Makonda kupandishwa kizimbani Kisutu leo | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 9 November 2016

Makonda kupandishwa kizimbani Kisutu leo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda

Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo atapanda kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujitetea dhidi ya kesi ya madai ya Sh200 milioni  iliyofunguliwa na waliokuwa makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mgana Msindai na John Guninita.

Makonda anayetetewa na wakili wa kujitegemea, Seneni Mponda atatoa utetezi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Kwa upande wa Msindai na Guninita wao wanatetewa na mawakili kutoka kampuni ya Uwakili ya BM, Benjamin Mwakagamba na Ester Shedrack.

Katika kesi hiyo ya madai namba 68 ya mwaka 2015, Msindai na Guninita kupitia wakili wao, Mwakagamba, walifungua kesi wakiiomba Mahakama hiyo ya Kisutu kumuamuru Makonda awaombe msamaha na kumlipa kila mmoja wao kiasi cha Sh100 milioni.

Wanadai kiwango hicho cha fedha kutokana na maneno ya kuwadhalilisha yaliyotolewa na Makonda wakati akiwa  Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), alipoitisha mkutano na waandishi wa habari.

Walalamikaji hao pamoja na hayo, wanaiomba Mahakama hiyo itoe zuio  la kudumu kwa Makonda  asizungumze  tena maneno ya kashfa dhidi yao wala kuyasambaza kama alivyofanya awali.

Pia, wanaomba Makonda kulipa riba na gharama za kesi.

Walidai kuwa Makonda  wakati akiwa katibu uhamasishaji chipukizi wa CCM,  katika mkutano wake alitoa maneno akidai kuwa Msindai na Guninita ni vibaraka wanaotumiwa kuharibu chama cha CCM kwa nguvu ya fedha.

Msindai na Guninita wanadai maneno hayo yaliyotolewa na Makonda  yamewadhalilisha kwa jamii na kuwafanya waonekane kuwa ni watu wasiofaa kuwa viongozi.

Source: Mwananchi

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us