KINGAZI BLOG: 04/27/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Thursday 27 April 2017

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA IKULU KUHUSU SUALA LA UHAKIKI WA VYETI.


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
                 KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
    OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kesho tarehe 28 Aprili 2017, atapokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti kwa Watumishi wa Umma katika Ukumbi wa Chimwaga Mkoani Dodoma.
Taarifa hiyo itawasilishwa kwa Mheshimiwa Rais na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Angellah Kairuki.
Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa Watumishi wa Umma liliendeshwa na Serikali kuanzia Mwezi Oktoba mwaka 2016.


Jaffar Haniu,
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU,
Chamwino, Dodoma.
27 Aprili, 2017

Eric Omondi - How To Be DONALD TRUMP(Comedy Video).| New Comedy Video




Eric Omondi - How To Be DONALD TRUMP(Comedy Video).| New Comedy Video

Umeipata hii???Kijana wa Miaka 21 Akiwa Ndani ya Mwili kama wa Mzee wa Miaka zaidi ya 100!!

 Mshukuru Mungu kwa kila Kitu, Usijivunie Mwili wala Muonekano maana ni zawadi ambayo Ulipewa sio kweli kwamba huyu Dogo alipenda yeye, Au sisi ni Bora kuliko yeye machoni pa Mwenyezi Mungu.

1:Anakuwa mara nane zaidi ya Ukuaji wa Mwanadamu wa kaidia

2:Wazazi wake walitaka kumuuza kwenye maonyesho.




Picha!! China imtengeneza meli kubwa ya kivita

China imetangaza kwamba imefanikiwa kuzindua manowari yake ya kwanza ya kujiundia yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita, Meli hiyo ya kivita ina uzani wa tani 50,000.

Hatua hiyo inachukuliwa kama ishara ya karibuni zaidi ya kujiimarisha kwa taifa hilo katika nguvu za jeshi lake la majini.

Vyombo vya habari nchini China vinasema meli hiyo, ambayo inawezesha ndege kuruka na kutua juu yake, ilisafirishwa kutoka eneo ambalo ilikuwa ikiundiwa Dalian na kuwekwa baharini, Inatarajiwa kuanza kazi rasmi mwaka 2020.






MAAJABU ya Dunia… Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne..!!!!


Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia familia moja kukumbwa na mauzauza baada ya watoto wa mama aliyefahamika kwa jina la Hawa Hassan Ngonyani kupatwa na mabadiliko ya maumbile ambapo mmoja ameota matiti na mwingine kuanza kuotwa na uvimbe shingoni.

Hawa anaishi na wanaye watatu maeneo ya Kinzudi Kata ya Goba, jijini Dar ambapo waandishi wetu walifika na kujionea hali halisi ya watoto hao.

Mara baada ya waandishi wetu kufika katika nyumba hiyo, walipokelewa na Hawa aliyeonekana kukata tamaa ya maisha kutokana na jinsi anavyoishi kwa malumbano na mumewe anayedaiwa kuitelekeza familia yake.

Akizungumza na mwandishi wetu nyumbani hapo, Hawa alisema aliolewa ndoa ya mkeka miaka kadhaa iliyopita huku mwanaume akimzalisha ‘fastafasta’.

Alisema mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na mbili anayesoma darasa la saba katika Shule ya Msingi Kinzudi, alizaliwa mzima huku akiwa na chuchu mbili tu hadi mwaka jana mwanzoni ndipo alipokumbwa na balaa hilo la kuota chuchu zingine sehemu za juu ya titi za kawaida ambazo hadi sasa zinazidi kukua siku hadi siku.

Akizidi kufafanua, mama huyo alisema mara baada ya kuona hali hiyo, aliamua kumshirikisha baba watoto wake ambaye ni kama amehama kabisa nyumbani, lakini alikosa ushirikiano kwa mumewe huyo kwani hadi sasa mtoto hajapelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi, kwani zile chuchu zinazidi kukua pamoja na kumkosesha amani mtoto huyo anayejiandaa na mitihani ya kuhitimu darasa la saba.

Hawa alisema wakati akihangaika na mwanaye huyo wa kwanza namna ya kumpeleka hospitali bila msaada, mtoto wake mwingine ameanza kuota uvimbe shingoni ambao unahitaji jitihada za haraka kuutibu kabla haujawa mkubwa.

Na alipomueleza tena mumewe, pia hakumpa ushirikiano.

“Yaani alichonijibu ni kuwa yeye kwa sasa ana madeni mengi hivyo hana fedha, nifanye michakato mingine nikawatibu yeye hana hela kwa sasa,” alisema bi mkubwa huyo huku akibubujikwa na machozi.

Hata hivyo, dada huyo alisema mumewe ni mkorofi kwani pia amewahi kumpiga hadi kusaidiwa na majirani.

