MBUNGE: Diamond Anadaiwa Milioni 400 Na TRA. | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 10 May 2017

MBUNGE: Diamond Anadaiwa Milioni 400 Na TRA.


Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia ameliambia Bunge kuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul ‘Diamond Platinumz’, anadaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zaidi ya Sh. milioni 400.

Mbunge huyo aliyasema hayo bungeni jana wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Amesema Wilaya ya Kinondoni ina wasanii wengi maarufu na wamekuwa wakitoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi kutokana na mauzo ya kazi zao na kwamba Diamond Platinumz amemueleza kuwa kwa sasa anadaiwa kodi ya zaidi ya Sh. milioni 400.

Naiomba serikali kuhakikisha inaimarisha mapambano dhidi ya wizi wa kazi zao badala ya kutilia mkazo kwenye ukusanyaji wa kodi pekee kwani msanii huyo na wenzake wanaingiza kiasi kikubwa cha fedha kutokana na kazi zao za sanaa,

Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi wa Elimu na Huduma kwa Walipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema suala hilo liko kwenye uchunguzi.

“Hilo liko kwenye hatua ambayo hatuwezi kulizungumzia kwenye vyombo vya habari. Liko katika ‘investigation’ (uchunguzi),” amesema

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us