Daraja la Kioo China Lasitishwa Kutumika Baada ya Wiki 2 | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 3 September 2016

Daraja la Kioo China Lasitishwa Kutumika Baada ya Wiki 2


Zhangjiajie, China:

Daraja la kioo ambalo limeelezwa kuwa liko juu zaidi liliziduliwa hivi karibuni nchini China ambapo lina urefu wa zaidi ya futi 1400, upana wa futi 20 na karibu futi 1000 kutoka kwenye ardhi na imeripotiwa kuwa kioo chake ni imara zaidi mara 25 zaidi ya kioo cha dirisha.

Daraja hilo la wapita kwa miguu lijulikanalo kwa jina la daraja la Zhangjiajie lilizinduliwa August 20 mwaka huu ambapo lina uwezo wa kuchukua watu hadi 800 kwa wakati mmoja. Imeelezwa kuwa daraja hilo limekuwa likitumika kwa shughuli mbalimbali za kiutalii.

Daraja hilo limelazimika kufungwa ili kufanyiwa maboresho ya ndani baada ya idadi kubwa ya watalii waliokusanyika kutembelea kweye daraja hilo. Daraja hilo ambalo liko Kusini mwa China liligharimu dola million 48 kujengwa, na lilifunguliwa August 20 na limesitishwa huduma zake leo.

Msemaji wa kivutio hicho aliiambia MailOnline kuwa daraja lilitengenezwa ili kuweza kuchukua kiwango cha juu cha watu ambao ni 800 kwa wakati mmoja, na limepokea takribani watu 10,000 ambao ni watalii tangu lifunguliwe, msemaji huyo alisisitiza kuwa ni sehemu ya kioo ya daraja ni salama.

source GPL

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us