Wakosoaji wa Castro wafurahia kifo chake | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Sunday 27 November 2016

Wakosoaji wa Castro wafurahia kifo chake

Wakosoaji wa mwanamapinduzi, aliyekuwa kiongozi wa Cuba, Fidel Castro, wanaoishi Miami, nchini Marekani, kilomita 200 kutoka ufuo wa Bahari wa Cuba, walifanya maadhimisho ya hadharani kufuatia kutangazwa kwa kifo cha kiongozi huyo.

Wengi wao walihamia Miami baada ya Castro kupindua Serikali yenye ufisadi mkubwa, iliyokuwa ikiungwa mkono na Marekani mwaka 1959.

Wengine wengi waliungana nao baada ya muungano wa Sovieti, taifa lililokuwa likifadhili Cuba, kusambaratika na kusababisha mfumuko mkubwa wa bei.

Wakaazi wengi waliokumbuka umaskini na mateso ya kisiasa na kidini aliyokuwa akiwalimbikizia Castro, wengi waliendesha magari yao wakipiga honi kwa shangwe
Wengi walisikika wakipiga makelelewa wakisema Cuba sio Castro No!.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us