Waliotimuliwa Udom wakibeba chuo Moro | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 10 October 2016

Waliotimuliwa Udom wakibeba chuo Moro

Morogoro. Baada ya kukaa miaka zaidi ya 50 bila ukarabati, hatimaye Chuo cha Ualimu Morogoro kimeanza kukarabatiwa ili kipokee wanafunzi 1,138 walioondolea Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Ukarabati huo unaofanywa chini ya ufadhili wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi utagharimu Sh700 milioni.

Mkuu wa chuo hicho, Augustine Sahili amesema huo ni mpango wa Serikali unaohusisha vyuo vyote vya ualimu ambavyo vitapokea wanafunzi walioondolewa Udom kutokana na kutokuwa na sifa za kujiunga na chuo kikuu.

Amesema ukarabati huo utakaomalizika mwezi huu unahusisha mabweni, madarasa na mfumo wa majitaka.

Pia, ameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kukarabati chuo hicho kwani tangu kilipoanzishwa mwaka 1926 hakijawahi kufanyiwa ukarabati mkubwa.

Mwalimu Anna Mushi aliyehitimu chuoni hapo, amesema majengo mengi na miundombinu vilikuwa chakavu.

“Vyuo vingi vya ualimu vya Serikali vilianza kabla ya Uhuru, hivyo vinahitaji ukarabati ili viendelee kuwa katika hali nzuri,” amesema mwalimu huyo.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us