Sallam atangaza ujio wa tamasha la Diamonds Are Forever 2017 | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 20 January 2017

Sallam atangaza ujio wa tamasha la Diamonds Are Forever 2017

Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK aka ‘Fundi Mitambo’ ametangaza ujio mpya wa tamasha kubwa la Diamonds Are Forever 2017 ambapo safari hii litafanyikia katika uwanja wa Taifa.

Muimbaji huyo alifanya tamasha hilo kwa mara ya kwanza nchini mwaka 2012 katika ukumbi wa Mlimani City show ambayo ilihudhuriwa na watu wengi kwa kiingilio cha Tsh 50,000.

Sallam akizungumza live na mashabiki katika mtandao wa Istangam (Insta Live) alisema show hiyo ipo kwenye maandalizi na itafanyika uwanja wa Taifa.

“Mjiandae na Diamonds Are Forever 2017, Diamonds Are Forever 2017 is back,” Sallam aliwaambia mashabiki.

Meneja huyo alidai safari hii tamasha hilo litafanyika uwanja wa taifa ili kuwapa fursa watu wengi zaidi ya kuudhuria.

Hata hivyo hakuweka wazi ni lini au mwezi gani tamasha hilo litafanyika.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us