Serikali Yasogeza Mbele Field Kwa Wanafunzi Wa Afya 2016 | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 1 October 2016

Serikali Yasogeza Mbele Field Kwa Wanafunzi Wa Afya 2016


Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia ,wazee na watoto inawatangazia wahitimu wote wa vyuo vikuu vya kada mbalimbali za afya wanaopaswa kufanywa mafunzo ya utarajali yani ‘internship’ ambao ni madaktari wa meno, wafamasia, wauguzi, wataalamu wa Radiolojia, wataalamu wa maabara na wataalamu wa afya ya mazingira kwamba pamoja na kuwa walipaswa kuanza mafunzo yao leo Oktoba 1, 2016  ambayo ilikuwa ni tarehe rasmi ya kuanza mafunzo hayo itatangazwa hapo baadae.

Wizara ya Afya imesema kuwa kuchelewa huko ni kutokana na juhudi zinazoendelea kufanywa na Wizara ili kuhakikisha kuwa mafunzo hayo yanaanza katika namna na mfumo uliobora zaidi.

Aidha Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Muhammad bakari kambi  (Pichani juu) amesema kuwa mara baada ya juhudi hizo kukamilika wataalamu tajwa watafahamishwa rasmi na hivyo kuwaomba wataalamu hawa na wadau wengine kuwa na subira.

“Tunapenda kuwafahamisha wahitimu ambao walikuwa hawajapangiwa vituo vya kufanyia mafunzo kwa vitendo, kuwa utaratibu unafanywa kuhakikisha kwamba wanapangiwa vituo hivi karibuni ambapo mtandao utafunguliwa na wahusika watapewa taarifa”. Amesema Prof. Muhammad Bakari



google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us