Mwanamke huyo alihitimisha kuomba msaada kwa taasisi na mashirika ya utetezi wa haki za binadamu wamsaidie kumuachanisha na mwanaume huyo ambaye pia inadaiwa hutumia kilevi.

Hawa alisema anahofia usalama wake kutokana na kupigwa mara kwa mara na mbaya zaidi wakati anampiga huwa anamvua nguo zote na kumdhalilisha mbele ya watoto hivyo kukimbilia kwa majirani akiwa mtupu.

Aidha, pia mtoto huyo mwenye tatizo la kuota matiti ya ziada, alisema anaamini manyanyaso ya kutopewa huduma na mama yake kudhalilishwa vinatokana na mchepuko wa baba yake ambapo kuna siku alinasa mazungumzo live ya baba yake akiongea na mchepuko wake, lakini kikubwa kinachomuuma ni kulala na njaa au kunywa uji ambao hauna sukari.

Kufuatia tuhuma hizo, gazeti hili lilimsaka baba wa watoto hao aliyefahamika kwa jina la Abdul Liloka ili kuelezea kwa nini amekuwa akiinyima haki za msingi familia yake na hapa anaelezea tuhuma hizo:

“Ndugu mwandishi kwanza ni kweli mke wangu alinipatia taarifa za wanangu kuumwa lakini hali ya Magufuli sasa ni ngumu, mimi nilikuwa na madeni kibao ila kwa sasa nimemaliza nikipata hela nitampeleka hospitali huyu mdogo mwenye uvimbe.”

Kuhusu huyu mwingine mwenye matiti manne pia alisema: “Jamani hayo maziwa yaliyoota huo ndiyo utamaduni wa familia yetu, wapo dada zangu wengi wameota pia kwa hiyo hapo hamna tatizo tena bora hata yeye ni madogo yupo shangazi yake mmoja anayo makubwa balaa.”

Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kuitesa familia yake kutokana na kuwa na mchepuko, Liloka alisema:

“Jamani mimi ni Muislam nina haki ya kuoa hata wanawake kumi si uwezo wangu, ni kweli nina mchumba mwingine nje hata huyo aliyewapa taarifa kwa maana ya mke wangu anamjua sana na kuhusu kumpiga ni kweli kuna siku nilimpiga kofi moja tu!”





Makubwa!!!Huyu ndiye Rais Mpya wa Ufaransa Emmanuel Marcon..Amemuoa Mwalimu Wake Aliyemzidi Zaidi ya Miaka 24..Alianza Kutembea Naye Toka Akiwa na Miaka 17..!!


EMMANUEL MARCON mwenye umri wa miaka 39 ndiye anayetarajiwa kuwa rais ajaye wa Ufaransa.

Pamoja na hayo, Marcon ambaye ameoa mke mwenye umri wa miaka 64 ,ana mambo mengi ya kufurahisha na kuvutia maishani mwake hususan kuhusiana na mkewe huyo ambaye anamzidi umri kwa kiasi cha miaka  zaidi ya 24.

Mkewe huyo alikuwa ni mwalimu wake wa darasa miaka ipatayo 24 iliyopita ambapo mwalimu wake wa darasa wakati huo alikuwa na binti ambaye alikuwa mwanafunzi mwenzake darasa moja.  Wakati huo, kila mtu, wakiwemo wazazi wake Marcon, walifikiri binti huyo wa mwalimu alikuwa rafiki yake, wakati hawakuwa hivyo.

Katika mlolongo huo wa vituko, Marcon alijikuta katika mapenzi na mwalimu wake wakati yeye akiwa na umri wa miaka 15 ambapo wakati huo, mwalimu huyo alikuwa ameolewa akiishi kwa furaha na akiwa na watoto watatu

Alipofikisha umri wa miaka 17, aliamua kumuoa mwalimu huyo, wakati huo akiwa na umri wa miaka 42.

apendanao hao walifunga pingu za upendo mwaka 2007 wakati huo ‘mlume’ huyo akiwa na umri wa miaka 30 na ‘mrembo’ wake akiwa anapiga hodi katika umri wa miaka 55.

Mwanandoa huyo wa kiume anatarajiwa kuapishwa kuwa Rais wa Ufaransa mwezi ujao akiwa amebakiza miezi sita kufikisha umri wa miaka 40 wakati ambapo kipenzi chake, yaani mkewe,  ana watoto  (watu wazima) watatu na wajukuu saba sasa.

Ni vyema pia kufahamu kwamba mtoto wa kwanza wa mkewe huyo anamzidi Marcon kwa umri wa miaka miwili, wakati ambapo mtoto wake wa pili, aliyekuwa kipenzi na mwanafunzi mwenzake  na Marcon wakiwa darasa moja, wanalingana umri.

