Kenya Nao Waiga usafiri wa Mwendokasi kama Tanzania..!! | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 19 April 2017

Kenya Nao Waiga usafiri wa Mwendokasi kama Tanzania..!!


Mara nyingi watanzania wamekuwa wanataja mafanikio ya nchi nyingine wakilinganisha na mazingira hafifu ya hapa nchini katika masuala ya Maendeleo.

Lakini  orodha ya mazuri yanayoigwa na nchi nyingine kutoka Tanzania itakuwa imeongezeka kwa jambo moja lingine ambalo ni Mabasi ya mwendo kasi.

Aidha, Mamlaka ya usafiri jiji la Nairobi imefufua mpango kupunguza foleni za magari kwa  kuanzisha usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi kama yanayotumika kwa sasa nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa Katibu wa Masuala ya usafirishaji Mwangi Mariga alisema ujenzi wa  mradi huo wa Mabasi ya  Mwendokasi  utahusisha miji mitano.

Naye  Katibu wa Baraza la Mawaziri James Macharia alishauri   mwaka jana kwamba mapendekezo maalum ya mfumo wa Mabasi ya  usafiri yalikuwa na changamoto kutokana na miundombinu iliyopo ya  barabara  kwa mabasi kuwa na msongamano.

Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi   umebuniwa kufuatia idadi ya watu wa Nairobi kuongezeka hadi milioni 3.3 kutoka 350,000 mwaka 1963 na idadi ya magari inakadiriwa kufikia 300,000 bila ongezeko sawa katika mtandao wa barabara.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us