KINGAZI BLOG: 05/20/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 20 May 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA WA WATANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA WA WATANZANIA

RAISI WA SERIKALI YA WANAFUNZI ST. JOSEPH AFUKUZWA CHUO KWA KUTETEA HAKI ZA WANAFUNZI WENZAKE

Katika hali ya kusikitisha sana na yenye kuumiza moyo kijana Bachubila Haruna ambae ni Raisi wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Cha Mtakatifu Yosefu kampasi ya luguruni amejikuta akipoteza haki yake ya msingi ya kupata elimu katika taifa lake kwasababu ya kutete haki za wanafunzi wenzake.

Mnamo Tarehe 27/03/2017 Raisi Bachubila aliandika barua kwenda Wizara ya Elimu na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) akiomba mrejesho wa serikali kutokana na maagizo aliyoyatoa Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako (mb) kwa uongozi wa chuo na Tume ya Vyuo Vikuu kuhakikisha Elimu na Mazingira ya kusomea Chuoni hapo yanaridhisha wakati wa mgomo wa wanafunzi uliofanyika mapema mwaka jana 2015. Pia Raisi Bachubila alitoa malalamiko ya matatizo mbalimbali na kuomba msaada kutoka ngazi hizo za juu.

Baada ya kuandika Barua hiyo taarifa kupitia mawakala wa Chuo walioko TCU ziliwafikia wahindi ambao ndio wamiliki wa chuo hiko na kwa hali ya kushtukiza walimuandikia Raisi Bachubila barua wakimlaumu kwa kuwasiliana na wizara bila kuwapa taarifa wao, kukichafua chuo nje na kuandika taarifa za uongo.

Baada ya hapo ukapita mda kidogo na kilikuja kukaliwa kikao cha inquiry committee( kamati ya nidhamu ya chuo) kumjadili na kumhoji Raisi Bachubila mnamo tarehe 02/05/2017. Kikao hiko kikatoka na maazimo ya kuishauri seneti ya chuo kupitisha maamuzi ya kumsimamisha chuo mwaka mmoja Raisi Bachubila.

Wakati maamuzi ya seneti yanasubiriwa kukawa kunatokea vuta ni kuvute baina ya wanafunzi na uongozi wa chuo wakitaka kujua nini hatma ya Raisi wao. Wakati huo huo Uongozi wa Chuo kipitia Dean of Students ukawa unamuita Raisi Bachubila ukimlazimisha aandike barua ya kukana barua alioandika kwenda wizarani na ajiuzulu nafasi yake.

Bachubila alikataa kufanya hivo na kubaki na msimamo wake wa kua mtetezi wa wanafunzi wenzake.

Kwa bahati nzuri sana tarehe 16/05/2017 Raisi Bachubila alipokea barua kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kupitia Katibu mkuu Wizara ya Elimu ikimjibu Raisi Bachubila kua imepokea na ikaipa maagizo Tume ya Vyuo Vikuu kufuatilia malalamiko hayo. Katika hali isiyo ya kawaida Raisi alishangazwa kupokea barua yake ikiwa tayari imeshafunguliwa na inaonyesha kucheleweshwa kupewa maana barua hiyo Ofisi ya Waziri Mkuu iliijibu tarehe 08/05/2017.

Baada ya barua hiyo kuja siku iliyofuata tarehe 17/05/2017 Chuo kilimuandikia Rasmi Raisi Bachubila kua kimemfukuza chuo kupitia Principal wa chuo.

Wanafunzi wengi hatujafurahishwa na hatua hii na tunaipinga vikali. Kwani ni uonevu wa wazi kwa mtetezi wetu. Msimamo wake juu ya maslahi yetu ya Elimu ndio umesababisha leo hii amefukuzwa chuo. Hivo sisi kama wanafunzi tuko tayari kufanya lolote hata kama ni kuacha shughuli za kitaaluma mpaka pale mwenzetu, kaka yetu na kiongozi huyu atakapo rudishwa masomoni kwa nafasi yake ile ile ya Uraisi.

Mbali na hapo serikali iyopita ya wanafunzi ilikua ikiwasiliana na wizara na TCU hadi kufanikiwa kumleta Waziri wa Elimu Profesa Ndalichako hapa chuoni ila hata siku moja haikuwahi kukipa chuo Taarifa yoyote na hamna kiongozi yoyote wa serikali zilizopita aliewahi kufukuzwa chuo kwasababu ya kudai haki katika mamlaka husika.