MAWAZIRI Waanzisha Chama Kipya..Wajipanga Kuiondoa CCM Madarakani..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 27/4/2017..!!!





‘Padri’ wa Kanisa Katoliki afunga ndoa Dar es Salaam

Miaka tisa baada ya kuvuliwa upadri wa Kanisa Katoliki, Privatus Kargendo jana alifunga ndoa na mchumba wake Rose Birusya. Ndoa hiyo ilifungwa katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es Salaam katika misa iliyoongozwa na Padri Stefano Kaombe.

Kabla ya kuvuliwa upadri, Karugendo alikuwa Padri wa Jimbo la Rulenge-Ngara kabla ya Papa Benedict XVI kumvua daraja hilo kwa madai ya kukiuka maadili ya kanisa katoliki.

Septemba 14, mwaka 2008 Karugendo alitangazwa kuwa ni muumini mlei asiye na daraja la upadri tena kupitia hati ya Papa yenye namba Protokali 4182/08.

Ingawa sababu za kuvuliwa kwake hazikuwekwa wazi kwa jamii zaidi ya kusema amekiuka kanuni za kanisa hilo, watu wengi walihusisha tukio hilo dhidi ya andiko lake kuhusu UKIMWI na matumizi ya mipira ya kiume (condoms).

Baada ya kuvuliwa cheo hicho, Karugendo sasa ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo gazeti la Mwananchi.

Waumini waliokuwamo katika misa ya ndoa hiyo, walimpongeza Karugendo na kusema kuwa uamuzi wake wa kufunga ndoa katika Kanisa Katoliki umeonyesha kuwa hana tatizo nalo licha ya kuvuliwa cheo hicho.

Mapadri wa Kanisa Katoliki hawaruhusi kuoa ikiaminika ili waweze kujikita zaidi katika kushughulikia masuala ya kanisa bila kuwa na kitu cha kuwaondoa humo ikiwa ni pamoja na familia.

Umeipata hii!!!Ray Kigosi afunguka Mambo Mazito kuhusu marehemu Kanumba Kuhusishwa na Uchawi na Freemason

Msanii wa filamu nchini Ray Kigosi amefunguka na kusema kuwa baadhi wa Watanzania ni wanafiki na wamekuwa wakikatisha tamaa watu katika mambo yao kutokana na unafiki wao.

Ray Kigosi amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Instgram na kusema kutokana na unafiki huo wa baadhi ya watu ulimfanya mpaka marehemu Kanumba kuvunjwa moyo katika kazi yake.

==>Ray Kigosi ameandika;
1. Kanumba alipoanza kuona mwanga wa kufanikiwa bila kujali juhudi zake kuna watu walimuita Freemanson, Mara anatumia nguvu za Giza. that is to say films zake hazikuwa nzuri but ziliuza sababu ya nguvu za Freemanson na nguvu za giza!!

2. Kanumba alipoenda Big Brother alipondwa Sana na kuitwa bogus kwa Madai hajui kiingereza, Ni watanzania Hawa Hawa walibebea bango hili huku baadhi ya waandishi uchwara wakieneza ujinga huu bila kujali juhudi zake. But Leo wanamsifia hakuna Kama Kanumba!

3. Kuna wakati Kanumba alionekana wazi kuvunjwa moyo na kukatishwa tamaa kwa kuonekana juhudi zake si kitu. But Alisema maneno machache Kuwa mtanikumbuka kama si Leo basi Ni Kesho.
And alichosema kimetimia, wale wale waliokuwa wakisema Ni Freemanson bila hata kujali juhudi zake kwenye game Leo ndio kwa unafiki wanasema hakuna Kama Kanumba !….. HAO NDIO BINADAMU NA TABIA ZAO
Je Kanumba kaondoka na Bongo Movie yake ya Freemanson ? Kama wengine mnavyodhani industry Ni Mtu sio system !

4. Diamond Platnumz nae baada ya kuona Njia ya mafanikio kuna watanzania, wasanii wenzake na hata baadhi ya wanahabari wanasema Ni Freemanson, wengine wanaonyesha chuki ya wazi kwake. Wanasema Hana muziki mzuri, Mara Ni Kiki tu ambazo hata Kanumba alikuwa akiripotiwa magazetini na kina Wema.

Hawaoni juhudi na thamani ya Diamond sasa ! Hatuombi baya limpate Diamond ili kudhibitisha tabia na unafiki wa binadamu. But HAO NDIO BINADAMU siku zote hawana Jema unafiki ni sehemu ya Maisha.

