KINGAZI BLOG: 02/14/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 14 February 2017

Maharusi waliotumia dola pekee waandaliwa harusi ya kifahari Kenya

HakiAALTONEN JUMBAImageHarusi ya marudio ya Wilson na Anne imeandaliwa katika bustani ya kifahari

Maharusi waliowasisimua wengi baada ya kutumia Sh100 pekee za Kenya kugharimia harusi, wameandaliwa sherehe ya harusi ya kufana jijini Nairobi.

Sherehe hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya Eden Bliss, Nairobi ulimwengu ukiandhimisha Siku ya Wapendanao.

Harusi ya Anne na Wilson Mutura ya awali iligharimu dola moja pekee ya Kimarekani lakini sherehe ya sasa inakadiriwa kwamba imegharimu takriban Sh3.5 milioni (Dola 35,000).

Sherehe hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya kifahari ya Eden Bliss viungani mwa Nairobi

Waliofanya harusi ya shilingi 100 za Kenya wapata usaidizi‘Mapenzi yetu yalizidi yote’

Pesa hizo zimegharimiwa na makundi mbalimbali yanayohusika katika uandaaji wa sherehe, ambayo yaliungana kwa pamoja na kuchanga pesa kuandalia Anne na Wilson sherehe ya kukata na shoka.

Wawili hao, wanaoishi eneo la Kasarani, Nairobi, walisifiwa kwa kuonyesha thamani halisi ya mapenzi badala ya kuongozwa na pesa.

Kando na kuandaliwa harusi hiyo, wametunukiwa shamba la kilimo cha kisasa, fungate kwenye hoteli ya kifahari na baada ya sherehe ya leo wanatarajiwa kwenda kwa fungate nyingine mjini Dubai.

HakiAALTONEN JUMBAImageWawili hao wamesafirishwa kwa magari ya kifahariHakiNDUNGU NYORO / FACEBOOKImageBw Wilson akisaidiwa kuweka sawa koti lakeHakiNDUNGU NYORO / FACEBOOKImageBi Anne wakati wa sherehe ya harusi ya marudio

Dola yenyewe walioyotumia Anne na Wilson katika harusi yao waliitumia kununua pete mbili.

Walikuwa wameahirisha harusi yao mara tatu baada ya kukosa fedha za kutosha kuandaa sherehe kubwa ya harusi.

Maombi yao kwa familia na marafiki kuwafanyia mchango, hayakutimizwa.

Baada ya muda, Bwana harusi, Wilson, hakuwa na la kufanya ila kumshawishi mpenzi wake kuhusu uwezo wake.

Harusi za kifahari zapigwa marufuku Somalia

"Wilson aliponieleza hali yake, sikukataa. Mapenzi yetu yalizidi yote," Ann aliambia BBC.

Ingawa walikuwa na uwezo wa kuishi kwa mtindo wa 'come we stay' uliomaarufu kwa vijana wengine ambapo wapenzi wanaishi pamoja bila kuoana, Wawili hao walikwenda kwa askofu Jasper Owach kutoka Kanisa la Community Christian worship centre mjini Nairobi kurasmisha harusi yao.

"Mapenzi yetu yalidumu kwa muda na ili kujistiri kutoka maovu baada ya kupata baraka ya wazazi, tuliamua kufanya mambo yetu rasmi," anasema Wilson.

ImageWilson Muturi na mkewe Ann walitumia dola moja pekee wakati wa harusi yao

Siku yenyewe ilipofika, bwana Harusi, Wilson aliwashangaza waumini baada ya kukimbia nje sherehe ikiendelea.

"Alitoka ghafla kununua pete ya harusi nilipokuwa naendelea na shughuli ya kuwafunganisha," alisema askofu Jasper Owach, ambaye aliongoza hafla hiyo.

Zsa Zsa Gabor, mwigizaji aliyeolewa mara tisa

Wilson alirejea na walipokuwa wanatamka kauli za ndoa, Wilson alitoa pete hizo zilizofungwa kwa gazeti na wakavikana pete.

