Mrembo Rayuu Afungukia Kuhusu ndoa yake Kuvunjika | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 29 April 2017

Mrembo Rayuu Afungukia Kuhusu ndoa yake Kuvunjika

BAADA ya madai kuzagaa kuwa ndoa yake imevunjika, msanii wa filamu Bongo, Alice Bagenzi ‘Rayuu’ ameibuka na kueleza kuwa madai hayo yametokana na watu waliozoea kuona akimuuzisha sura mumewe mtandaoni lakini ameamua kusitisha tu na siyo kwamba ndoa haipo. 

Akipiga stori na chanzo chetu, Rayuu alisema, awali alikuwa anapenda kumuanika mumewe kwenye mitandao ya kijamii lakini kutokana na maneno ya hapa na pale ya watu wasioitakia mema ndoa yake akaona bora asimuweke lakini ndoa yao ipo imara na hawafi kirii kuachana.

“Naweza kusema hii ndoa imenikuza, kwa maneno ya watu nimejifunza mengi kwenye hii dunia yaani utoto wote umeisha, wengi wanajadili kuwa tumeachana sababu hawaoni nikimuweka kwenye mitandao kama mwanzo, kwani nimegundua hakuna faida bali ni kujiletea matatizo yanayoweza kuvunja ndoa, japo kukosana ni kawaida kwenye mapenzi,” alisema.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us