5. kila siku Ni kuzua hii na kile, Mara ooh Diamond Ni mchawi, kasema mleteni huyo mganga wangu mkashindwa kumleta, akajitokeza mganga fake sijui na Madai juu Kuwa Diamond atashuka kimuziki kwa sababu ananipuuza niliyempa nyota, Diamond akasema sawa namtegemea Mungu. Miaka 4 sasa tangu yaliyoitwa ya mganga Diamond hashuki ndio anazidi kupaa. HAO NDIO BINADAMU kusema lolote Ni haki Yao.

Kazi za Kanumba sasa zinapewa thamani na ubora uliovuka mipaka na viwango ambao hakupewa kipindi yupo hai ! HAO NDIO BINADAMU na tabia zao. Ni tabia tu ya baadhi ya watu kubebea mabango mabaya ya Mtu au uzushi na kuacha mazuri yake then baadaye wakishikwa Uchawi wanageuza walichoamini Ni nyeusi kiwe nye.



Hukumu ya Babu Seya, Papii, Mapya Tena

Tumaini jipya! Mtoto wa kiume wa mfungwa anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking ‘Babu Seya’, Mbangu Nguza ameibuka na kusema kuwa, mwaka 2017 ndiyo wa mwisho kwa baba yake na mdogo wake, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ kuendelea kutumikia kifungo chao cha maisha jela.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Amani mwanzoni mwa wiki hii, Mbangu alisema kuwa, turufu ya mwisho ya hukumu ya ndugu hao ipo kwenye mikono ya Mahakama ya Haki za Binadamu Afrika (AfCPHR) yenye makazi yake jijini Arusha ambayo kimsingi vikao vitatu vya awali vimeshakaa na kubaini kuwa, hukumu ya Babu Seya na Papii ilikuwa na kasoro.

“Unajua watu hawafahamu, kule ambako hukumu ya mzee na bwana mdogo (Papii), ilipelekwa kuna hatua. Kwanza kabisa, wale majaji wanatoka nchi mbalimbali, kwa hiyo siyo kwamba wanakwenda tu Arusha na kupitia hukumu, hapana.

“Kilichofanyika ni kwamba, kuna watu walikaa mara tatu kupitia hukumu ili wajiridhishe kama kuna makosa ambayo majaji wakikaa watayaona?

“Kwa hiyo vile vikao vimeshakaa mara tatu zote na kubaini kuwa, kweli hukumu ya baba na bwana mdogo ilikuwa ina kasoro.

“Sasa ndiyo majaji wameitwa ili kupitia na kutoa hukumu yao ya haki. Hii kazi ingekuwa imeshafanyika muda mrefu ila sasa, kilichotokea ni kwamba, kuanzia Novemba mwaka jana kama sikosei, watu wa mahakamani walikuwa likizo ndefu mpaka kwenye Februari mwaka huu, ndiyo wamerudi.

“Kingine kimechelewesha ni mwaka jana kustaafu kwa rais wa ile mahakama, Jaji Augustino Ramadhani (kutoka Tanzania), kukawa na kitambo cha kusubiri kumpata rais mpya, tayari yupo (Sylvain Ore kutoka Cote d’Ivoire).

“Kwa hiyo bwana, baada ya sasa, wakati wowote ule, majaji watatua Arusha na kukaa kupitia, naamini, tena narudia kusema, naamini, baba na bwana mdogo wangu mwaka huu watakuwa huru.

“Hili suala la wao kuwa huru liko pia kiroho, hata kama mahakama hiyo isingekaa, bado wale ndugu wangetoka tu, lazima. Kwani Mungu ninayemtegemea mimi ameshaniambia watatoka,” alisema Mbangu ambaye kwa sasa ni Mwinjilisti wa Neno la Mungu.

TUMEFIKAJE HAPA?

Nguza na wanawe watatu walikamatwa Oktoba 12, mwaka 2003 na kufikishwa Kituo cha Polisi Magomeni, Dar, walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Oktoba 16, mwaka 2003 wakituhumiwa kubaka na kunajisi watoto 10.

Baada ya kusikilizwa kesi hiyo Juni 25, 2004, Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar, Addy Lyamuya aliwatia hatiani Babu Seya na wanaye kwenda jela maisha kwenye Gereza la Ukonga, Dar es Salaam.

Januari 27, mwaka, 2005, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa yao iliyokuwa ikipinga hukumu.

Awali mwaka 2004, baada ya kukutwa na hatia katika kesi hiyo, Babu Seya, Papii Kocha na wakili wao, Mabere Nyaucho Marando walikata rufaa ya pili ambayo ilitupiliwa mbali.

Mwaka 2010 waliomba tena rufaa ambayo marejeo yake yalisikilizwa na kutolewa hukumu Februari, 2010. Mahakama iliridhia hukumu ya kifungo cha maisha kwa Babu Seya na Papii Kocha, ikawaachia huru watoto wake, Mbangu na Francis Nguza.

 

Gallery

Popular Posts

About Us