Wawili hao, wamewarai vijana kutozuiwa na uwezo wao wa kifedha na hivyo basi kuhalalisha mapenzi yao kupitia ndoa.

CHANZO NI BBC SWAHILI

Breaking news: Hali yazidi kuwa tete kwa YUSUPH MANJI akiwa bado Muhimbili ,Ofisi zake zakaguliwa na polis wa uhamia na kukutwa na jambo hili.

Image result for yusuph manji



Hali imezidi kuwa tete kwa mwenyekiti wa klabu ya Yanga YUSUPH MANJI baa da ya kuendelea kukumbwa na kadhia mbalimbali kipindi ikiwemo ya kutajwa katika orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya hapa nchini.
 Hali ya afya yake ilibadilika ghafla juzi wakati akiendelea na mahojiano na polisi kuhusu tuhuma zinazomkabili hali iliyopelekea kukimbizwa na gari la wagonjwa mpaka Taasisi ya Moyo Ya JAKAYA KIKWETE ndani ya Hospitali ya muhimbili.
Huku akiendelea na matibabu, Askali wa uhamiaji walifika katika ofisi zake na kufanya ukaguzi  na upekuzi na kukuta PASSPORT za raia wa kigeni 126 ambazo zinaonekena ni wafanya kazi wake ambao amewaajili bila kibali cha kuishi bila kibali kutoka idara  uhamiaji ambavyo ni kinyume cha sheria.
ZAIDI BOFYA VIDEO  HAPA CHINI 



UBUYU wa chini chini Joti amefunga ndoa !! ?? BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI !!

Nyepesi nyepesi zilizozagaa mtandaoni zikionyeza picha ya mchekeshaji JOTI jina halisi Lukas mhuvile ikimuonyesha akiwa ndani ya suti kali huku pembeni yake kukiwa na mwanamke aliyevalia gauni la harusi, Swali ni Je, Amefunga ndoa ya kimya kimya au ni kiki za msimu tu ???

TRUE STORY: INASIKITISHA SANA, USIPITWE NA MKASA HUU WA KUSISIMUA==AMENITENDA HIVI!!


Image result for KUTENDWA KATIKA MAPENZI

SOMA STORY FUPI YA MAPENZI YA KUHUZUNISHA YENYE MAFUNZO KWENU HASA HASA WAKINA DADA. NI STORY YA KWELI KABISA
"Nilipoingia katika mahusiano naye nilimuamini, nikampa kila kitu nilichoweza. Nakumbuka enzi zile 
nyumbani tulikuwa tuna ng’ombe, niliiba maziwa kila siku na kumpelekea kwao. Akanenepa!! Penzi letu 
likawa huru alipoanza maisha yake mwenyewe. Sikuwa najua lolote kuhusu mapenzi. Alinifundisha.

Nikaegemeza maisha yangu yote kwake. Akanifanya nikawa mtumwa wa ngono kila nikienda chumbani 
kwake. Kama haikutosha sasa akaanza kunifundisha kunywa pombe. Niliamini kuwa ndiye mume wangu 
mtarajiwa, kwa nini nikatae? Nilimkubalia kila kitu.

Alinilazimisha ngono hata nilipokuwa katika siku zangu. Kweli nilikuwa msomi na niliyajua madhara ya 
kufanya hivyo lakini sikutaka kumuudhi huyo niliyeamini kuwa ni mume wangu. Nilipenda tutumie kinga 
lakini aliipinga sana.
Nikapata mimba ya kwanza!! Hakuwa na pesa lakini alinilazimisha niitoe. Nikaiba pesa nyumbani 
nikafanyaalivyotaka. Kwa mara yakwanza nika toa mimba. Haikuniuma sana!! Niliamini kuwa ni yeye 
atakuja kunioa na atanifichia aibu hii.

