KINGAZI BLOG: 12/09/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 9 December 2016

Hofu yatanda binti aliyechunwa ngozi karatu


HOFU imetanda wilayani Karatu katika Mkoa wa Arusha baada ya tukio la kwanza la uchunaji ngozi kuripotiwa katika mji mdogo wa Karatu.

Binti mdogo mwenye umri wa miaka tisa, ameuawa mjini Karatu baada ya kutekwa nyara na watu wasiojulikana wakati akielekea machungani na mifugo.

Mtoto huyo, Witness Andrew ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa Darasa la Kwanza kwenye Shule ya Msingi ya Sumawe, alipatikana Jumatano usiku, akiwa tayari amekufa, baada ya kuripotiwa kupotea kwa zaidi ya saa 24 tangu alipoondoka nyumbani kwao akiwa anaswaga ng’ombe na mbuzi, Jumanne iliyopita.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kiwandani ambako mwili wa mtoto huyo ulipatikana, Alexander Lulu amesema maiti ta mtoto huyo ilikutwa ikiwa imetupwa shambani na baadhi ya viungo vikiwa vimenyofolewa pamoja na ngozi iliyochunwa na kuondelewa kabisa.

Witness pia alikutwa bila mguu, mkono na sehemu zake za siri na baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Tloma wanadai ni masuala ya ushirikina. Mtoto huyo ndiye wa kwanza kuchunwa ngozi katika eneo la Karatu na tayari hofu imeanza kutanda hapa, watu wakihofia kuwa wachuna ngozi watakuwa wamevamia wilaya hiyo.

Baba ya marehemu, Andrea Paulo na Mama Paulina Petro wanasema mtoto wao alipotea tangu Jumatatu wiki hii alipotoka na mifugo kwenda kuchunga kwenye uwanda wa Tloma, lakini hakurudi nyumbani, na kwamba mifugo aliyokuwa nayo ilirejea yenyewe.

“Tulimtafuta mtoto kila mahali, lakini bila mafanikio, hata tulipoikuta maiti yake eneo la Kiwandani, tulishangaa maana tulishapita kwenye mashamba hayo mapema, lakini hatukumuona,” walisema wazazi.

Wanakijiji wa Tloma wanaamini kuwa mtoto huyo alitekwa na kupelekwa eneo jingine ambako ndiko alichinjwa kabla ya wauaji wake kumrudisha na kumtupa Kiwandani

YULE MZEE MWENYE TANGAZO LA KUTAFUTA MKE TAYARI AMEPOKEA MAOMBI YA NDOA 30...WANAWAKE WAZIDI KUMIMINIKA



MZEE Athuman Mchambua (76), ambaye ameweka tangazo nyumbani kwake la kutafuta mke, ameongeza sharti jipya kwa mke anayemuhitaji.

Amesema licha ya kupokea simu nyingi kutoka maeneo mbalimbali nchini, lakini amewataka wanawake ambao atawafanyia usaili, hasa kwa yule ambaye atakuwa ameshinda, kutobweteka kwani atakuwa katika kipindi cha mpito cha ndoa yake.

Mzee huyo amelieleza gazeti la Mtanzania kuwa amefikia hatua hiyo ili kuanza kupitia majina ya wanawake zaidi ya 30 ambao tayari wamejaribu bahati ya kuolewa naye.

Alisema kuwa haoni haja tena ya kuendelea kuweka tangazo hilo kwa kuwa asilimia kubwa ya wanawake wanaojitokeza hushindwa kukidhi vigezo anavyovihitaji.

Alivitaja vigezo sita muhimu vya mwanamke anayemuhitaji kuwa ni awe mcha Mungu na mwenye kutunza watoto wake.

“Vigezo vingine awe na sifa ya ndoa, awe na sifa ya mume, awe na sifa ya kilimo, awe na sifa ya kutunza watoto na awe na sifa ya usafi wa hali ya juu.

“Tangu kuanza nimepata wanawake zaidi ya 30 ambao wanne kati yao wamefika hapa nyumbani kwangu, lakini wengine wamekuwa wakiona aibu kuja hapa moja kwa moja na hivyo wamekuwa wakitumia simu. Leo (jana) nimewafanyia usaili wanawake watano kwa simu, lakini hakuna hata aliyefuzu nusu ya vigezo, wengi wamekuwa wakiteleza sifa ya kilimo,” alisema.

 

Gallery

Popular Posts

About Us