PICHA RAIS OBAMA ALIPOKUTANA NA DONALD TRUMP IKULU KWA MARA YA KWANZA | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 11 November 2016

PICHA RAIS OBAMA ALIPOKUTANA NA DONALD TRUMP IKULU KWA MARA YA KWANZA

Rais wa Marekani, Barack Obama leo amekutana na Rais Mteule wa nchi hiyo, Donald Trump ambapo wamefanya mazungumzo baina yao wawili kuhusu mambo mbalimbali ya nchi hiyo na baada ya hapo kuzungumza na waandishi wa habari waliokuwa wamejitokeza kwa wingi katika Ikulu ya Marekani ‘White House.’Trump na Mkewe waliwasili katika Ikulu ya Marekani saa nne unusu asubuhi (saa za Marekani) na kutumia mlango wa nyumba ambao waandishi wa habari hawakuweza kumuona akiingia.
Wakizngumza na waandishi wa habari, Barack Obama amesema kuwa amekuwa na mazungumzo mazuri na Donald Trump ambapo wamezungumzia kuhusu masuala ya sera za mambo ya nje, mambo ya ndani na masuala ya ulinzi na kubwa kuhusu makabidhiano ya ofisi yatakayofikia tamati Ijumaa, Januari 20, 2017 wakati Trump atakapoapishwa kuwa Rais wa 45 wa Marekani.
Kwa upande wa Trump alisema kuwa ni furaha kwake kukutana na kuzungumza na Rais Obama kwa mara ya kwanza na anatarajia kukutana na kushirikiana naye mara nyingi zaidi.
Kwa upande wa mke wa Trump, yeye amekutana na mke wa Rais Obama, Michelle Obama ambao nao wamefanya mazungumzo kuhusu ofosi ya Mama wa Taifa (First Lady).Hapa chini ni picha za Rais wa Marekani na Rais Mteule wa Marekani wakizungumza na waandishi wa habari baada ya mazungumzo yao.






google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us