Mourinho asema ""nitabaki Yuda namba moja"" | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Tuesday 14 March 2017

Mourinho asema ""nitabaki Yuda namba moja""

Kocha wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amewajibu mashabiki wa Chelsea waliokuwa wakimuita ‘Yuda’ katika mechi ya Kombe la FA robo fainali dhidi ya Chelsea.

Sehemu moja ya mashabiki ilipiga kelele “F*** off Mourinho”, “Wewe si Special tena” na “ni Yuda” wakimaanisha msaliti katika ushindi wa Chelsea wa 1-0 katika uwanja wa Stamford Bridge.

Katika mahojiano na waandishi wa habari baada ya mechi hiyo Mourinho alijibu.

“Wanaweza kuniita chochote wapendacho. Hadi watakapopata meneja anayewashindia mataji manne ya Ligi ya Uingereza, Mimi ni nambari moja,” alisema Mourinho ambaye alitupiwa virago Chelsea msimu uliopita.

Katika vipindi viwili tofauti kama meneja wa Chelsea (2004-2007 na 2013-2015), Mourinho aliinoa Chelsea na kuipa mataji manne ya ligi, moja la FA na matatu ya Kombe la Ligi.

“Watakapopata mtu wa kuwapa mataji manne ya Ligi ya Uingereza, basi nitakuwa namba mbili. Lakini hadi sasa Yuda bado ni namba moja.”

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us