Wasanii: Paul Makonda Anajua Alipo Roma, Atafutwa Vituo Vyote vya Polisi Dar Bila Mafanikio. | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 7 April 2017

Wasanii: Paul Makonda Anajua Alipo Roma, Atafutwa Vituo Vyote vya Polisi Dar Bila Mafanikio.


Wasanii kupitia kwa kikao chao kilichofanyika leo Tongwe records wamepaza sauti na kushusha lawama kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ndugu Paul Makonda kuwa anajua vizuri alipo msanii Roma Mkatoliki. 

Wasanii hao wamesema kuwa watekaji hao walitamka wazi kuwa wanamtaka msanii Roma na producer wake na walipoona watajulikana ndipo walipoamua kuondoka na watu wote waliokuwepo ndani ya studio za Tongwe records siku hiyo ya alhamisi juzi. 

Aidha Babu Tale ambaye ni meneja wa wasanii kadhaa akiwemo Diamond amesema kuwa kwa hili kamwe hamuogopi Paul Makonda na amemtaka kumrejesha mara moja msanii mwenzao. 

Aidha Babu Tale amesema kuwa anashangaa kuona Paul Makonda yupo kimya juu ya hili huku yeye akiwa kama kiongozi mkuu wa ulinzi na usalama ndani ya Dar es Salaam.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us