Nilitegemea sasa tutaanza kutumia kinga. Lakini hapana haikuwa hivyo. Aliendelea kunilaghai. Tayari 
aliujua udhaifu wangu. Alinishika hapa na pale. Nikishtuka tayari amefanya anavyojua. Pombe kidogo 
na nyingine kidogo. Nikazoea lakini nikawa na wahi kulewa. Akautumia udhaifu huu kunifanyia jambo 
baya lililonifanya niandike haya kwako. Akaniingilia kinyume na maumbile. Alinilawiti!! Nilishindwa 
kumshtaki popote. Nikavumilia kwa kuwa alikuwa mume wangu mtarajiwa. Mume asiyejulikana hata kwa 
wazazi.

Mchezo ule ukaendelea. Akajitetea eti hataki nipate mimba tena, hivyo hiyo ni mbinu mbadala. Najuta 
kumuamini!! Lakini huyo alikuwa mume wangu. Miaka ikapita, ule urembo wangu niliozoea kuuona 
katika kioo ukatoweka, simu za mara kwa mara kutoka kwake zikatoweka, akawa mkali sana kwangu. 
Hakutaka niende kwake. Wakati huo nilikuwa nasoma chuo. Pesa ya mkopo ikitoka ananitafuta na 
tunakuwa marafiki tena. Anasema ananipenda na atanioa. Ananilewesha na kunitumia kinyume na 
maumbile. Pesa ikiisha na mapenzi yanaisha nabaki mwenyewe katika msoto.

Sasa akaanza kubadilisha wasichana waziwazi. Ningesema nini mimi? Ninajua alishindwa kusema neno 
moja tu. Tuachane!! Nilijuatayari ameniacha!!! Afya yangu ikadolola sana, nikalazimika kwenda kupima 
hospitali. Sikuwa na virusi. Nikapewa ushauri nikautumia.

Siku zikasonga nikampata mwanaume mwingine. Huyu alikuwa ananijali sana. Nikaanza kumsahau yule 
aliyenitenda. Nilipomaliza chuo akajitambulishanyumbani na alitaka kunioa. Akanioa kweli. Maisha 
yakaanza. Mwaka wa kwanza, mwaka wa pili na hadi wa tatu. Sikuwa nabeba mimba. Mume wangu 
alikuwa mvumilivu sana, hakuwahi kunilaumu. Lakini niliumizwa na mawifi. Nikaamua kwenda hospitali.

Nikaambiwa kizazi changu kiliharibiwa kwa kutoa mimba mara kwa mara. Pia mapenzi ya kinyume na 
maumbile yamenivuruga kabisa.Nililia sana huku nikimkumbuka yule aliyeuleta uchungu huu kwangu. 
Dunia haikuwa mahali pangu sahihi. Nimekuandikia baruahii mdogo wangu. Uisome mwenyewe!! Lakini 
uwasimulie wengi baada ya kifo changu.

Uwasimulie bila kuchoka wasichana wa kileo wanaodanganyikanakufanya mambo magumu 
kuwaridhisha wapenzi wao. Waambie watakufa kwa mateso kama mimi. Wasipokusikiliza usijisikie 
vibayamaana hata mimi nilikuwa siwasikilizi watu waliponambia lolote kuhusu yule mume mdanganyifu. 
Sitajiua lakini nitakufa kabla ya wakati!!!

Nimekuandikia wewe kwa kuwa u mwandishi. Japo kwa sasa u mtoto mdogo najua utaipata nafasi siku
moja ya kuwafikishia wasichana hawa. Usilie kwa sababu nitakufa. Lia kwasababu mwanaume 
mwenzako
AMENITENDA HIVI!!!
LIKE & SHARE



Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa

Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover likifuata kwa nyuma.
Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za mgonjwa.
Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 14.

Bwakila atoa list mpya ya watumia unga



MR.Kamwene___VALENTINE DAY


 

Gallery

Popular Posts

About Us