SERIKALI YAREKEBISHA TENA MFUMO HUU WA ELIMU | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 15 November 2016

SERIKALI YAREKEBISHA TENA MFUMO HUU WA ELIMU


Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako. 

Dar es Salaam.Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imeendelea kuufumua mfumo wa elimu uliopigiwa kelele na wadau wakati wa Serikali iliyopita kwamba unashusha ubora wa elimu baada ya Alhamisi iliyopita kutoa waraka mpya unaobatilisha programu za mafunzo ya ualimu.

Mabadiliko mengine ya elimu yaliyofanyika katika Serikali ya Awamu ya Tano ni kuwaondoa wanafunzi wa cheti na stashahada maalumu ya ualimu wa sayansi Chuo Kikuu cha Dodoma, kufuta GPA na kurejesha Divisheni na kufuta mtihani wa pili (paper two) kwa watahiniwa binafsi.

Katika mkakati wa hivi karibuni, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imetoa Waraka wa Elimu Namba 5 wa mwaka 2016, unaolipokonya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte) mamlaka ya usimamizi wa vyuo vya elimu ngazi ya cheti na stashahada na kuyarejesha wizarani chini ya uangalizi wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).

Hivyo, Necta ndiyo itatahini na kutoa tuzo ya mafunzo ya ualimu wa cheti na stashahada kuanzia mwaka 2016/17.

Source: Mwananchi

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us