CHOMBEZO - KIDUKU CHA MGUU MMOJA | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 25 February 2017

CHOMBEZO - KIDUKU CHA MGUU MMOJA

Image result for masogange agnes

>>>>> BOFYA HAPO KUONA KIONJO CHA VIDEO HII 18+ onl

“Mambo vipi kaka Eddy mzima wewe, samahani kaka sijui unakumbuka ulichoniahidi???…..najua haukumbuki lakini mimi nitakukumbusha ni kuhusu kunifundisha kucheza mziki” aliongea maneno hayo mwanadada Yasmin kupitia simu ya mkononi akimwambia Eddy, ambaye ndio kwanza alikuwa ametoka usingizini.
Eddy kwa hali ya kawaida alikuwa amesahau kabisa kuwa aliwahi kumuahidi mwanadada Yasmin kuwa atamfundisha kucheza mziki katika staili tofauti tofauti. Hiyo ilikuwa baada ya Yasmin kumwambia kuwa anatamani sana siku moja aweze kucheza mziki
“Aaah!!! Ok! Nimekumbuka sasa tufanye lini na wapi?? Samahani jamani” aliuliza Eddy huku akiomba radhi
“Mama amesafiri kaenda Pemba kumpeleka mdogo wangu kutembea kwa bibi yaani nimebaki peke yangu hapa nyumbani kwa hiyo sitaweza kutoka hapa labda uje wewe jamani samahani eeh!!” alijibu kwa sauti nyembamba ya kike mwanadada huyu.
Jibu hilo lilimtia Eddy nguvu sana na kumfungua akili yake. “Mama hayupo na baba hayupo kifuatacho???” alijisemea kimoyo moyo huku akiyakariri maneno ya Yasmin. 
“Basi nitakuja, ulisema unataka staili gani vile nimesahau maana na wewe unapenda staili nyingi sana”
“Mdogo wangu ananicheka eti sijui kucheza kiduku na mimi nataka nijue halafu na kucheza mapanga yale ya TMK ya Wanaume Family….” Alijibu Yasmin huku sauti yake ikimuumbua kuwa alikuwa na aibu
“Ah!! Mapanga ya kizamani hayo nitakufundisha kiduku sawa dada….”
“Yaani nitafurahi kweli kikitoka huko Pemba nitakiringishia kweli” alijibu tena kwa furaha binti huyu kutoka familia bora sana aliyekuwa anaishi maeneo ya “masikini hajengi” ya Kidichi Spice mjini  Zanzibar.
“Kwa hiyo lini nije” aliuliza Eddy
“Siku yoyote saa yoyote unayotaka chamsingi mimi nijue kucheza kiduku, si nitajua upesi eeh!!….”
Baada ya maongezi marefu na kufikia muafaka wa lini waonane Eddy alikata simu na baada ya muda akaongezewa muda wa maongezi wenye thamani ya shilingi elfu moja kutoka kwa Yasmin. Pale pale Eddy akajiunga huduma maarufu ya vijana wasiokuwa na pesa za kupiga simu yaani “Epic Nation ya Tsh 500/=” pale akawa ameunganishwa moja kwa moja na huduma ile ambapo alijinyakulia sms 300 na dakika 15 za Zantel kwenda Zantel, na kuanza kuchat na Yasmin.
Eddy: hivi Yasmin utaweza kucheza kiduku kweli
Yasmin: ntaweza kwani wanaoweza wana nini?? Kwani  ni kigumu sana eenh??
Eddy: Unajua staili ngapi za viduku?? Eddy akawa ameanza ualimu wake
Yasmin: Mi huwa nasikia kiduku kujiremba, kiduku mcharuko, kiduku cha kukuna nazi na cha kuendesha mtumbwi
Eddy: mh!! Hayo maviduku ya zamani kweli mimi nitakufundisha mpya kabisa hata watu hawaijui
Yasmin: Kinaitwaje hicho jamani yaani natamani hata ungekuja leo ili nijifunze upesi kabla dogo halijarudi.
Eddy: kinaitwa ‘kiduku cha mguu mmoja’ mdogo wako anakiweza hicho!!!
Yasmin:mh! Sijawahi kumsikia akisema hakiwezi hicho labda ndo maana hasemi, anavyopenda sifa angekuwa keshanambia
Eddy: sasa nitakuja leo jioni kukufundisha sawa?
Yasmin: usiache Eddy
Akili ya Eddy ilijizungusha haraka haraka na kuamini huu ulikuwa muda muafaka wa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na Yasmin kwa kutumia fursa hii ya kumfundisha kucheza kiduku.
Ni siku nyingi sana alikuwa anajaribu kumjengea mazingira ya kimapenzi lakini hata hisia za Yasmin hazikuonekana wazi kwake na yeye Eddy alishindwa kumtamkia.

