KINGAZI BLOG: 01/24/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 24 January 2017

Ajali mbaya ya Basi na Lori la Mbao Yaua na Kujeruhi 32 Iringa.


Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 32 kujeruhiwa vibaya baada ya basi la Vitu Laini linalofanya safari zake kutoka vijiji vya Kilolo kwenda Iringa Mjini kugongana na lori la mbao karibu likiwa limekaribia kufika Iringa Mjini.

Akizungumza  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Peter Kakamba amethibitisha kutokea kwa ajli hiyo na kueleza kuwa majeruhi wote wa ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa.
“Ni kweli ajali imetokea leo asubuhi nje kigogo ya Mji wa Iringa, basi ndilo limelogonga lori kwa nyuma na kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyeaga dunia palepale na kusababisha majeruhi 32.

“Majeruhi wote tumewapeleka katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa ambako wanaendelea kupatiwa matibabu mpaka sasa.
Alisema Kamanda Kakamba.Kuhusu chanzo cha ajali hiyo haijafahamika kama ni matatizo ya gari au mwendoksasi wa dereva hivyo Kamanda Kakamba amesema watatoa taarifa rasmi baabdaye kuhusu tukio hilo.

LEO NI SIKU YA KUZALIWA YA MWANANGU ANAITWA MOUREEN

Happy birthday my lovely daughter god give a hundred of year be blessed in every thing you do

Rais Donald Trump kawafuta kazi Mabalozi wote wa Marekani duniani

Kwa mujibu wa  The Independent naParsToday wanasema kuwa Rais Donald Trump wa Marekani amewafuta kazi mabalozi wote wa nchi hiyo kote duniani na wanaohudumu katika mashirika ya kimataifa ambapo uamuzi huo umefanyika katika siku yake ya kwanza kazini.
 

Trump ambaye aliapishwa Ijumaa January 20, 2017 kuwa Rais wa 45 wa Marekani, amewataka mabalozi wote walioteuliwa na mtangulizi wake, Barack Obama kuondoka kazini mara moja bila hata kuwapa muda wa kujitayarisha kuondoka kama ilivyo kawaida.
 

Inaelezwa kuwa zaidi ya mabalozi 80 wa Marekani katika nchi mbalimbali duniani walifutwa kazi Ijumaa tarehe 20 Disemba saa sita mchana ikiwa ni mara baada ya Trump kuapishwa.
 

Hatua hiyo ya Trump inatazamiwa kuvuruga uhusiano na washirika muhimu kama vile Ujerumani, Uingereza na Canada ambapo ripoti zinasema nchi hizo zinaweza kukaa bila mabalozi kwa miezi kadhaa kwani baada ya Trump kuteua mabalozi wapya watalazimika kuidhinishwa na Bunge la Congress kabla ya kuanza kazi zao.
 

Donald Trump anakosolewa kwa kuacha nafasi nyingi wazi na hivyo kuvuruga shughuli za kawaida za serikali ya Marekani na hii haya yanajiri huku maandamano yakiripotiwa kuendelea sehemu mbalimbali kupinga utawala wa kiongozi huyo. 
 

Nchini Marekani katika siku ya pili ya utawala wa Trump kumeripotiwa maandamano ya watu milioni tatu na imeripotiwa kumefanyika maandamano 637 katika maeneo mbalimbali ya Ulaya, Asia na Afrika kumpinga rais mpya wa Marekani.

MUHIMU :TAARIFA MUHIMU KWA WAKAZI WA JIJI LA DAR KUTOKA SUMATRA


Watoto wachanga watumiwa na Boko Haram, kushambulia


Wanawake wanaojitoa mhanga nchini Nigeria wameanza kutumia watoto kuepuka vizuizi vya ukaguzi, jambo ambalo, serikali nchini humo inasema linaweza kuwa mwelekeo wa hatari.

Tahadhari hiyo imekuja baada ya wanawake wawili waliokuwa wamebeba watoto mgongoni kufanya mashambulizi ya kujitoa mhanga katika mji wa Madagali siku 10 zilizopita.

Januari 13 mwaka huu, wanawake wanne waliokuwa wakijitoa mhanga walifika kwenye mji wa Maddaggalee katika jimbo la Adamawa, wawili walitambuliwa na walinzi waliokuwa katika vizuizi na kutakiwa kusimama, baada ya mbinu zao kugundulika.

Lakini wengine wawili walifanikiwa kupita bila ya kugunduliwa. kubeba kwao watoto kulifanya wasigunduliwe na kuweza kusababisha maafa yaliyosababisha vifo vya watu wanne, wao wenyewe kufariki na watoto wawili pia waliokuwa wamewabeba katika mawili tofauti.

Kundi la Boko Haram linajulikana kwa kuwatumia wanawake, hususan wasichana katika mabomu ya kujitoa mhanga, Hata hivyo ni mara ya kwanza katika maasi hayo kutumia watoto wachanga.