Ni ukweli kusema kwamba Chuo hiki cha St. Joseph ndugu watanzania wenzetu kimegubikwa na uchafu na wizi mkubwa wa kitaaluma na fedha za watanzania. Hapa chuoni tunalipa ada kubwa TSH 3000000/= na tunalazmishwa kuilipa yote kwa mkupuo lakini cha kushangaza katika idara mbalimbali wameajiri walimu wakihindi ambao hata elimu ya kuweza kufundisha Chuo Kikuu hawana ila tunalazmishiwa hivo hivo wakati hata lugha ya kufundishia ambayo ni kingereza hawajui.

Chuoni kwetu mitihani imekua ikisahishwa ovyo ili kuwapa wanafunzi Suplementary nyingi. Hatukatai kua hata katika vyuo vingine vya uhandisi Supp hutolewa kwa wingi ila tofauti ni kua wenzetu hao hua hawalipii Supp ila sisi tunalipia Supp shilingi 10000/= kwa somo moja. Hivo uongozi wa chuo umefanya kama mtaji wa kupata kipato cha ghafla.

Ikumbukwe kua Chuo hiki kilinyimwa intake ya wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza mwaka uliopita huku wizara ikikipa mda wa kujifanyia marekebisho ili kipate intake mwaka huu, ila cha kushangaza chuo kimeendelea na utaratibu mbovu usiokidhi.

Tunawaomba watanzania kwa ujumla, Viongozi wa nchi na Wizara pamoja na TCU waliangalie hili kwa jicho la tatu maana kama chuo hiki kitaendelea kutoa wahandisi feki basi ni hatari mno kwa maendekeo ya taifa letu.

Tunawaomba wadau mbalimbali wa Elimu nchini na wapenda haki kuingilia kati swala hili maana sisi wanafunzi na uongozi wa chuo inaonekana hatuwezi kufikia muafaka bora. Wanahabari mtusaidie kutangaza hili ili jamii ijue kiundani kinachoendelea St. Joseph.

Tchaooo
IMG-20170520-WA0013.jpg

BREAKING NEWS : PICHA Kikosi Maalumu cha Makomando US, waanza mazoezi ya Kuvamia na Kuharibu Silaha za Maangamizi NK

[​IMG]
[​IMG]
[​IMG]
[​IMG]
Makomando wa kimarekani Wamemaliza DRILL ya Zoezi maalumu liitwalo "Warrior Strike 7" huko South Korea katika mji wa uijeongbu kambini kwao Stanley.....

Zoezi hilo limehushisha meli za kivita za korea kusini, na mazoezi ya kupambana ufukweni.
REjereo
RT


My take
Wakuu, tusiilaumu US, kwa wanachokifanya duniani. Tukumbuke kabla ya WW2. Wamarekani walijitenga na mambo ya kidunia na kufanya yao. Sasa ni dunia ndio iliyoiita na kuishinikiza ijiingize kwenye mambo ya kidunia wakiaza na WW2. Kuna haja ya kuwaacha waendelee na yao kwa faida ya Taifa lao.

SOURCE
JAMII FORUMS 

BASHITE Avutiwa Pumzi...Hbari Vichwa vya Magazeti y Leo Jumamosi 20/5/2017.



UTATA Waibuka Wakili Aliyefia Sebuleni Dar..Maiti Yake Yakutwa na Damu Kichwani.


WAKILI wa kujitegemea, Noel Ndalu, amekutwa amefariki sebuleni nyumbani kwake Sinza jijini Dar es salaam, kifo ambacho kimeacha maswali kadhaa kutokana na mazingira yake.

Jana, Nipashe ilifika nyumbani kwa wakili huyo aliyekuwa akiishi Sinza kwa Remmy wilayani Kinondoni na kupata simulizi zenye kuibua maswali juu ya kifo hicho.

Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na sababu za kifo chake kilichoonekena kuwa cha ghafla, hasa kwa kutambua kuwa kazi zake huhusisha kesi zitokanazo na masuala mbalimbali ya migogoro ya kisheria wanayokumbana nayo wateja wake.

“Inasikitisha sana…kifo chake ni cha ghafla na kwakweli hatujui ni kitu gani kimemkuta…labda alikuwa akisumbuliwa na maradhi kama ya kifafa ambayo wakati mwingine huwafanya watu wanaoishi peke yao wapoteze maisha kwa namna hii. Hakuna anayejua kwakweli,” mmoja wa majirani aliiambia Nipashe kuhusiana na taarifa za kifo cha wakili huyo.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda, hakuweza kuzungumzia tukio hilo jana baada ya kueleza kuwa ametingwa na kikao, lakini baadhi ya majirani wameeleza kushangazwa na kile kilichomtokea mwenzao huyo.