Majira ya saa kumi na mbili jioni Eddy mtoto wa Mboriborini uswahilini alikuwa akipata juisi baridi ya embe katika sebule pana iliyopulizwa na kiyoyozi wakati wote, Yasmin alikuwa amevalia pensi iliyokuwa imembana na ilionekana dhahiri hakuwa na hakuwa na kitu chochote ndani.
Mate ya uchu yalimjaa mdomoni Eddy na kwa jicho la wizi wizi aliweza kuchungulia cheni iliyong’ara kutokea kiunoni mwa Yasmin. Maungo yake yakamsisimka!!!
“Yasmin usiku unaingia, nenda ukavae nguo za kuchezea Kiduku cha mguu mmoja” Eddy alimwambia.
“Ndio zikoje hizo mwalimu wangu unadhani mimi nazijua basi…..” alijibu Yasmin huku akimkata jicho la mahaba Eddy. Eddy nae  akakwepesha macho!!!
“Kavae kanga na kitop nadhani hapo itakuwa sawa” alijibu huku akiona haya kidogo kwa jambo alilotamka.
“Haya Mwalimu wangu…..” alijibu huku akiondoka
“pia usisahau kuweka hii Cd wimbo namba tatu…” alisisitiza Eddy.
Baada ya dakika kumi Yasmin alirejea, kama Eddy alivyoagiza Yasmin alikuwa amevaa kanga moja pekee na kitop kilichoachia kitovu chake nje kidogo.
Kwa mwendo wa kunyata aliisogelea redio na kuweka ile Cd kisha akachagua wimbo namba tatu, ulikuwa wimbo wa taarabu uitwao ‘mama nipe radhi’. Eddy aliangalia kwa wiziwizi upande wa nyuma wa Yasmin akatamani kumrukia, kwa kitendo cha haraka haraka bila Yasmin kugundua Eddy alitumbukiza mkono wake katika suruali yake akaweka mambo sawa asije kuaibika!!
Eddy akamsogelea Yasmin pale alipokuwa na kuizungusha mikono yake katika kifua cha Yasmin.
“Sasa inatubidi tuanzie kiduku cha kawaida halafu cha mcharuko kisha tutamalizia kiduku cha mguu mmoja. Yasmin hakuwa na pingamizi lolote alikubali kila kitu alikuwa na hamu kubwa ya kujua kucheza kiduku!!!, mikono ya Eddy ilivyogusa kifua cha vuguvugu cha Yasmin alihisi kuishiwa pumzi zake, alijaribu kufundisha lakini somo lilikuwa haliendi, kwa ujasiri mkubwa alipandisha mikono yake katika chuchu ndogo za Yasmin na ni wakati huo huo ulikuwa umemalizika wimbo wa Mama nipe radhi na kuingia wimbo wa marehemu Nasma Khamis Kidogo uitwao
‘SABALKHERI’ (wale wapenzi wa muziki wanautambua wimbo huu wa chombezo) Katika taarabu za asili ni wimbo huo uliomkosha sana Eddy na alikuwa amekariri mashairi yaliyokuwa yakiimbwa na mwanaume hivyo alishindwa kujizuia kuigiza sauti ile na bila kutegemea alishangaa mashairi ya Nasma Khamis Kidogo yakijibiwa kiustadi kabisa na Yasmin ambae wakati huo pumzi zake zilipishana kwa kasi tofauti na mwanzo
Eddy: Sabalkheri mpenzi waonaje hali yako
Yasmin: albanur azizi hali yangu kama yako
Eddy: wawaonaje wazazi nyumbani utokeapo
Yasmin: kawanusuru mwenyezi hali hofu yao juu yako,hebu nitoe majonzi unijuze shida yako.
Eddy:Shida yangu sijiwezi,dawa yangu sura yako.
 Mwingine we achomozi nakupenda peke yako
Yasmin:Daima nitakuenzi silitupi pendo lako
Yasmin: usiingie simanzi sura yangu mali yako
Eddy: nakuikosa siwezi sikia langu tamko
Yasmin: mwingine we hachomozi nakupenda peke yako
Eddy: nimefanya uchunguzi nakiri maneno yako, Naiona waziwazi ishara ya pendo lako.
Yasmin: milele nitakuenzi natoa ahadi kwako………
Eddy: kibaya sikivumbuwi ndani ya maungo yako
Yasmin: na mimi simtambui mwenye sifa kama zako……………..wallah sijitambui mgonjwa kwa raha zako
Waliendelea kujibishana maneno yale kwa sauti za chini wakati huo kanga ikiwa tayari imeanguka chini na Eddy akihesabu idadi ya cheni alizokuwa amevaa mwanadada Yasmin zilikuwa nne na shanga tatu!!!!, mwanga wa taa nyekundu pale ndani uliwapa hamasa zaidi hadi wakajikuta wote wapo uchi wa mnyama pale pale sakafuni wakati huo ukilindima wimbo wa mwanamziki  aliyejizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania Ommy Dimpoz uitwao “Baadae” tayari Eddy alikuwa juu ya kifua cha Yasmin na kilichokuwa kinaendelea pale ni “KIDUKU CHA MGUU MMOJA”, wakati miguu miwili ikiwa imetulia tuli mguu mmoja uliosalia ulikuwa bize ukicheza kiduku.
“Kumbe unakiweza kiduku dah!!!” Eddy alimsifu Yasmin aliyekuwa anaona haya wakati akivaa nguo zake

“Kumbe hicho ndo kiduku cha mguu mmoja?????” alihoji Yasmin, Eddy hakumjibu bali aliachia tabasamu tu!!!!!

Kiduku cha mguu mmoja kikawa kimechezwa katika mazingira ya ajabu.


Swali likabaki kwa Yasmin je atajisifia kwa mdogo wake kuwa anaweza kucheza Kiduku cha MGUU MMOJA????.





google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us