MAGAZETI YA TANZANIA YALICHAONDIKA LEO JUMANNE YA JAN 24



Hii hapa Mikataba 9 Iliyosainiwa na Serikali ya Tanzania na Uturuki Leo


Serikali ya Tanzania na Serikali ya Uturuki zimesaini mikataba tisa ya makubaliano ya kiuchumi inayolenga katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa maendeleo baina ya nchi hizo.

Mikataba hiyo inahusisha sekta za uchukuzi, mawasiliano, habari, elimu, utalii, utafiti, viwanda, afya na ulinzi.

Akizungumza mara baada ya kusaini kwa mikataba hiyo  leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alisema ujio wa Rais wa Uturuki na ujumbe wake ni kielelezo cha ukuaji wa mahusiano baina ya Tanzania na Uturuki katika nyanja ya biashara na kimaendeleo baina nchini hizo.

Rais Magufuli alisema katika mazungumzo yake aliyofanya na Rais Recep Erdogan kuhusu ujenzi wa Reli ya Standard Gauge nchini, alimjulisha kiongozi huyo kuwa miongoni mwa wakandarasi walioomba zabuni ya ujenzi wa reli hiyo kuwa ni kampuni kutoka Uturuki, hivyo endapo itashinda zabuni hiyo itasaidia kukuza uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili.

Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa, Serikali ya Tanzania inatarajia kuomba  mkopo kupitia Benki ya Exim ya Uturuki katika kujenga sehemu ya kipande cha ujenzi wa reli hiyo.

Rais magufuli alisema Tanzania inaendelea kunufaika na uwepo wa Shirika la Ndege la Uturuki kwa kufanya safari zake za moja wka moja kutoka nchini Uturuki, kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa idadi ya watalii nchini na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo.

Kwa upande wake Rais wa Uturuki, Recep Erdogan alisema kuwa uwepo wa mikataba hiyo baina ya Tanzania na Uturuki itasaidia kupata matokeo mazuri ya uhusiano pamoja na fursa mbalimbali za ushirikiano katika nyanja ya Kilimo, Utalii, Ulinzi, Reli ambazo zitawezesha kukuza uchumi wa mataifa hayo.

Rais Erdogan alisema kuwa Uturuki imelenga kukuza ushirikiano uliopo baina yake na  Tanzania kupitia makongamano ya wafanyabiashara yenye malengo ya kukuza uchumi, kuongeza ajira pamoja na kukuza ujasiriamali baina ya Tanzania na Uturuki.

“Kiwango cha Biashara ya uwekezaji katika nchi ya Uturuki ni Dola za kimarekani 150 ambapo lengo letu ni kufika Dola za kimarekani 500,” alisema Rais huyo.

Aidha Rais Erdogan alisisitiza kuwa kufanya kazi kwa pamoja kutasaidia nchi hizi kusonga mbele na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali.

Nae Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe alisema kuwa makubaliano ya mkataba baina ya Tanzania na Uturuki katika Sekta ya Utalii yatasaidia katika kutangaza vivutio vilivyopo nchini, kubadilishana wataalamu, kubadilishana taarifa na kuongeza idadi ya watalii nchini.

Prof. Magembe aliongeza kuwa makubaliano hayo yatakuza sekta ya utalii katika kuvutia uwekezaji wa katika maeneo ya hoteli, fukwe na mbuga za wanyama zilizopo nchini.

Kwanini Kipindi cha Orijinal Komedi Hakionyeshwi Kwenye Luninga Siku Hizi? Joti Asema Haya

Kwako mfwatiliaji wa mabingwa wa kuchekesha wanaoishikilia rekodi ya wachekeshaji waliotazamwa sana kwenye TV nchini Tanzania kuanzia time hiyo ya Ze Comedy mpaka Orijino Komedi walivyokuwa wanawafanya watu wawahi TV zao kila Alhamisi jioni.

Ni kitambo kidogo hatujawaona Orijino Komedi kwenye TV (TBC 1) na inawezekana maswali tuliyonayo ni mengi lakini hakuna hofu tena maana tumempata Joti na amekubali kuongelea kwa ufupi.

‘Kama kundi tuna taratibu zetu na ndio maana tumejaribu kutumia muda wa mwaka mmoja kupumzika maana toka tuanze kufanya kazi hatujawahi kupumzika, tulivyopumzika pia sio kukaa kimya tukaangalia project za kila mtu binafsi na ndio maana unaona kila mtu na shughuli zake‘ – Joti

‘Ukimfatilia Mpoki kuna shughuli zake anafanya na inajulikana, Masanja pia vivyo hivyo… na mimi nimefungua Youtube channel yangu ya Joti TV, nafikiri mwaka huu tunaweza kurudi kazini pia.

Je mazungumzo ya huyu bwana mdogo yana ukweli? au baada ya huu utawala wa kiimla walipigwa stop,mpaka watakapopangiwa vyakuigiza. karibuni kwa mjadala

 

Gallery

Popular Posts

About Us