Baba Mzazi Wa Ben Saanane Kukagua Maiti Iliyowekwa Kwenye Kiroba | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 20 December 2016

Baba Mzazi Wa Ben Saanane Kukagua Maiti Iliyowekwa Kwenye Kiroba

Wakati polisi wakisema kuwa wanaufanyia mchakato wa vipimo vya vinasaba (DNA), mwili wa mtu anayedaiwa kuuawa nje kidogo ya mji wa Moshi na kuwekwa kwenye kiroba na kuchomwa moto, familia ya Ben Saanane, msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye hajulikani aliko imesema inaenda kuuangalia mwili huo. 

Hatua hiyo ya polisi kupima DNA ilielezwa na Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa baada ya hadi jana, mwili huo kutotambuliwa. 

Mauaji hayo yaligunduliwa Ijumaa iliyopita, baada ya watu waliokuwa na gari ndogo ambao hawajafahamika, kumchoma moto mtu huyo katika Kijiji cha Ongoma na kisha kutoweka kusikojulikana. 

Kamanda Mutafungwa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mtu huyo hajafahamika na wala hakuna mtu aliyejitokeza kuutambua mwili huo hivyo kulilazimu jeshi kufanya uchunguzi huo wa kisayansi. 

Kamanda Mutafungwa alitoa wito kwa ndugu, jamaa na marafiki waliopotelewa na ndugu, wafike katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC kuutambua mwili huo. 

Kuhusu madai ya marehemu kwamba alikuwa amevaa suruali inayofanana na sare za wafungwa, Kamanda Mutafungwa alisema si kweli kwani nguo iliyoonekana ni blanketi jepesi la rangi ya chungwa. 

Mzazi wa Saanane 

Wakati polisi ikijiandaa kwa mchakato huo, baba wa Saanane, Focus Saanane, jana alikuwa anajiandaa kwenda KCMC kuangalia mwili huo. 

Akizungumza jana mjini Moshi, Saanane alisema japokuwa mtoto wake alipotelea Dar es Salaam, watakwenda kuuangalia mwili huo ili kujiridhisha. 

Juzi Saanane alikaririwa akiiomba Serikali kufanya uchunguzi wa kupotea kwa mwanaye akisema ndiyo pekee yenye vyombo vya kiuchunguzi. 

Kuokotwa kwa mwili huo kunashabihiana na tukio la kupatikana kwa miili mingine saba katika Mto Ruvu mkoani Pwani ikiwa imefungwa katika viroba na kuwekewa mawe ili izame. 

Miili hiyo ilizikwa na wananchi wanaoishi jirani na mto huo bila kufanyika kwa vipimo vya DNA wala kutoa tangazo la watu waliopotolewa na ndugu zao kujitokeza kutambua maiti hizo hali iliyoibua utata. 

Tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alishaagiza kufanyika kwa uchunguzi wa miili hiyo na kutaka wale wote waliohusika na mauaji hayo watafutwe na kukamatwa.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us