utaratibu

Miongoni mwa wateule wake ni Naibu Spika, Dk Tulia Ackson. Novemba mwaka 2015 Naibu Mwanasheria Mkuu huyo wa zamani alichukua fomu za kuwania uspika kupitia CCM kabla ya kujitoa dakika za lala salama kisha akateuliwa na Rais Magufuli kuwa mbunge wa viti maalumu.

Baada ya kujitoa, alijitosa kuwania unaibu Spika ambapo wabunge 250 walimpigia kura ya ndiyo.

Wengine walioteuliwa kuwa wabunge na akawapa wizara ni; Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Augustino Mahiga, Profesa Makame Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu), Dk Philip Mpango (Fedha) na Dk Abdallah Posi  ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu.

Hata hivyo, Posi aliteuliwa kuwa balozi kufuatia dosari ya kikatiba katika uteuzi wa wabunge 10 wa kuteuliwa na Rais ambapo Ibara ya 66 (1)(e) inaeleza katika nafasi hizo,  wabunge watano au zaidi wanapaswa kuwa wanawake. Baada ya kuondolewa Posi, Rais alimteua Anne Kilango kuwa Mbunge.

Hivi karibuni, Rais alimteua Salma Kikwete kuwa mbunge na kufanya idadi ya wabunge wanawake wa kuteuliwa na Rais kuwa wanne, kubaki nafasi moja ya uteuzi ambayo ni lazima awe mwanamke.

Mwingine aliyeteuliwa na Rais kuwa mbunge ni Abdlallah Bulembo na kufanya idadi ya wabunge walioteuliwa na kiongozi mkuu huyo wa nchi bila kupewa uwaziri kuwa watatu.

Kwa mantiki hiyo, kama Rais Magufuli atazingatia utaratibu wake wa kuteua mbunge na kumpa wizara, safari hii atalazimika kuteua mbunge mwingine mwanamke.

Iwapo hatateua na kuamua kubadili utaratibu wake, huenda Salma na Kilango wakakumbukwa, huku kukiwa na kila dalili ya baadhi ya mawaziri kuhamishiwa Wizara ya Nishati na Madini.

Wanasiasa, wasomi

Katika maelezo yake, Mbowe alisema madini yanahusisha mafuta, gesi na vito hivyo vikichanganywa na nishati ni mzigo mkubwa.

Alibainisha kuwa wizara hiyo inakabiliwa na vishawishi vingi kutokana na fedha zinazopatikana kwa wawekezaji, jambo ambalo huwa ni mtego kwa mawaziri.

Huku akikosoa mikataba ambayo Serikali imeingia na wawekezaji wa sekta ya nishati na madini, Mbowe alisema ikifuatiliwa kwa undani hakuna atakayebaki salama.

“Yupo Waziri Mkuu mmoja aliondoka kwa kashfa ya wizara hii. Kusema nani atatosha ni ngumu sana kwa wizara hii,” alisisitiza Mbowe.

Mwenyekiti wa Chama Cha Kijamii (CCK), Constatine Akitanda aliitaja wizara hiyo na ya Maliasili na Utalii, kukiri kuwa ni ngumu kuziongoza.

Alidai kuwa mambo mengi yanayoikumba nchi kwa sasa ni matokeo ya nchi kuingia mikataba mibovu, hasa katika utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu.

“Tunachopaswa kufanya ni kuangalia mfumo na mikataba iliyoingiwa. Imetawaliwa na nguvu ya pesa, hakuna waziri atakayekuwa salama,” alisema Akitanda.

Kwa upande wake, kada wa Chadema na mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila alisema:”Madini na nishati ni rasilimali zinazoongozwa kwa rushwa duniani, ni ngumu kutulia.”

Kafulila alisema nchi kadhaa duniani zinapigana kwa sababu ya nishati na madini, jambo alilodai kuwa linaakisi nchini.

Rais wa zamani wa Chama kilichofutwa cha APPT-Maendeleo, Peter Mziray alisema, “Kama Mkapa angeona mbali haya mambo yasingetokea hivi sasa. Alishiriki ubinafsishaji ambao umenufaisha wageni.”

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Frank Tilly alisema kinachoikumba wizara hiyo ni matokeo ya nchi kukosa muundo madhubuti wa uongozi, kusababisha viongozi kufanya mambo wanavyojisikia.

Credit - Jambo Leo

Sakata la Mchanga wa Madini..Chenge Amchana Live Rais Magufuli..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumamosi 27/5/2017..!!!



 

Gallery

Popular Posts

About Us