Akizungumza na Nipashe, mama mwenye nyumba aliyokuwa amepanga wakili huyo, iliyopo katika Mtaa wa Mtendaji, Salama Shaaban (50), alisema Wakili Noel alikutwa amefariki sebuleni kwake juzi majira ya saa 4:00 asubuhi.

Alisema mara ya mwisho kuonana na mpangaji wake huyo ilikuwa ni Jumanne, saa 12:00 jioni wakati wakili huyo akimkabidhi stakabadhi ya uniti za umeme wa Luku aliokuwa amenunua.

“Jumanne alikuja hapa akaniambia mama nimekuletea umeme, nikamwambia ahsante mwanangu na alikuwa ni mzima wa afya...na tangu siku hiyo nikawa sijamuona kwa sababu anaishi upande wa pili wa nyumba yangu na ana geti lake,” alisema Salama.

Alieleza kuwa, hawakuwa na kawaida ya kuonana mara kwa mara na ndiyo sababu hakushtuka kutomuona kwa siku zote hizo.

“Hapa wako wapangaji wawili, marehemu na mwingine. Sasa jana asubuhi, nikiwa ndani kwangu, alikuja mpangaji mwenzake, akaniambia mama simu inaita muda mrefu ndani kwa Noel na hakuna anayepokea na yeye hajamuona akitoka,” alisema.

Alisema baada ya kupewa taarifa hizo, alitoka yeye na kijana wake kwenda hadi kwenye mlango mkubwa wa wakili Noel na kuanza kugonga. Walifanya hivyo kwa muda mrefu bila majibu na ndipo nao wakingiwa na wasiwasi.

“Chini ya mlango kuna uwazi hivyo mwanangu aliamua kuchungulia, akaniambia mama sioni kitu lakini nasikia harufu ya kitu kilichooza inatoka ndani,” alisema Salama.

Alisema mtoto wake huyo alichukua fimbo ndefu na kuipitisha chini ya mlango ambao upo karibu na dirisha kwa ajili ya kusukuma pazia ili waweze kuchungulia dirishani.

“Tulifanikiwa kusogeza pazia na tukachungulia ndani… tukamuona Noel akiwa amelala chali chini ya sakafu kuelekea mlango wa chumbani na kwenye paji lake la uso kulikuwa na damu zimechuruzikia kwa chini,” alisema.

Alisema baada ya kuona hali hiyo, waliamua kwenda kuwaita wajumbe wa mtaa wao ambao walifika na kushuhudia tukio lile kabla ya kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mabatini.

“Baadaye Polisi walikuja na gari. Waliamuru mlango uvunjwe, wakaingia ndani na kuuchunguza mwili. Wakakuta amechanika kwenye paji la uso wake,” alisimulia Mama Salama.

Alisema pia alikutwa amevaa kaptura na hawakukuta silaha ya aina yoyote. Baada ya hapo polisi waliuchukua mwili huo na kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Mwananyala.

Akisimulia namna anavyomfahamu, Salama alisema wakili huyo binafsi ambaye alikuwa na ofisi yake Temeke jijini Dar es Salaam, ameishi kwenye nyumba yake kwa miaka mitatu.

Alisema awali alikuwa akiishi na mwanamke ambaye aliondoka miaka miwili iliyopita, na hivyo hadi umauti ukimkuta alikuwa akiishi peke yake.

“Mke wake aliondoka na mtoto wa miezi miwili. Kwa hiyo alikuwa akiishi peke yake,” alisema Salama.

Alisema baada ya kifo hicho, mjomba wake alifungasha mali za wakili huyo na kuondoka nazo na kwamba jana, waliuaga mwili wake katika Hospitali ya Mwananyamala na kusafirisha kwenda Dodoma kwa maziko.

“Baba yake anaishi Dodoma hivyo leo (jana) walienda Mwananyamala saa 4:00 kwa ajili ya kuuchukua mwili kuusafirisha,” alisema.

MAWAKILI WAMLILIA

Aidha, Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLC), kilitoa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mwanachama wao mwenye namba ya usajili 4644, Noel Ndalu .

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TLC kwa wanachama wake, ilieleza kuwa, mwanachama huyo alifariki Jumanne ya wiki hii, Mei 16 na kwamba aliagwa jana katika Kanisa la Kaloloni Chang’ombe na baadae kusafirishwa kuelekea mkoani Dodoma kwa maziko

POLISI Waua Majambazi Matatu Katika Vita ya Majibizano ya Risasi Iliyoshangaza Watu Mwanza..!!

WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuawa kwa risasi jijini Mwanza jana katika kile kinachoelezwa kuwa ni matokeo ya vita kali ya kurushiana risasi baina ya watuhumiwa hao na askari wa Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema tukio hilo limetokea katika eneo la viwanja vya ST. Mary’s Mtaa wa Ndofe wilaya ya Nyamagana, ambako polisi walikuwa wameweka mtego baada ya kupata taarifa kuwa watuhumiwa walipanga kufanya uhalifu.

Ilielezwa zaidi kuwa polisi waliwafikia watuhumiwa baada ya kumkamata mganga wa kienyeji aitwaye Ayubu Nyamweru (45), mkazi wa Katoro mkoani Geita, ambaye alikutwa akiwa na kompyuta mpakato tatu na simu moja aina ya Sumsung vilivyokuwa imeibwa katika tukio la kuvunja nyumba maeneo ya Nyamanoro.

Tukio la kuporwa kwa vitu hivyo lilihusisha pia kuporwa kwa bastola aina ya Duty CZ 75P-07 na fedha, siku ya Mei 13 mwaka huu na kufunguliwa jalada lenye namba NY/IR/3773/2017.


Ilielezwa na polisi kuwa baada ya mganga Nyamweru kuhojiwa, alitaja wenzake anaoshirikiana nao katika kufanya matukio mbalimbali ya uvunjaji na unyanga’anyi jijini Mwanza na maeneo ya jirani.

Ilielezwa kuwa kufuatia maelezo ya mganga huyo, ndipo polisi walipofuatilia na kumkamata mtuhumiwa mwingine (Benedicto Thobias) kabla ya kuweka mtego uliosababisha kutokea kwa majibizano ya risasi baina yao na majambazi hao.

Akizungumza jana, Kamanda Msangi aliwataja watuhumiwa wlaiofariki kwa kupigwa risasi katika mapambano hayo kuwa ni Benedicto Thobias ambaye ni mkazi wa Nyamatara Buhongwa na wengine waishio pia Mwanza ni Mabula Segeja na Charles Thomas.

 “Mnamo Mei 19 mwaka huu, katika viwanja vya ST. Mary’s mtaa wa Ndofe wilaya ya Nyamagana walifika watu watano ambao walikuwa ni wenzake na mtuhumiwa Benedicto. Askari walipowaamuru wajisalimishe walikaidi amri hiyo na kuanza kufyatua risasi uelekeo wa askari,” alisema Msangi na kuongeza:

“Ndipo askari wakajibu mapigo na kuwajeruhi majambazi wawili na zile risasi walizozipiga ziliweza kumjeruhi mwenzao (Benedicto) aliyekuwa amewapeleka askari kwenye eneo lile… wote watatu walifariki dunia wakati wanapelekwa hospitali kwa matibabu.”

Aidha, Kamanda Msangi alisema kuwa katika tukio hilo, polisi walifanikiwa kukamata silaha mbili ambazo ni bastola aina ya Duty CZ 75P -07 yenye namba B.512637 ikiwa na risasi 15 na magazini mbili na short gun iliyofutika namba ikiwa na risasi mbili na maganda mawili ya risasi, mali ya Suleimani Waziri aliyekuwa akiimiliki kihalali.

Kwa mujibu wa Kamanda Msangi, miili ya watuhumiwa hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi zaidi wakati msako wa kuwasaka wenzao waliotoroka na wengine waliokuwa wakishirikiana nao bado ukiendelea.

Credit - Nipashe

UTATA Waibuka Wakili Aliyefia Sebuleni Dar..Maiti Yake Yakutwa na Damu Kichwani.


WAKILI wa kujitegemea, Noel Ndalu, amekutwa amefariki sebuleni nyumbani kwake Sinza jijini Dar es salaam, kifo ambacho kimeacha maswali kadhaa kutokana na mazingira yake.

Jana, Nipashe ilifika nyumbani kwa wakili huyo aliyekuwa akiishi Sinza kwa Remmy wilayani Kinondoni na kupata simulizi zenye kuibua maswali juu ya kifo hicho.

Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na sababu za kifo chake kilichoonekena kuwa cha ghafla, hasa kwa kutambua kuwa kazi zake huhusisha kesi zitokanazo na masuala mbalimbali ya migogoro ya kisheria wanayokumbana nayo wateja wake.

“Inasikitisha sana…kifo chake ni cha ghafla na kwakweli hatujui ni kitu gani kimemkuta…labda alikuwa akisumbuliwa na maradhi kama ya kifafa ambayo wakati mwingine huwafanya watu wanaoishi peke yao wapoteze maisha kwa namna hii. Hakuna anayejua kwakweli,” mmoja wa majirani aliiambia Nipashe kuhusiana na taarifa za kifo cha wakili huyo.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda, hakuweza kuzungumzia tukio hilo jana baada ya kueleza kuwa ametingwa na kikao, lakini baadhi ya majirani wameeleza kushangazwa na kile kilichomtokea mwenzao huyo.

