Ofisi ya Republican yarushiwa bomu Marekani | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 17 October 2016

Ofisi ya Republican yarushiwa bomu Marekani


Afisi ya chama cha Republican iliopigwa bomu katika kaunti ya Orange nchini Marekani
Image captionAfisi ya chama cha Republican iliopigwa bomu katika kaunti ya Orange nchini Marekani
Afisi moja ya chama cha Republican katika jimbo la North Carolina imeharibiwa na moto huku jengo lililo karibu yake likipakwa rangi ya nembo inayopinga chama cha Republican,mamlaka imesema.
Chupa iliojazwa mafuta yanayoweza kushika moto ilirushwa katika dirisha la makao makuu ya chama cha Republican kaunti ya Orange,chama hicho kimesema.
Mkurugenzi wa chama cha Republican, Dallas Woodhouse alisema kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa,na kwamba tahadhari ya kiusalama imetumwa katika afisi nyengine za chama hicho.
''Wanachama wa Nazi walio katika chama cha Republican ni sharti waondoke mjini''.
Mgombea wa Democrat Hillary Clinton ameandika katika mtandao wake wa Twitter kwamba shambulio hilo ni ''la kutisha na halitakubalika''.
Afisi ya chama cha Republican ilishambuliwa kwa bomu nchini Marekani
Image captionAfisi ya chama cha Republican ilishambuliwa kwa bomu nchini Marekani
Lakini Mgombea wa chama cha Republican Donald Trump alionekana akiwalaumu wafuasi wa chama cha Democrat kwa kutekeleza kitendo hicho.
''Wanyama wanaomwakilisha Hillary Clinton huko North Carolina walirusha bomu katika ofisi yetu ya kaunti ya Ornge kwa sababu tunashinda'',alisema katika mtandao wake wa Twitter

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us