Akizungumza na Nipashe, mama mwenye nyumba aliyokuwa amepanga wakili huyo, iliyopo katika Mtaa wa Mtendaji, Salama Shaaban (50), alisema Wakili Noel alikutwa amefariki sebuleni kwake juzi majira ya saa 4:00 asubuhi.

Alisema mara ya mwisho kuonana na mpangaji wake huyo ilikuwa ni Jumanne, saa 12:00 jioni wakati wakili huyo akimkabidhi stakabadhi ya uniti za umeme wa Luku aliokuwa amenunua.

“Jumanne alikuja hapa akaniambia mama nimekuletea umeme, nikamwambia ahsante mwanangu na alikuwa ni mzima wa afya...na tangu siku hiyo nikawa sijamuona kwa sababu anaishi upande wa pili wa nyumba yangu na ana geti lake,” alisema Salama.

Alieleza kuwa, hawakuwa na kawaida ya kuonana mara kwa mara na ndiyo sababu hakushtuka kutomuona kwa siku zote hizo.

“Hapa wako wapangaji wawili, marehemu na mwingine. Sasa jana asubuhi, nikiwa ndani kwangu, alikuja mpangaji mwenzake, akaniambia mama simu inaita muda mrefu ndani kwa Noel na hakuna anayepokea na yeye hajamuona akitoka,” alisema.

Alisema baada ya kupewa taarifa hizo, alitoka yeye na kijana wake kwenda hadi kwenye mlango mkubwa wa wakili Noel na kuanza kugonga. Walifanya hivyo kwa muda mrefu bila majibu na ndipo nao wakingiwa na wasiwasi.

“Chini ya mlango kuna uwazi hivyo mwanangu aliamua kuchungulia, akaniambia mama sioni kitu lakini nasikia harufu ya kitu kilichooza inatoka ndani,” alisema Salama.

Alisema mtoto wake huyo alichukua fimbo ndefu na kuipitisha chini ya mlango ambao upo karibu na dirisha kwa ajili ya kusukuma pazia ili waweze kuchungulia dirishani.

“Tulifanikiwa kusogeza pazia na tukachungulia ndani… tukamuona Noel akiwa amelala chali chini ya sakafu kuelekea mlango wa chumbani na kwenye paji lake la uso kulikuwa na damu zimechuruzikia kwa chini,” alisema.

Alisema baada ya kuona hali hiyo, waliamua kwenda kuwaita wajumbe wa mtaa wao ambao walifika na kushuhudia tukio lile kabla ya kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mabatini.

“Baadaye Polisi walikuja na gari. Waliamuru mlango uvunjwe, wakaingia ndani na kuuchunguza mwili. Wakakuta amechanika kwenye paji la uso wake,” alisimulia Mama Salama.

Alisema pia alikutwa amevaa kaptura na hawakukuta silaha ya aina yoyote. Baada ya hapo polisi waliuchukua mwili huo na kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Mwananyala.

Akisimulia namna anavyomfahamu, Salama alisema wakili huyo binafsi ambaye alikuwa na ofisi yake Temeke jijini Dar es Salaam, ameishi kwenye nyumba yake kwa miaka mitatu.

Alisema awali alikuwa akiishi na mwanamke ambaye aliondoka miaka miwili iliyopita, na hivyo hadi umauti ukimkuta alikuwa akiishi peke yake.

“Mke wake aliondoka na mtoto wa miezi miwili. Kwa hiyo alikuwa akiishi peke yake,” alisema Salama.

Alisema baada ya kifo hicho, mjomba wake alifungasha mali za wakili huyo na kuondoka nazo na kwamba jana, waliuaga mwili wake katika Hospitali ya Mwananyamala na kusafirisha kwenda Dodoma kwa maziko.

“Baba yake anaishi Dodoma hivyo leo (jana) walienda Mwananyamala saa 4:00 kwa ajili ya kuuchukua mwili kuusafirisha,” alisema.

MAWAKILI WAMLILIA

Aidha, Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLC), kilitoa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mwanachama wao mwenye namba ya usajili 4644, Noel Ndalu .

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TLC kwa wanachama wake, ilieleza kuwa, mwanachama huyo alifariki Jumanne ya wiki hii, Mei 16 na kwamba aliagwa jana katika Kanisa la Kaloloni Chang’ombe na baadae kusafirishwa kuelekea mkoani Dodoma kwa maziko

 

Gallery

Popular Posts

About Us